DINI JE, DINI NI MUHIMU?

Similar documents
John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane

There is one God Mungu ni mmoja 1

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI)

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume

Bismillah ar-rahman ar-raheem SHAHADA 1 YALIYOMO

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags:

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

HALI YA UISLAMU. Maelezo ya kumsaidia Mkristo aufahamu Uislamu

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh)

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

AHMAD AL-RAYSUNI. SWAHILI VERSION idara ya Lugha na ukalimani ya Chuo Kikuu cha waislamu cha Morogoro. IIIT Mfululizo wa Vitabu kwa Muhtasari

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu

NEW INTERNATIONAL VERSION

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili

Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir

Kuishi Maisha Tele. Katika mwanzo wa mwaka mpya, Niliwapa changamoto

Published on Al-Islam.org ( Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu

Ukweli wa hadith ya karatasi

2002 Version of the Basic Talk on "Using African Proverbs, Sayings, Idioms, Riddles, Stories, Fables, Play

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (

Ujasiri wa Kimaadili. Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani

Gazeti la kwanza la Kiislam kutolewa kwa lugha ya Kiswahili - mwaka 1936

Je, Umesikia Juu Ya Kanuni Nne Za Kiroho?

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT RHAMU

February 9, 2017 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 16 MOMBASA COUNTY ASSEMBLY

Toleo la kwanza: June, 2007 (Jamaadi Aakhar, 1428) Vitabu ii.

MOROGORO JARIDA LA. ISSN Toleo Na.4 Julai 2005 BODI ZA AFYA ZA WILAYA - SAUTI YA WANANCHI

IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE.

Zanzibar itafutika-mwanasheria

NEW INTERNATIONAL VERSION

Rainbow of Promise Journal

UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI

Imam Mahdi katika Usunni Na Ushia

YA AL HABBIB SAYYEID

Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya

Uwezo Kenya National Learning Assessment 2014

Ukoo Wake Na Kunasibika Kwake:

TUMERITHI TUWARITHISHE

HOTUBA YA JAJI MKUU MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA SIKU YA SHERIA, DAR ES SALAAM, TAREHE 1 FEBRUARI, 2018

No. Book Name Category Type Price 1 AFYA MARIDHAWA -1 SWAHILI SUBSCRIPTION 2, AFYA NA UZIMA SWAHILI SUBSCRIPTION 8,500.00

HAKIBulletin RAIS AMTEUA PROF. JUMA KUWA JAJI MKUU WA TANZANIA. Ndani: JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA

Vitendawili Vya Swahili

MRADI WA METHALI (SANALASKUJA PROJEKTI)

JUNE 4, Acts 2:1-12 and Offering...Pastor Maromy Samuel All Hail the Power of Jesus Name led by Haitian Congregation Worship Team

KITABU CHA MAFUNZO KWA WATOA DAWA KATIKA MADUKA YA DAWA MUHIMU

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS IJARA CONSTITUENCY AT IJARA BARAZA PARK

TAARIFA YA HISTORIA YA MKOA WA MWANZA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Mashairi ya Masaibu ya Karbala

HAKIBulletin JAJI MKUU AWAASA WAHITIMU WA SHERIA KUJIENDELEZA KITAALUMA HALIUZWI! BENKI YA DUNIA USULUHISHI MUAFAKA MAHAKAMA MAWAKILI MAHAKAMA KUU,

Ripoti ya Warsha Ya Washikadau Ihusuyo Mpango wa Uendeshaji wa Mazingira Wilayani Rufiji Iliyofanyika Utete Rufiji Juni 2000

NGUO-NYINGI MKOTI: MWANZISHAJI WA MJI WA NGOJI (ANGOCHE)

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

WELCOME TO GOD S SERVICE A.C.K. ST. LUKE S PARISH UMOJA & TENA CHURCH QUOTE OF THE WEEK PRAYER OF THE DAY

TALKING ABOUT ONESELF TO ACT IN THE WORLD: A SWAHILI AUTOBIOGRAPHY (SHAABAN ROBERT, MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI

WELCOME TO GOD S SERVICE ACK ST. LUKE`S PARISH UMOJA Theme: Endeavoring to touch the heart of God, (Matt 25:40). Kuazimia kumpendeza Mungu

Ahadi za Serikali II. Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007

2

In Search of Contact: Rhetorical Questions in the Communicative Frame of the Funeral Sermon

NAIROBI CITY COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)

The Lord be with you And with your spirit

MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU SHEIKH MUZAFFAR AHMAD DURRANI

HOLY COMMUNION ACCORDING TO THE KENYAN RITE

REPUBLIC OF KENYA COUNTY ASSEMBLY OF KILIFI THE HANSARD. Wednesday, 29 th March, 2017

Yassarnal Quran English

(Cell) (Cell) (Cell) (Landline) (Cell)

MASHAIRI YA WAADHI "VERSES OF ADMONITION": the people of Mombasa rebuked by P J. L Frank! and Yahya Ali Omar

Ezra 3 Lessons Download or Read Online ebook ezra 3 lessons in PDF Format From The Best User Guide Database

MANIFESTATION OF COMMON MAN LANGUAGE IN EPIC POEMS: A CASE STUDY OF UTENDI WA SIRI LI ASRARI

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

VACATION BIBLE SCHOOL VBS. Newsletter. #Rebuilding through prayer, hard work & perseverance.

December 6, 2017 PARLIAMENTARY DEBATES 1 NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL REPORT. Wednesday, 6 th December The House met at 9.30 a.m.

Where is Africa? 2. What is African heritage? 3. What is the African heritage in the Bible? 6. What are African ways of worship?

AND REACTION IN SWAHILI POETRY.

TAUS RETREAT NEWS LETTER # 1

JINA KAMILI CHEO SIMU YA OFISINI Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwandishi Mwendesha Ofisi

Youth and Faith A collection of texts on the subject A collaborative Magazine Content

Modern Swahili: the integration of Arabic culture into Swahili literature

ATONEMENT IN AFRICAN PLURALISTIC CONTEXT: EXAMPLES FROM THE LUHYA OF WESTERN KENYA

Wisdom Heaven. from. Martin Luther College Choir

3 rd of 3 files Appendix and References

AFRIKA FOCUS, Vol.3, Nr.3-4, 1987, PP

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT ELWAK

A COLLECTION OF 100 MAKONDE (KENYA) PROVERBS AND WISE SAYINGS

I Peter 2:9-12 Who Are You?

Compassionate Together:

2

Immaculate Conception Church

Cultural Considerations Tanzania Excursion

Transcription:

SURA YA KWANZA DINI Hivyo, Mwislamu wa kweli ni yule ambaye hufuata mafundisho ya Uislamu wakati wote. Kama tu Waislamu wa kweli, basi lazima tufuate sheria za Ki-Islamu tukiwa ndani na nje ya nyumba zetu, yaani madarasani, katika viwanja vya michezo, Misikitini, mitaani na popote tutakapokuwa. Katika Istilahi za Ki-Islamu, neno "Dini" limetumika kama religion (kwa lugha ya Kiingereza). Lakini neno Dini (kwa lugha ya kiarabu) lina maana pana sana katika ukubwa wake kuliko neno la Kiingereza-Religion. Mbali na dini nyingine ambazo zimejihusisha na ibada tu, Uislamu hutoa: Mfumo kamili wa maisha Mfumo wa tabia. Mfumo sahihi wa maingiliano ya jamii. Katiba kamili ya utawala. Silabasi linganifu ya elimu pana. Mwelekeo sahihi wa dhamira ya utafiti wa Kisayansi. Dini maana yake mfumo makhususi wa imani na ibada. Kama tunaamini juu ya kitu kwa Umadhubuti na uimara, tunasema hii ni dini yangu. Hivyo kwa ufafànuzi, kama hatutendi kwa mujibu wa imani na itikadi ya dini yetu, ina maana kwamba hatuna imani na dini yetu. Quran Tukufu imetueleza kuhusu watu kama hawa. "Miongoni mwa watu kuna baadhi ambao huseme: Tunaamini katika Allah na siku ya mwisho;lakini (kwa hakika) hawaamini." (2:8) Quran Tukufu haitambui mtu yeyote kwamba Mwislamu kama hatekelezi mafundisho yake. JE, DINI NI MUHIMU? Kuna watu wengi katika ulimwengu huu ambao hawaamini katika dini. Wanafikiria kwamba dini sio muhimu. Hutoa baadhi ya hoja ambazo hazina msingi kuunga mkono dhana yao. Kwa mfano, wanasema: 1. Mtu hujua lililo zuri na lililo baya kwake yeye. Hivyo hahitaji Mtume yeyote kumfundisha. 2. Kuna dini nyingi tofauti katika ulimwengu huu na mafundisho tofauti kabisa na dhana zinazopingana. Chakushangaza zaidi, dini zote zinadai kwamba wao tu peke yao ndio wenye ukweli wote ambapo wengine wapo katika makosa. Vipi itaweza kuwa kweli? 3. Makatazo na amri za dini hutumia nguvu nyingi na muda wa mwanadamu. Hivyo dini ni kikwazo katika maendeleo ya kisayansi. 4. Dini haituruhusu kufurahia maisha. Tunaweza tukathibitisha kwamba hoja zote hizi ni bure kabisa na, hazina uthabiti kwao Hebu ngoja tuchambue yaliomo katika kila hoja, moja baada ya moja. 1 2

1. Ni kweli kwamba Allah (s.w.t) amempa mtu ubongo wa ajabu ambao unaweza kutambua jema na baya. Lakini bado tunaona watu wanahitilafiana sana katika maamuzi yao kuhusu mambo mema na mabaya. Kwa mfano; watu wengi hupendezewa kukaa uchi, kunywa pombe, kamari na matendo mengine mengi kama hayo ambayo yanaonekana kwa wengine kama jinai za uovu. Aidha, ubongo wa mwanadamu una mipaka fulani ambayo nje yake huwezi kuitambua. Tunaweza kujua kwa utafiti wa kisayansi kinachotokea katika mwezi, Mars na katika sayari zote nyingine. Lakini kamwe hatuwezi kujua kwa tekinolojia yoyote ukweli wa kaburi na barzakh, na matukio ambayo yatatokea katika akhera. Kwa taarifa zote hizo, tunahitaji Mtume ambaye ana mawasiliano ya moja kwa moja na Allah (s.w.t), Mola wa ulimwengu. Hivyo, bila shaka watu ni viumbe wenye akili lakini kwa hakika wanahitaji msaada wa Mitume takriban katika kila fani ya elimu. Tunaweza kuona leo kwamba wanasayansi wakubwa wa ulimwengu, wanafanya kosa kubwa sana kwa sababu hawafuati mafundisho ya Mitume watukufu. Hakuna ubishani kwamba leo maendeleo ya Kisayansi na ya Kitekinolojia yamekuwa tishio kwa mwanadamu. Hivyo akili za mwanadamu hazitoshi kugundua ukweli wote wa ulimwengu. Dini ya kweli hutufundisha mambo yale yote ambayo hakuna anaye weza kuyagundua kwa juhudi zake. 2. Ni kweli kuna dini nyingi tofauti zenye mafundisho tofauti na hakuna hata moja ya hizo iliyo ya kweli isipokuwa moja. Dini ya kweli inaweza kugunduliwa na kila mtu baada ya utafiti. Kwa mfano, katika soko tunajua kwamba vitu vyote safi na vichafu, halisi na bandia, vizuri na vibovu vinauzwa na watu. Kila mmoja hudai kwamba anavyo vitu visafi, halisi na vizuri ambapo wakati wote sio sahihi. Kwa kawaida huwa tunafanya nini katika hali zote hizo? Je, tuna acha kununua vitu kwa sababu wengi wanauza vitu vichafu au vibovu ama kila mtu anadai kwamba yeye peke yake anavyo, vitu bora na safi? La hasha. Tunafanya juhudi zote zinazo wezekana kutafuta duka ambalo linauza vitu sahihi. Halikadhalika, kama mtu anatambua umuhimu wa dini, anaweza kuitambua dini ya kweli baada ya utafiti na kusoma. 3. Hoja ya tatu vile vile ni ya makosa kabisa. Tunatumia wakati mwingi katika kula, kulala, kupumzika, kucheza na kuchanganyika na watu wengine (katika hafla na dhifa za kijamii-mathalani). Utumiaji wa muda na nguvu katika mambo yote haya ya kawaida ni wa juu sana. Lakini kamwe hatulalamiki kwamba matendo hayo (kulala, kula na mikutano) yanapoteza muda wetu mwingi na nguvu na kwa hiyo yatupasa kuyaacha ili kuendelea katika sayansi na tekinolojia. Kusema kweli, tunatambua kwamba kula kwa wasitani, kulala, na kucheza huzalisha nguvu za kufanya kazi zaidi. Halikadhalika, kumwabudu Allah (swt) huongeza uwezo wetu wa kufanya kazi zaidi za kisayansi. Mtu ambaye kwa unyeyekevu humwabudu Allah (swt) na ujuzi, kamwe hatapoteza muda wake katika kuangalia picha (za sinema) zisizo na maana, kusikiliza muziki, kucheza kamari katika nyumba za starehe au vitu vingine vya aina hiyo. Watu hupoteza idadi kubwa ya nguvu zao na muda katika kufanya mambo ambayo yamekatazwa katika Uislamu. 4. Hoja ya nne vile vile sio sahihi. Dini ya kweli huyafanya maisha yetu kujaa furaha. Magonjwa mengi sugu kama vile UKIMWI, saratani, na matatizo ya moyo huyafanya maisha ya mwanadamu kuwa ya mateso. Hakuna mtu yeyote anayeweza kufurahia, maisha na hofu ya kwamba anaweza kuwa muathiriwa mwigine wa moja ya magonjwa haya hatari. Lakini wafuasi wa kweli wa dini ya kweli hawana hofu. Wanajua kwamba maisha katika ulimwengu huu ni ya muda na hatimaye watauacha ulimwengu huu kwenda ulimwengu mwingine wa kudumu. Hivyo, kwa madhumuni maalumu na maisha yenye mafanikio, dini ni muhimu. Hata hivyo, chaguo la dini isiyo sahihi, linaweza kuharibu maisha ya hapa na ya kesho Akhera. Mwisho tunaweza kuthibitisha kwamba dini ni muhimu, kwa kujichambua sisi wenyewe. Tuna silika za kiasili za kujijua sisi wenyewe. Tunaweza kuhisi huu msisitizo katika nyakati ambapo tuko huru kutokana na shinikizo za nje. Kwa mfano, imewahi kuonekana katika ajali nyingi mbaya za magari, kwamba mtu aliyezimia akipata fahamu, mara moja anauliza maswali mengi kwa watu walio mzunguuka. Huuliza, niko wapi? Nimekujaje hapa? Nani aliyenileta hapa? Ni kitu gani kimenitokea kwangu? Je, niko salama? Maswali yote haya kwa uwazi huonyesha kwanza mtu anayo silika 3 4

ya asili ya kujua ni wapi alikotoka na hatimaye ni wapi atakwenda. Dini ya kweli inayo majibu sahihi ya maswali haya. Kama mtu yeyote anapuuza maswali haya, basi ina maana kwamba hana akili timamu. Hivyo ndivyo Amir-i-Muuminina Ali (as.) alivyosema katika moja ya khotuba zake: "Watu wanalala, wataamka baada ya vifo vyao". Dini ya kweli hutuambia mambo mengi ambayo hatuwezi kamwe kuyajua kutoka chanzo kingine chochote. Kwa mfano, Uislamu hutupa majibu sahihi kwa maswali magumu yafuatayo: Nani ameumba ulimwengu? Nani ameumba aina za mamilioni ya jamii zinazoishi? Nani amewafanya binadamu kuwa bora kushinda viumbe vyote? Kwa nini ametuumba? Hakuna mtu awazae kujua vipi ulimwengu na kila kitu kilicho kuwemo ndani yake vimekuja kuwepo. Wanachotuambia wanasayansi kuhusu asili ya ulimwengu na viumbe wanaoishi ni kazi yao ya kukisia. Hii ndio sababu kuna hitilafu nyingi za nadharia katika sayansi pamoja na maelezo yenye kuhitilafiana mno. Kwa mfano, nadharia ya kishindo kikubwa (Big-Bang Theory), nadharia ya hali ya kutulia (kwa ardhi) na nadharia ya mabadiliko (evolution) hutoa hadithi tofauti kuhusu kuwepo kwa ulimwengu. Mpaka sasa, hakuna mwanasayansi awezae kusema kwa yakini kwamba anajua kwa hakika kuhusu asili ya ulimwengu na uhai. Lakini Quran Tukufu hutuambia kwa uwazi kuhusu asili ya ulimwengu: "Ameumba mbingu na ardhi kwa haki. Hufunika usiku juu ya mchana, na hufunika mchana juu ya usiku. Na amefanya jua na mwezi vitumike. Kila kimoja kinakwenda kwa kipindi kilicho wekewa. Jueni mtanabahi! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe! (39:5)" KIINI CHA FIKRA Lengo la msingi la somo hili ni kukupa silaha kupigana kwa akili na propoganda za bandia za Magharibi ambazo wamekuwa wakizifanya kwa ujanja dhidi ya dini. Wanafunzi lazima watambue kwamba dini ni muhimu katika maisha. 5 6

SURA YA PILI JINSI YA KUTAMBUA DINI YA KWELI "Basi uelekeze uso wako sawasawa kwenye dini, (hilo) ndilo(jambo ambalo) Allah alilowaumbia watu..." (30:30) Je, sio mantiki kuipima imani yako? Kuna maelfu ya dini katika ulimwengu. Dini kubwa ambazo zina idadi ya wafuasi ni, ya Kiyahudi, Ukristo, Ukonfyushasi (falsafa na maadili ya china), Uzoroastrian, Uhindu, Ubudha, Ujaini, Utao, Ushinto na Usikh. Vipi tutaitambua dini ya kweli wakati wafuasi wa dini zote wanadai kwamba ya kwao ndio dini ya kweli? Hii sio kazi ngumu. Mtu anaweza kutafiti dini ya kweli kutoka kwenye dini nyingine, kama ni mnyofu na mkweli katika utafiti wake na uchunguzi. Kwa mfano, kama utasoma na kuchunguza dini zote kubwa za ulimwengu, matokeo ya utafiti wako usio na chuki na upendeleo yatakuwa kama ifuatavyo: (a) Uislamu ndio dini pekee ambayo hukubaliana na maumbile ya mwanadamu. Kwa mfano, wahandisi siku zote hujaribu kuangalia mambo ya mbele yanayo husiana na mwanafunzi katika maeneo kama ya usalama na mazingira wakati wanafanya usanifu wa jengo la shule. Halikadhalika, sheria za Uislamu zimefanywa na Allah (SWT) kwa mujibu wa muundo ambao kwamba amemuumba mwanadamu na mazingira ambayo kwayo yamepangwa kuishi. "Ambae ameumba mbingu saba kwa matabaka. Huoni tofauti yoyote katika uumbaji wa Mwingi wa Rehema. Hebu rudisha nadhari! Unaona kosa lolote? (67:3) "Tena rudisha nadhari mara mbili, nadhari yako itakurejea mwenyewe hali ya kuwa imehizika nayo imechoka" (67:4). Mpango kamili na wenye kuafikiana katika anga kubwa mno, inayoonekana au isiyoonekana kwetu, hufuatia sheria sahihi za mwendo (laws of motion), huthibitisha umoja kamili na utawala wa hali ya juu sana wa Muumba Mmoja. Sheria nyingi za aina za maumbile zimeunganishwa kwa ukaribu na kila moja katika mwendelezo wa ufanyaji kazi za ulimwengu. Hakuna mwanya, hakuna kupishana wala kukatika (kwa mfuatano). Tukio hili ni moja ya ishara za umoja wa Muumba. Hivyo, sheria za dini na sheria za ulimwengu zina asili ile ile na kwa hiyo suala la kupingana halitokei. (c) Uislamu ni dini pekee ambayo hutoa msisitizo mkali juu ya tafakari, kuhoji na kufikiri kwa akili, Uislamu huwataka wafuasi wake kuelewa 7 8

Quran Tukufu na kisha kuonyesha utekelezaji wake kimatendo katika maisha. Quran imekariri mara kwa mara kuwashauri Waislamu kutafakari, kuakisi na kuelewa ujumbe wake. Quran imeweka wazi kabisa kwamba inazungumza kwa wale watu tu ambao wana akili. "...Namna hivi tunazieleza ishara kwawatuwanaojua" (7:32) "...Namnahivi tunazipambanua Aya zetukwa watu wenye akili."(30:28) "... Hakika katika hayo bila shaka zipo ishara kwa watu wanaofikiri" (39:42) Quran iliteremshwa katika lugha ya kiarabu ambayo ndio iliyokuwa lugha ya Waarabu. "Hakika sisi tumeiteremsha Qurani kwa Kiarabu ilimpate kuzingatia." (12:2) Punde tu baada ya kuingizwa kwa Uislamu katika nchi zisizo za Kiarabu, watu wa nchi ile waliitafsiri (Quran) katika lugha yao wenyewe. Watu wengine walijifundisha Kiarabu kwa sababu tu ya kuielewa Quran. Wakristo na Wayahudi ambao waliishi katika nchi zinazo zungumza kiingereza vile vile walihitaji tafsiri ya Biblia. Lakini tafsiri ya kwanza ya Biblia kwa lugha ya kiingereza ilitokea katika miaka ya 1380. Martin Luther alitafsiri biblia kwa lugha ya kijerumani mwaka 1534. Kwa nini biblia ilichelewa hivyo kutafsiriwa katika lugha za watu? Kwa sababu wainjilisti kamwe hawakuruhusu tafsiri zipangwe na kuwakatisha tamaa watu kuisoma katika lugha zao Halikadhalika, Wahindu, kundi maalumu la watu wajulikanao kama Wabrahmin waliruhusiwa kusoma vitabu vya dini. (a) (b) Uislamu ni dini pekee ambayo hukataa kabisa kufuata kimbumbumbu na hoja zisizo na mantiki. Hii ndio dalili ya wazi ya dini ya kweli. Quran imewalaumu wale watu ambao hufuata nyayo za wazee wao bila ujuzi. Uislamu ndio dini pekee ambayo kamwe hailazimishi imani yake juu ya mtu yeyote kuikubali au kumsihi aikubali. Uislamu unahitaji ujuzi kamili wa kiini cha fikra kabla mtu hajaikubali. "Hakuna kulazimishana katikadini." (2:256) Hakuna haja ya kutumia aina yoyote ya nguvu au shinikizo juu ya mtu ili kuukubali Uislamu. Mantiki ya mafundisho ya Uislamu huvutia watu sawasawa kama sumaku inavyovutia chuma kwa asili yake ya maumbile. Punde tu tutawaonyesha Ishara Zetu katika upeo wa mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka iwabainikie kwamba haya ni kweli. Je! Haikutoshi kwamba Mola wako Yeye ni Shahidi wa kila kitu? Hivyo, tunawajua watu wengine katika ulimwengu huu ambao waligundua dini ya kweli kwa juhudi zao za kweli na unyofu. Mtu mmoja mkubwa kama huyo alikuwa Salman Farsi. Salman el-farsi alizaliwa Iran. Jamaa ya familia yake yote na raia wenzake, amma walikuwa wakristo au wazoroastria. Salman vile vile alifundishwa na wazazi wake misingi ya imani na kanuni za uzoroastria. Lakini Salman hakukinaishwa na dini hii kwa sababu ya mafunzo yake yasiyokuwa ya kawaida na imani za uwongo. Historia hutuambia kwamba Salman alikubali na kukataa dini moja baada ya nyingine lakini akawa hapendezewi mpaka alipomkuta Mtukufu Mtume na akaukubali Uislamu. Salman alifurahi mno na kukinai baada ya kumkuta Mtukufu Mtume na 9 10

kugundua dini ya kweli. Halikadhalika, Wahindu, wakristo, Mayahudi na wafuasi wa dini nyingine walikubali Uislanu baada ya utafiti wao wa kweli na mnyofu. Tuna orodha ndefu ya watu kama hao waliosilimu. Hebu ngoja nikupeni mfano mmoja wa wakati wetu. Dr, Maurice Bucaille bingwa maarufu wa upasuaji wa Kifaransa wa wakati wetu, ni mmoja wao wa wale ambao walikubali Uislamu baada ya utafiti wake wa kina katika Quran Tukufu. Dr.Bucille alikuwa Mkristo kwa kuzaliwa. Aliandika kitabu (kiitwacho) Biblia, Quran na Sayansi ambacho kwacho alithibitisha kisayansi kwamba Uislamu ndio dini pekee ya kweli ulimwenguni. Wasomi wengine wengi walikataa dini zao za uwongo, lakini hawakupata ukweli kamili. Mtu mmoja kama huyo mwenye kipaji alikuwa ni Bertrand Russell. Anasifiwa na wanahistoria miongoni mwa mafilosofa wakubwa na mabingwa wa hisabati wa miaka ya 1900. Vile vile akiitwa mwana mantiki (bingwa katika mantiki) muhimu mno tangu mwanafilosofia wazamani wa kigiriki aitwaye Aristotle. Russell alizaliwa Mkristo, lakini alikataa imani yake katika ukristo. Aliandika kitabu, (Kiitwacho) Kwa nini mimi sio Mkristo (Why I am not a Christian 1927) ambacho ndani yake amefichua imani yake ya mwanzo isiyo ya kimantiki. Russell ni mfano wa kipaji kilichoharibika. Amegundua uwongo lakini hakuweza kugundua ukweli. MSINGI WA KANUNI ZA HUKUMU dhana na mafundisho ya dini tofauti, basi tunaweza kuchagua dini ya kweli na kukataa dini ya uwongo. Zifuatazo ni kanuni tatu za msingi za kuchunguza dini kwa ajili ya kutambua ukweli na asili ya uwongo wa dini: 1. Kupatana na sheria za kimaumbile. 2. Umoja pamoja na sheria za kibaolojia (elimu ya viumbe). 3. Uzito katika yaliyomo. Kupatana na Kanuni za kimaumbili Dini ya kweli kamwe haipingani na sheria za maumbile. Ni wazi kabisa, kwa sababu kama dini inatoka kwa Mungu, ambaye ni Muumba pekee wa ulimwengu, basi hakuwezi kuwa na migongano kati ya sheria za ulimwengu na mafundisho ya dini ile, kwa vile vyote vina asili moja. Mgongano kwa hakika utatokea kati ya kanuni za dini na sheria za kimaumbile zinazo fanya kazi katika ulimwengu, kama dini haitoki kwa Bwana wa ulimwengu, ambaye ametengeneza sheria za ulimwengu. Leo muundo wa msingi wa dini zote, isipokuwa Uislamu, umevunjwa vunjwa kwa mashambulizi ya watafiti wa kisayansi. Ukweli wa maumbile ulio gunduliwa na wanasayansi umeziweka uchi na kufichua uwongo wa kubuni wa dini. Dini za kishirikina zinazo hubiri kuabudiwa kwa jua, mwezi, nyota, wanyama na maelfu mengine ya miungu kama hiyo, haziwezi kuishi sasa. Siyo vigumu kuyakinisha utambulisho wa dini ya kweli na kuitofautisha na dini ya uwongo. Kama tunapima kwa haki msingi wa Jumba la ushirikina limeporomoka kabisa baada ya ugunduzi wa kweli wa kisayansi. Katika mwaka wa 1969, wanaanga wa Apollo 11 na Apollo 12 walitua kwenye kichwa cha mungu (mwezi) wa washirikina. Hiyo ilikuwa siku ya aibu kubwa kwa waabudu mwezi wote, wakati mmoja wa mungu wao alipokuwa chini ya miguu ya mtu. Sayansi imewavunjia heshima karibu miungu wote wa washirikina kwa kufichua ukweli wao. Mtangulizi wa matukio ya ajabu ya sayansi ya kisasa ni Mtume Muhammad (s.a..w) ambaye aliondoa vikwazo vya anga za juu kwa ajili ya kutua mwezini miaka 1400 iliyopita. Historia hutuambia jinsi Mtukufu 11 12

Mtume (s.a.w) alivyovunja muundo wote wa miungu ya kimfano, ambayo ilikuwa ikiabudiwa na watu. Uchunguzi wa kweli unaweza kuthibitisha kwamba dini zote, isipokuwa Uislamu, zina mgongano wa moja kwa moja na ukweli ulio thibitishwa wa kisayansi. Dr. Maurice Bucaille ametambulisha makosa mbali mbali katika Biblia. Vile vile ameridhika kwamba hakuna kosa hata moja la kisayansi katika Quran Tukufu. Hivyo uchambuzi wa kisayansi kwa dini sio wa chuki au wa upendeleo na ni njia ya kuaminika ya kutambua dini ya kweli na ya uwongo. Muafaka wa pamoja na sheria za kibaolojia. Sifa nyingine muhimu ya dhahiri ya dini ya kweli ni kwamba kanuni za msingi huonyesha umoja kamili pamoja na maisha ya sheria za kibaolojia. wake kujizoesha kujiwekea nidhamu na kujiepusha na vitu vilivyo katazwa hata kama vinawavutia. Kama kweli dini inatoka kwa Mungu, ambaye ni muumba wa watu, basi mafundisho ya kidini lazima yapatane na mahitaji ya kimaumbile ya mwili wa mwanadamu. Kanuni hii vile vile inabatilisha dini zote isipokuwa Uislamu. Uislamu ndio dini pekee ambayo sio tu inaruhusa bali pia inafundisha wafuasi wake kuchukuwa faida za juu kabisa kutoka kwenye maumbile. Halali na Haramu ya Uislamu haituzui sisi kufurahia kitu chochote, bali kurekebisha silka zetu za kimaumbile ili kuchukuwa faida kamili baraka za Allah (s.w.t) zisizo na idadi. Quran Tukufu imeweka wazi kabisa katika aya ifuatayo: "Sema: Ni nani aliyeharamisha Pambo la Allah alilowatolea waja wake, na vilivyo vizuri katika riziki. Sema, hivyo ni kwa walio amini katika uhai wa dunia, na Siku ya Kiyama vitakuwa vyao tu..." (7:32) Kusema kweli, Quran imewalaani wale watu ambao bila sababu yoyote wanajiepusha na vitu vya halali na kufanya maisha yao kuwa yenye taabu. Hata hivyo, kwa hakika Uislamu huhitaji kutoka kwa wafuasi Dini nyingine huzuia kabisa mahitaji sahihi ya mwili na jamii au kuyaachilia huru kabisa kuchosa nguvu zao za thamani katika wingi wa ukubwa wa Maumbile. Mifano michache ya aina hii inatolewa hapa kuonyesha tofauti iliyowazi kati ya dini ya Mungu na sheria zilizo tungwa na watu. USEJA: Useja maana yake kujizuiya kutokana na uhalali wa mahusiano ya kijinsia kwa ajili ya sababau za kidini, yaani, hakuna kuoa (au kuolewa) kwa ajili ya kutafuta ridhaa ya Mungu. Watawa wa Kikristo na wa Kibudha huuona useja kama maadili ya kidini. Kwa sheria, Mapadre wote wa Roman Catholic lazima wawe waseja, 13 14

yaani lazima wabakie bila kuoa au kuolewa kwa maisha yao yote. Katika makanisa ya ulaya ya mashariki, wanaume waliooa wanaweza kuwa Mapadre, lakini Askofu lazima atekeleze useja. Mtu anaweza kuuliza swali sahihi: kwa nini Papa, Maaskofu, watawa wanawake, ambao pia wana matamanio ya kimaumbile ya kijinsia kama binadamu wengine, hawaruhusiwi na dini kuoa au kuolewa? Kama ndoa inamchukiza Mungu, basi kwa nini ameumba mfumo wote wa uzazi wa jinsia? Kwa nini viumbe wote wanaoishi ukijumuisha na wanadamu wameumbwa na Mungu wakiwa na viungo maalumu vya kufanyia tendo la kijinsia? Kama Mungu haidhinishi mahusiano ya kijinsia kwa wanaume na wanawake, basi kwa nini msingi wa mwendo ambao kwao Mungu ameumba wanadamu zaidi, na zaidi hutegemea kabisa juu ya uhusiano wa kijinsia. Mifumo ya uzazi ya wanaume na wanawake katika wanadamu na aina nyingine za jamii zinazoishi imesaniwa maalumu na Mungu kwa ajili ya kuzaa, kulisha, na kulea watoto wao wanaohusika. Kama mantiki ya useja ingelikuwa ni mfano bora wa kufuatwa na wanadamu kama udhihirisho wao wa upendo kwa Mungu, basi ungekomesha kabisa mpango wa uumbaji. Kama wafuasi wote wa Ukiristo watafuata mfumo wa maisha ya Papa, ambaye lazima achukuliwe na wafuasi wake kama mtu bora zaidi, basi ulimwengu wote wa kikristo ungelitoweka katika kizazi kimoja. Vile vile, wakristo wote wanawatambua Hadhrat Ibrahim (a.s), Hadhrat Musa (a.s) na Mitume wengi wengine kama wajumbe wa Mungu. Mitume wote hawa walikuwa wanao wake na watoto. Hivyo, kitendo hiki cha kidini ya Ukristo na Ubudha huleta mgongano wa moja kwa moja na mpango wa Mungu na mpango wa utendaji kazi wake wa kuendelea kuumba. Hii ni kinyume na dini ya Mungu. Uislamu hauruhusu tu taasisi ya ndoa, bali huweka msisitizo maalumu juu yake. Quran Tukufu inasema: "Oeni wanawake wa chaguo lenu," (4:3) Mtukufu Mtume (s.a.w) alionyesha kutoridhishwa kwa watu kubakia bila kuoa au kuchelewesha ndoa bila sababu. Mtume (s.a.w) alisema: "Ndoa ni sunnat yangu, yeyote yule anayejiepusha na Sunnat yangu sio miongoni mwangu". Kuna hadithi nyingi za Mtukufu Mtume (s.a.w) na Maimamu kuhusiana na suala hili. Uchinjaji wa Wanyama: Halikadhalika, Wahindu, Wajaini, na Wabudha hawali nyama na wanachukulia uchinjaji wa wanyama kwa ajili ya nyama zao kama ukatili na unyama. Tunaweza kuchambua kimantiki iwapo kuchinja wanyama ni ukatili au la. Tunajua kwamba kuna wanyama wengi ambao zaidi sana hula nyama. Wanyama kama hao wana tabia ya kuzaliwa na miili iliyofanywa kwa ajili ya mawindo juu ya wanyama wanaokula majani. Mungu amewapa wanyama hawa meno makali mno na yenye kupasua, misuli na taya yenye nguvu na mahitaji mengine muhimu ya kuwindia. Kama kuwinda, kuchinja na ulaji wa nyama ni ukatili na kitendo cha ushenzi, basi kwa nini Mungu Mwenye upole mno na Mwenye huruma amewaumba wanyama walao nyama ambao hawawezi kula chochote isipokuwa nyama. Mamilioni ya mbuzi, kondoo na ngombe wanachinjwa kila siku kwa madhumuni ya kula. Lakini kamwe hakujakuwa na upungufu wa wanyama hawa halali. Hivyo, kula nyama hakuwezi kuchukuliwa kama kitendo cha kishenzi. Hata hivyo, Uislamu husisitiza ulaji wa wastani wa nyama za wanyama na kwa kushauri kuzingatia kanuni zihusianazo na ustawi wa maisha ya jamii zote zenye uhai. Mwisho, dini ya kweli ya Mungu inaweza kwa urahisi kutambuliwa 15 16

kwa uwezo wake wa kuongoza watu katika kila fani ya maisha yake. Vita kati ya Waislamu na wafuasi wa dini zote nyingine ni juu ya suala la uzito wa mafundisho ya Ki-Islamu. Wanahoji kwamba dini ni kitu cha binafsi na haipaswi kujitokeza kuingiliana na mambo ya kijamii na kazi ya kiofisini. Mara nyingi Mwislamu wa vitendo hukabiliana na maneno kama haya ya uchokozi; usilete dini yako katika ofisi, tafadhali iweke msikitini au nyumbani kwako. Watu hawa hawajui kitu kimoja cha msingi kuhusu Uislamu na hicho ni uzito wa asili ya Uislamu. Kinyume na dini nyingine, Uislamu huchukuwa nafasi ya kila kipengele cha maisha ya mwanadamu na kwa hiyo huhitaji wafuasi wake kutekeleza mafundisho yake katika kila fani ya maisha yao. Hivyo uchambuzi wa uangalifu wa dini unaweza kumsaidia mtu mwenye fikira za kimantiki kutofautisha kati ya dini ya kweli na ya uwongo. KIINI CHA FIKRA: Lengo la somo hili ni kukuwezesha wewe kuitambua imani yako katika njia ya kiakili. Kufuata kimbumbumbu na kurithi dini ya baba bila ujuzi wa kweli wa imani hakuna maana katika Uislamu. Kigezo cha kwanza cha imani kilichowekwa na Quran Tukufu ni: Kuthibitisha na kwa akili kutambua imani za msingi zilizomo. Kutekeleza sharti hili la msingi kunahitajika juhudi za ukweli ili kupata ujuzi wenye manufaa na kufanya baadhi ya utafiti. Hii ndiyo sababu, kutafuta elimu ni wajibu kwa kila Mwiislamu mwanaume na mwanamke. 17 18

SURA YA TATU FAIDA ZA DINI YA KWELI Faida za dini ya kweli ni nyingi. Mtu ambaye hana dini au amechagua dini isiyo sahihi ni mwenye hasara kubwa. Hakuna kitakachofidia hasara hiyo. Tunaona watu wengi wasioamini wametuzunguuka ambao wana utajiri, uwezo na mali. Watu wengi wanafikiri kwamba ni watu wenye bahati sana katika ulimwengu. Lakini walikuwepo watu wengi kama wao zamani ambao sasa wamekufa. Kila mtu anajua bila shaka yoyote kwamba wameacha utajiri wao wote, uwezo na heshima. Vitu ambavyo walikuwa wakifurahia wakati wa muda wao na maisha. Hivyo kifo ni mwisho wa starehe za kiulimwengu na vitu vya kidunia. Quran Tukufu imeonyesha ukweli huu katika aya zifuatazo: "Mabustani mangapi, na chemchem ngapiwaliziacha Na mimea na vyeo vitukufu! Na neema walizokuwa wakijistareheshea! Ndio hivyo! Na tu kawarithisha haya watu wengine. Si mbingu wala ardhi hazikuwalilia,wala hawakupewa muhula.(44:25-29) "Enyi mlioamini! Nikuonyesheni biashara itakayokuwaokoa na adhabu iliyo chungu?muaminini Allah na Mtume Wake, na piganeni jihadi katika njia ya Allah kwa mali zenu na nafsi zenu. Haya ni bora kwenu, ikiwa ninyi mnajua. Atakusameheni dhambi zenu, na atakutieni katika bustani zipitiwazo na mito kati yake, na maskani nzuri nzuri katika bustani za milele. Huku ndio kufuzu kukubwa". (61:10-12) Quran Tukufu imerudia rudia kutuonya kwamba kila kitu ambacho tunamiliki katika ulimwengu huu tutakiacha. Watu wenye akili ni wale ambao hununua neema ambayo inaweza kubakia pamoja nao hata baada ya kufa. Mtu mwenye ujuzi, hata kama siyo Mwislamu anaweza kuitambua. Jean-Jacques Rousseau (1712-1778) filosofa mkubwa wa Kifaransa na mwandishi muhimu sana wa zama za mantiki, alitoa baadhi ya maneno ya hekima, wakati alipoandika kwa mwanae kuhusu ukweli wa maisha ya ulimwengu huu: "Najua kwamba mwisho wa safari yangu ni kufa; basi, yapasa nitengeneze kiambatanisho kwa ajili yangu katika ulimwengu huu? Katika ulimwengu ambako vitu vyote vinabadilika na kupita, mimi mwenyewe ni punde tu nitatoweka. Viambatanisho vina faida gani kwangu? Emile, mwanangu, kama nikikosa, nini kitabakia kwa ajili yangu? Hata hivyo lazima nijitayarishe mweyenwe kwa ajili ya hatima isiyovumilika, kwa sababu hakuna mtu awezaye kunihakikishia kwamba nitakufa kabla yako. Hivyo kama unapenda kuishi kwa raha na kwa akili, tegemeza moyo wako kwenye vitu vizuri visivyotoweka; jaribu kuweka mpaka wa matamanio yako na ichukulie kazi katika heshima ya juu kuliko mengine yote. Tafuta vile vitu tu ambavyo havivunji sheria ya maadili, na jizoweshe kupoteza vitu bila huzuni. Usikubali chochote, mpaka vinginevyo dhamira yako ikuruhusu. Kama utafanya yote haya, hakika utakuwa na furaha". Rousseau hakuwa Muislamu lakini alitiwa msukumo wa moyo na 19 20

filosofia ya Ki-Islamu. Mtu wa kufikiri hivi anaweza kuwaongoza watu wake kuleta mapinduzi. Filosofia ya Rousseau iliwavutia watu wa wakati wake ambayo ilisababisha mapinduzi ya Ufaransa. Sasa ngoja tuonyeshe baadhi ya faida za kutambua dini ya kweli. Dini hutoa utambuzi wa kujitukuza. Kutokana na mtazamo wa Ki-Islamu, binadamu wote huzaliwa kama Waislamu, ni wazazi wao ambao huwafanya Wahindu, Wakristo, Mayahudi au Wapagani. Kuna aina zaidi ya millioni 2 za viumbe wanaoishi na katika hao, watu ndio viumbe wa juu sana. Jukumu la kwanza na la muhimu zaidi la mtu ni kujua cheo chake na hadhi yake katika ulimwengu na uumbaji. Ni hapo tena, anaweza kudumisha nafasi yake na anaweza kuendelea zaidi katika ubadilikaji wake wa kukua na maendeleo. Quran na hadithi ndiyo vyanzo pekee vya kuaminika vya kujua asili ya mwanadamu. Ni muhimu kuona kwamba Quran imetoa msisitizo maalum kuonyesha nafasi sahihi ya mtu kwa ajili ya kujitambua kwake. Tamko la Unaibu wa Mungu. Allah (s.w.t) alimteuwa mtu kama khalifa wake katika ardhi. Quran inasema: "Naye ndiye aliyekufanyeni makhalifa wa duniani, na amewanyanyua baadhi yenu juu ya wengine daraja kubwa kubwa, ili akujaribuni kwa hayo aliyokupeni. Hakika Mola Mlezi wako ni mwepesi wa kuadhibu, na hakika Yeye ni Mwenye Kusamehe, Mwenye kurehemu.(6:165) Sherehe ya kutawazwa kwa mtu. Allah (s.w.t) alitayarisha sherehe maalum ya kutawazwa kwa mtu ambayo kwayo viumbe wote waliopo wa wakati huo walitakiwa kuhudhuria. Washiriki ambao walikuwa sana ni malaika, waliamrishwa na Allah (s.w.t), kuinama chini mbele ya Adam (a.s) muwakilisha wa mfano wa mwanadamu. Quran inasema: "Na Mola wako alipowaambia malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura. Basi nitakapomkamilisha na nikampulizia roho Yangu, basi mumuangukie kumsujudia. Basi malaika wote pamoja walimsujudia. Isipokuwa Iblisi. Yeyealikataa kuwa pamojana waliosujudu. (15:28-31) Malaika wote na malaika mkuu (Jibril) kwa heshima walifuata amri ya Allah (s.w.t) na wakasujudu, isipokuwa Shetani (jinni), ambaye kwa fedheha alitolewa katika pepo kwa kutokukubaliana kwake na amri ya Mungu. Quran iliendelea kueleza hadhi ya mtu na wepesi na neema ambazo kwamba amepewa na Mola wa walimwengu. 21 22

"Kwa hakika tumewatukuza wanaadamu, na tumewapa vya kupanda nchi kavu na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa kuliko wengi miongoni mwa tuliowaumba. (17:70) "Kwani hamuoni kwamba Allah amevifanya vikutumikieni vilivyomo mbinguni na kwenye ardhi, na akakujalizieni neema zake, za dhahiri na za siri?." (31:20) Yeye ndiye aliye idhalilisha ardhi kwa faida yenu, basi tembeeni katika pande zake na kuleni katika riziki zake. Na kwake Yeye(pekee) ndio marejeo. [Qur'an 67:15] Quran hutuambia kwamba mtu ana cheo kikubwa mno miongoni mwa viumbe wote wa Allah (s.w.t). "Na tukakufadhilisheni juu ya walimwengu wote". Mtu alipewa uwezo wa kutamaliki ulimwengu. Kila kitu kilichomo ulimwenguni ni kwa ajili yake. Ilichosema Quran miaka 1400 iliyopita kinathibitishwa sasa. Tunaona kwamba mtu anachukuwa nafasi ya juu katika viumbe wa Allah (s.w.t). Anautawala ulimwengu. Wanyama, mimea, milima na hata mwezi na nyota viko kamili chini ya matumizi yake. Hii ni heshima kubwa. Lakini wanasayansi wa leo huwatabakisha watu miongoni mwa wanyama. Wanabiolojia husema kwamba wanadamu ni wa tabaka la wanyama waitwawo mamalia (yaani wanyonyeshao) ambao hujumuisha mbwa, paka, punda na wanyama wote wengine. Kwa hakika, wakati mtu anajifikiria mwenyewe kuwa kizazi cha punda, basi mtu asishangae kama anakuwa na tabia kama za wanyama. Haya maoni ya kujitweza yalijitokeza kwa sababu hawana dini ambayo inaweza kusukuma nyoyo zao kujua hadhi yao halisi. Matokea ya kutweza hadhi ya mtu ni kwamba baada ya kupanda kwenye kilele cha mwezi, mtu bado yuko chini kama alivyokuwa katika zama zake za ujinga. Hivyo jukumu la kwanza na muhimu sana la kila mwanadamu ni kujua hadhi yake na nafasi yake katika viumbe wa Allah (s.w.t). Baada ya kujitambua mwenyewe, atakuwa na uwezo wa kutambua madhumuni ya kuumbwa kwake na sababu ya ukuu wake na neema kubwa za Mungu. Bila kutambuwa ukweli wa mtu na hadhi yake halisi, juhudi zote za mwanadamu na bidii, ziwe za kisayansi au za kiroho, zitakuwa hazina maana na za hali ya chini mno. Mtukufu Imam Hadhrat Ali (a.s) alieleza ukweli huu katika njia nyingi tofauti: "Yeyote yule ajitambuaye mwenyewe amemtambua Mola wake". "Nashangaa mtu ambaye hutaka alichokipoteza ambapo amekipoteza mwenyewe na hakitafuti". "Nukta ya mwisho ya elimu ni kwa mtu kufikia kujitambua". Hivyo dini ndio chanzo pekee cha kuaminika cha kujitambua, ambayo ndiyo mwanzo wa masuala yote ambayo yanamhusu mtu. 23 24

Dini huleta amani na utulivu. Wanasayansi wengi hawaamini Mungu na husema kwamba hakuna aliyeumba wanadamu au chochote ambacho tunakijua katika ulimwengu. Matokeo ya dhana hii potofu itakuwa kwamba ulimwengu na vyote vilivyomo ndani yake havina maana. Kusema kweli, hivi ndivyo wanasayansi wa kisasa wanavyoamini na hatimaye hutaraji kuhubiri: Hakuna Mungu, ambapo kwa usahihi maana yake- hakuna dinihakuna madhumuni- hakuna lengo- hakuna mwisho wa safari. Kwa ujumla wanakataa kila kitu. Mtu ambaye huamini katika dini ya kweli, ambayo kwa usahihi hueleza kuhusu maisha baada ya kifo, atapata utambuzi sahihi wa maisha yake. Hatimaye itaiangaza akili kugundua madhumuni halisi ya maisha. Hivyo, matokeo ya kutarajia (yasio epukika) ya imani hii yatakuwa:; taarifa iliyoandikwa katika Jarida la Times International Magazine: watu 28,000 katika America, 25,000 katika Uswisi na idadi kama hiyo hiyo ya watu katika Ujapani hujiua wenyewe kila mwaka. Kiwango cha wanaojiua katika Amerika kinaongezeka taratibu kuanzia mwisho wa Miaka ya 1950. Wengi wa watu wanaojiua wenyewe ni wazee, vijana wakubwa na vijana wa makamo, 75% yao ni wanaume. Katika mwaka 1980, kitabu kilichouzika vizuri sana katika Japani kilikuwa "Jinsi ya Kujiua Mwenyewe". Katika kitabu hiki, mwandishi amesanifu miundo tofauti ya mtu kujiua mwenyewe. Mauzo makubwa ya kitabu hiki kwa usahihi huonyesha kwamba idadi kubwa ya watu katika Japani wameelekea kujiua wenyewe. Uwezekano ni kwamba wangeweza kujiua wenyewe baadae. Atamaliza nguvu zake zote kwa matayarisho hayo. Atatoa mhanga kitu chochote na kila kitu ikihitajika hivyo kwa vile ana ujuzi wa malipo kamili. Kamwe hatafanya makosa katika kutambua asili halisi ya vitu. Kamwe hatajisikia kushindwa kama anapoteza kitu chochote cha kiulimwengu. Mtu mwenye akili kama huyo ataishi kwa furaha na ataruhusu wengine kuishi kwa amani. Leo, ulimwengu ulioendelea mno wa kitekinilojia una kila kitu isipokuwa amani. Tunajua vizuri sana kwamba hatuwezi kufurahia kitu chochote kama hatuna amani ya akili. Wale ambao hawaamini katika maisha baada ya kifo, wauana wenyewe kwa wenyewe ili kupata kila kitu. Hii hutokea katika ulimwengu huu katika madaraja yote. Hivyo, faida ya dini ya kweli ni kwamba huleta amani na utulivu katika ulimwengu huu halikadhalika na kesho akhera. Dini huleta hali ya usalama. Kwa dhahiri huonyesha kwamba watu wa ulaya magharibi, ambao hawaamini katika dini, ni watu waliotosheka zaidi. Lakini kwa mujibu wa Kwa nini watu wajiuwe wenyewe? Swali hujitokeza, kwa nini watu wanaoishi katika nchi zenye neema na utajiri wanajiua wenyewe? Nchi hizi zina matatizo kiasi kidogo ya kiuchumi, kijamii, na kisiasa ukilinganisha na nchi zinazoitwa ulimwengu wa tatu kama India, Pakistani na Bangladeshi. Taarifa inasema kwamba sababu kubwa ya kawaida ya watu kujiua wenyewe ni hali ya ukosefu wa usalama. Lakini tunajua kwamba katika nchi hizi zilizoendelea, watu walio wengi wana hali nzuri, na vile vile serekali zina taratibu mbali mbali za usalama na mawakala kwa ajili ya kuangalia kwa ujumla ustawi wa watu. 25 26

Basi, kwa nini watu hawa wapatwe na hisia za kutokuwa na usalama kiasi kwamba hatimaye iwasababishie kujiua wenyewe. Mwanasaikolojia mmoja alitoa maelezo ya kupendeza. Anasema kwamba sisi wanadamu wote kwa asili tumezoea aina maalum ya usalama. Ukosefu wa imani katika mungu na maisha yasiyo na malengo hufyatua hali ya kutokuwa na usalama ambayo huzaa mfadhaiko wa akili na hatimaye husababishia mtu kujiua mwenyewe ili kuondokana na hofu hiyo isiyojulikana. Hii ndio sababu kwamba maelfu ya watu hujiua wenyewe na kuua kwa ajili ya hisia zao za ndani za kuvunjika moyo na hisia ya kutokuwa na usalama. nipo karibu. Naitikia maombi ya mwombaji anapo niomba. Basi na waniitikie Mimi, na waniamini Mimi, ili wapate kuongoka". (2:186) Dini hutoa madhumuni katika maisha. Hivyo dini ya kweli ndio suluhisho pekee la mfadhaiko wa akili na kutokuwa na usalama. Quran inathibitisha kwamba amani halisi ya akili inaweza tu kupatikana kwa ukumbusho wa Allah (s.w.t) wa kisomi. "Wale walioamini na zikatua nyoyo zao kwa kumkumbuka Allah. Hakika kwa kumkumbuka Allah ndio nyoyo hutua!"13:28. Mtoto hujisikia hali ya usalama kamili katika wakati akijiona mwenyewe yuko karibu ya mama yake. Ni kwa sababu ya imani kubwa ya mtoto kwamba mama yake atamuokoa kutokana na balaa yoyote. Mtoto asiye na hatia hajui kwamba pamoja na mama yake kumpenda sana, lakini hawezi kumuokoa katika matatizo yote. Ni Mungu pekee ambaye anatupenda Sisi (kwani yeye ndiye aliyetengeneza upendo kwa ajili ya mtoto katika moyo wa mama), na vile vile ni Mwenye nguvu zote. "Na waja wangu watakapo kuuliza habari zangu, waambie kuwa Mimi Kama tujuavyo kwamba idadi kubwa ya wanasayansi hawaamini Mungu na kumchukulia mtu kama kizazi cha kibahati ya maumbile. Hatimaye kwao wao, mtu hana madhumuni katika maisha isipokuwa ambacho amekianzisha kwa ajili yake mwenyewe. Lakini dhana yao hiyo huenda kinyume kabisa na ugunduzi wao wenyewe. Hebu ngoja tuangalie vipi hawa wanaoitwa watu wasomi wanavyosigana wenyewe. Wanasayansi wa uganga wamechunguza kila sehemu ya mwili wa mwanadamu. Sasa wanajua mpango mzima wa mwili, kutoka kwenye sehemu ndogo sana mpaka kwenye sehemu kubwa sana. Juu ya msingi wa uchunguzi huu wanasema kwamba mwili wa binadamu umetengenezwa kwa matirilioni ya chembe chembe za uhai. Chembe chembe hizi ni za aina nyingi kama vile chembe chembe za damu, chembe chembe za misuli, na chembe chembe za neva. Kila aina ya chembe chembe ina sifa maalumu na baadhi kazi makhususi. Kama viungo maalum vyenye changamano ya hali ya juu kama vile moyo, figo, mapafu, ini nk. Viungo vyote hivi vina kazi maalum na 27 28

madhumuni yaliyo fafanuliwa vizuri ya kuwepo kwao. Swali lazima liulizwe kwa watafiti hawa wa uganga ambao wenyewe wameufichua ukweli huu. Kwamba, kila chembe chembe na kila kiungo katika mwili wa mwanadamu vina kazi maalum ya kufanya, basi ni nini kazi maalum ya mwili wote wa mwanadamu? Je, ni busara kuchukulia kwamba, chembe chembe zote, mwili na viungo vina madhumuni na kazi, lakini wanadamu ambao wametengenezwa na chembe chembe na viungo hivi hawana madhumuni yaliyo fafanuliwa vizuri? Hivyo, mtu mwenye akili ya kawaida atakubali kwamba wakati kila kiungo cha mwili kimepewa kazi maalumu, basi wanadamu vile vile lazima wana madhumuni maalum ya maisha. Quran tukufu hutufundisha kwa usahihi madhumuni ya Mungu ya uumbaji, malengo na shabaha ya kila mwanadamu. Wale ambao hutekeleza madhumuni na kufanya kazi zao husemwa kwamba wana maisha ya maana. "Sikuwaumba majini na watuila waniabudu Mimi" (51:56) Hivyo Allah (s.w.t) ametupa mwili kamilifu ambao ndani yake kila chembe chembe na kiungo bila kuchoka hutuhudumia. Katika mwili wetu, mamilioni ya mashine changamano zinafanya kazi kwa ajili yetu kutekeleza mahitaji yetu na kutuweka wakakamavu na hai. Mamilioni ya kurasa yahitajika kueleza kazi na harakati za mashine hizi ambazo hutuhudumia saa zote. Mwanafunzi wa uganga huchukua miaka mitano mpaka saba ili kupata tu elimu ya kazi za viungo hivi. Kwa ufupi, hapa tunaeleza tu shuguli ya baadhi za viungo: Mapafu huupa mwili oksjeni na wakati huo huo kutoa kaboni daoksaidi. Moyo ambao ni pampu yenye nguvu sana, hupiga mara 100,000 kila siku kama inavyo pampu lita 4.5 za damu kwa dakika moja kwenye mwili. Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula husaga chakula tunachokula kwenye viini vyepesi ambavyo vinaweza kutumiwa na chembe chembe za mwili. Mfumo wa mkojo huondoa vitu visivyo takiwa kutoka kwenye damu na kuvimwaga kutoka mwilini. Mfumo wa neva hurekebisha na kuunganisha harakati za mifumo yote ya mwili na huwezesha mwili kujirekebisha kwenye mabadiliko ambayo hutokea ndani yake wenyewe na katika mazingira ya jirani. Mfumo wa tezi hudhibiti kazi za mwili kwa kuzalisha homoni ambazo hufanya kazi kama wahudumu wa kemikali. Mfumo wa mishipa ya maji una mtandao wa mirija ibebayo maji meupe ya ugiligili yaitwayo limfu. Hukogesha na kurutubisha chembe chembe za tishu za mwili. Mfumo wa kinga, huukinga mwili wakati wote kutokana na ugonjwa- unaozalisha jems, virusi na aina nyingine ya viini vyenye madhara. Chembe chembe zilizowekwa maalum hupinga na kuharibu aina yote ya wavamizi ambao wanaweza kuwa tishio kwa afya yetu. Sasa akili yenye wepesi na kuhisi lazima ifikirie kwamba ni utii ulioje wa timu ya vyombo vya wafanyakazi katika mwili wetu unaotuhudumia wakati wote kama watumwa watiifu. Yatupasa tujiulize wenyewe, je, hatuwajibiki kumuabudu Allah (s.w.t), ambaye amewaumba na kisha akawafanya watumwa wetu bila malipo. Wanasayansi ambao walichunguza mpangilio huu waajabu katika mwili kwa macho yao matupu na bado wanakataa kutokuwepo kwa Mungu hawastahili chochote bali moto wa jahannamu, ambako wataishi milele kuona matokeo ya ujinga wao mkubwa na kutokua na shukrani kusikoelezeka. Wale ambao hawaamini Mungu muumba watakuwa hawana uwezo wa kukamilisha madhumuni ya kuumbwa kwao. Hii ina maana kwamba watu kama hao hawana thamani kabisa, wawe ni wanasayansi wakubwa ulimwenguni au marais au watu matajiri. Vitu vyote wanavyomiliki havina thamani kwao kwa sababu siku moja watavipoteza daima dawamu. 29 30

Quran tukufu imeeleza kutokuwa na thamani kwa kazi kama hizo. "Na waliokufuru vitendo vyao ni kama sarabi (mazigazi) Uwandani, Mwenye kiu huyadhania ni maji. Hata akiyaendea hapati chochote. Na atamkuta Allah hapo naye amlipe hisabu yake sawa sawa. Na Allah ni Mwepesi wa kuhisabu." (24:39) Hivyo wanasayansi wote wakubwa wa ulimwengu, wakuu wa nchi, mawaziri wakuu na watu matajiri ambao huonekana kuwa watu wakubwa sana na wakushangaza ni kama mazigazi katika jangwa kama hawaamini katika Mungu na amri zake. KIINI CHA FIKRA: Dini haipaswi kuwa kama alama ya biashara ya mtu. Kama mtu anafuata dini makhususi, lazima aone faida ya dini hiyo katika maisha yake. Leo wanasayansi wanachunguza kila sehemu ya mwili wa mwanadamu kwa ajili ya kujua tu madhumuni yao na kazi zao haswa. Wanajua kwamba kila kiungo kina jukumu maalum la kufanya katika mwili. Je, si jambo la kushangaza, kwamba wanasayansi wale wale ambao wana amini kwa nguvu kwamba kila kiungo katika mwili kina madhumuni makhususi, lakini hawatambui madhumuni yoyote ya wazi ya mwili mzima wa mtu. Hivyo kukataa kuwepo kwa Mungu maana yake kukataa kila kitu. Mtu ameumbwa katika maumbile ya kuhisi kuwepo kwa Muumba wake. Hisia hii yenyewe ni dini. Uislamu ndio dini ambayo hutafsiri hisia hii ya kiasili katika lugha ya mwanadamu. SURA YA NNE: UISLAMU NDIYO DINI PEKEE YA KWELI YA MUNGU. Ingawa wafuasi wa kila dini wanasema kwamba dini yao ndiyo pekee ya kweli, lakini hakuna mtu mwingine kama Mwislamu awezaye kulithibitisha hilo kimantiki. Hebu ngoja tutoe nukta zenye nguvu katika kuunga mkono imani yetu ambayo hakuna awezaye kuzivunja chini ya sababu thabiti za kiakili. 1. Waislamu kamwe hawadai kwamba Uislamu ni dini mpya, bali wanaamini kwamba ni dini ya kwanza na ya zamani sana ambayo iliteremshwa kwa mtu wa kwanza na mtume wa kwanza, Adamu (a.s) ambaye alikuja juu ya sayari ya ardhi kwa amri ya Allah (s.w.t.). 2. Waislamu huamini katika msingi wa mafundisho ya Mtume Ibrahim (a.s), Mtume Musa (a.s), Mtume Isa (a.s) na kuonyesha kwamba Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa Mtume wa mwisho wa Mitume yote ambaye alishuhudia na kukamilisha ujumbe wa Mungu. Yaani ni kwamba, Mitume wote kutoka Hadhrat Adamu (a.s) mpaka kwa Hadhrat Muhammad (s.a.w) wana imani za msingi ule ule. 3. Quran Tukufu ni Kitabu pekee cha Mungu ambacho mpaka sasa kiko katika muundo wake wa asili na kamwe hakijabadilishwa hata kidogo au kuchanganywa na mambo mengine au kufanyiwa uovu katika njia yoyote ile. Hakuna kitabu kingine kinacho daiwa kama kitabu cha Mungu kinachopatikana katika muundo wake wa asili au katika lugha ile ile ambayo kwayo iliteremshwa (isipokuwa Qur'an tu). 4. Uislamu hujumuisha kila kipengele cha maisha ya mwanadamu na hutoa ulinzi kamili katika kila eneo la masilahi ya mwanadamu. Una mfumo kamili wa ustawi wa maisha. Hakuna dini nyingine iliyo na mwenendo huu wa sheria za jamii. 5. Imani za msingi na sheria za jamii za Uislamu kamwe hazigongani 31 32

zenyewe kwa zenyewe. Vile vile, imani za msingi na msingi wa mafundisho ya Uislamu na ukweli uliothibitishwa wa kisayansi huonyesha kupatana na kila moja. Ukweli huu ni kinyume kwa dini nyingine za ulimwengu. 6. Uislamu unatueleza kwa uwazi kabisa, tumetoka wapi, kwa nini tuko hapa, na hatimaye tutakapo kwenda. Uislamu kwa uwazi hufafanua lengo la kuumbwa kwetu na madhumuni ya maisha yetu. Dini nyingine zote hazijibu maswali haya ya msingi kwa uwazi. 7. Uislamu ni dini ya pekee ya kweli yenye kuamini Mungu mmoja ambayo hutufundisha kuamini katika umoja kamili wa Mungu. 8. Wakristo wanadai kwamba wanaamini katika Mungu mmoja, lakini vile vile wanamini katika utatu, yaani, wasema 1+1+1=1 ambayo sio sahihi. Halikadhalika, Wahindu wanadai kwamba wao vile vile wanaamini katika Mungu mmoja lakini wanaabudu miungu mingi. Sasa tutathibitisha kwamba mafundisho ya asili ya dini ya Wayahudi, Ukristo na dini nyingi nyingine hushuhudia imani za msingi za Uislamu. Dini hizi sasa ni tofauti kwa sababu zimebadilishwa na watu ili kutekeleza haja zao wenyewe. Dini ya asili ya Wayahudi na Ukristo huthibitisha Uislamu. Wafuasi wa dini ya Wayahudi wanajulikana kama Wayahudi. Dini ya Wayahudi katika muundo wake wa asili si chochote bali ni Uislamu. Wayahudi bado wanamwamini Hadhrati Musa (a.s) ambaye alikuwa mjumbe wa kweli wa (Mungu) Allah (s.w.t). Jina la Hadhrati Musa (a.s) limetokea mara 136 katika sura tofauti 37 za Qurani Tukufu. Hadhrati Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume watano wakubwa. Allah (s.w.t) amependezewa na juhudi za unyofu wake na mchango mkubwa katika Qurani Tukufu. "Na mtaje Musa katika Kitabu. Hakika yeye alikuwa ni mwenye kuchaguliwa na alikuwa Mtume, Nabii". (19:51) Hadhrati Musa (a.s) alihubiri kwenye taifa lake Amri kumi, ambazo zinaelezewa katika Qurani Tukufu. Aliwafundisha watu wake kwamba, hakuna Mungu isipokuwa Allah na mimi (Musa) ni mjumbe wake. Kama ambavyo Qurani Tukufu ilivyo teremshwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w), Tawrati iliteremshwa kwa Hadhrati Musa (a.s). Quran Tukufu imethibitisha kwamba Tawrati ilikuwa kitabu cha kweli cha Mungu ambacho kiliteremshwa kwa Mtume Musa (a.s). "Amekuteremshia kitabu kwa haki, kinachosadikisha yaliyokuwa kabla yake. Naaliteremsha Taurati nainjili". (3:3) "Hakika sisi tuliteremshataurati yenye uwongofu na nuru." (5:44) Lakini leo vitabu vya kidini vya Wayahudi, vitabu vitano vya Biblia, ambavyo vinaitwa Pentateuch au Agano la kale au Tawrati, sio kitabu kilekile ambacho kiliteremshwa kwa Hadhrati Musa (a.s). Hivyo Waislamu wanaamini kwamba Tawrati, kitabu cha dini cha asili cha Wayahudi, ni kitabu cha kweli cha Mungu ambacho kiliteremshwa kwa Hadhrati Musa (a.s) kutoka kwa Allah (s.w.t) lakini hawatambui Tawrati iliyopo sasa kama kitabu cha Mungu kwa vile kimebadilishwa. Ni muhimu kufahamu kwamba baadhi ya hadithi za Hadhrati Musa (a.s) ambazo hazibadiliki, ambazo Wayahudi hawakuweza kuzibadilisha na ambazo bado wanazitekeleza, zimo katika Uislamu. Kwa mfano: a) Wayahudi bado wanafanya ukeketaji (utahiri)ambayo pia ni lazima katika Uislamu (kwa wanaume tu). b) Wayahudi hawali Nguruwe ambayo pia imekatazwa sana katika Uislamu. c) Wayahudi hawali kamba, na aina nyingine wa chaza au kobe. 33 34

d) Wayahudi wanafuata vitendo fulani vya uchinjaji wa Ki-Islamu. e) Viongozi wa kidini ya Kiyahudi (Rabbi) wanafuga ndevu na kufunika vichwa vyao. f) Wayahudi hutekeleza taratibu za mazishi kwa haraka iwezekanavyo. Inashangaza kuona kwamba Wakristo, ambao vilevile humtambua Hadhrati Musa (a.s) kama Mtume wa Mungu na huichukulia Tawrati kama sehemu ya Biblia yao, hawafuati sheria yoyote hapo juu. Wayahudi vilevile humuamini Hadhrati Ebrahim (a.s), Mtume mkubwa wa Uislamu na babu (mhenga) wa mtukufu Mtume wa Uislamu, Hadhrati Muhammad Mustafa (s.a.w). Mjukuu wa Hadhrati Ibrahim (a.s) alikuwa ni Hadhrati. Yakuub (a.s), ambaye vile vile aliitwa Israil. Alikuwa na watoto 12. Waliasisi makabila 12 ambayo yamekuwa Wana Israili. Kwa kipindi cha muda, wengi wao (kizazi cha Hadhrati Yakuub) waliloea katika nchi ya Misri, ambako hatimaye walikuwa watumwa. Katika miaka ya 1200 BC, Hadhrati Musa (a.s) aliwakomboa kutoka kwenye utumwa wa Firauni na akawatoa Misri na kuwapeleka Cannon (Palestina). Ni bahati mbaya kwamba wafuasi wa Hadhrati Musa (a.s) na kizazi cha Hadhrati Yakuub (a.s) na Hadhrati Ibrahim (a.s) walikuwa maadui wakubwa wa mtukufu Mtume (s.a.w) Halikadhalika wafuasi wa Ukristo wanajulikana kama Wakristo. Wakristo wanadai kwamba Ukristo umetegemea juu ya maisha na mafundisho ya Hadhrati Isa (a.s) (Yesu) (a.s). Wanaamini kwamba Mungu alimtuma Hadhrati Isa (a.s) kama muokozi wa wanadamu. Lakini Ukristo katika muundo wake wa asili haukuwa chochote bali ni Uislamu. Hadhrati Isa (a.s) aliwafundisha watu wake kwamba Mungu ni mmoja na hana mshirika, hana mtoto, hana baba na kwamba yeye ni mjumbe wake. Leo Wakristo wanaanimi kwamba Hadhrati Isa (a.s) ni mtoto wa Mungu na ni sehemu ya Mungu. Wanamuita Bwana wa ulimwengu na kumshirikisha na Mungu. Hivi ni kinyume kabisa na ukweli na mafundisho ya asili ya Hadhrati Isa (a.s). Quran hutuambia kwa ukweli kabisa kwamba Hadhrati Isa (a.s) hakusema kile wanachoamini Wakristo, bali alisema kile Waislamu tunachoamini. Quran vilevile huthibitisha kwamba wafuasi wa kweli wa Hadhrati Isa (a.s) walikuwa Waislamu. "Na nilipowafunulia wanafunzi kwamba waniamini Mimi na Mitume Wangu, wakasema: Tumeamini na shuhudia kuwa sisi ni Waislamu". (5:111) Na pale Allah atakaposema: Ewe Isa bin Mariamu, je, wewe uliwaambia watu: nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Allah? (Na Isa) atasema: Utukufu ni Wako, vipi mimi ningesema kile ambacho sina haki nacho? Kama nimethubutu kusema hivyo, kwa hakika ungelijua hilo. Wewe unajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi Yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyofichikana. Sikuwaambia lolote ila uliyo niamrisha, nayo ni: Muabuduni Allah, Mola 35 36

wangu na Mola wenu. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao. Na uliponifisha ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi juu ya kila kitu. Ukiwaadhibu basi hao ni waja Wako. Na ukiwasamehe, basi Wewe ndiye Mwenye nguvu na Mwenye hekima. [Qur'an 5:116-118] Hii huonyesha kwamba dai la Wakristo kwamba wanafuata mafundisho ya Hadhrati Isa (a.s) sio sahihi. Hadhrati Isa (a.s) kamwe hakuwafundisha kile wanachoamini Wakristo leo. vinywa vyao: wanayaiga maneno ya waliokufuru kabla yao. Allah awaangamize!wanageuzwanamna gani hawa!". (9:30) Dini nyingine kama Uhindu, na Uzoroasti nk, zimebadilishwa vibaya mno kiasi kwamba ni vigumu kufuatilia na kujua asili zao. Hatuwezi kusema kitu chochote kuhusu asili ya mafundisho na asili ya imani zao. Ubudha, Ujaini, Ukonfusia, Ushinto, na Usikh ni fikira za akili za binadamu na haziwezi kuchukuliwa kama dini ya Mungu. Hivyo wafuasi wa kweli wa Hadhrati Isa (a.s) siyo Wakristo bali ni Waislamu. Waislamu vile vile huamini kwamba Injili kilikuwa kitabu cha Mungu ambacho kiliteremshwa kwa Hadhrati Isa (a.s) kutoka kwa Allah (s.w.t). Biblia ya sasa (agano jipya) ambayo Wakristo wanaamini kama kitabu cha Mungu siyo kitabu cha asili cha Mungu (Injil) ambacho kiliteremshwa kwa Hadhrati Isa (a.s). Hivyo, Waislamu huamini kwa nguvu kwamba Hadhrati Isa (a.s) alikuwa mjumbe wa kweli wa Allah (s.w.t) ambaye alifundisha imani za msingi na mafundisho ya Uislamu. Leo Wakristo wanafanya mambo mengi ambayo ni kinyume kabisa na mafundisho ya Hadhrati Isa (a.s). Kituo cha kidini ya Ukristo ni Roma, ambacho kamwe hakijawahi kutembelewa na yeye (Yesu). Hivyo historia huonyesha kwamba Ukristo hauna mafungamano na Hadhrati Isa (a.s) na msingi wa mafundisho yake. Hivyo, wote Wayahudi na Wakristo wanadai kwamba dini zao zimetegemezwa juu ya umoja wa Mungu, lakini hawaamini katika umoja kamili wa Mungu. Quran inaonyesha: "Na Wayahudi wanasema: uzeri ni mwana wa Mungu, na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa 37 38