IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE.

Similar documents
John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane

There is one God Mungu ni mmoja 1

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU

NEW INTERNATIONAL VERSION

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI)

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania

DINI JE, DINI NI MUHIMU?

Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (

AHMAD AL-RAYSUNI. SWAHILI VERSION idara ya Lugha na ukalimani ya Chuo Kikuu cha waislamu cha Morogoro. IIIT Mfululizo wa Vitabu kwa Muhtasari

NEW INTERNATIONAL VERSION

Published on Al-Islam.org ( Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh)

Bismillah ar-rahman ar-raheem SHAHADA 1 YALIYOMO

Je, Umesikia Juu Ya Kanuni Nne Za Kiroho?

HALI YA UISLAMU. Maelezo ya kumsaidia Mkristo aufahamu Uislamu

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags:

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES

Ukweli wa hadith ya karatasi

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1

Kuishi Maisha Tele. Katika mwanzo wa mwaka mpya, Niliwapa changamoto

Vitendawili Vya Swahili

Rainbow of Promise Journal

YA AL HABBIB SAYYEID

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT RHAMU

No. Book Name Category Type Price 1 AFYA MARIDHAWA -1 SWAHILI SUBSCRIPTION 2, AFYA NA UZIMA SWAHILI SUBSCRIPTION 8,500.00

Gazeti la kwanza la Kiislam kutolewa kwa lugha ya Kiswahili - mwaka 1936

Ujasiri wa Kimaadili. Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani

2002 Version of the Basic Talk on "Using African Proverbs, Sayings, Idioms, Riddles, Stories, Fables, Play

February 9, 2017 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 16 MOMBASA COUNTY ASSEMBLY

Zanzibar itafutika-mwanasheria

Imam Mahdi katika Usunni Na Ushia

NGUO-NYINGI MKOTI: MWANZISHAJI WA MJI WA NGOJI (ANGOCHE)

UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI

MOROGORO JARIDA LA. ISSN Toleo Na.4 Julai 2005 BODI ZA AFYA ZA WILAYA - SAUTI YA WANANCHI

WELCOME TO GOD S SERVICE A.C.K. ST. LUKE S PARISH UMOJA & TENA CHURCH QUOTE OF THE WEEK PRAYER OF THE DAY

Toleo la kwanza: June, 2007 (Jamaadi Aakhar, 1428) Vitabu ii.

JUNE 4, Acts 2:1-12 and Offering...Pastor Maromy Samuel All Hail the Power of Jesus Name led by Haitian Congregation Worship Team

Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya

Ukoo Wake Na Kunasibika Kwake:

Uwezo Kenya National Learning Assessment 2014

HOTUBA YA JAJI MKUU MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA SIKU YA SHERIA, DAR ES SALAAM, TAREHE 1 FEBRUARI, 2018

MRADI WA METHALI (SANALASKUJA PROJEKTI)

WELCOME TO GOD S SERVICE ACK ST. LUKE`S PARISH UMOJA Theme: Endeavoring to touch the heart of God, (Matt 25:40). Kuazimia kumpendeza Mungu

HAKIBulletin RAIS AMTEUA PROF. JUMA KUWA JAJI MKUU WA TANZANIA. Ndani: JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA

The Lord be with you And with your spirit

TUMERITHI TUWARITHISHE

HAKIBulletin JAJI MKUU AWAASA WAHITIMU WA SHERIA KUJIENDELEZA KITAALUMA HALIUZWI! BENKI YA DUNIA USULUHISHI MUAFAKA MAHAKAMA MAWAKILI MAHAKAMA KUU,

Mashairi ya Masaibu ya Karbala

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS IJARA CONSTITUENCY AT IJARA BARAZA PARK

KITABU CHA MAFUNZO KWA WATOA DAWA KATIKA MADUKA YA DAWA MUHIMU

Ahadi za Serikali II. Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007

TALKING ABOUT ONESELF TO ACT IN THE WORLD: A SWAHILI AUTOBIOGRAPHY (SHAABAN ROBERT, MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

Ezra 3 Lessons Download or Read Online ebook ezra 3 lessons in PDF Format From The Best User Guide Database

Ripoti ya Warsha Ya Washikadau Ihusuyo Mpango wa Uendeshaji wa Mazingira Wilayani Rufiji Iliyofanyika Utete Rufiji Juni 2000

2

TAARIFA YA HISTORIA YA MKOA WA MWANZA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA

HOLY COMMUNION ACCORDING TO THE KENYAN RITE

Yassarnal Quran English

(Cell) (Cell) (Cell) (Landline) (Cell)

VACATION BIBLE SCHOOL VBS. Newsletter. #Rebuilding through prayer, hard work & perseverance.

In Search of Contact: Rhetorical Questions in the Communicative Frame of the Funeral Sermon

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)

NAIROBI CITY COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

Where is Africa? 2. What is African heritage? 3. What is the African heritage in the Bible? 6. What are African ways of worship?

REPUBLIC OF KENYA COUNTY ASSEMBLY OF KILIFI THE HANSARD. Wednesday, 29 th March, 2017

AND REACTION IN SWAHILI POETRY.

ATONEMENT IN AFRICAN PLURALISTIC CONTEXT: EXAMPLES FROM THE LUHYA OF WESTERN KENYA

MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU SHEIKH MUZAFFAR AHMAD DURRANI

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

TAUS RETREAT NEWS LETTER # 1

Builders in Australia are required to be completely committed to the building project. This is achieved through a legally binding contract.

Youth and Faith A collection of texts on the subject A collaborative Magazine Content

MASHAIRI YA WAADHI "VERSES OF ADMONITION": the people of Mombasa rebuked by P J. L Frank! and Yahya Ali Omar

MANIFESTATION OF COMMON MAN LANGUAGE IN EPIC POEMS: A CASE STUDY OF UTENDI WA SIRI LI ASRARI

3 rd of 3 files Appendix and References

Modern Swahili: the integration of Arabic culture into Swahili literature

Immaculate Conception Church

Cultural Considerations Tanzania Excursion

AFRIKA FOCUS, Vol.3, Nr.3-4, 1987, PP

I Peter 2:9-12 Who Are You?

December 6, 2017 PARLIAMENTARY DEBATES 1 NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL REPORT. Wednesday, 6 th December The House met at 9.30 a.m.

Wisdom Heaven. from. Martin Luther College Choir

Immaculate Conception Church

Proofs Of A Conspiracy Against All The Religions And Governments: The Secret Meetings Of Freemasons, Illuminati And Reading Societies By John Robison

Compassionate Together:

A COLLECTION OF 100 MAKONDE (KENYA) PROVERBS AND WISE SAYINGS

Transcription:

IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE. Na Ngowi Dennis. "*Natazamia Mbingu mpya na Nchi mpya* 1

YALIYOMO: SHUKRANI:... 5 UTANGULIZI KWA WASOMAJI WA BIBLIA!... 6 AGANO LA KALE... 7 AGANO JIPYA... 8 USOMAJI WA BIBLIA NA UCHAMBUZI WA MAANDIKO.... 9 HISTORIA YA BIBLIA KATIKA KUTAFSIRIWA KATIKA LUGHA MBALIMBALI!... 11 VITABU VYA APOKRIFA.... 14 MUHTASARI WA KITABU CHA MWANZO.... 19 MUHTASARI WA KITABU CHA KUTOKA... 23 MUHTASARI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI!... 25 MUHTASARI WA KITABU CHA HESABU:... 27 MUHTASARI WA KUMBUKUMBU LA TORATI... 29 MUHTASARI WA KITABU CHA YOSHUA.... 31 MUHTASARI WA KITABU CHA WAAMUZI.... 33 MUHTASARI WA KITABU CHA RUTHU.... 37 USHUHUDA WA RUTHU KWA KANISA LA LEO!... 38 MUHTASARI WA KITABU CHA KWANZA CHA SAMWELI.... 39 MUHTASARI WA KITABU CHA PILI CHA SAMWELI.... 41 DAUDI MTU SHUJAA NA MASHUJAA WAKE!... 43 MUHTASARI WA KITABU CHA WAFALME.... 46 HABARI ZA MFALME SULEMANI!... 48 UFALME WA ISRAELI.... 51 UFALME WA YUDA.... 55 MANATI YA MFALME UZIA... 59 MAOVU YA MFALME MANASE.... 61 HEKALU.... 63 MUHTASARI WA KITABU PILI CHA WAFALME.... 65 TAIFA (DOLA) LA ASHURU.(KINGDOM OF ASSYRIA.)... 67 MUHTASARI KITABU CHA MAMBO YA NYAKATI.... 69 MUHTASARI WA KITABU CHA MAMBO YA NYAKATI WA PILI.... 72 MUHTASARI KITABU CHA EZRA!... 74 2

MUHTASARI WA KITABU CHA NEHEMIA!... 76 MUHTASARI WA KITABU CHA ESTA... 78 MUHTASARI WA KITABU CHA AYUBU.... 81 MUHTASARI KITABU CHA ZABURI!... 84 MUHTASARI: KITABU CHA MITHALI!... 87 MUHTASARI: KITABU CHA MHUBIRI!... 89 MUHTASARI WA KITABU CHA WIMBO ULIO BORA... 91 KATIKA UBORA WAKE!... 91 MUHTASARI KITABU CHA ISAYA!... 94 MUHTASARI KITABU CHA YEREMIA... 96 MUHTASARI, KITABU CHA MAOMBOLEZO.... 98 MUHTASARI WA KITABU CHA EZEKIELI.... 100 MUHTASARI WA KITABU CHA DANIELI.... 102 MUHTASARI KITABU CHA HOSEA!... 104 MUHTASARI WA KITABU CHA YOELI!... 106 MUHTASARI WA KITABU CHA AMOSI.... 107 MUHTASARI WA KITABU CHA OBADIA!... 108 MUHTASARI KITABU CHA YONA!... 109 MUHTASARI KITABU CHA MIKA!... 110 MUHTASARI WA KITABU CHA NAHUMU.... 111 MUHTASARI WA KITABU CHA HABAKUKI.... 112 MUHTASARI WA KITABU CHA SEFANIA.... 113 MUHTASARI WA KITABU CHA HAGAI.... 114 MUHTASARI WA KITABU CHA ZEKARIA!... 116 MUHTASARI WA KITABU CHA MALAKI.... 118 KATI YA MALAKI NA MATHAYO NINI KILIENDELEA.... 120 MUHTASARI WA KITABU CHA MATHAYO.... 125 MUHTASARI WA KITABU CHA INJILI YA MARKO.... 127 MUHTASARI WA KITABU CHA LUKA... 130 MUHTASARI WA KITABU CHA INJILI YA YOHANA!... 132 MUHTASARI WA KITABU CHA MATENDO YA MITUME!... 135 MUHTSARI WA KITABU CHA WARUMI.... 137 3

MUHTASARI WA KITABU CHA 1.WAKORINTHO... 138 MUHTASARI WA WAKORINTHO 2:... 140 PAULO WA TARSO!:... 142 MUHTASARI WA WARAKA WA WAGALATIA.... 144 MUHTASARI WA KITABU CHA WAEFESO.... 145 MUHTASARI WA WARAKA KWA WAFILIPI.... 147 MUHTASARI WA WARAKA WA WAKOLOSAI.... 148 MUHTASARI WA WARAKA KWA WATHESALONIKE 1:... 149 MUHTASARI WA WARAKA 2 WATHESALONIKE!... 150 MUHTASARI WA TIMOTHEO WA KWANZA!... 151 MUHTASARI WA KITABU CHA 2 TIMOTHEO!... 153 MUHTASARI WA KITABU CHA TITO!... 154 MUHTASARI WA WARAKA KWA WAEBRANIA.... 155 MUHTASARI WA WARAKA WA YAKOBO.... 157 MUHTASARI WA WARAKA WA FILEMONI... 159 MUHTASARI WA WARAKA WA KWANZA WA YOHANA!... 161 MUHTASARI WA WARAKA WA PILI WA YOHANA!.... 163 MUHTASARI WA WARAKA WA TATU WA YOHANA!.... 164 MUHTASARI WA WARAKA WA PETRO WA KWANZA!... 165 MUHTASARI WA WARAKA WA PETRO WA PILI!.... 167 MUHTASARI WA WARAKA WA YUDA.... 169 MUHTASARI WA KITABU CHA UFUNUO WA YOHANA!... 171 RATIBA YA KUISOMA BIBLIA.... 174 VITABU REJEA!... 186 4

SHUKRANI: 5

UTANGULIZI KWA WASOMAJI WA BIBLIA! Biblia ina mweleza Mungu pande zote kwa wanadamu. Biblia ni ufunuo wa Mungu ulioandikwa kuhusu mapenzi ya Mungu kwa wanadamu. Biblia ni kitabu zaidi ya, kuliko kitabu kingine chochote. Biblia ni kitabu cha ajabu! Ni kitabu cha Vitabu,kitabu kilichovuviwa,ni kitakatifu kwa sababu kina maneno ya mwandishi mkuu ambae ni mtakatifu.ni kitakatifu kwa sababu mjumbe wake ni mtakatifu,maandiko yake ni matakatifu! Ni kitakatifu kwa sababu maudhui yake ni kutufanya kuwa watakatifu. Biblia ina vitabu 66 vilivyo andikwa na waandishi 40, kwa muda usiopungua miaka 1500; (yaani kuanzia 1400 K.K hadi 100 B.K). zaidi ya vizazi 40, katika mazingira tofauti,wakati tofauti,nyakati tofauti,ktk mabara 3(asia,ulaya na Afrika) ktk lugha 3( kiebrania,kiaramu na kiyunani)karibu Agano la Kale lote liliandikwa kwa lugha ya Kiebrania isipokuwa mafungu machache kwenye kitabu cha Danieli yaliyoandikwa kwa lugha ya Kiaramu. Agano Jipya limeandikwa kwa lugha ya Kigiriki\kiyunani. Sasa, mwanzoni mwa mwaka 2007; Biblia nzima tayari imekwi shatafsiriwa kwa lugha tofauti yaani. 429 Na Agano Jipya au Agano la Kale tu zimekwishatafsiriwa kwa lugha tofauti 1144. Na Biblia nzima tayari imekwishatafsiriwa kwa lugha za Afrika mia moja sitini. (160) Steven Lagton (1228) Aliigawanya Biblia ktk sura. R Nathan (1488) aliigawanya agano la kale ktk aya na Robert Stephanus(1551) aliigawaya Agano jipya katika aya. Biblia ilikuwa kitabu cha kwanza kuchapishwa na machine mwaka 1455 na Johann Gutenberg Vitabu vingine huchakaa lakini kitabu hiki Biblia hupita juu ya karne zote. Vitabu vingine lazima vibadilishwe kufuatana na umri. Bali wazee kwa vijana huipenda Biblia. Vitabu vingi ni kwa ajili ya sehemu ndogo ya watu na huwavutia watu wa lugha ile tu, lakini kitabu hiki Biblia, sivyo. Katika Biblia kuna vitabu 66. Katika Agano la Kale kuna vitabu 39 na katika Agano Jipya 27. Katika Biblia kuna sura 1,189; Agano la Kale kuna sura 929.Na Agano Jipya 260. Katika Biblia ya kiswahili kuna mistari 31,102. Ambazo ni mistari 23,145 katika Agano la Kale. Na mistari 7,957 katika Agano Jipya. Wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu. (2 Petro 1:21). 6

AGANO LA KALE Kuna vitabu 5 vya Sheria( Pentatuki); Mwanzo, Kutoka, Mambo ya walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati. Vitabu 12 vya historia. Yoshua,Waamuzi,Ruthu,I Samweli, II Samweli,I Wafalme,II Wafalme,I Mambo ya Nyakati,II Mambo ya Nyakati, Ezra,Nehemia na Esta. Vitabu 5 vya mashairi; Ayubu,Zaburi,Mithali,Mhubiri na wimbo ulio bora!. Vitabu 17 vya unabii Manabii wakubwa 5: Isaya,Yeremia,Maombolezo,Ezekieli na Danieli. Manabii wadogo 12; Hosea,Yoeli,Amosi,Obadia,Yona,Mika,Nahumu,Habakuki,Sefania,Hagai,Zekaria na Malaki Kwa maelezo zaidi ni kuwa;katika Agano la Kale. Kitabu cha katikati ya Biblia : Mithali; Sura ya katikati : Ayubu 29; Aya ya katikati : II Mambo ya Nyakati 20:17; Aya ndefu zaidi : Esta 8:9; Aya ya katikati katika Biblia nzima : Zaburi 118:8; Sura ndefu zaidi : Zaburi 119; Sura fupi na ya katikati mwa Biblia : Zaburi 117. Tunaweza kuwaza kwamba Agano la Kale ni kama msingi. Na Agano Jipya ni kama jengo juu yake. Msingi haufai kama jengo halijengwi juu yake. Jengo haliwezekani kama msingi haupo. Kwa hiyo Agano la Kale na Agano Jipya hutegemeana. Kama unasoma Agano la Kale tu au Agano Jipya tu, ni sawa na kuruka kwa mguu mmoja. Agano la Kale ni kama mguu mmoja na Agano Jipya mguu mwingine. Ikiwa unatembea kwa miguu miwili, basi unakwenda vizuri. 7

AGANO JIPYA Vitabu : 27; Sura :260; Aya : 7,957 ; Waandishi : 8 ; Kitabu cha katikati : 2Thesalonike Sura ya katikati: Warumi 13: Aya ya katikati : Matendo 17:17: Aya fupi? Kitabu kirefu : Luka; Kitabu kifupi : 2Yohana. Kitabu vya mwanzoni kabisa kuandikwa NI II Thesalonike,Yakobo,Wagalatia, cha mwisho NI ufunuo Wa Yohana. Vitabu vya Agano Jipya tunaweza kuvipanga hivi: Injili Vitabu 4 MATHAYO, MARKO, LUKA na YOHANA. Historia kitabu 1, MATENDO YA MITUME. Nyaraka 21. Paulo aliandika nyaraka 13 ama 14, Warumi,I Korintho,II Korintho,Wagalatia,Waefeso,Wafilipi,Wakolosai,I Thesalonike,II Thesalonike,I Timotheo,II Timotheo,Tito,Filemoni ( Waebrania); Nyaraka nyingine 7; Yakobo, I Petro,II Petro,I Yohana,II Yohana,III Yohana, Yuda. Hatujui, ni nani hasa aliandika waraka wa WAEBRANIA (pengine ni Paulo), Kitabu cha unabii kimoja UFUNUO.. ANGALIZO: Biblia ya kiyahudi INA vitabu 51 tu! Agano la kale 24 na Jipya 27. Kwanini.?, @vitabu vya manabii wadogo12 vimekusanywa na kuwa kitabu kimoja,vivyo hivyo kwa Ezra- Nehemia,Mambo ya Nyakati,wafalme na Samweli zote mbili, Biblia ya Roman Catholic(Vulgate) INA vitabu 72 kutokea vitabu 80 vya awali,vitabu 46 Agano la kale na 27 agano jipya..hii NI kutokana na kuvikubali vitabu vya apokrifa; Tobithi,Judithi,Hekima ya Yoshua bin Sira,Baruku,Makabayo Wa 1&2, na hekima za Sulemani pia Danieli sura 13&14,Esta sura za mwishoni. Hivyo maandiko katika Biblia zanaweza kuwa sawa kasoro itaonekana kwenye vitabu nyongeza na sura nyongeza! 8

USOMAJI WA BIBLIA NA UCHAMBUZI WA MAANDIKO. NI mengi yaliyoandikwa duniani,mamilioni ya vitabu,magazeti,majarida, na masomo mbalimbali yahusuyo mambo mbalimbali katika dunia yetu. Biblia NI Neno la Mungu lililovuviwa na kuleta tofauti kubwa kati ya kitabu Biblia na vitabu vingine vyote. Ndani ya kitabu hiki Biblia kuna maneno makuu mawili yanayo eleza moja ya sifa kuu ya Biblia yaani Neno la Mungu. 1. Neno la kiyunani " logos" 2. Neno la kiyunani " Rhema" Maneno haya hutumika sana katika usomaji na kuelewa uzito Wa andiko,uvuvio wake na ukuu wake. Neno " logos" humaanisha yaliyoandikwa! yaani kumbukumbu fulani juu ya kila unachotaka kujua,habari zake zilisha andikwa. mfano; Yesu akamjibu shetani " imeandikwa, MTU hataishi kwa mkate tu!( logos).neno la pili " rhema" humaanisha lililokusudiwa,vuviwa kwa majira na kwa wakati huu! mfano; "Bali kila neno litokalo kinywani mwa BWANA!( rhema) ndio maana tangu enzi na Torati hadi na leo,biblia imekuwa ikisomwa na Neno likihubiriwa ama kufundishwa lakini ujumbe wake haujaisha,hauja chakaa,hajapitwa na wakati,unawafaa watu wote,maususi kwa kila jambo,tukio na kuwa na nguvu ya kuathiri jamii,mtu na taifa unaposikilizwa! Wahubiri wakubwa waliowahi kuhubiri sana, mfano; Billy Graham,Catherine Kuhlman, Bonke,Myles,Benny,Maxwell nk, hata ikatokea wakakutembea Leo nyumbani kwako, utashangaa atasoma Mathayo ama Hosea sura na aya/mistari ile ile usomayo kila siku! Nitakushangaa sana ikiwa kwa kujiona unajua,unaelewa sana maandiko,umekomaa kiroho,wewe NI mshirika Wa Siku nyingi kanisani; hutaki kuonywa,kusahihishwa,kupewa ushauri eti kwa sababu hilo andiko wanalokusomea unalijua,'nilijua tu utanisomea hilo andiko' (logos). Hii NI sawa na kusema umefikia level ya kuipita Biblia hivyo hakuna jipya usilolijua! " Neno la Mungu li hai..." (rhema) Uchambuzi Wa Biblia/maandiko! Shule za sekondari wanafundisha juu ya tahakiki,yaani uchambuzi Wa vitabu vya Riwaya,Tamthilia na ushairi. Kwa namna kwamba mwanafunzi hupaswa kukisoma kitabu fulani,kisha akakielezea kwa kuchambua NANI mhusika mkuu,hadhira yake,maudhui yake,dhima kuu ya kuu,mada mbalimbali Ndani yake nk. Hivyo NI sawa na kueleza alivyokielewa kwa muhtasari kitabu hicho!kadhalika kwa Biblia njia kama hii unaweza kuitumia kuielewa na kuvielezea vitabu vya Biblia! Kuoanisha na kuonesha nini wazo kuu katika kitabu cha mwandishi,sura hii na nyingine katika Biblia. Kutafsiri/kufasiri maandiko hakuji kwa namna tunavyo taka sisi bali atakavyo Mungu! Epuka kujilisha/kuwalisha watu tango pori! 9

Kuna kanuni zenye kubeba funzo kuu( Doctrine) za maandiko na kuna kanuni za mahubiri ya kawaida Mfano: mafunzo juu ya utakatifu huhusisha toba ya kweli,kuonya juu ya dhambi! nk. Kwa upande wa mahubiri juu ya mafanikio! Huusisha mambo kama utoaji, panda na uvune Baraka yako. Hivyo lazima mkazo uwe kwenye kanuni kuu za mafundisho ili MTU/watu waelimike sio kumsisimua. Biblia Neno la Mungu lina kina,urefu,upana na kimo ambacho mpaka sasa bado hatujakifikia pengine hata robo yake! Soma sana, soma tena,tafakari,chambua,fafanua na ishi(direct application) ya ulichojifunza"nataka nimjue Yesu,na nizidi kumfahamu, Mapenzi yake nifanye Yale yanayompendeza!" BWANA MUNGU NA AKUBARIKI KWA KUDHAMIRIA KWA MAKUSUDI KUMFAHAMU YEYE!!!Amen. 10

HISTORIA YA BIBLIA KATIKA KUTAFSIRIWA KATIKA LUGHA MBALIMBALI! "Gombo la chuo" NI neno lililotumika sana katika Agano la kale,likimaanisha maadiko matakatifu.sehemu ama jumla ya maandiko ya nabii Fulani ama torati! Huitwa chuo,."chuo" ni neno lingine lililokuwa likimaanisha maandiko yaliyokuwa yanaandikwa katika ngozi laini,na kusokotwa kwa kuviringisha wakati unasoma ama unafunga ili kuhifadhi maandiko hayo!. Mfano; chuo cha nabii Isaya. Biblia NI mkusanyiko Wa chuo mbalimbali,yaani torati,manabii,injili, na nyaraka. Hivyo wakati mwingine wako waliozoea kusema Gombo la chuo akimaanisha kitu kilekile! Lakini vitabu vyote 39 vya Agano la kale viliandikwa kwa kiebrania! Na vile 27 vya Agano Jipya viliandikwa kwa kiyunani! Je ikawaje sasa Biblia ikatafsiriwa kwa lugha mbalimbali hadi za makabila ya watu? Ooh! Haikuwa kazi ndogo hata kidogo,wako waliochomwa kama nyama za mshikaki wakafa. kisa na mkasa wametafsiri Biblia kwa lugha isiyoruhusiwa! Sasa tuone ilivyokuwa hapo zamani za kale! Mnamo mwaka 250 K.K pale Alexandria Misri,jopo la watu 72 lilikusanyika kutafsiri Biblia kutoka kiebrania kwenda kiyunani! Waliongeza vitabu 14 vya Apokrifa kwenye vitabu vile 39 vya Agano la kale. Mwaka 382 B.K Jerome alitafsiri Biblia kwenda Kilatini akiviweka na vitabu vile visivyo rasmi,vitabu 14 vya Apokrifa hivyo Biblia aliyoitafsiri(vulgate) ikawa na vitabu 80. Chini ya utawala Wa Mapapa Wa kanisa la Roman Catholic walipiga marufuku kufasiri/kutafsiri Biblia kwenda lugha zingine isipokuwa kilatini tu. Mwaka 1384 John Wycliffe Profesa wa Oxford,mwana zuoni na mtheologia! akamwa MTU Wa kwanza kuitafsiri Biblia kwenda lugha ya kiingereza! Alinakili mkono kwa mkono,yaani teknologia ya kuchapisha ilikuwa bado haijavumbuliwa.miaka 44 baada ya kifo chake,nakaza kadhaa za maandiko yake yakamfikia Papa,alikasirika sana, kusikia kuna MTU mmoja aliyetafsiri Biblia kwenda kiingereza! Aliamuru kaburi lake lifukuliwe,mifupa yake ipondwepondwe kisha itupwe mtoni. Mtu yeyote aliyekutwa,ama kukamatwa na nakala zozote za Biblia zisizokuwa kwa kilatini,walihukumiwa hukumu ya kifo. mwaka 1415 B.K, kama vile utani,mwanafunzi Wa John Wycliffe,John Hus alikamatwa akiwa na nakala kadhaa ambazo zilitumika kumchoma kama mwizi mbele ya kadamnasi ya watu. kabla hajafa akasema maneno haya! Namnukuu.. ""Kwa miaka 100 ijayo Mungu atamwinua MTU, ambae wito wake kwa mageuzi hauwezi kuzuiliwa!""".mwisho Wa kumnukuu! Kama alivyotabiri mwaka 1517 B.K, Martin Luther akaanzisha mageuzi ya wazi dhidi ya kanisa Katoliki kwa kugongelea mlangoni mwa kanisa,wakati kabla ya misa/ibada kuanza,mambo 95 kinyume na Neno la Mungu yanayofanywa na Kanisa katoliki mjini Wittenberg! kitabu cha Foxe kilichokuwa kikiandika mashahidi Wa Imani(wafia dini) waliouwawa kwa kosa la kulipinga,ama 11

kwenda kinyume na kanisa Katoliki;kilieleza mwaka huo Wa 1517 watu 7 walichomwa hadharani kwa kosa la kuwafundisha watoto wao kusali sala ya Bwana kwa lugha ya kiingereza/kimombo badala ya kilatini. Martin Luther alienda mbali zaidi katika kuitafsiri Biblia kwenda kijerumani huku akihimiza kila MTU asome Biblia mwenyewe! Asisubiri kusomewa kanisani. Mwaka 1450 huko Mainz,Ujerumani Johann Gutenberg akawa MTU Wa kwanza kutengeneza mashine ya kuchapisha Biblia! Ikarahisisha Biblia kunakiliwa kwa haraka,na kusambazwa kwa kasi,tofauti na hapo kabla! ambapo nakala za Biblia zilikuwa chache na ziliuzwa ghali sana! Matajiri tu ndio walioweza kununua. William Tyndale,mwana zuoni,mbobevu tena kapteni Wa jeshi la mageuzi alikuwa anazungumza lugha 8 tofauti kwa ufasaha kana kwamba ndizo alizozaliwa nazo! Alichapisha Biblia(Agano Jipya) kwa lugha ya kiingereza. Alitumia karibu miaka 11 kuikamilisha Agano Jipya kwa lugha ya kiingereza,akinakili kutoka kwa Erasmus aliyewahi pia kutafsiri Agano Jipya kutoka Kiyunani kuja kilatini! Mwaka 1530 kazi yake ilipata soko sana kwa sababu kila MTU alitaka apate nakala yake! Hivyo zilifichwa kwenye mabarota ya pamba na magunia ya unga kama bidhaa za magendo ili ziwafikie Wateja wake! Ambao wengi walikuwa watumishi Wa Mfalme. Kila aliyekamatwa na kopi/nakala hizo alihukumiwa kufa,la sivyo aiteketeze kwa moto kabla hajakamatwa! Maparoko,mapadri walizitafuta nakala hizo kwa waumini wao ili kuwazuia wasizisome kwa madai zilikuwa na makosa mengi! na ndugu Tyndale alitafutwa kwa udi na uvumba,mwisho nakala hizo zilifika hadi chumbani mwa Mfalme Henry VIII Wa Ungereza. Mwaka 1536 William alikamatwa baada ya kusalitiwa na rafiki yake,akafungwa kwa siku 500,kisha akanyongwa na akachoma moto hadi kuwa majivu. Kabla hajafa akasema " Ee Bwana naomba ufungue macho ya Mfalme Wa Ungereza"!. Mwisho Wa kumnukuu. Miaka 3 baadae Mfalme Henry VIII akatoa amri,akaidhinisha mchakato Wa kuitafsiri Biblia yote kwa kiingereza iliyopewa jina la 'Biblia kubwa' chini ya Askofu Thomas Cranmer Wa jimbo la canterbury alimteua Myles Coverdale kuichapisha biblia hii iliyokuwa na kimo cha inchi 14! Kuanzia April 1539 hadi Desember 1541 yalichapishwa matoleo 7 ya Biblia hii. John Calvin mwana zuoni,mthelogia,mwenye fikra za mageuzi, huko Geneva uswizi alianzisha chuo cha Biblia na John Knox Wa Scotland walisimamia mpango Wa Biblia iliyoitwa "Geneva study Bible" ilikusudiwa kuwafundisha watoto wao wakati wao wako uhamishoni,ama kifungoni! Ilikuwa Biblia ya kwanza kutumia Sura/mlango na aya/mstari kila ukurasa ukiwa na mistari 42! kwa kipindi cha miaka 100 iliongoza kuwa bora zaidi ya nyingine! Ilikuwa ya kwanza kupelekwa bara la Amerika. Mwaka 1560-1644 matoleo 144 yalichapishwa katika juhudi ya kuboresha na kuihakiki maana halisi ya kila neno likilotumika kuitafsiri. Mwaka 1611 NI mwaka Wa historia kubwa katika Biblia kwani mfalme James VI alifadhili mpango Wa kuchapisha Toleo la Bibli litakalomaliza ubishi na kuwa bora kuliko yote yaliyopita. Miaka 6 ilitumika kuikamilisha! Mwaka 1605-1606 utafiti ulifanyika, 1607-1609 uchambuzi na kuikusanya 1610 kuichapisha, 1611 ilikamilika 12

yenye urefu Wa kimo inchi 16 kwa ukubwa. Ndio hadi Leo inatumika kama standard ya nyingine zinazotafsiriwa! Zingine zilizochapishwa 1885 ilichapwa tena 1971 new American standard Bible(NASB) 1973 new international version(niv) 1982 new king James version (NKJV) 2002 English standard version (ESV) Biblia kwa lugha ya kiswahili, Union Version(SUV) ilichapwa kwa mara ya kwanza mwaka 1952, 1997: na lugha iliyotumika inajulikana kama kiswahili cha kimvita!na Kiunguja. Ndio maana maneno kama "maseyidi,"mashehe," yametumika! Na sinagogi wakitafsiri kama sinagogi la wayahudi! Japokuwa Mbingu na nchi zitapita! Neno la Mungu ladumu hata milele! 13

VITABU VYA APOKRIFA. Je umewahi kuisoma/kusikia Biblia yenye vitabu 72? Je vitabu nyongeza 7 vimeingiaje na vina nini? Mnamo mwaka 250 K.K( kabla ya Kristo) kufuatiwa na kutafsiriwa kwa sheria(pentateuch) yaani vitabu 5 vya Musa huko Alexandria(Misri) na vitabu vingine kwa jopo la waandishi 70,kulipelekea kutolewa na kuchapishwa kwa toleo la Septuaginta(lxx) la Biblia lililotowewa zamani kwa ajili ya wayahudi wa mataifa,lililoandikwa kwa kiyunani.lilianza kusomwa katika masinagogi ya wayahudi wamataifa.lilikuwa pia limekusanya vitabu 14 visivyo rasmi. Hivyo kufanya Biblia toleo kwanza (katoliki) LA kilatini lililotafsiriwa na Jerome kuwa na vitabu 80! Baadae walivipunguza hadi 72.Apokrifa=imefichwa! MAJINA YA VITABU VYA APOKRIFA. 1.Tobithi 2.Judithi 3.Hekima ya Yoshua bin Sira 4.Baruku 5.I Makabayo 6.II Makabayo 7.Hekima ya Sulemani 14

1. TOBITI. Uandishi: 400-200 K.K. mbali na Palestina labla Misri. Toleo la kwanza liliandikwa kwa lugha ya kisemitiki likapotea. Kinasimulia habari za jamaa za Tobiti,kina tafsiri nyingi zinazohitafiliana. Ni simulizi za kale zisizo na msingi wa neno la Mungu wala maandiko.mfano jini asmodeo,malaika Rafaeli.Kutukuza wafu,kuhimiza watu kuwashughulikia marehemu. mfano, kuwaombea.tobiti anasimuliwa kama mtu aliyeishi baada ya kifo cha mfalme Sulemani na kugawanyika kwa ufalme. Kitabu hiki hakikupokelewa na wayahudi na waporestanti katika orodha ya vitabu rasmi. 2. YUDITHI. Uandishi: 100 K.K. Inaonekana kitabu hiki kimetungwa katika Palestina kati ya miaka 120-80 K.K. Mwanamke Yudithi anasimuliwa kuwakomboa wayahudi kutoka kwa jemedari Holofene aliyetumwa na Nebukadreza huko Betulia.Tafsiri zinatofautiana kati ya Vulgata na nyingine,historia ya geografia haikuzingatiwa.kitabu hiki hakikupokelewa na wayahudi na waporestanti katika orodha ya vitabu rasmi. I MAKABAYO Uandishi : 100 K.K. Kitabu kinasimulia vita vya wayahudi na wafalme waseleusidi,vita vya kupata uhuru wa dini na siasa. Yuda(Makabayo) alikuwa kama shujaa mkuu(mhusika mkuu) na ndugu zake/wenzake, kama Matathia,Yonathani na Simoni. Tukio la mfame Epifani IV, alipotoa sadaka ya nguruwe katika madhabahu ya hekalu la wayahudi(chukizo la uharibifu ilikuwa Des 8,167 K.K.) Kitabu hiki hakikupokelewa na wayahudi na waporestanti katika orodha ya vitabu rasmi. 4. II MAKABAYO. Uandishi :120 K.K.,baada ya mwaka 124 K.K. Tabia ya utungaji wa kitabu wa Makabayo wa kwanza,ni tofauti sana na na kitabu cha pili,kinaandikwa kwa lugha ya kiyunani. Ni muhutasari wa wa vitabu 5 vilivyoandikwa na Yasoni mtu wa Kirene. Ni kwa ajili ya wayahudi wa Iskanderia(Misri).Sala kwa ajili ya marehemu(sura ya 12:41-46) Dhima kuu ni kuwafurahisha wayahudi/kuwaimarisha watu na kuwavuta wayahudi wa Misri ili kushikamana zaidi na wayahudi wa Yerusalemu. 5. YOSHUA BIN SIRA. Uandishi : 190-132 K.K. Kiliandikwa/kutungwa huko Misri na kufasiriwa mwaka 38 wa mfalme Ptolomeo VII Evergete.Kinahimiza watu kutumia kileo ilimradi mtu asilewe:(sura 31:25-31). Kutokana na tafsiri ya Septuaginta,waporestanti walikihesabu miongoni mwa Apokrifa. 15

Vingine ni :Hekima ya Sulemani,Baruku n.k. Nyongeza nyinginezo. Waraka wa Yeremia, Danieli sura ya 13-14,Wimbo wa Azaria katika tanuru, Wimbo wa vijana 3,Suzana na hukumu ya Danieli,Belina na Joka.Baadhi ya sura ktk Kitabu cha Esta;ndoto ya Mordekai,nakala ya barua ya mfalme Artashata,sala ya Mordekai,sala ya Esta na amri mpya ya mfalme Muunganiko wa Ezra na Nehemia(Esdras) UMUHIMU WA BAADHI YA VITABU. Kitabu cha 3 Esdras na Makabayo 1. Katika taaluma ya historia ya Biblia na theolojia vinasaidia wanazuoni(wasomi) kufahamu mambo yafuatayo; Nini kilikuwa kinaendelea katika dini na taifa la kiyahudi katika miaka ile ya giza (400) kati ya Malaki na Mathayo. Kufahamu mazingira(context) ya siasa,dini,tamaduni aliyozaliwa Yesu. Kujua taifa,historia,siasa na taasisi za dini ya kiyahudi zilizoanza au kukubalika katika kipindi hiki cha miaka 400;mfano mafarisayo,masadukayo,n.k Je kazi ya umisheni ya kumtangaza Yehova kwa mataifa iliendeleaje katika kipindi hiki?(intertestimonial period). Kujua chanzo cha ibada za wafu katika kanisa Katoliki na viongozi wakuu walioanzisha. SABABU ZA KUKATALIWA KATIKA BIBLIA Havikukubaliwa na Waebrania na dini yao hata wakati mmoja,talmud-kitabu cha mapokeo ya wayahudi kinasema baada ya malaki, Roho Mtakatifu aliondoka Israel.Hii ina maana unabii au uandishi wowote baada ya Malaki ulikuwa hauna uvuvio wa Mungu.Maneno yaliyomo katika Apokrifa hayakutajwa katika Agano Jipya. Josephus na Philo(Yosefu na Filo) wana falsafa wataalam waliobobea katika historia ya wakati ule walivikataa vitabu hivi. Havikuwamo na haviko katika orodha yeyote ile ya maandiko matakatifu kabla ya mwaka 400 k.k 16

Jerome mwandishi na mtaalam anayeheshimika katika historia ya kanisa,alikuwa pamoja na kanisa Katoliki alivikataa kabisa vitabu hivi. Waandishi wenyewe wa vitabu hivi vya Apokrifa hawakudai hata mara moja kuwa ni vya Mungu. Havina unabii wa kweli wala havisemi hili ndilo neno la BWANA au asema BWANA wa majeshi Vina makosa mengi ya usahihi wa historia,vinapingana,havipatikani katika mambo makuu muhimu ya historia(theologia). Havina mafundisho ya kiroho kwa viwango vya ki-biblia. Maneno mengi ni ya hadithi,ya kigeni,yakuchekesha na yaliokosa dhima kuu ya ujumbe. Yesu hakuwahi kunukuu katika vitabu hivi. Mitume na manabii pia hawakuwahi kunukuu toleo,kifungu katika vitabu hivi. Vilianza kutumika(kutumiwa) rasmi na kanisa Katoliki mwaka 1546 B.K. Katika kukabiliana na matengenezo yaliyokuwa yakifanywa na Martin Luther na wenzake. Ni baraza kuu la Katoliki lililoitwa (council of trent) lililovunja kanuni za Biblia na kuingiza rasmi vitabu hivi. Chini ya Papa Paul III,wa wakati huo vitabu hivi vilikubalika na wajumbe wachache na wasio na taaluma. Waliokuwa wajumbe katika baraza hili walibishana sana,na sio wote waliokubali jambo hili. Baraza hili ndilo lililopitisha kuwa yeyote anayekataa vitabu hivi na alaaniwe! anathema! Vitabu hivi havifai kutumika katika kanisa wala kusomwa wakati wa ibada. Vitabu visivyokubaliwa na yeyote. Kitabu cha Henoko,Siri za Henoko,Ufunuo wa Baruku,Kuchukuliwa kwa Musa,Ufunuo wa Musa,Kupaa kwa Isaya,ufunuo wa shija,wosia wa Adam,Mausia ya Ibrahim na Isaka na Yakobo, ufunuo wa Ibrahimu,Maisha ya Asenati(mke wa Yusufu),kitabu cha Nuhu. 17

Utangulizi wa Agano la Kale. Vitabu 5 vya Musa Vitabu vitano vya kwanza vya Biblia ambavyo katika utamaduni wa kidini wa Wayahudi vilijulikana kwa jina moja: Torah jina lenye maana ya Sheria au Mwongozo. Wayahudi waliozungumza lugha ya Kigiriki waliviita vitabu hivyo vyote vitano Pentateuko yaani Kitabu katika sehemu tano. Vitabu hivyo vinajulikana pia kama Vitabu vya Musa, na tafsiri nyingine huvitaja kama Kitabu cha kwanza cha Musa (Mwanzo), Kitabu cha pili cha Musa (Kutoka) n.k. 18

MUHTASARI WA KITABU CHA MWANZO. Kina sura 50: Kina mistari 1,533. Mwandishi: Musa. Mwaka Wa Uandishi: 1450-1410 k.k Matukio ya kitabu hiki yalimalizika karne 3 kabla ya kuzaliwa kwa Musa. Matukio ya kitabu hiki yamechukua muda mrefu sana kuliko kitabu kingine chochote! Hivyo Musa aliandika kwa kifupi tu baadhi ya matukio makuu muhimu yaliyokuwa yakionesha mpango Wa Mungu kwa mwanadamu kama alivyooneshwa na Mungu juu ya mlima Sinai. Neno Mwanzo (Kitabu cha Mwanzo) linamaanisha: Chimbuko, chanzo, asili; nalo linatumiwa kukitaja kitabu hiki cha kwanza cha Agano la Kale kwani chenyewe kinasimulia hasa juu ya jinsi ulimwengu ulivyoanza kuwako, asili au chimbuko la binadamu na asili ya Waisraeli. Jina la kitabu kwa Kilatini ni GENESIS, maana yake ni kuzaliwa, mwanzo. Tafsiri zingine zinatumia majina ya Ki latini: GENESIS. Na zingine: KITABU CHA KWANZA CHA MUSA. Biblia ya Kiswahili inatumia jina: MWANZO. Kiebrania kitabu hiki kinaitwa BERE SHIT. Maana yake ni Mwanzoni. Kuandikwa; mwaka wa 1807 K.K. Kitabu kinatueleza mwanzo wa mambo yote isipokuwa Mungu, Yesu na Roho Mtakatifu. Wao hawana mwanzo. Ndani ya kitabu hiki kuna mianzo mingi. Kwa mfano: kuna mwanzo wa uli mwengu, mwanzo wa taifa la wana damu, mwanzo wa dhambi ulimwe nguni. Kuna mwanzo wa ahadi ya ukombozi. Na pia mwanzo wa maisha ya familia. Mwanzo wa ustaarabu wa wanadamu na mwanzo wa mataifa ya ulimwengu. Na pia mwanzo wa taifa la Wayahudi yaani mwanzo wa taifa la Waebrania. Kitabu hiki ni historia ya kushindwa kwa mtu. Lakini tunaona kwamba kila mara mtu ali poshindwa Mungu alikuwapo kumwo koa. Yeye ni Mwokozi wa ajabu! Kitabu cha Mwanzo chaweza kugawanyika katika sehemu mbili kuu: Sura 1 11: Historia ya awali ya kale juu ya ulimwengu na binadamu. Simulizi hili linatokana na imani thabiti kwamba ulimwengu wote uliumbwa na Mungu na kwamba watu walitokana na wazazi wa kwanza walioumbwa na Mungu, kwamba uovu, mateso na kifo duniani chanzo chake ni watu wenyewe. 19

Baada ya historia hiyo ya awali ya kale tunasimuliwa jinsi Mungu alivyowaadhibu watu kwa gharika kuu na jinsi Nuhu alivyookolewa katika maangamizi hayo. Kisha tunafahamishwa juu ya asili ya mataifa na lugha tofauti katika simulizi la Mnara wa Babeli (Sura 11.) Sura 12 50: Historia ya kale ya Waisraeli. Mungu alijichagulia watu wa Israeli ili kwa kupitia kwao mataifa mengine yamjue Mungu na kubarikiwa. Kwa hiyo, Mungu alimwita Abrahamu (12:1 25:18) ambaye anasifika kwa imani yake na utii wake kwa Mungu, kisha mwanawe wa pili, yaani Isaka, halafu Yakobo (25:19-37:1) ambaye alipewa jina ambalo limekuwa jina la taifa hilo Mungu alilochagua Israeli. Yakobo alikuwa na wanawe kumi na wawili ambao walikuwa chanzo cha makabila kumi na mawili ya Israeli. Mmoja wao, Yusufu, (37:2 50:28) alikuwa baba wa makabila mawili: Efraimu na Manase. 1. Simulizi la awali kuhusu ulimwengu na mtu, Sura 1 11 (a) Kuumba ulimwengu (1 2) (b) Uasi na kuanguka kwa mtu (3) (c) Uasi unaongezeka (4 5) (c) Nuhu na gharika (6 9) (d) Mnara wa Babeli (10 11) 2. Historia ya awali ya Waisraeli, Sura 12 50 (a) Habari za Abrahamu na watoto wake (12 24) (b) Habari za Yakobo (25 36) (c) Habari za Yusufu (37 50) Huo ndio utangulizi mfupi juu ya kitabu cha Mwanzo! Kwa maelezo zaidi soma kitabu cha mwandishi huyu huyu: SIMULIZI ZA MPANGO WA MUNGU TOKA ADAMU HADI WEWE! 20

UTANGULIZI WA KITABU CHA KUTOKA! Tangu mwaka wa 1807 K.K. hadi mwaka wa 1558 K.K. ilikuwa katikati ya MWANZO na KUTOKA na ilikuwa miaka 250. Biblia haisemi mambo yaliyotokeo hapo katikati. Wakati huo wana wa Israeli waliongezeka huko Misri. Waliishi kwenye jimbo la Gosheni. Waliongezeka kwa kasi sana na waka athiri mambo yote kuanzia siasa,uchumi,biashara,tamaduni na mambo ya kijamii ya wamisri! Wakatapakaa kila kona ya maamuzi! Wamisri wakaona kama vile wachaga walivyo kila kona ya inchi ila bora wachaga NI watanzania! Wayahudi/waebrania sio wamisri! Jamii ya kifalme Babeli wa kwanza ilitawala. (1894-1595) Hammurabi, mwanasheria maarufu, alikuwa mfalme (1792-1750 K.K.). Kwenye mwaka wa 1730 kabila la Hyksos liliwatawala Wamisri. Lilikuwa na magari ya farasi ya kivita na hivyo Wamisri hawakuweza kitu. Kabila la Hyksos lilitawala Misri miaka 150. Kabila la Hyksos lilitoka kaskazini na lilikuwa jamaa ya Shemu. Huko Misri, katika mji wa Thebe farao Sekenenre (1600 K.K.) alipigana na kabila la Hyksos lakini aliuawa katika mapigano. Inawezekana aliuawa wakati wa vita. Fuvu la kichwa chake kilichojeruhiwa liko katika jumba la makumbusho huko Kairo. Kijana wake farao Ahmose (aliyetawala 1580-1558 K.K.) pamoja na ndugu yake Kamose walifaulu na kuwafukuza wa Hyksos toka Misri. Farao Amenhotepi I (alitawala 1558-1525 K.K.) aliyemfuatia farao Ahmose, alianza kuwatesa sana wana wa Israeli. Aliogopa kwamba Waisraeli watakapopata nguvu zaidi watawatawala Wamisri na kuwaweka chini ya utawala wao, kama watu wa Hyksos walivyofanya kabla. Waebrania wala wazo la kurudi kwao kaanani jalikuwepo vichwani mwao! Raha mustarehe ziliwafanya kuona Gosheni NI inchi yao halali,sasa ili watoke Misri acha mateso yaanze! Ule msemo usemao "akufukuzae hakiambii toka".. 1558-1447 K.K. KUTOKA. Ilichukua miaka 111. Farao= Nyumba kubwa. 1558 K.K. Farao Amenhotepi I (1558-1525) alichukua utawala. (KUT 1:8) 1531 K.K. Haruni alizaliwa. 1529 K.K. Farao Amenhotepi I alitoa amri: "Watoto wa Waisraeli wote wakiume watupwe mtoni, mto Nile." (KUT 1:22) 1528 K.K. Musa alizaliwa. Binti wa farao Amenhotepi I (jina lake Hatsepsuti) alimchukua mtoto Musa. (KUT 2) 21

1525 K.K. Farao Amenhotepi I alifariki na farao Tho times I I (1525-1508) alichukua utawala. Musa alikuwa na miaka 3. 1508 K.K. Farao Thotmesi I alifariki na farao Thotmesi II (1508-1504) alichukua utawala. Musa alikuwa na miaka 20. 1504 K.K. Farao Thotmesi II alifariki. Musa alikataa kuwa farao. (EBR 11:24) Hatsepsuti, mama yake wa kambo alichukua utawala (1504-1492). Wakati huo alizaliwa Thotmesi III, mtoto wa dada au wa kaka yake Hatsepsuti. 1497 K.K. Yoshua alizaliwa. 1487 K.K. Musa alianza kuwatetea Waebrania waliokuwa watumwa Misri. Musa alikuwa kinyume cha Wamisri. Farao Hatsepsuti akaogopa kwamba Musa, atakapokuwa mfalme, angehamisha utawala kutoka Misri kwenda kwa Waebrania yaani wa Waisraeli.Ili mambo hayo yasifanyike, Hapsepsuti alitoa amri Musa auawe. Musa akakimbia mpaka Midiani. (KUT 2:11-15) 1482 K.K Farao Thotmesi III (1482-1450) alichukua utawala. 1450 K.K. Farao Amenhotepi II (1450-1425) alichukua utawala. 1448 K.K. Musa mbele ya kijiti cha moto. (KUT 3) Musa alirudi Misri 22

MUHTASARI WA KITABU CHA KUTOKA Kina sura 40 Kina mistari 1,213. Mwandishi: Musa. Mwaka Wa Uandishi: 1445-1405 k.k Kuzaliwa kwa taifa la Israeli kwa uchungu Na kumalizia kwa ukombozi Wa kutoka Misri.Katikati ya MWANZO na KUTOKA kuna miaka 250-300 Wakati huo Biblia imenyamaza kimya. Wakati huo taifa la Israeli waliongezeka huko Misri toka watu kama mia moja hadi watu milioni mbili hadi tatu. Kitabu cha KUTOKA kinaitwa Kilatini: EXO DUS. Maana yake: Kuondoka, Toka nje, Kwenda, Maandamano wa kuondoka. Tafsiri zingine zinatumia jina: EXODUS, au KITABU CHA PILI YA MUSA, au kama tafsiri ya Kiswahili: KUTOKA. KUTOKA ni kitabu cha ukombozi kinachotueleza kuokoka kutoka wapi, ina wezekanaje na mwanadamu anaokoka kwenda wapi? Anaokoka kutoka utumwa wa Misri anatoka kupitia damu ya mwanakondoo wa pasaka, anapita Bahari ya Shamu. Ni mfano: mtu anaokoka kutoka dhambi. Kupita Bahari ya Shamu ni mfano wa ubatizo. (1KOR 10:1,2). Ni mifano ya mambo ya Agano Jipya. Na baadaye mtu anatembea jangwani kue lekea nchi ya ahadi. Mungu alitaka akae kati ya watu wake na kwa ajili ya hii akawaamuru wajenge Hema ya kukutania. Taarifa za kutoka! Katika utawala Wa 18 Wa mafarao waliowahi kuitawaka Misri: ndipo Mungu akamtuma Musa kuwatoa wana wa Israeli Misri. Ilichukua mda wa siku moja Mungu kuwatoa Wana wa Israeli Misri lakini ilichukua miaka 40 Misri kutoka ndani ya mioyo ya wana wa Israeli! Kutoka kunaonesha mwanzo wa taifa la Israeli,mwanzo wa Kalenda yao,walianzia katika utumwa wanamalizia katika ukombozi! Maisha ya Musa yamechukua 1/7 ya Biblia nzima! Aliishi, ikulu miaka 40,akaishi jangwani(midiani)miaka 40 na akawaongoza wana wa Israeli kwa miaka 40! Egypt is a type of the world. Moses is a type of Jesus Christ. Passover is a type of the death of Jesus Christ. The Exodus is a type of salvation. The crossing of the Red Sea is a type of victory over the world. The pillar of cloud and of fire is a type of the presence of God in the believer. God had Israel spoil the Egyptians to provide for the Tabernacle. 23

Mgawanyo wa Sura katika kitabu cha Kutoka Kitabu cha Kutoka ni kitabu cha pili katika orodha ya vitabu vya Agano la Kale, cha kwanza kikiwa Kitabu cha Mwanzo. Jina la kitabu hiki KUTOKA ni tafsiri ya jina la Kigiriki eksodos ambalo lahusu tukio maalumu kabisa katika historia ya Waisraeli: Kutolewa kwao utumwani Misri, kuvuka bahari ya Shamu na safari yao jangwani hadi mlima Sinai.Kule mlimani Sinai, Mungu alijijulisha kwao, akaratibisha uhusiano wake nao kwa kuwawekea agano lake na mwongozo utakaoimarisha uhusiano huo, yaani amri kumi na maagizo mengine kuhusu namna ya kuishi.mhusika mkuu katika kitabu hiki ni Musa. Musa aliitwa na Mungu kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri. Yeye anaonekana katika kitabu hiki kuwa msemaji wa Mungu kwa watu wa Israeli. Aliwaongoza safarini kwa niaba ya Mungu na kuwajulisha matakwa ya Mungu. Kwa jumla, kitabu hiki chatuonesha hasa juu ya uhuru wa kweli, uhuru ambao Mungu anawapatia watu wake wapate kuwa na uhusiano mwema naye, na baina yao wenyewe.! 24

MUHTASARI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI! Kitabu kimeandikwa mara baada ya mwanzo wa safari jangwani, hema ya kukutania ilipokamilika. Hema ya kukutania ilikamilika mwaka (1447). Kabla ya Kristo. Jina la kitabu kwa Kilatini ni LEVITICUS, maana yake ni: Kinawahusu Walawi. Tafsiri zingine zinaitwa: KITABU CHA TATU CHA MUSA. Au MAMBO YA WALAWI, kama tafsiri ya Kiswahili. Kina sura 27 ; mistari/aya 659. Kitabu hiki kimeandikwa 1445-1444K.K Mazingira ya uandishi; chini ya mlima Sinai Wahusika wakuu! Walawi na namna ya kuwaongoza watu katika kumwabudu,kumtumikia na kumtii Mungu! Dhima kuu: Utakatifu! Kutengwa kwa ajili ya Mungu! Waisraeli walipaswa kutengwa na wanadamu (kukaa jangwani) ili waweze kumwakilisha na kuwasilisha Sera, ilani na tabia ya Mungu kwa mataifa mengine! Katika kabila zote 12 za Israeli, kabila la Lawi lilitengwa kwa ajili ya kazi ya utakatifu,wao hawakupewa urithi,wale na kuishi madhabahuni,wahudumu madhabahuni,waishi kwenye miji yao iliyotengwa! Ndani yao kulikuwa na koo 3 ambazo NI Merari, Kohathi na Gersoni. Kohathi walitoka makuhani na watu cream/mahususi waliotakaswa zaidi kwa ajili ya patakatifu pa patakatifu,mfano Musa na Haruni; Merari alifuatia kwa nafasi ya patakatifu na Gersoni kwa nafasi ya ua wa nje,hema na vifaa vyake,ulinda lindo nk! MAMBO YA WALAWI ni kitabu cha uta kaso. Maana ya utakaso au kutakasa ni kufanya takatifu au kutangaza au kutambua hali ya utakatifu. Neno Utakatifu limetumika mara 87 katika kitabu hiki! Shule ya utakaso inaanza kwa kujifunza dhabihu.bila dhabihu huwezi kujita kasa. 1. Bwana akamwita Musa, na kusema naye kutoka katika hema ya kukutania, akamwambia, 25

2. Nena na wana wa Israeli, uwaambie, mtu wa kwenu ata ka pomtolea Bwana matoleo, mtatoa matoleo yenu katika wanyama wa mifugo, katika ng ombe na ka tika kondoo. (LAW 1:1,2) Mwanzoni mwa kitabu hiki kuna dhabihu kuu tano: Sadaka ya kuteketezwa. Sadaka ya kuteketezwa ni mfano wa Kristo, ambaye... alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa. (Ebr 9:14). Sadaka ya Unga ni mfano wa Yesu Kristo aliyechu kua ubinadamu mbele ya watu na ya Mungu. Sadaka za amani ni mfano kwamba ku pitia Yesu sisi tuna mawasiliano na Mungu. Sadaka ya dhambi. Sadaka ya dhambi ni sadaka kwa Wakristo wanyonge. Na anayejua yeye si Mkristo mkamilifu bali dhambi ikaayo ndani yake. Sadaka ya hatia ni mfano kwa Kristo kwa wasioa mini, anayetafuta wokovu. Na sadaka ya hatia ni pia Kristo kwa Mkristo aliyeanguka dhambini lakini anayetaka kurudi.. " Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana. Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa ahadi. Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri.Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto." NI maneno ya Paulo kwa kanisa la Leo tujifunze kiini cha utakatifu tupate kuhesabiwa haki baada ya kutengwa kama vile Ibrahimu alivyotengwa mbali na inchi yake kwa yeye Sera, ilani,wokovu ukatufikia sisi tuliokuwa mbali na Mungu! Haleluya!!! UTAKATIFU, MTAKATIFU,UTUKUFU UNA YEYE LEO,SASA NA HATA MILELE! AMINA! 26

MUHTASARI WA KITABU CHA HESABU: Katika kitabu cha Hesabu ambacho kimeandikwa na Musa eneo kubwa la kitabu hicho kimeandikwa kuhusu sensa ambazo Mungu aliruhusu zifanywe pia tunasoma kuhusu wapelelezi waliotumwa kuipeleleza nchi ya Kaanani. Jambo linaloonekana kugusa mahusiano ya mwanadamu na Mungu katika kitabu hichi ni jambo hasi linaroharibu mahusiano. Jambo hilo ni manunguniko. Kinatokana na hesabu za sensa 2 zilizofanyika jangwani! Mwandishi: Musa Mwaka Wa uandishi: 1450-1410 K.K Idadi ya sura : 36 Idadi ya aya/mistari :1288 Kitabu cha manunguniko! Kitabu cha misafara( msafiri na mpitaji) Kimechukua miaka 39 katika matukio yake. Hesabu 1:1-10:11 imechukua nafasi ya siku 21. Hesabu 10:1-33:38 imechukua miaka 38. Hesabu 33-38 katika Kumbukumbu 1:3 imechukua miezi 6: Safari ya kutoka Misri baada ya miezi 13 ndio kitabu cha Hesabu kinaanza! Safari ya siku 11 inageuka na kuwa safari ya miaka 40! Kadesh barnea kilikuwa NI kituo cha mwisho kuikaribia Kaanani NI maili 150 toka Sinai na NI maili 50 kufika Beersheba mji Wa kusini Wa Yuda! Taarifa ya wapelelezi 12 waliokwenda kuipeleleza Inchi ya ahadi kwa siku 40 wale 10 wakasababisha safari yao ya upelelezi Wa siku 40 iwe adhabu ya miaka 40 kuifikia kaanani! Kadesh barnea ilikuwa 75% ya safari yao ikageuka ikawa 7% ya safari yao maana walitumia miaka 38 kutoka Kadesh barnea kufika Kaanani!. HESABU YA MATUKIO YA MANUNG'UNIKO! Kutoka mlima Sinai [nyika ya Sinai] walisafiri hadi kufika Tabori ambako moto uliteketeza hema za waliokuwa wananungunika. Wakazidi kwenda mbele hadi Kibroth-hataava walikopewa Kware baada ya hapo wakafika Haserothi;Miriam na Haruni wakamnena vibaya Musa. Kutoka Haserothi wakasafiri hadi Rithma wakafika Rimon-peresi kisha Libna wakatokea Risa na kufika Keheletha wakapanda mlima Sheferi na kushukia Harada wakapita tambarare ya makelothi na tahathi na tera na mithka wakatua Hashmona wakazidi kwenda mbele wapitia moserothi kuingia beneyakani hadi hor-hagidgad na kisha wakafika gudgotha[nchi ya vijito vya maji]. Kutoka godgoda hadi yotbatha na abrona wakaingia mlima seir[esion-geberi] na kuanza kuuzunguka mlima huu ambako Miriam alikufa Nyika ya Sini(Kadesh Barnea); Mateto mengine ya wana wa Israeli juu ya maji ya meriba.upelelezi wan chi ya kaanani kwa siku 40. Matokeo ya taarifa mabaya ya wapelelezi 27

ilipelekea adhabu ya watu wote kufa jagwani na safari yao kuwa ya miaka 40..(miaka 38 kutoka Kadesh barnea hadi Kaanani). Walitaka kwenda kwa hasira na haraka wakapigwa na Wakaanani.Ndipo uasi wa Kora,Dathani na Abiramu na watu 250 wateule wakamezwa na ardhi. Watu 14,700 walikufa kwa tauni. Kutoka Kadesh-Barnea hadi mlima Hori(Edomu);Haruni alipanda,mlimani akafa huko. (Akiwa na miaka 123).Mfalme wa kaanani alipigwa mbele ya Israeli(Aradi)Negebu aliyesikia habari..horma. Walianza kuzunguka zunguka nchi ya Edomu(milima ya Seyiri) kwa miaka 38. Kutoka mlima Hori hadi Salmona wakaenda Punoni(alipotengeneza nyoka wa shaba) wakaendelea mbele hadi Obothi kisha Iye abarimu(moabu) safari yao ikazidi kwenda mbele mpaka Dibon gadi(zeredi),almoni,diblathaimu,milima Abarimu kuikabili Nebo,beeri,matana,Nahalieli,Bathmoth (kilele cha Pisga)Milima Abarimu kwenda Shitimu(tambarare za moabu;kisa cha balaki na balaam)baal-peori wakafika Yeriko ngambo ya Yordani. Sensa ya 2 ya wana wa Israeli. Kifo cha Musa&kurithi kwa Yoshua.Tohara kwa wana wa Israeli.Habari za Balaki na Balaam,Pigo la Baal Peori (watu 24000 kufa) Hotuba za Musa: mwaka 40 mwezi 11 siku ya 1 Walikuwa wengi kuanzia Beth-yeshimothi hadi abeli-shitimu kama mchanga Wa bahari! Kutoka horebu/sinai walijifunza utakatifu (mkazo Wa kitabu cha Mambo ya Walawi) lakini walimchokoza Mungu na Musa kadiri walivyoweza! Hadi Musa akapoteza nafasi ya kufika Kaanani pia! Inawezekana nawe NI miongoni mwa wale waliookoka vizuri lakini kumsumbua na kumpa mawazo mchungaji wako NI jambo la kawaida sana! Pengne Mchungaji/viongozi wako Wa kiroho wamefikia mahali pa kuikosa mbingu kwa sababu yako! Je hili NI Jema? Tafakari! 28

MUHTASARI WA KUMBUKUMBU LA TORATI. Mwandishi:Musa Mwaka Wa uandishi: kati ya 1408-1405 K.K Maana ya jina: sheria ya pili,torati iliyojirudia Idadi ya sura: 34 Aya/mistari: 957 Kitabu hiki huitwa ; kitabu cha kumbukumbu! Matukio yake yamechukua kipindi cha mwezi mmoja! Safari ya wana Wa Israeli sasa imefikia karibu kabisa na nchi ya ahadi!,kwenye tambarare za moabu ng'ambo ya Yordani! Kimezaliwa kizazi kipya cha jangwani,wengine wamezaliwa baada ya kuondoka mlima Sinai hivyo hawajui chochote wala kushuhudia matendo makuu ya Mungu kama;kuvushwa bahari ya shamu,amri 10,mwamba kutoa maji na mengineyo! kizazi kile kilichopewa amri 10 katika mlima Sinai baada ya kutoka Misri kimekufa chote jangwani! Kutokana na uasi wao juu ya Mungu! Miaka ile 40 kama adhabu inafikia ukingoni!wapo wachache walio pata NEEMA ya kuishi hadi wakati huo; nao NI Musa,Joshua na Kalebu. Sasa Musa anatoa habari,taarifa,hotuba kwa hiki kizazi kipya! Akiwausia kwa kuwasomea kumbukumbu la Torati kabla ya Yeye kufa! HOTUBA KUU 3 ZA MUSA! Hotuba ya kwanza: sura 1:1-4:3 historia fupi ya taifa la Israeli tangu walipotoka mlima Sinai,uasi uliotokea Kadesh Barnea,manung'uniko ya jangwani,wosia Wa Musa. Hotuba ya pili : sura ya 4:44-26:19 Nini dhima kuu ya agano! Amri na sheria zote zihusuzo mambo mbalimbali. Hotuba ya tatu: sura ya 27-34 Kutoa toleo jipya, kuliboresha toleo lile la agano, maonyo ya Musa, ahadi ya Baraka kwa kutii,na laana kwa kukaidi, Musa kumsimika Yoshua kuwa kiongozi baada Yake,wimbo Wa Musa, mausia ya Mungu kwa Musa, baraka za Musa kwa kabila 12 za Israeli 29

Kifo cha Musa! Inawezekana sura ya mwisho iliandikwa na Yoshua akimtolea sifa nabii,mtu mpole,mzee,mwenye miaka 120,kiongozi maarufu asiye taka utukufu wakati harufu za kifo zinavyomzunguka anapopanda kwenye safu ya mlima akiiona kwa mbali Nchi ya ahadi akiishangilia nafsini moyoni mwake!. "Wala hajainuka tena katika Israeli nabii kama Musa, ambaye BWANA alimjua uso kwa uso; katika ishara zote na maajabu yote, ambayo BWANA alimtuma kuyatenda katika nchi ya Misri, kwa Farao, na kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote; na katika ule mkono wa nguvu wote, tena katika ule utisho mkuu wote, alioutenda Musa machoni pa Israeli wote." Je unakumbuka? Je una kumbukumbu yeyote kwa kizazi kijacho? Tangu unafundishwa Neno la Mungu hadi sasa hatua gani umepiga? Dua yangu! Ee BWANA,MUNGU MWENYEZI fufua kazi yako katika kizazi hiki cha zinaa na dhambi! Wakati wengine wanaongeza viwango vya uovu na iwapo NEEMA ya kuwawezesha wengine kuongeza viwango vyao vya utakatifu! 30

MUHTASARI WA KITABU CHA YOSHUA. Kwa hiyo imesemwa katika chuo cha Vita vya BWANA, Yoshua: wokovu! "Mungu huokoa" Alizaliwa kama mtumwa Misri,akawa shujaa Wa kuipeleleza Kaanani akiwa na miaka 50,akawa kiongozi baada ya Musa akiwa na miaka 85 akaingia Kaanani kama shujaa na majeshi ya Israeli! Akatawala kwa kuendesha vita miaka 25 akafa akiwa na miaka 110.alikuwa Wa kabila la efraim mwana Wa Yusufu! Kama vile babu yake alivyokufa na miaka 110 nae aliifikia miaka hiyo! Aliwasomea torati yote kila baada ya miaka 7 kwenye sikukuu ya vibanda! Hivyo enzi ya uhai wake walisomewa Mara 3! Torati yote! Kitabu kina sura 24 Kitabu hiki kina mistari 658. Kuitwa nchi ya Kaanani ilihusisha vita ktk maeneo makuu 3! Katikati ya Kaanani: Yoshua 6-8 Kusini mwa Kaanani: Yoshua 9-10 Kaskazini mwa kaanani: Yoshua 11-12 Mambo yaliyomo katika sura za kitabu hiki! maagizo ya Mungu kwa Yoshua! Makabila 3; Reubeni,Gadi na 1/2 ya Manase walishapewa urithi ng'ambo ya Yordani baada ya kuwapiga Waamori; Ogu mfalme Wa Bashani na Sihoni mfalme Wa heshboni ila waliahidi watavuka mto kupigana kwa ajili ya ndugu zao kisha watarudi kazi ya utekaji ikimalizika!. Habari za Rahabu kahaba na wapelelezi, kuvuka MTO Yordani, Tohara kwa wana Wa Israeli, Kuanguka kwa ng'ome ya Yeriko, dhambi ya Akani, Kuharibiwa kwa Ai,kutoa dhabihu,kusomewa torati na kuandikwa kwenye mwamba huko Ebali na Gerizimu, 31

Udanganyifu Wa Wagibeoni,Jua na mwezi kusimama, vita kaskazini mwa kaanani, orodha ya wafalme 31 waliouwawa na Yoshua, kutomalizika kwa utekaji maeneo, ugawanyo Wa urithi Wa makabila, miji ya makimbilio,miji ya walawi, zile kabila 3 kurudi ng'ambo ya Yordani, Mausia ya Yoshua na kifo cha Yoshua na Eliazeri. Miaka na Matukio! 1408-1387 K.K. KITABU CHA YOSHUA. Matukio yalichukua miaka 21. 1408 K.K. Chini ya uongozi wa Yoshua wana wa Israeli waliingia nchini Israeli. Kutekwa kwa Yeriko. (Yos 6) 1402 K.K. Nchi iligawanywa kati ya makabila ya Israeli.(Yos 13-21) 1401 K.K. Hema ya kukutania ilisimimishwa Shilo. (Yos 18:1) 1400 K.K. Makabila ya Reubeni, Gadi na 1/2 ya kabila la Manase walirudi mashariki ya Yordani. (Yos 22) 1387 K.K. Yoshua alifariki akiwa na miaka 110. (Yos 24:29) Kumalizika kwa kitabu cha YOSHUA. Yoshua = Yesu = Yehova anaokoa. Yehova ni wokovu The English and Hebrew title is based on the name of the central character, Joshua. His original name was Hoshea ( Salvation ) before Moses changed it to Yehoshua ( The Lord is Salvation ). It is tranditionally spelled Joshua in English while in the Greek language it is Jesus. The captain of the Lord s army (5:15) Jesus took the same name meaning the one who saves people from their sin, Christ is "Messiah" 32

MUHTASARI WA KITABU CHA WAAMUZI. Utangulizi. Sehemu ya 1! Kina sura 21: Kina aya/mistari 618 Mwaka Wa uandishi 10043-1004! Dhima kuu: dhambi na madhara ya dhambi! WAAMUZI 1387-1070. K.K. (Kilichukua miaka 317/335) Miaka ya Giza! Wakati mwingine Giza tororo! Matukio ya kitabu hiki yalifanyika 138O-1045 K.K. Matukio ya KITABU CHA WAAMUZI yalichukua zaidi ya miaka mia tatu. Matu kio katika kitabu hiki hayako katika mpangilio wa miaka, kwani sura za mwisho zilifanyika kabla ya yale yaliyotangu lia. Sura za nyuma zinaeleza jinsi anguko lilivyowapeleka wana wa Israeli mbali mapenzi ya Mungu. Ujuzi wa Wayahudi wanafikiri nabii Samweli amekuwa mwandishi wa kitabu cha Waamuzi. Biblia ina mifano ya aina mbali mbali. Katika vitabu vya Musa mifano hiyo inatu eleza namna ya kutoka katika utumwa wa Misri (yaani - kuokoka), tunavyovuka bahari ya Shamu (ni - ubatizo). Tunavyosafiri jangwani kuelekea nchi ya ahadi (maana yake - safari ya imani). Mfano katika kitabu cha Yoshua ni tofauti. Inatueleza kuhusu kutekwa kwa nchi ya Kanaani. Ni mfano kwetu kwamba baada ya kuo koka tuna anza safari ya maisha ya rohoni na ahadi za Mungu zinavyotimizwa kwetu kadri tunavyozidi kusonga mbele. Kitabu cha Waamuzi kinaendeleza kitabu cha Yoshua. Jina la kitabu hiki kinatokana na kujazwa roho wale viongozi 12, walio itwa na Mungu kuwasaidia wana wa Israeli. Hekalu lilikuwa huko Silo, lakini watu wa lipomkataa Mungu walishindwa kuka taa kuingia kwa maadui. Mahakimu waliwakomboa kwanza Waisra eli na baadaye wa kaanza kazi zao za utawala. Walishughulika sehemu mbali mbali na sehemu zingine walitawala kwa pamoja. Kitabu cha waamuzi kinaelezea kipindi cha giza ndani ya maisha ya Israeli katika nchi ya ahadi. Shindi zilizoko katika kitabu cha Yoshua ziligeuka hasara na uhuru ukawa utumwa na badala ya amani wakaanza kukosa imani. Kuendelea kukaanza kupungua wakapoteza macho ya kiroho na badala yake watu walianza kuwaza kiulimwengu. Uaminifu kwa Mungu ukapungua badala ya furaha huzuni ikaingia, na badala ya nguvu kukaja unyonge. Umoja ukatoweka na kuzorota. Zamani dhambi ilihukumiwa lakini sasa dhambi ilikubaliwa. Watu walianza kumwacha Mungu naye aka waacha mikononi mwa maadui. Israeli ilipoanguka lakini walipojuta na kumlilia 33

Mungu yeye akawainulia mwamuzi/ha kimu aliyewakomboa.kitabu kinaeleza kuhusu nyakati 7 za ku jiuzulu, nyakati 7 za utumwa na 7 za kuwekwa huru. Waisraeli walianza kumsahau Mungu polepole. (Amu 3:12-14) Farao Amenhotepi IV, yaani Ekhnaton, alitawala nchi ya Misri (1370-1352). Mama malkia Teje. Mke Nefertiti. 1368 K.K. Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia aliwatesa wana wa Israeli. (AMU 3:8) 1360 K.K. Kijana wa ndugu yake Kalebu, Othnieli aliwapa uhuru Waisraeli. (AMU 3:10) Othnieli akiwa mwamuzi. Amani miaka 40. Waamuzi walitawala sehemu mbali mbali za Israeli, na wachache kwa wakati moja.ndiyo maana miaka inalaliana na hata hivyo hatuna uhakika na miaka kamili. (AMU 3:10) 1320 K.K. Egloni mfalme wa Moabu aliwatesa wana wa Israeli. Na aliteka mji wa Mitende, yaani Yeriko. (AMU 3:12-14) 1302 K.K. Ehudi Mbenyamini mwenye mkono wa kushoto, aliwapa uhuru Waisraeli, na alimwua mfalme Egloni. (AMU 3:15-30) Ehudi akiwa mwamuzi na baada yake Shamgari. Wakati wa amani ulichukua miaka 80. (AMU 3:31) 1222 K.K. Mfalme aliyetawala kaskazini mwa Palestina mfalme wa Kanaani Yabini pamoja na mkuu wa jeshi Sisera, waliwatesa wana wa Israeli. (AMU 4:1-3) 1202 K.K. Baraka aliondoka kwenda kupigana na Sisera baada ya kuambiwa na hakimu wa kike nabii Debora. Israeli ilipata uhuru. (Amu 4:4-24).Wimbo wa Debora. (Amu 5).Amani ilikuwepo miaka 40. (Amu 5:31) 1162 K.K. 34