Ujumbe wa Urais wa Kwanza, Machi 2010 Na Rais Henry B. Eyring Mshauri wa Kwanza katika Urais wa Kwanza Ujasiri wa Kimaadili Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani ni kumuonyesha Mungu kwamba tutatii amri Zake ilihari hii huitaji ujasiri. Tulipita mutihani huo katika ulimwengu wa kiroho. Lakini thuluthi moja ya majeshi ya mbinguni yaliasi dhidi ya pendekezo kwamba watajaribiwa katika kuishi kimwili ambapo palikuwepo na hatari kwamba wangeweza kuanguka. Kabla hatujazaliwa, tulimjua Mungu Baba na Mwanawe, Yesu Kristo, kibinafsi. Tungeweza kuwaona Wao na kuwasikiliza Wao jinsi walivotufunza na kutuhimiza sisi. Sasa pazia imewekwa juu ya akili zetu na kumbukumbu zetu. Shetani, baba wa uwongo, anajinufaisha kwa sababu ni lazima tuone uhasili wa kujua sisi ni kina nani kupitia macho ya imani, ilihali miili yetu inatufanya kuwa chini ya majaribio na udhaifu wa kimwili. Tuna usaidizi mkuu wa kutupatia ujasiri katika maisha haya. Mkuu ni Upatanisho wa Yesu Kristo. Kwa sababu ya kile alichofanya, dhambi zinaweza kuoshwa katika maji ya ubatizo. Tunaweza kufanya upya hio baraka wakati tunashiriki katika sakramenti kwa imani na kwa moyo wa toba. Vipawa vya Kiroho ni usaidizi mwengine Tunapokea Roho wa Kristo wakati wa Kuzaliwa. Hiyo inatupatia uwezo wa kujua wakati uchaguzi ulio mbele yetu utatuelekeza kwenye maisha ya milele. Maandiko ni kielelezo cha kweli tunapoyasoma pamoja na Roho Mtakatifu kama mwenzi wetu. Roho Mtakatifu utuacha tukaonyesha shukrani na kuuliza usaidizi katika maombi kwa uwazi na uhakika tuliofurahia tulipokuwa na Baba wetu wa Mbinguni na ambao tutakuwa nao tutakaporudi Kwake. Kwamba mawasiliano na Mungu yanasaidia kuondoa hofu kutoka katika mioyo yetu yanajenga imani na upendo wa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Ukuhani mtakatifu unatupatia sisi ujasiri katika huduma yetu. Katika ibada zake tunapokea uwezo wa kuwatumikia watoto wa Mungu na kustahimili mvuto wa uovu. Anapotuita sisi kuhudumu, tuna ahadi hii: Na yeyote awapokeaye, hapo nitakuwepo pia, kwani nitakwenda mbele ya nyuzo zenu. Nitakuwa mkononi mwenu wa kulia na wa kushoto, na Roho wangu atakuwa mioyoni mwenu, na malaika wangu watawazingira, ili kuwabeba juu (M&M 84:88). Nabii Joseph Smith katika huduma yake alikuwa na sababu ya kuwa na hofu. Lakini Mungu alimpatia ujasiri kwa uhakikisho huu wa mfano wa Bwana: Kwa maana utatupwa ndani ya shimo, au katika mikono ya wauaji, na hukumu ya kifo ikapitishwa juu 1
yako; kama utatupwa kilindini; kama mawimbi makali yatakula njama dhidi yako; kama upepo mkali utakuja kuwa adui yako; kama mbingu zitakusanya giza, na vitu vyote vya asili vikiungana ili kuzingira njia yako; na juu ya yote, kama mataja yale ya jahanamu yataachana kinywa wazi kwa ajili yako, fahamu wewe, mwanangu, kwamba mambo haya yote yatakupa wewe uzoefu, na yatakuwa kwa faida yako. Mwana wa Mtu ameshuka chini yao wote. Je, wewe u mkuu kuliko yeye? (M&M 122:7 8) Mungu ametupatia sisi usaidizi wa kupindukia wa kuondoa hofu na kutupatia ujasiri, katika chochote tutakachokabiliana nacho. Tunapotafuta usaidizi Wake, Anaweza kutuinua kuelekea ule uzima wa milele tunaotafuta. Kufunza kutoka kwa Ujumbe Huu Yesu Kristo, Bwana Mwalimu, kila mara aliuliza maswali ya kuwahimiza watu kutafakari na kutumia kanuni Alizofunza.... maswali Yake yalichochea fikra, kujiuliza nafsini, na kuweka sharti Teaching, No Greater Call [1999], 68). Jaribu kubuni na kuuliza maswali kadhaa ya kuwasaidia watu kufahamu na kutumia kweli zilizofunzwa katika huu ujumbe. Kwa mfano, unaweza kuuliza, Je, ni usaizidi gani Mungu amekupatia wewe wa kuondoa hofu na kukupatia ujasiri? au Mungu amekusaidia vipi wewe kushinda hofu? Himiza watu kutafakari maswali kabla ya kujibu. Vijana Hakuna aliye Kamili Na Shauna Skoubye Mimi siku zote nimetamani kuwa kama Nefi: mtiifu wa dhati, muaminifu mkuu,na mwenye roho ya kina. Katika macho yangu Nefi alikuwa mfano mkuu wa wema. Vitu vichache vinanipendeza mimi zaidi ya dhana ya kukua na kuwa kama yeye au angalau kuanza kuwa na hata sehemu ya ubora wake. Siku moja nilikuwa na matatizo madogo, yaliyoletwa na hisia za kutojitosheleza. Nilikuwa na tamaa kuu na malengo mengi. Lakini nilikuwa nikioenekana kutopata mafanikio yoyote. Nikiwa na Majozi ya kukata tamaa, nilielezea hisia hizi kwa baba yangu. Mara moja alisimama, na kutembea hadi kwenye kasha la vitabu, na akatoa mojawapo ya nakala zake za Kitabu cha Mormoni. Bila kusema neno, aliifungua kwenye 2 Nefi 4 na akaanza kusoma mstari wa 17. Mzizimo ulizangaa kwenye mwili wangu wote kama umeme nilipokuwa nikisikiliza maneno haya ya nguvu: Ewe mimi mtu mwovu Fikira zangu zilikimbia. Nefi, shujaa wangu na mfano, angelisema vipi kwamba alikuwa mtu mwovu? Kama alikuwa mtu mwovu, hicho kilifanya mimi kuwa nani? Tena, umeme ulivuma ndani yangu baba yangu alipokuwa akisoma mstari 28: Amka,roho yangu! Usilemewe na dhambi. Nilisikia kama vile wingu la giza katika akili yangu lilitawanywa na kuondolewa ili kufunua shauku na wangavu wa wingu wazi la bluu na jua angavu. Sio rahisi kuelezea vile huu mstari uliangaza nafsi yangu. Mistari michache ya maandiko yamenijaza tumaini, maongozi, na furaha kama hii ilivyofanya. Katika mstari wa 30, Nefi alisema hasa kile nilichokuwa nikifikiria, tu katika maneno ya umbuji mwingi: Nafsi yangu itashangilia kwaajili yako, Mungu wangu, na mwamba wa wokovu wangu. Mstari huu ulileta hisia ya amani na shukrani kwa nehema nyororo za Bwana na upendo. Baba yangu alifunga kitabu na kuelezea kwamba mistari hii mara nyingine uitwa zaburi ya Nefi. Alafu alinifunza kwa makini kwamba hata watu wakuu katika dunia sio kamili, na watu hawa sharti watambue ukosefu wao au kwa vingine watakuwa na kiburi na, kwa hivyo, wasiwe wakuu. Nilifahamu. Kwa sababu tu nilikuwa na unyonge haikumaanisha nilikuwa siwezi kuwa kama Nefi. Kutambua unyonge wangu ulinileta karibu na hadhi ya Nefi. Nefi alikuwa mkuu kwa sababu, vile vile akiwa mtiifu na mwaminifu, alikuwa mnyenyekevu na tayari kukubali makosa yake. Tangu uzoefu huu, nimeyathamini sana maneno haya ya Nefi. Kila wakati ninapoyasoma, napata muemuko huo huo na maangozi kama yale ya kwanza nilipoyasoma. Mistari hii inaniimbia kwamba mimi ni binti wa Mungu, mwenye uwezo mkuu zaidi ya vile ningeweza kudhania. Najua kwamba kama nitakuwa mwaminifu na kusonga mbele, baraka zisizoweza kusemeka zimehifadhiwa. 2
Watoto Vipawa Ambavyo vinatupatia Ujasiri Rais Eyring anatuambia juu ya vipawa kadhaa ambavyo vinatupatia ujasiri. Soma kila maandiko yaliyopo chini, na uandike jina la kila kipawa katika pengo Ongea na familia yako juu ya jinsi hicho kipawa kinaweza kukupatia ujasiri. 1. Matendo ya Mitume 22:16 2. 2 Nefi 4:15 3. M&M 59:8 9 4. 2 Nefi 32:5; Yohana 14:26 27 5. 1 Wathesalonike 5:17 2010 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Imechapishwa USA. Kiingereza kiliidhinishwa: 6/09. Tafsiri Iliidhinishwa: 6/09. Tafsiri ya First Presidency Message, March 2010. Swahili. 09363 743 3
Ujumbe wa Mwalimu Mtembelezi, Machi 2010 Kuimarisha Imani katika Mungu Baba na Yesu Kristo kupitia Masomo ya Maandiko ya Kibinafsi Funza maandiko na dondoo hizi, au, ikihitajika, kanuni nyingine ambayo itabariki akina dada unaowatembelea. Toa ushuhuda wa fundisho hili. Alika wale unaowafundisha kushirikisha walichohisi na kujifundisha. Nilipokuwa bibi arusi mpya,... nilialikwa kwa mlo wa chakula cha mchana wa kina dada wote wa Muungano wa Usaidizi wa Akina Mama katika kata yangu ambao walikuwa wamesoma kati ya Kitabu cha Mormoni au kitabu kifupi cha historia ya Kanisa. Nilikuwa mzembe katika kusoma maandiko, kwa hivyo nilihitimu kuudhuria chakula cha mchana kwa kusoma kitabu kifupi kwa sababu kilikuwa rahisi na kilichukua muda mfupi. Nilipokuwa nikila chakula changu cha mchana, nilikuwa na hisia nzito kwamba hata kama kitabu cha historia kilikuwa kizuri, ningesoma Kitabu cha Mormoni. Roho Mtakatifu alikuwa ananishawishi kubadilisha tabia yangu ya kusoma maandiko Siku hiyo hiyo nilianza kusoma Kitabu cha Mormoni, na sijawahi kusimama kamwe.... Kwa sababu nilianza kusoma maandiko kila siku, nimejifunza juu ya Baba wangu wa Mbinguni, Mwanawe Yesu Kristo, na kile ninachohitaji kufanya ili kuwa kama Wao.... Kila mwanamke anaweza kuwa mwalimu wa injili nyumbani mwake, na kila mwanadada Kanisani anahitaji elimu ya injili kama kiongozi na mwalimu. Kama bado hujaanza tabia ya kusoma maandiko kila siku, anza sasa na uendelee kujifunza ili kujitayarisha kwa majukumu yako katika maisha haya na katika milele. 1 Julie B. Beck, Rais mkuu wa Muungano wa Usaidizi wa Akina mama. Kujifunza kwa maandiko kutasaidia ushuhuda wetu na ushuhuda wa wanafamilia wetu. Watoto wetu leo wanakua wakizingirwa na sauti zinazowashawishi kuachilia kile kilicho sawa na kufuata, badala yake, anasa za ulimwengu. Wasipokuwa na msingi imara katika injili ya Yesu Kristo, ushuhuda wa kweli, na azimio la kuishi vyema, watakuwa wanaweza kuathirika na mvuto huu. Ni jukumu letu kuwalinda na kuwakinga. 2 Rais Thomas S. Monson. Tunataka kina dada zwtu wawe wasomi wa maandiko.... Mnahitaji Usaidizi kwa Mwalimu Mtembelezi Wakati wa matembezi, jibu maswali na shirikisha utambuzi ukitumia maandiko. Toa ushuhuda wa jinsi mafundisho ya maandiko yameimarisha imani yako. Muulize dada unayemtembelea kushirikisha jinsi kusoma kwake kwa maandiko kumeimarisha nyumba yake na familia yake. Matayarisho ya Kibinafsi Yohana 5:39 2 Timotheo 3:1 17 2 Nefi 9:50 51; 31:20; 32:3 5 M&M 138:1 11 uzoefu na ukweli wake wa milele, kwa ufanisi wako mwenyewe, na kwa madhumuni ya kuwafundisha watoto wenu wenyewe na wale wengine wanaokuja katika ushawishi wenu. 3 Tunataka nyumba zetu zibarikiwe na akina dada wasomi wa maandiko hata kama ujaolewa au umeolewa, kijana ua mzee, mjane au unaishi katika familia. Mmwe wasomi wa maandiko sio kuwaweka wengine chini, lakini kuwainua juu! 4 Rais Spencer W. Kimball (1895 1985). 1
Muhtasari 1. Julie B. Beck, My Soul Delighteth in the Scriptures, Liahona May 2004, 107 9. 2. Thomas S. Monson, Three Goals to Guide You, Liahona, Nov. 2007, 118. 3. Spencer W. Kimball, Privileges and Responsibilities of Sisters, Ensign, Nov. 1978, 102. 4. Spencer W. Kimball, The Role of Righteous Women, Ensign, Nov. 1979, 102. 2010 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Imechapishwa USA. Kiingereza kiliidhinishwa: 6/09. Tafsiri Iliidhinishwa: 6/09. Tafsiri ya Visiting Teaching Message, March 2010. Swahili. 09363 743 2