Ukweli wa hadith ya karatasi

Size: px
Start display at page:

Download "Ukweli wa hadith ya karatasi"

Transcription

1

2 Ukweli wa hadith ya karatasi Kimeandikwa na: Abdilahi Nassir

3 Haki ya kunakili imehifadhiwa na Abdilahi Nassir, 2003 Chapa ya Kwanza 2003 Kinatangazwa na MARKAZI YA AHLUL BAYT S.L.P MOMBASA (KENYA) Simu:

4 YALIYOMO Utangulizi Hadith Ya Karatasi Hoja zake zinajibiwa Uchambuzi wa Hadith ya Karatasi Mtume Kuzuiliwa Kuandika Wasia Tuyalinganishe na ya Khalifa Abu Bakar Kuna na ya Khalifa Umar Athari mbaya za kitendo hiki Kitabu Cha Mwenyezi Mungu Kinatosha Matokeo mabaya ya maneno hayo Athari mbaya za hatua zilizochukuliwa Mzozo Na Zogo La Maswahaba Athari mbaya ya zogo la maswahaba

5 SHUKRANI Shukrani nyingi kwa Baraza la Ilimu ya Kiislamu (The Islamic Education Board of the World Federation of Khoja Shia Ithna-Asheri Muslim Communities) la London, Uingereza kwa kugharimia uchapaji wa kitabu hiki. Mwenyezi Mungu awalipe malipo mema, amin.

6 UTANGULIZI Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Bwana wa viumbe vyote. Na rehema na amani zimshukie Mtume Wake mtukufu, na aali zake wazuri waliotwahirika, na wote wenye kuwafuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo. Tarehe 8-12 Oktoba, 1998 nilikwenda Dar es Salaam (Tanzania) kwa uwalishi wa chama cha WIPAHS (World Islamic Propagation and Humanitarian Services) kushiriki katika semina ya kukifungua chuo chao cha wasichana kiitwacho Wali ul Asr Education Centre (Markazi ya Elimu ya Wali ul Asr) huko Kibaha, kiasi cha kilomita 30 hivi magharibi ya Dar es Salaam. Nilipokuwa huko nilipata toleo Na. 170 la gazeti la An-Nuur la Jamaadul Aakhir 1419 / 0ktoba 9-15, Nilipokuwa ninalipitia, na nikafikia uk. 7, niliona makala katika mfululizo wa Elimu ya Dini ya Kiislamu kwa Shule za Sekondari. Makala hayo, yaliyokuwa ni ya historia kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha Nne, yalikuwa na kichwa cha habari hiki: Maoni tofauti kuhusiana na uchaguzi wa Khalifa wa Kwanza. Mara tu baada ya kuyasoma makala hayo nilipigwa na mshangao; nikawa sijui nikasirike kwa jinsi makala hayo yalivyoipotoa historia, au nicheke kwa jinsi mwandishi wayo alivyoufedhehi ujuzi wake wa historia hiyo! Hata hivyo, niliamua nisifanye pupa, bali niendelee kuusoma mfululizo huo mpaka niupate ukomo wake. Hivyo niliwaagizia sahibu zangu wa Tanzania waniletee makala yote juu ya mada hiyo - yaliyokwisha kutoka, na yatakayo endelea kutoka. Nikaletewa makala ya toleo Na. 169 la Jamaadul Aakhir 1419 /2-8 Oktoba, 1998 na yote yaliyofuatia hilo hadi kijitabu hiki kilipochapishwa. 1

7 Kwa kuwa makala yenyewe yamekusudiwa vijana wa shule, nilihuzunika sana kuona jinsi tunavyowalea watoto hao kwa kutowaeleza ukweli wa mambo yalivyokuwa. Ili kuirakibisha hali hiyo ndipo nilipoamua kukiandika kijitabu hiki - ambacho ni cha kwanza katika mfululizo wa vingi vyengine - ili wanafunzi hao, na hata wasiokuwa wanafunzi, waujuwe ukweli wa historia ya Ukhalifa ulivyo. Hilo tu ndilo lengo langu. Sina lengo jengine; na Mwenyezi Mungu ndiye shahidi wangu. Katika maandishi haya - kwa malezi ambayo wengi wetu humu Afrika ya Mashariki tumekulia nayo - hwenda baadhi ya wasomaji wayo wakachemkwa na damu. Kama itakuwa hivyo basi, ninawaomba wasomaji hao wasikasirike na mimi, wala wasiwe wepesi kunilani! Maana yote yaliyomo humu siyasemi mimi. Yametangulia kusemwa na kuandikwa na mashekhe wakubwa wakubwa wa Kisunni, katika vitabu tulivyovinukuu humu, kwa lugha isiyokuwa ya Kiswahili. Kubwa nililolifanya mimi ni kuyafasiri maneno hayo kwa lugha hii ambayo wengi wa watu wa Afrika Mashariki huielewa, ili sisi tuzijuazo hizo lugha nyengine tusiwapunje! Kwa hilo, mimi ni mjumbe tu. Jee! Mjumbe huuwawa? Mombasa, Kenya 15 Shaaban, 1419 Disemba,1998 Abdilahi Nassir 2

8 HADITH YA KARATASI Hii ni Hadith iliyo mashuhuri sana. Wanazuoni wa Hadith wameitaja katika vitabu vyao, na vile vile wanahistoria kadha wa kadha wameitaja katika vitabu vyao. Na kati ya wote hao hakuna hata mmoja aliyekikanusha kisa hicho, wala kukitilia shaka. Kati ya vitabu vya Hadith vilivyosimulia kisa hiki ni Sahih Bukhari. Kwa masunni, hiki ndicho kitabu kilicho sahihi mno, na kwa hivyo kuaminiwa mno, baada ya Qur ani Tukufu. 1 Katika kitabu hicho muna riwaya sabaa zinazosimulia kisa hicho. Kwa faida ya wasomaji wetu, hapa chini tunazidondoa zote: 1. Imepokewa kwa Ibn Abbas akisema: Mtume s.a.w.w. alipozidiwa na maradhi yake, alisema: Nileteeni (karatasi ya) kuandikia, niwaandikie maneno ambayo baada yake hamutapotea. Lakini Umar akasema: Hakika Mtume s.a.w.w. amezidiwa na maradhi, na sisi tunacho Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Kinatutosha. Hapo basi (maswahaba) wakakhitalifiana, na zogo likazidi, (Mtume s.a.w.w.) akasema: Niondokeeni! Haifai kuzozana mbele yangu. Ibn Abbas akatoka huku anasema: Msiba ulioje wa Mtume s.a.w.w. kuzuiwa kuandika (alichotaka kuandika). Hadith hii imo katika Kitaabul Ilm, Mlango wa Kitaabatil Ilm. Kwa tafsiri ya Kiingereza ya kitabu hicho, ni Hadith Na. 114, uk. 86 wa Juzuu ya Kwanza. 2. Imepokewa kwa Said b. Jubayr kwamba alimsikia Ibn Abbas r.a. akisema: Siku ya Alkhamisi! Na ni ipi hiyo siku ya 1 Taysiiru Mustwalanil Ahaadiith ya Twahhaan, uk. 36 3

9 Alkhamisi? Kisha akalia mpaka mawe yakaroa kwa machozi yake. Nikamuuliza: Ewe Ibn Abbas! Ina nini hiyo siku ya Alkhamisi? Akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alizidiwa na maradhi yake. Akasema: Nileteeni mfupa wa bega niwaandikieni maneno ambayo baada yake hamutapotea abadan. (Maswahaba) hapo wakazozana, wala haifai kuzozana mbele ya Mtume s.a.w.w. Na wakauliza: Ana nini? Amepiswa? Muulizeni (ili mujue hali yake). Yeye s.a.w.w. akasema: Niacheni! Niliyonayo ni bora kuliko hayo munayonitaka nyinyi niyafanye. Hapo (Mtume s.a.w.w.) akawaamrisha mambo matatu. Akasema: Watoeni Bara Arabu washirikina wote, wapeni zawadi wajumbe (wa kigeni wanapokuja kwenu) kama nilivyokuwa nikiwapa mimi. Msimuliaji akaongeza: La tatu ni jambo la kheri ambalo ama Ibn Abbas alilinyamaza, au alilitaja lakini nimelisahau! Hadith hii imo katika Kitaabu Fardhil Khumsi, Mlango wa Ikhraajil Yahudi Min Jaziratil Arab. Kwa Kiingereza ni Hadith No. 393, uk. 260 wa Juzuu ya Nne. 3. Maneno ya hii Hadith ya tatu karibu yote ni sawa na yale ya Hadith Na. 2 hapo juu. Nayo imo katika Kitaabul Maghaazil, Mlango wa Maradhin Nabiyyi s.a.w.w. wa Wafaatihii. Kwa Kiingereza, ni Hadith Na. 716, uk. 511 wa Juzuu yo Tano. 4. Imepokewa kwa Ubaydullah kwamba Ibn Abbas r.a. amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alipouguwa maradhi ambayo ndiyo aliyofia, na nyumbani mwake mukawa muna watu akiwamo Umar miongoni mwao, alisema: Njooni niwaandikie maneno ambayo hamutapotea baada yake. Umar akasema: Hakika Mtume s.a.w.w. amezidiwa na maradhi, na nyinyi munayo Qur ani. Kinatutosha Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Watu waliokuwapo hapo nyumbani wakazozana. 4

10 Wengine walisema: Njooni karibu ili Mtume s.a.w.w. awaandikie maneno ambayo hamutapotea baada yake. Na wengine wakasema alivyosema Umar. Walipozidisha zogo lao na ikhtilafu zao mbele ya Mtume s.a.w.w., Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alisema: Niondokeeni! Ubaydullah anasema: Ibn Abbas alikuwa akisema: Msiba ulioje wa Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. kuzuiwa kuyaandika maneno haya kwa sababu ya ikhtilafu zao na zogo lao. Hadith hii imo katika Kitaabul Mardhwaa, Mlango wa Qawlil Mariidhwi Quumuu Annii. Kwa Kiingereza ni Hadith Na. 573, uk. 389 wa Juzuu ya Sabaa. 5. Maneno ya hii Hadith ya tano karibu yote ni sawa na yale ya Hadith Na. 4 hapo juu. Nayo imo katika Kitaabul I tiswaami Bil Kitaabi was Sunnah, Mlango wa Karaahiyatil Ikhtilaaf. Kwa Kiingereza ni Hadith Na. 468, uk wa Juzuu ya Tisia. Kitabu chengine kinachosimulia Hadith hii ni Sahih Muslim. Kitabu hiki, kwa masunni, ndicho cha pili (baada ya Sahih Bukhari) 2 kilicho sahihi mno baada ya Qur ani Tukufu. Maneno ya Hadith iliyomo humu 3 ni karibu sawa na yale yaliyonukuliwa na Bukhari katika Hadith Na. 2 hapo juu. Hapa ningependa tukumbushane wanavyosema wanazuoni wa kisunni wa fani ya Hadith. Wao wanasema: Iwapo Hadith imepokewa na Bukhari na Muslim (wote wawili pamoja), basi Hadith hiyo huhisabiwa kuwa i sahihi mno. Ya pili kwa usahihi ni ile iliyopokewa na Bukhari peke yake. Ya tatu ni ile ya Muslim peke 2 Kama hapo juu, uk Katika nuskha ya Kiingereza ni Hadith Na iliyomo uk. 869 wa Juzuu ya Tatu. Na katika ya Kiarabu ni Kitaabul Waswiyya, Mlango wa Tarkil Waswiyya... 5

11 yake. Baada ya hapo zinafuatia zile zilizopokewa na maimamu wengine wa Hadith. 4 Hivyo, kwa kuwa hii Hadith ya Karatasi imepokewa na Bukhari na Muslim, lazima iwe i sahihi mno. Lakini mwandishi wa makala yaliyochapishwa uk. 7 wa toleo la 170 la gazeti la An-Nuur la tarehe 9-15 Oktoba 1998, amekataa hilo. Yeye amesema kuwa tukio hili halina ukweli! Na bila shaka ametoa sababu zake za kuamini hivyo ambazo tutazijadili hapa chini baadaye. Kwa hivi sasa, hata hivyo, ningependa ieleweke kwamba kisa hiki hakikusimuliwa katika Sahih Bukhari na Sahih Muslim peke yake. Kimeelezwa katika vitabu vyengine vya Hadith pia, k.v. Kanzul Ummaal na Musnad Ahmad; mbali vitabu vya historia vikubwa vikubwa vya tangu zamani, k.v. Twabaqaat Ibn Sad, chapa ya Beirut (Jz. 2, uk. 244), Taarikhut Twabari (Jz. 3, uk. 193), Taarikh Ibn Kathir (Jz. 5, uk ), Taarikhudh Dhahabi (Jz. 1, uk. 311), Taarikhul Khamis (Jz. 1, uk. 186), Al-Bad u wat Taarikh (Jz. 5, uk. 59), na Taarikh Abil Fidaa (Jz. 1, uk. 151). Hoja zake zinajibiwa Kama tulivyodokeza hapo juu, mwandishi wa makala tunayoyajadili humu alitoa sababu zake za kukatalia usahihi au ukweli wa tukio hilo la karatasi. Sababu zake alizozitaja ni sabaa. Hapa chini tunazidondoa pamoja na majibu yetu: (i.) Ibn Abbas, ambaye khabari ya kisa hiki imepokewa kwake, "yeye binafsi hakushuhudia tukio hilo." Halafu akatwambia tutizame uk. 220 wa Juzuu ya Kwanza ya Fat-hul Baari. Jibu: Tumeiangalia hiyo Fat-hul Baari. Katika nuskha niliyonayo mimi, 5 katika kuisherehe Hadith Na. 1 hapo juu (uk. 209), 4 Kama Na.1 hapo juu, uk Iliyochapishwa na Al-Maktabatus Salafiyya na kusahihishwa na kuthubutishwa na Sheikh Abdulaziz b. Abdalla b. Baaz. 6

12 hapana mahali popote palipoandikwa kwamba Ibn Abbas yeye binafsi hakushuhudia tukio hilo. Lililoelezwa hapo ni mradi wa maneno: Ibn Abbas akatoka huku anasema... katika Hadith hiyo, hivi: Dhahiri ya maneno haya ni kwamba Ibn Abbas alikuwa pamoja nao, na katika hali hiyo alitoka huku akisema maneno hayo. Lakini ukweli si hivyo inavyoeleweka kwa dhahiri isipokuwa kwamba maneno ya Ibn Abbas yaliyotajwa katika Hadith hii aliyasema pale alipokuwa anaisimulia Hadith hii.. Na imechukuliwa kinyume cha dhahiri ilivyo kwa sababu Ubaydullah ni taabii 6 wa tabaka ya pili. Yeye hakukidiriki kisa hicho wakati kilipotendeka, kwa sababu yeye alizaliwa baada ya Mtume s.a.w.w. kwa muda mrefu. Kisha ndipo alipokisikia kwa Ibn Abbas baadaye kwa muda mwengine. Kwa hivyo lengo la maelezo ya Fat-hul Baari, kama yalivyo wazi hapo juu, ni kufafanua tu kwamba Ibn Abbas alisema maneno yake hayo alipotoka mle alimokuwa akisimulia Hadith hiyo, wala sio alipotoka nyumbani kwa Mtume alimokuwa akiugulia. Na vivyo hivyo ndivyo ilivyoelezwa katika uk. 365 wa Mjallada wa Kwanza wa Irshaadus Saari 7 sherehe nyengine ya Sahih Bukhari, katika kuisherehe Hadith hiyo. Sasa tuitizame sababu yake ya pili: (ii.) Hakuna ushahidi wa kutosha kama tukio hili limetokea kweli au ni maandishi tu yenyewe yaliyopachikwa ili kukidhi haja ya waliyobuni tamko hili. Jibu: Ushahidi wetu wa kuwa tukio hilo limetokea kweli ni huo tulioutoa hapo juu, wa vitabu vya Hadith na vya historia. Kwa hivyo, kama mwandishi wetu huyo anabisha hilo, ni wajibu wake 6 Taabi i ni Mwislamu wa kizazi kilichofuatia kizazi cha maswahaba. 7 Chapa ya kwanza (l410h/1990bk) iliyochapishwa na Daarul Fikr. 7

13 atutolee ushahidi wa wataalamu waliolikataa hilo nasi tuweze kutoa majibu yetu. Sio yeye tu akatae hilo. Kwani yeye ni nani, katika usomi, mbele ya wataalamu tuliovitaja vitabu vyao? Hebu najitambulishe. Sababu yake ya tatu ni: (iii.) Ni muhali kudhania kuwa Mtume anaweza kuzuiwa na swahaba au na yoyote asiye Allah (s.w.t) kutekeleza jambo la utume wake. Jibu: Kwa nini mwandishi wetu huyo anaona muhali wa hilo? Kwani yeye hajapata kuyasoma hayo katika vitabu vyao? Kama hajapatapo, basi hebu nimdokeze mawili matatu, tena ya yuyo huyo aliyezuiya Mtume s.a.w.w. asipawe karatasi, yaani Umar bin Khattaab! Kwanza ni yale yanayoelezwa katika Hadith Na. 367 iliyomo uk wa Juzuu ya Sita ya tafsiri ya Kiingereza ya Sahih Bukhari. 8 Humo tunaona jinsi Umar alivyoshindwa kuzuiya hasira zake pale, katika mwaka wa 6H, Mtume s.a.w.w. alipoamua kuandika Mkataba wa Suluhu ya Hudaybiya na washirikina wa Makka. Hadith hiyo inaeleza hivi:.. Umar bin Khattaab alimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akamwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Jee, sisi hatuko katika haki, na wao katika batili? Jee, wale waliouliwa upande wetu hawamo Peponi, na waliouliwa upande wao Motoni? Mtume akajibu: Kwani! Umar akasema: Basi kwa nini tuitie doa dini yetu, na kurejea (Madina) kabla ya Mwenyezi Mungu kuhukumu baina ya wao na sisi? (Mtume s.a.w.w.) akamjibu: Ewe mtoto wa Khattab! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu hatanitupa abadan. 8 Kwa Kiarabu ni Kitaabut Tafsiir, Mlango wa Idh Yubaayi uunaka Tahtash Shajara 8

14 Hapo Umar akaondoka kwa hasira. 9 Hakuweza kusubiri mpaka akenda kwa Abu Bakar, 10 akamwambia : Ewe Abu Bakar! Jee, sisi hatuko katika haki, na wao katika batili? (Abu Bakar) akajibu: Kwani! Akamuuliza: Jee, waliouliwa upande wetu hawamo Peponi, na waliouliwa upande wao Motoni? (Abu Bakar) akajibu: Kwani! Hapo (Umar) akasema: Basi kwa nini tuitie doa dini yetu, na kurejea (Madina) kabla ya Mwenyezi Mungu kuhukumu baina yao na sisi? Abu Bakar akamjibu: Ewe mtoto wa Khattaab! Hakika yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu hatamtupa abadan. Hapo Mwenyezi Mungu akateremsha Suratul Fat-hi (ya 48). Hadith No iliyomo uk wa Juzuu ya Tatu ya tafsiri ya Sahih Muslim 11 inaeleza: Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akamtuma mtu kumwita Umar, na akamwambia aisome. Akauliza: (Mkataba) huu ni ushindi? (Mtume s.a.w.w.) akamjibu: Ndiyo. Hapo Umar akafurahi 12 na kurejea. Pili ni yale yaliyomo katika Hadith Na. 192 iliyomo uk. 153 wa Juzuu ya Sita ya tafsiri ya Kiingereza ya Sahih Bukhari. 13 Hadith yenyewe inazungumzia pale Abdalla bin Ubayy bin Salul alipokufa. Inaeleza hivi: Mtoto wake, Abdalla bin Abdalla, alikuja kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Akamuomba ampe kanzu yake (Mtume s.a.w.w.) ili amkafinie babake. Akampa. Kisha 9 Angalia mambo hayo! Anaondoka kwa hasira hata baada ya Bwana Mtume s.a.w.w. kumhakikishia kwamba yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kwamba Mwenyezi Mungu hatamtupa abadan? Hasira hizo anamfanyia nani? Mwenyezi Mungu au Mtume Wake? 10 Angalia! Hakutosheka na aliyoambiwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu, anataka hakikisho kwa Abu Bakar? Wa kufuatwa hapo ni nani; Mtume wa Mwenyezi Mungu au Abu Bakar? Soma Sura 10: Kwa Kiarabu ni Kitaabul Jihaadi Was Siyar, Mlango wa Sulhul Hudaybiyya Jee, kama haukuteremshwa wahyi huo ndiyo asingefurahi na kurejea?! 13 Kwa Kiarabu ni Kitaabut Tafsiir, Mlango wa Istaghfir Lahum aw laa Tastaghfir Lahum... 9

15 akamuomba amswalie. Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akasimama kumswalia. Lakini Umar akasimama na kuishika nguo ya Mtume s.a.w.w. (kumzuiya), 14 akamwambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Unamswalia (mtu huyu) hali Mola wako amekuzuiya kumswalia? Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akamjibu: Hakika Yeye ameniachia khiari kwa kunambia: Uwaombee msamaha, (au) usiwaombee msamaha: hata kama utawaombea msamaha mara sabiini... (Sura 9:80) Kwa hivyo nitaomba zaidi ya mara sabiini. Umar akamjibu: Lakini yeye (Abdalla bin Ubayy) ni mnafiki! 15 Hata hivyo, Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alimswalia 16 ndipo Mwenyezi Mungu alipoteremsha: 17 Wala usimswalie yoyote atakayekufa miongoni mwao, wala usisimame kwenye kaburi lake. (Sura 9:84) Tatu ni yale yanayoelezwa katika Hadith Na. 50 iliyomo uk wa Juzuu ya Kwanza ya Kiingereza ya Sahih Muslim. 18 Hadith hiyo inasimulia ujumbe ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alimpa Abu Huraira kwa kumpa bishara mtu yoyote atakayekutana naye, ambaye anashuhudia kwamba hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu, kuwa ataingia Peponi. Abu Huraira anasema katika Hadith hiyo: Mtu wa kwanza niliyekutana naye alikuwa ni Umar. Akaniuliza: Ni viatu gani hivyo, ewe Abu Huraira? Nikamjibu: Hivi ni viatu vya Mtume wa Mwenyezi Mungu ambavyo amenipa ili kwavyo nimbashirie yoyote nitakayekutana naye, ambaye anashuhudia kwamba 14 Angalia ujasiri huo! Mtume hapo ni nani; ni Muhammad s.a.w.w. au ni Umar?! 15 Kwa hivyo Umar alikuwa na ghera zaidi na dini kuliko Mtume wa Mwenyezi Mungu? 16 Kwa kitendo hicho cha Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w., cha kuendelea na kuswali, mkosa ni nani? Ni Mtume wa Mwenyezi Mungu au ni Umar? 17 Kwa hivyo Umar amepata, Mtume s.a.w.w. amekosa! Astaghfirullah. Maneno gani haya? Wala si kisa hiki tu. bali kuna na vyengine vinavyosimuliwa vitabuni ambavyo ni vya kumtweza Bwana Mtume s.a.w.w. mbele ya Umar!! 18 Kwa Kiarabu ni Kitaabul Iimaan, Mlango wa Man Laqiyal Laaha Bil Iimaan... 10

16 hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu, akiwa na yakini ya hilo moyoni mwake, kwamba ataingia Peponi. Hapo Umar akanipiga kituani nami nikaanguka kingalingali 19 Kisha akanambia: Rejea, ewe Abu Huraira. Kwa hivyo nikarejea kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. na huku machozi yananilengalenga. Umar naye akanifuata nyuma. Hapo tena Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akaniuliza: Una nini, ewe Abu Huraira? Nikamjibu: Nilisadifu kukutana na Umar, nikampa ule ujumbe ulionituma kuutoa. Lakini yeye alinipiga kifuani, nikaanguka kingalingali, na akaniamrisha nirejee. Kusikia hivi, Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akamuuliza: Ni nini lililokufanya ufanye hilo, ewe Umar? Yeye akajibu: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mamangu na babangu watolewe fidia kwa ajili yako! Ulimtuma Abu Huraira na viatu vyako kumbashiria yoyote atakayekutana naye, na ambaye anashuhudia kwamba hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu, akiwa na yakini ya hilo moyoni mwake, kwamba ataingia Peponi? Mtume s.a.w.w. akajibu: Ndio! Umar akamwambia: Tafadhali usifanye hivyo 20 maana ninaogopa kwamba watu wataliamini hilo peke yake. Waache waendelee kufanya mema. Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akasema: Haya, waachie. 21 Kutokana na Hadith tulizozinukuu hapo juu, ni wazi kwamba haikuwa mara ya kwanza Umar kumpinga Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. katika hilo tukio la karatasi. Alitangulia kumpinga mara kadhaa kabla ya hapo, na hata baada ya Mtume s.a.w.w. kutawafu! Jee, mjumbe huuwawa? Kosa la Abu Huraira hapo ni lipi hata apigwe hivyo? 20 Ho! Mtume wa Mwenyezi Mungu anakatazwa kufanya jambo na asiyekuwa Mtume, tena baada ya Mtume mwenyewe kutoa amri hiyo?! Basi Mtume hapo ni nani; ni Muhammad au ni Umar? Soma tena Sura 10: Kwa hivyo uamuzi ni wa Umar! Linakubalika hilo? Mtume s.a.w.w. tumweke wapi hapo? Soma Sura 49:1; 33:36; na 4: K.m. aliziondoa mut a mbili: ya hijja na ya ndoa; alizifanya talaka tatu ni tatu: alizua swala ya tarawehe kwa jamaa, na mengineyo ambayo - kwa dhiki ya nafasi - hatuwezi kuyataja yote. 11

17 Sasa tuangalie sababu yake ya nne inayosema: (iv.) Inashangaza zaidi kuwataja maswahaba kuwa waweza kumpinga Mtume s.a.w.w. katika Utume wakati huu akiwa katika kitanda cha mauti. Jibu: Hilo ni kwa ambaye labda hajayasoma yaliyoandikwa vitabuni. Lakini kwa aliyesoma. hilo si geni wala halishangazi asilan. Hapa tutaja mifano miwili tu: Mmoja ni ule wa Suluhu ya Hudaybiya tuliyoitaja chini ya majibu (i) hapo juu (uk. 8). Katika Hadith ndefu sana (Hadith Na. 891) iliyomo uk wa Juzuu ya Tatu ya tafsiri ya Kiingereza ya Sahih Bukhari 23 muna kipande hiki:... Alipomaliza kuandika huo mkataba wa Suluhu, Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alipowambia maswahaba wake: Simameni, muchinje (wanyama wenu), halafu munyoe (vichwa vyenu). Wallahi, hakuna mtu aliyesimama. Akatoa amri hiyo mara tatu! Ilipokuwa hakusimama yoyote, (Mtume s.a.w.w.) aliingia kwa Ummu Salama akamtajia yaliyomkuta kwa watu wake... Hayo! Tunaona hapo Mtume s.a.w.w. alivyowaamrisha maswahaba wake, na wao wakamwasi. Akawaamrisha mara tatu, na mara zote tatu wakamwasi, mpaka akamshtakia mke wake? Jee! Hapa bado lipo la kumshangaza mwandishi wetu? Mfano wa pili ni ule wa maswahaba kumkataa na kumtia aibu kiongozi aliyeteuliwa na Mtume s.a.w.w. Hayo yamo katika Hadith Na. 552 iliyomo uk. 387 wa tafsiri ya Kiingereza ya Juzuu ya Tano ya Sahih Bukhari 24 isemayo: Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. alimteua Usama kuwa amiri wa watu. Wakambeza 23 Kwa Kiarabu ni Kitaabush Shuruutwi, Mlango wa Ash Shuruutwi Fil Jihaadi Wal Muswaalaha Kwa Kiarabu ni Kitaabul Maghaazii, Mlango wa Ghazwati Zayd Bin Haaritha. 12

18 katika uamiri wake. Mtume s.a.w.w. akasema: Mkiubeza uamiri wake (hapana la ajabu), maana mumekwisho kuubeza uamiri wa babake 25 kabla. Ninaapa kwa Mwenyezi Mungu! Yeye alistahiki kuwa amiri, na alikuwa kipenzi changu mno. Na huyu (Usama) ni kipenzi changu mno baada yake. Jee! Baada ya ushahidi kama huo hapo juu, bado mtu hushangazwa na tukio la karatasi? Hao waliowabeza walioteuliwa na Mtume s.a.w.w. kuwa maamiri - mtu na babake - ni kina nani? Sio maswahaba? Tatu ni lile jeshi ambalo lilikuwa liongozwe na Usama tuliyemtaja hapo juu, wakati Bwana Mtume s.a.w.w. alipokuwa mgonjwa. Vitabu vya historia 26 vinatueleza kwamba - na hapa tunaeleza kwa mukhtaswari tu - Mtume Muhammad s.a.w.w. aliliandaa jeshi la kwenda kuwashambulia Warumi. Jeshi hilo lilikuwa lishiriki katika mashambulizi ya mwisho katika zama za uhai wa Mtume s.a.w.w. Miongoni mwa muhaajir na ansaar wakubwa wakubwa waliokuwamo humo ni Abu Bakar, Umar, Abuu Ubayda, Sa d b. Abii Waqqaas, Qatada b. Nu man, Salama b. Aslam na mfano wao. Ili kuwapa moyo maswahaba wake, na kuzidi kuwahimiza, Mtume s.a.w.w., yeye mwenyewe alilishughulikia jeshi hilo. Tarehe 26 Swafar, mwaka wa 11H, jeshi hilo liliundwa. Siku ya pili asubuhi, tarehe 27 Swafar, alimwita Usama akamwambia: Nenda kule alikouliwa babako. 27 Wakanyagekanyage kwa kwato za farasi. Mimi nimekuteua wewe amiri wa jeshi hili. Washambulie 25 Babake alikiitwa Zayd b. Haaritha. Yeye aliteuliwa na Mtume Muhammad s.a.w.w., pamoja na wenziwe wawili (Ja far b. Abii Twalib na Abdalla b. Rawaaha), kuongoza jeshi la kupambana na Warumi katika mwaka wa 8 H. Uamiri huo ndio alioukusudia Mtume s.a.w.w. kwa maneno yake hayo. 26 Kama Twabaqaat ya Ibn Sa d. Al Kaamil ya Ibn Athir, Siiiratul Halabiyya, Siiratun Nabawiyya ya Zayn Dahlan, Taartikhut Ya quubii, Taarikhut Twabari. 27 Yaani Ubna. Taz. Na. 28 hapa chini. 13

19 watu wa Ubna 28 asubuhi. Pandeni farasi wanaokwenda shoti. Fanyeni haraka kwenda huko kabla khabari za kufika kwenu hazijafika huko. Mwenyezi Mungu akijaalia kuwashinda, msikae sana huko. Chukua watu wa kukuongoza njia, na tanguliza wapelelezi, majasusi na watu wa kukuletea habari. Tarehe 28 Swafar, Mtume s.a.w.w. akaanza kushikwa na maradhi ambayo ndiyo atakayokuja kufia. Alishikwa na homa kali na kichwa kumuuma. Kulipokucha tarehe 29 Swafar, na akaliona jeshi hilo bado halijaondoka, Mtume s.a.w.w. alilitokea na kulihimiza liondoke mara moja. Ili kuwatia mori na kuwapa moyo, Mtume s.a.w.w. yeye mwenyewe aliifunga bendera akampa Usama kwa mkono wake mtukufu. Kisha akamwambia: Shambulia kwa jina la Mwenyezi Mungu na katika njia ya Mwenyezi Mungu. Na pigana na wasiomwamini Mwenyezi Mungu. Usama akatoka na hiyo bendera akampa Buraida. Jeshi likaondoka, likenda nje ya Madina. Likapiga kambi mahali paitwapo Jurf. Tena lilikaa hapo bila ya kuondoka, kinyume na amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. Hapo ndipo baadhi ya maswahaba walipoutaaradhi uteuzi wa Usama kama amiri-jeshi wao. Kitendo hicho kilimkasirisha mno Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. hata ikambidi atoke nyumbani kwake na kwenda msikitini huku amejifunga kitambaa cha kichwa na kujigubika shuka yake mwili mzima kwa homa aliyokuwa nayo! Hapo ilikuwa ni Jumamosi, tarehe 10 Rabi ul Awwal (Mfungo Sita), siku mbili tu kabla ya kutawafu kwake. Alipofika msikitini alipanda mimbari, akasema maneno kama yale tuliyoyanukuu katika mfano wa pili hapo juu. 28 Ubna ni mahali karibu na Balqa huko Sham (Syria). Iko baina ya Asqalaan na Ramlah karibu na Mau tah. 14

20 Baada ya kutoa khutba hiyo, aliwahimiza tena maswahaba waondoke bila ya kuchelewa. Nao wakaagana naye na kurejea kambini kwao, huko Jurf. Aliendelea kuwahimiza wasichelewe kuondoka mpaka ugonjwa wake ukamzidi. Hata hivyo, aliendelea kuyarudia rudia maneno yake ingawa maswahaba nao, kwa upande wao, waliendelea kutotwii! Siku ya pili, tarehe 12 Rabi ul Awwal, Usama akenda nyumbani kwa Mtume s.a.w.w. kutoka kambini kwake. Kwa mara nyengine tena Mtume s.a.w.w akamwambia: Ondoka mapema asubuhi kwa baraka za Mwenyezi Mungu aliyetukuka. Hapo wakaadiana, naye akarejea kambini. Kisha akarejea ameandamana na Umar na Abuu Ubayda. Walipofika kwa Mtume s.a.w.w., walimkuta yu katika sakaratil mawti. Akatawafu siku hiyo hiyo: na jeshi likarejea Madina na bendera yao! Jee! Ni nani hao walioasi amri ya Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. mpaka pumzi zake za mwisho? Sio maswahaba? Kwa mifano miwili hiyo, ni matumaini yangu kwamba mwandishi wetu huyo hatashangaa tena anapoambiwa kwamba maswahaba wanaweza kumpinga, na kwa kweli walimpinga, Mtume katika Utume wakati akiwa katika kitanda cha mauti. Sasa tujadili sababu yake ya tano kwamba: (v.) Kwa kuwa Mtume s.a.w.w. aliishi siku nne zaidi baada ya tukio hilo akiwa katika hali isiyo mbaya sana hata Abu Bakar akarudi kitongojini kwake, kulipokuwa na umbali wa maili mbili hivi kutoka mjini Madina... kwa nini basi usia huu usiandikwe? Jibu: Mmoja kati ya wanazuoni waliolijadili tukio hili, katika 15

21 majadiliano yake na aliyekuwa Mufti wa Al-Azhar wa wakati huo (Sheikh Salim al-bishri), alilijibu swali hilo 29 hivi: Sababu ya Mtume s.a.w.w. kutoandika wasia huo baada ya hapo, ni kwamba maneno yao hayo yalimuhuzunisha hata ikambidi asiuandike. Maana lau angeliuandika, matokeo yake yangelikuwa ni fitina na ikhtilafu kuendelea baada ya hapo, kwa kuulizana: Alipouandika, jee alikuwa amepiswa au la? kama walivyokhitalifiana na kuleta zogo mbele yo macho yake. Hivyo, hakuwa na la kufanya isipokuwa kuwambia: Niondokeeni! kama ulivyoona hapo juu. Lau angelishikilia kuuandika, na akauandika, basi wangelirejelea neno lao la kupiswa na wafuasi wao wangeliendelea kutaka kuthubutisha kwamba kweli alikuwa amepiswa - Mwenyezi Mungu apishe mbali. Hivyo wangeliyarikodi hayo katika nganu zao, wakayajaza katika magombo yao, kuwa ni majibu ya maandishi hayo na kwa yoyote anayeyatolea hujja. Kwa ajili hiyo, kwa hikima kubwa, Mtume s.a.w.w. aliamua kuacha kuuandika ili wale wapinzani wake, na waunga-mkono wao, wasije wakaufungua mlango wa kuubezea Utume - Mwenyezi Mungu apishe mbali. Pia Mtume s.a.w.w. alikuwa na hakika kwamba Ali, na wanaomuunga mkono, watayafuata yaliyokusudiwa kuandikwa humo - yaandikwe ama yasiandikwe - na wasiokuwa wao wasingeliyatendea kazi wala kuyatia maanani hata kama yangeliandikwa. Katika hali kama hiyo, kwa hivyo, hikima ililazimisha iachwe kuuandika kwa sababu usingelikuwa na athari yoyote, baada ya upinzani wote huo, isipokuwa kuzuka fitina, kama ilivyo wazi. Hayo ndiyo majibu ya Sayyid Abdulhusein Sharafud Din al-muusawi kwa mufti huyo wa Al-Azhar yaliyomo katika Barua Na. 86 katika kitabu chake kiitwacho Al-Muraaja at. Kitabu hicho 29 Suali hiyo ilikuwamo katika barua Na. 85 iliyochapishwa katika uk. 257 wa Al-Muraaja at (uk. 380 wa The Right Path). 16

22 pia kina tafsiri yake ya Kiingereza iitwayo The Right Path. 30 Hapa tungependa ieleweke kwamba, kwa miaka kadhaa kabla ya Mtume s.a.w.w. kuugua mpaka baada ya hijja yake ya mwisho, alikuwa ameshawausia Waislamu japokuwa ni kwa mdomo - kwamba wasii wake baada ya yeye kutawafu ni Ali b. Abi Twalib. Hayo tutayaona kwa tafsili katika kitabu chetu kinachofuatia hiki, kinachoitwa Wasia wa Mtume Muhammad s.a.w.w. Kama, baada ya Hadith zote hizo tutakazozitaja (zilizotasua na zilizoashiria tu), wapinzani wa Imam Ali a.s. hadi hii leo hawajakosa taawili na vipengee vyengine vya kuzikatalia, pana hakika gani kwamba, hata kama huo wasia ungeliandikwa, mambo yangelikuwa tafauti? Hivyo, hujja ya Sayyid Sharafud Din hapo juu, ni sawa kabisa. Ikumbukwe kwamba pale Mtume s.a.w.w. alipotangaza mbele ya halaiki ya maswahaba wasiopungua 90,000 (kwa tafsili tiz. Wasia wa Mtume Muhammad s.a.w.w.), wakiwamo Abu Bakar na Umar, kuwa Ali ndiye atakayeshikilia uwongozi wa Waislamu baada yake, si mwengine bali ni Khalifa Umar aliyemwendea Imam Ali a.s. akamkongowea kwa kumwambio: Hongera! Hongera! Ewe mwana wa Abu Twalib! Umekuwa mtawalia mambo yangu na mtawalia mambo ya kila muumini mwanamume na mwanamke. Kisha Umar yuyo huyo, mara tu baada ya Mtume s.a.w.w. kufariki dunia, ndiye aliyekuja kupendekeza Abu Bakar achaguliwe kuwa Khalifa wa Kwanza! Subhaanallah. Sasa tujadili sababu yake ya sita isemayo: (vi.) Mbaya zaidi ni tukio hili linavyonasibishwa na maudhui ya Sura 49:1-3 hali sura hiyo ilishushwa zamani kabla ya tukio la karatasi. 30 Wale wasiojua Kiarabu, wanaojua Kiingereza, ni muhimu wakisome kitabu hicho. Wanaweza kukipata katika ofisi yoyote ya Bilal Muslim Mission ya Dar es Salaam, Nairobi au Mombasa. 17

23 Jibu: Hebu kwanza tutizame sura hiyo inasemaje. Kwa tafsiri ya hizo aya tatu za kwanza, inasema hivi: Enyi mlioamini! Msitangulize lolote lenu mbele ya la Mwenyezi Mungu na Mtume Wake! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mjuzi. Enyi mlioamini! Msiinue sauti zenu juu ya sauti ya Mtume, wala msiseme naye kwa sauti ya nguvu kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, zisije amali zenu zikapomoka na hali hamutambui. Kwa hakika wale wanaoziangusha sauti zao mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amezisafisha nyoyo zao kwa ucha-mungu. Wao watapata maghufira na malipo makubwa. Kwa kweli, hakuna mwanachuoni yoyote - wa Kisunni wala wa Kishia - anayezinasibisha aya hizo na tukio la karatasi kwa kusema kwamba ziliteremshwa wakati wa tukio hila. Wanazuoni wote wanakubali kwamba aya hizo zilishuka kabla sana ya tukio hilo. Hata hivyo wanazitaja aya hizo katika fuo la tukio hilo, hufanya hivyo tu kuonyesha kwamba aya hizo, khaswa mbili za kwanza, hazikutiwa maanani wakati wa tukio hilo. Maana tumeona katika Hadith tulizozinukuu huko nyuma kwamba maswahaba walizozana na kuleta zogo mpaka Mtume s.a.w.w. akawafukuza! Jee, mahali penye kundi la watu (kama hao waliokuwako nyumbani kwa Mtume s.a.w.w.), pakatokea mzozo na zogo, huweza kuwa hivyo bila ya hao wanaozozana kupandishiana sauti zao? Hasha! Hivyo kitendo chao hicho si kinyume na aya ya pili ya sura hiyo? Basi pana ubaya sana gani hapo panaposemwa kwamba, kwa kuzozana kwao na kufanya zogo mbele ya Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. akiwa mgonjwa kitandani, maswahaba hao waliasi amri ya Mwenyezi Mungu ya kutoinua sauti zao mbele ya Mtume Wake? Uamuzi tunakuachia wewe, msomaji mtukufu. Mwisho, tuijadili sababu yake ya sabaa isemayo: (vii.) Baya kuliko yote yaliyokwishatajwa ni kumsingizia 18

24 Mtume (s.a.w.w.) kuwa amepoteza fahamu. Jibu: Lakini aliyemsingizia Mtume s.a.w.w. kuwa amepoteza fahamu au amepiswa sio sisi. Ni Umar b. Khattaab! Hivyo ndivyo Sahih Bukhari na Sahih Muslim zinavyosema. Wala hilo siyo baya hivyo ukilinganisha na mengine yaliyomo katika Sahih Bukhari kuhusu Mtume s.a.w.w. kupoteza fahamu! Kuna makubwa na mabaya zaidi kwa mno! Hapa chini nitatoa mifano miwili tu: Wa kwanza ni ule wa Hadith Na. 823 iliyomo uk wa Juzuu ya Tatu ya tafsiri ya Kiingereza ya Sahih Bukhari, 31 isemayo kwamba imepokewa kwa Bibi Aisha r.a kwamba amesema: Mtume s.a.w.w. alimsikia mtu anasoma (Qur ani) msikitini, nikasema: Mwenyezi Mungu amrehemu. Amenikumbusha aya kadhaa ambazo nimezisahau za sura kadhaa..! Jee! Unayaonaje hayo? Ni madogo? Ya Mtume s.a.w.w. kuzisahau aya za Qur ani? Si hatari hiyo? Riwayo kama hiyo imo pia katika Hadith Na. 347 iliyomo katika uk wa Juzuu ya Nane ya hiyo hiyo tafsiri ya Sahih Bukhari. 32 Wa pili ni ule wa Hadith Na. 490 iliyomo uk. 317 wa Juzuu ya Nne ya tafsiri ya Kiingereza ya Sahihi Bukhari 33 isemayo kwamba imepokewa kwa Bibi Aisha r.a. kwamba amesema: Mtume s.a.w.w. alirogwa mpaka akawa anatakhayali 34 kuwa anafanya kitu wala hakifanyi...! Hadith kama hiyo utaipata pia katika uk wa Juzuu ya Sabaa (Hadith Na. 658), 35 na uk wa Juzuu ya Nane (Hadith Na. 400) ya hiyo hiyo Sahih Bukhari Kwa Kiarabu ni Kitaabush Shahaadaat, Mlango wa Shahaadatil A maa wa Nikaahihii Kwa Kiarabu ni Kitaabud Da awaat, Mlango wa Waswalli Alayhim Kwa Kiarabu ni Kitaabu Bad il Khalq, Mlango wa Swifati Iblisi wa Junuudihii Anahisi bila ya kuwa kweli; anaota hali yu macho. 35 Kwa Kiarabu ni Kitaabut Twibbi, Mlango wa As Sihri Kwa Kiarabu ni Kitaabud Da awaat, Mlango wa Takriirid Du aai. 19

25 Pia imepokewa kwa Bibi Aisha, katika hiyo hiyo Sahih Bukhari, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu alirogwa mpaka akawa hudhania kwamba anawaingiliya 37 wake zake hali hawaingilii Sufyan akasema: Huwo ulikuwa nl uchawi mkali mno. Hiyo ni Hadith Na. 660 iliyomo uk. 443 wa Juzuu ya Sabaa 38 ya tafsiri ya Kiingereza. Pia taz. Hadith Na. 89 iliyomo uk wa Juzuu ya Nane. 39 Basi kama mwandishi wetu huyo anaona lililo baya kuliko yote... ni kumsingizia Mtume s.a.w.w. kuwa amepoteza fahamu wakati alipokuwa mgonjwa (na hayo yalisemwa na Umar bin Khattaab), atasemaje kuhusu yaliyosimuliwa na Bibi Aisha (mke wa Mtume s.a.w.w) kuwa Mtume s.a.w.w. - akiwa si mgonjwa, bali mzima na afya yake - alizisahau baadhi ya aya za Qur ani, na kwamba alikuwa akiota anafanya mambo fulani hali hayafanyi?! Lipi lililo kubwa zaidi hapo? Mwandishi wetu huyo anasema katika toleo la 170 la hilo gozeti la An-Nuur (uk. 7): Hakuna ushahidi wa kutosha kama tukio hili (la karatasi) limetokea kweli au ni maandishi tu yenyewe yaliyopachikwa ili kukidhi hoja ya waliyobuni tamko hili. Kama ni hivyo tungependa tuambiwe ni nani huyo aliyeyapachika maneno hayo? Ni Ibn Abbas? Ni hao waliopokea kwake? Ni Bukhari? Ni nani? Na ni ipi hiyo haja yao waliyotaka ikidhiwe? Mpaka hapa tumeshazijadili sababu zote sabaa alizozitoa mwandishi wetu huyo kukatalia ukweli wa tukio la karatasi, na kutoa majibu yetu. Lililobakia sasa ni uamuzi wako msomaji mtukufu kwamba zimejibika sababu hizo au hazikujibika. Kazi kwako! 37 Yaani anawajamii. 38 Kwa Kiarabu ni Kitaabut Twibbi, Mlango wa Ash Shirki Was Sihri Kwa Kiarabu ni Kitaabul Adab, Mlango wa Innal Laaha Ya muru Bil Adli Wal Ihsaani... 20

26 Uchambuzi wa Hadith ya Karatasi Katika kuichambua Hadith hii, kuna mambo matatu muhimu yanayojitokeza ambayo ingependeza tuyajadili: (i.) Kitendo cha kumzuilia Mtume s.a.w.w. kuandika wasia wake, na athari yake. (ii.) Kauli ya Umar b. Khattwaab kwamba kinatutosha sisi Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na athari yake. (iii.) Mzozo na zogo la maswahaba mbele ya Mtume s.a.w.w., na athari yake. MTUME KUZUILIWA KUANDIKA WASIA Hapana ajabu yoyote Mtume s.a.w.w kuugua, maana yeye ni binadamu. Na binadamu kuugua ni maumbile yake. Lakini, pamoja na kuugua kote huko, hakusita kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, wala hakusita kuwa kiongozi wa Waislamu. Hivyo aliendelea kuwa na haki ya kutekeleza wajibu wake wa utume na uwongozi bila ya mtu yoyote kuwa na mamlaka ya kumzuiya kufanya hivyo. Tunapotizama sharia na mila za watu wote duniani tunaona kwamba mgonjwa ana haki ya kuusia kwa kusema analotaka, na kwamba wale waliopo mbele zake wana wajibu wa kumkubalia hilo, na kusikiliza atakayoyasema. Baada ya hapo wanayo hiari: ya kufuata na kutekeleza huo wasia wake, au kuupuuza. Lakini kumzuilia mgonjwa kusema alitakalo, au kumchagiza mpaka ashindwe kuandika wasia wake, na kuwazuilia watu wake kufaidika nao; hilo ni kioja, halina mfano wake katika historia ya binadamu wowote. Lakini jee! Unajua ni mgonjwa gani huyo aliyenyimwa haki yake hiyo? Sio mtu wa kawaida. Ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kiongozi wa umma wa Kiislamu, Muhammad b. Abdillahi s.a.w.w.! 21

27 Jee! Unajua walitoa kisingizio gani cha kumzuilia kuandika wasia wake? Walisema kwamba alikuwa amezidiwa na maradhi. Hivyo walimuhurumia na hawakutaka kumkalifisha! Lakini walisahau kwamba - kwa kuzozana kwao mbele zake, na kuleta zogo - tayari walikuwa wameshampa taklifu, hata ikambidi awafukuze! Pia walisema kuwa amepiswa (Mwenyezi Mungu apishe mbali)! Lakini walisahau kwamba Mwenyezi Mungu ametuhakikishia kwamba Mtume s.a.w.w. hasemi anayoyasema kwa matamanio yake, isipokuwa huwa ni wahyi alioteremshiwa (Sura 53:3-4). Wakasahau pia, kama alivyonukuu Ibn Sa d 40 kwamba mara nyingi ambazo Jibril a.s. alikuwa akimwendea Mtume s.a.w.w. ni alipokuwa ni mgonjwa! Tuyalinganishe na ya Khalifa Abu Bakar Mtume wa Mwenyezi Mungu aliugua; na Abu Bakar naye akaugua. Mtume wa Mwenyezi Mungu alizungumza yu mgonjwa; na Abu Bakar naye alizungumza akiwa mgonjwa. Abu Bakar alizidiwa na maradhi mpaka akazimia na kupotewa na fahamu! Mtume wa Mwenyezi Mungu naye alizidiwa na maradhi, lakini hakuzimia na wala hakupotewa na fahamu. Na kwenye maradhi ya wote wawili Umar alikuwako. Lakini Mtume wa Mwenyezi Mungu alipotaka kuusia, Umar alisema: Kinatutosha sisi Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu amezidiwa na ugonjwa. Amepiswa. Lakini kwa Abu Bakar haikuwa hivyo. Yeye alipotaka kuandika wasia wake, Umar alisema: Enyi watu! Sikilizeni na mlitwii neno la Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu. Haya! Huyu hapa Muhammad: Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na huyu hapa Abu Bakar: swahaba wake. Mtume wa Mwenyezi Mungu ndiye kiongozi na raisi wa dola. Na Abu Bakar pia ni kiongozi na raisi wa dola, lakin! baada ya Mtume wa Mwenyezi 40 Al Khutwatus Siyaasiyya Litawhiidil Ummatil Islaamiyya Cha Ustadh Ahmad Husayn Ya qub, uk

28 Mungu s.a.w.w. Vipi basi Abu Bakar anaruhusiwa kuandika na kusema anayoyataka akiwa ni mgonjwa, na Mtume s.a.w.w anazuiliwa na mtu huyo huyo - kuandika au kuyasema anayoyataka? Si ajabu hiyo? Abu Bakar aliandika, na aliyoyaandika yakapokewa kwa sharafu na taadhima, na kutekelezwa yote neno kwa neno. Lakini ya Mtume wa Mwenyezi Mungu yakapingwa, alipotaka kuyaandika, pamoja na kwamba aliyoyataka kuyaandika yeye yalikuwa na hakikisho kwamba hatutapotea baada yake abadan!! Kweli, duniani kuna mambo!! Kuna na ya Khalifa Umar Kama inavyojulikana katika historia, 41 Khalifa Umar bin Khattaab alidungwa jambia. Twabibu wake akasema: Sidhani kama utaishi. Kama unalo ulilotaka kulifanya, lifanye. Hapo akamwita mwanawe, Abdalla, akamwambia: Niletee mfupa wa bega. Akaufuta. Kisha akasema kwa kuzidiwa na maradhi: Lau kama ningelikuwa na vyote vilivyochwelewa na jua ningelijikomboa kwavyo na khofu ya mauti. Hapo kichwa chake kilikuwa mapajani mwa mtoto wake, Abdalla. Akamwambia mwanawe: Liweke shavu langu juu ya ardhi, usiyekuwa na mama wee! Ole kwa Umar, na mama Umar kama Mwenyezi Mungu hatamsamehe Umar! 42 Lakini, pamoja na kuumwa kote huko, Umar alitoa wasaa wake, akaratibu kundi la shuura, akahakikisha kwamba Uthman bin Affaan atakuwa khalifa baada yake, akahakikisha kwamba hakuna Bani Hashim atakayekuwa kiongozi wa watu, na akaamrisha kukatwa kichwa yoyote atakayekwenda kinyume na wasia huo! Al Imaama Was Siyaasa ya Ibn Qutayba, uk. 21 na 22. Twabaqaat Ibn Sa d, Mjallada wa pili, uk An Nidhwaamus Siyaasiy ya Ustadh Ahmad Husayn Ya qub, uk Twabaqaat Ibn Sa d, Juz. 3, uk

29 Swali yetu hapa ni: Vipi iliruhusiwa Umar kuandika alilotaka kuliandika, na kulisema alilotaka kulisema, bali na kuliusia, hali amezidiwa na maradhi na yu karibu na kufariki, na wasia wake ukatekelezwa bila ya mtu yoyote kumtaaradhi au kumzuia asiuandike, wakati ambao Mtume wa Mwenyezi Mungu alizuiwa kuandikwa wasia wake kwa kisingizio cha kuzidiwa na maradhi, na kwamba Qur ani peke yake inatosha? Ajabu! Athari mbaya za kitendo hiki Kitendo hiki cha kumzuia Mtume s.a.w.w. kuandika wasia wake kilileta na kuacha athari mbili mbaya kwa Waislamu: (i) Kiliwagawanya. Kabla ya hapo, Waislamu walikuwa kitu kimoja. Wote walikuwa wakimfuata Mtume Muhammad s.a.w.w. kama kiongozi wao, na ruwaza njema kwao. Hakuna aliyethubutu kuipinga amri yake kwa sababu kufanya hivyo ni kinyume na mafunzo ya Qur ani (Sura 59:7). Lakini baada ya Umar kuzuia watu wasimletee Mtume s.a.w.w. alichotaka, Waislamu waligawanyika makundi mawili. Kundi moja ni Iile lililomtwii Mtume s.a.w.w. kwa kusema kwamba apawe alichotaka. Jengine ni lile la Umar bin Khattaab: lililomsikiliza yeye na kutompa Mtume s.a.w.w. kile alichotaka! Na makundi hayo yangaliko hadi hii leo! Shia wanashikilia kwamba lilikuwa ni kosa kubwa kwa Umar bin Khattaab kuzuia watu kumletea Mtume wa Mwenyezi Mungu kile alichokitaka. Sunni hawaoni hivyo, bali hutoa nyudhuru mbalimbali za kutetea usawa wa Umar kufanya hivyo. (ii) kufungua mlango wa kuamini kwamba ziko hali fulani ambapo Mtume s.a.w.a. anaposema neno katika hali hizo, haipasi kufuatwa! Hili nalo limewagawanya Waislamu vile vile. Wale wanaompinga Umar hawakubali hilo. Wao wanaamini kwamba Mtume wa 24

30 Mwenyezi Mungu s.a.w.w hasemi neno lolote kwa matamanio yake (Sura 53:3). Neno lake si la mshairi wala la kuhani (Sura 69:41-42). Wala yeye si mwendawazimu (Sura 81:22). Analolisema huwa linatokana na wahyi alioteremshiwa (Sura 53:4). Kwa hivyo, awe na furaha au hasira, hasemi isipokuwa haki. 44 Kwa ajili hii yeye ni ma sum: hafanyi dhambi wala kosa, wala hasahau. Lakini wale wanaomuunga mkono Umar, wao hawaamini hivyo. Kwa kukubali usawa wa kitendo cha Umar katika hiyo Hadith ya karatasi, vitabu vyao vimejaa Hadith za kuthubutisha kwamba Mtume s.a.w.w. sio ma sum! Alikuwa akikosea! Akisahau! Wakati mwengine akikosolewa hata na maswahaba wake! Kwao wao, yote hayo si mambo ya kushangaza! KITABU CHA MWENYEZI MUNGU KINATOSHA Baada ya kuzuia Mtume s.a.w.w. kupawa karatasi ya kuandikia wasia wake, kama tulivyoona katika Hadith tulizozitaja hapo juu (uk. 3-5 ). Umar bin Khattaab alitoa udhuru wake kwa kusema Sisi tunacho Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Kinatutosha! Lakini, kusema kweli, hivyo ndivyo? Jibu ni la! Sivyo! Wala haingii akilini kuwa hivyo. Kitabu cha Mwenyezi Mungu ni kitabu. Kinahitajia kufafanuliwa. Kwa hivyo kinahitajia mfafanuzi wa kutufafanulia makusudio ya Mwenyezi Mungu. Lau ingelikuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu, choo peke yake, kinatosha kututatulia matatizo ya binadamu, pasingelikuwa na haja ya kutumwa mitume na manabii. Ingelitosha tu, Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu kututeremshia nakala za Kitabu Chake kutoka mbinguni, kwa njia anayotaka. Lakini hilo hakulifanya hata mara 44 Musnad Ahmad, Juz. 2, Uk. 162 na

31 moja. Alilofanya ni kuteua Mtume, halafu akamteremshia Kitabu Chake na kumpa wadhifa wa kuwafafanulia wafuasi wake yale yaliyokusudiwa na Mola wao. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa hata kwa Mtume Muhammad s.a.w.w. (Sura 16:44) Kwa hivyo kutokana na mpango huo, ni wazi kwamba ufafanuzi wa Mtume - Mtume yoyote - hauwezi kutengwa na ujumbe wa Mwenyezi Mungu aliotumwa kutuletea. Maana vilivyo ni kwamba yeye (Mtume) ndiye anayejua na kufahamu zaidi kanuni za Ujumbe huo kuliko yoyote, na ufafanuzi wake wa Ujumbe huo huwa ndio hasa makusudio ya Mwenyezi Mungu. Kwa wako hilo basi, tunaona kwamba Kitabu hakikwasiki na Mtume, kama ambavyo Mtume hakwasiki na Kitabu. Kila mmoja anamhitajia mwenziwe ili mambo yakamilike. Maana kumtwii Mtume ndiko kumtwii Mwenyezi Mungu, kama ambavyo kumwasi Mtume ndiko kumwasi Mwenyezi Mungu (Sura 4:80). Kama tunavyoelezwa na historia, Muhammad s.a.w.w. ndiye aliyeongoza ulingano wa Mwenyezi Mungu kwa muda wa miaka 13. Na ulingano huo ulipoingia kipindi cha kuwa dola, yeye ndiye aliyekuwa raisi wa dola hiyo kwa muda mwengine wa miaka 10. Hivyo Uislamu ukawa si maneno matupu, bali na harakati pia; wala si nadharia tupu, bali na utendwa-kazi pia. Kutokana na maelezo hayo basi, maadamu dini ni: (i.) Kitabu kilichoteremshwa na Mwenyezi Mungu, (ii.) Mtume aliyetumwa na Mwenyezi Mungu; vipi tutatosheka na Kitabu bila ya Mtume s.a.w.w.? Kwa mantiki gani? Kwa mfano, lau bedui angelimwendea Mtume s.a.w.w. akamwambia: Mimi ninakikubali Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na ninashikamana na kila kilichomo humo; bas! Sipendelei kupokea chochote chengine kwako, kwa sababu Qur ani peke yake inanitosha! Bila shaka yoyote Mtume s.a.w.w. angelimjibu kwa 26

32 kumuhurumia: Ewe ndugu! Hutaweza kuifahamu Qur ani na makusudio yake bila ya ufafanuzi wangu. Na kama bedui huyo atashikilia lilo hilo lake, ni wazi kabisa kwamba Mtume s.a.w.w. abadan hatamkubalia! Maana Qur ani, na ufafanuzi wa Mtume wayo, ni pande mbili za sarafu moja. Kwa mfano, pamoja na kuwa swala ni nguzo kubwa ya dini, kwa kutosheka na Qur ani peke yake huwezi kujua namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake, umbo lake.. Kuweza kuyajua hayo yote, utahitajia ufafanuzi wa Mtume s.a.w.w. Na vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa hukumu na kanuni nyingi nyenginezo. 45 Kwa hivyo maneno aliyoyasema Umar bin Khattaab siku hiyo, kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinatutosha, ni maneno ambayo hayaingii akilini, mbali na kwamba yanapingana na maneno ya Mwenyezi Mungu Mwenyewe 46 pamoja na Mtume Wake s.a.w.w. 47 Matokeo mabaya ya maneno hayo Maneno hayo hayakubaki ni maneno ya mdomo tu, bali yalitimizwa kwa vitendo khaswa na baadhi ya watawala walioshikilia uwongozi wa Waislamu baada ya Mtume s.a.w.w. kutawafu. Wa kwanza kufanya hivyo ni Abu Bakar bin Abi Quhaafa, Khalifa wa Kwanza. Yeye, kwa mujibu wa Tadhkiratul Huffaadh ya adh-dhahabii (Juz. 1, uk. 2-3), alikusanya watu akawambia: Nyinyi mnasimulia Hadith za Mtume wa Mwenyezi Mungu 45 Al Khutwatus Siyaasiyya Litawhiidil Ummatil Islaamiyya ya Ustadh Ahmad Husayn Ya qub, uk K.m soma Sura 4:59; 5:104; 47:33; 5:7. 47 Kama (a) alivyosema katika khutba yake ya mwisho kuwa anatwachia vitu viwili ambavyo tutashikamana navyo hatutapotea baada yake kabisa: Katabu cha Mwenyezi Mungu na sunna yangu ; na (b) ile Hadithi isemayo: mazungumzo mnazuri kuliko yote ni (ya) kitabu cha Mwenyezi Mungu, na uwongozi bora ni uwongozi wa Muhammad 27

33 ambazo mnakhitalifiana katika usimulizi wazo. Na watu baada yenu watazidi kukhitalifiana. Kwa hivyo msisimulie chochote kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu! Yoyote atakayewauliza nyinyi kitu, mwambieni: Baina yetu sisi na nyinyi ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Basi kihalalisheni kilichohalalishwa nacho, na kiharamisheni kilichoharamishwa nacho. Lakini Khalifa Abu Bakar hakutosheka na kusema maneno hayo tu, ambayo ni sawa na yale yaliyosemwa na Umar bin Khattaab wakati wa maradhi ya Bwana Mtume s.a.w.w., bali alichukua na hatua hasa ya kulitekeleza hilo! Kwa mujibu wa hiyo hiyo Tadhkiratul Huffaadh tuliyoitaja hapo juu (Juz. 1, uk. 5), Bibi Aisha anaeleza: Babangu alikuwa amekusanya Hadith 500 za Mtume s.a.w.w. Siku moja asubuhi alinijia akanambia: Lete Hadith ulizonazo. Nikamletea. Akazichoma, na akasema: Ninaogopa nisije nikafa nikakuacha nazo! Wa pili ni Umar bin Khattaab, Khalifa wa Pili. Kwa kuwa yeye ndiye hasa aliyeanzisha ule mwito wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinatutosha, ni wazi kwamba aliposhikilia madaraka alihakikisha mwito huo umetekelezwa. Inavyoonyesha ni kwamba ile amri ya Khalifa Abu Bakar, ya watu watosheke na Kitabu cha Mwenyezi Mungu, haikuhishimiwa kwa ukamilifu. Bado kulikuwa na baadhi ya watu waliokuwa wakiendelea kuzieneza, na kuziandika, Hadith za Mtume s.a.w.w. Watu kama hao, alikuwa akiwambia wamletee Hadith walizokuwa nazo. Na walipompelekea, aliamrisha zichomwe. 48 Wala Khalifa Umar hakutosheka na kuzichoma Hadith zilizoandikwa tu, bali alizuiya pia zisienezwe. Alifanya hivyo (i.) kwa kuwaamrisha maswahaba wasizisimulie, na (ii.) kwa kuwazuiliya kusafiri! 48 Twabaqaat Ibn Sa d, Juz.7 uk

34 Imepokewa kwa Qurdha bin Ka b kwamba: Tulipotoka Madina kwenda Iraq, Umar alifuatana na sisi mpaka viungani. Kisha akatuuliza: Mnajua kwa nini nimefuatana nanyi? Tukamjibu: Umetaka kufuatana nasi na kutukirimu. Akasema: Pamoja na hayo, nina haja nyengine pia. Nyinyi mtakutana na watu wa miji wanaoisoma Qur ani kwa mvumo 49 kama mvumo wa nyuki. Kwa hivyo msiwashughulishe kwa Hadith za Mtume wa Mwenyezi Mungu. Nami ni mshirika wenu. Anasema Qurdha: Baada ya hapo sikusimulia tena Hadith yoyote kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu! 50 Na katiko riwaya nyengine, watu walipomuomba awasimulie Hadith, aliwajibu: Umar ametukataza! Pia imepokewa kwamba Abdulrahman bin Awf amesema: Umar bin Khattaab hakufa kabla ya kuweta maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu kutoka sehemu mbalimbali, k.v. Abdalla bin Hudhayfa, Abud Dardaa, Abuu Dharr, Uqba bin Amir. Akawauliza: Nini hizi Hadith za Mtume wa Mwenyezi Mungu munazozieneza kila mahali? Wakamuuliza: Unatuzuiya? Akawajibu: La! Lakini kaeni nami. Wallahi! Hamutaniondokea maadamu niko hai. Sisi tunajua zaidi. Tutachukua kwenu, na tutawarejeshea. Nao hawakumondokea mpaka akafa. 51 Na kwa mujibu wa Tadhkiratul Huffadh (Juz. l, uk. 7): Umar aliwazuia kusafiri watu watatu: Ibn Mas ud, Abud Dardaa, na Abuu Mas ud al-answaari. Akasema: Mmekithirisha (kusimulia) Hadith za Mtume wa Mwenyezi Mungu. Ibnul Athir 52 naye anasema: Umar alikuwa akiwambia maswahaba: Punguzeni kusimulia riwaya kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi 49 Yaani watu wengi wanaoisoma Qur an kwa sauti, lakini kila mtu peke yake peke yake. 50 Tadhkiratul Huffadh, Juz. 1 uk.7; na Al Mustadrak ya Haakim, Juz. 1, uk Kanzul Ummaal, Juz. 1 uk. 239, Hadithi Na Al Kaamil yake, Juz. 8, uk

35 Mungu isipokuwa zile za kufanyiwa amali. 53 Wa tatu ni Uthman bin Affaan, Khalifa wa Tatu. Yeye, akijua hali ilivyokuwa chini ya utawala wa watangulizi wake, alipanda mimbari siku moja akasema: Si halali kwa yoyote kusimulia Hadith ambayo hakuisikia katika enzi ya Abu Bakar, wala enzi ya Umar. 54 Hizo basi ndizo hatua zilizochukuliwa na makhalifa watatu wa kwanza kutekelezea neno la Umar la Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinatutosha! Lakini hatua hizo ziliacha athart gani mbaya katika msingi wa pili wa dini ya Kiislamu, yaani Sunna za Mtume Muhammad s.a.w.w.? Athari mbaya za hatua zilizochukuliwa Mpaka hapa tushaona kwamba, katika enzi za makhalifa watatu wa kwanza, kufuatia mwito wa Khalifa Umar kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinatutosha, watu walikatazwa kusimulia Hadith za Mtume s.a.w.w. na kuziandika. Zilizoandikwa, zilichomwa. Waliokuwa wakizisimulia kwa wingi, walikanywa wasifanye hivyo. Hata wengine walizuiwa kusafiri nje ya Madina ili wasije wakazieneza zile walizokuwa wakizijua. Hatua hizi (bila ya kujali nyudhuru nzuri zinazotolewa kuzitetea, ambazo hapa si mahali pake kuzijadili) zimeleta athari mbaya juu ya sunna kama msingi wa pili wa sharia ya Kiislamu. Athari ya kwanza mbaya ya kuzuiya Hadith kuandikwa, kinyume na maamrisho ya Bwana Mtume s.a.w.w., 55 ni kupotea kwa Hadith 53 Yaani kama zile zinazokhusu swala, saumu, hijja, na kadhaalika. 54 Muntakhabu Kanzil Ummal iliyo pambizoni mwa Juz. 4, uk. 64 wa Musnad Ahmad. 55 Mtume Muhammad s.a.w.w aliamrisha Hadithi zake ziandikwe. Hayo yameelezwa katika vitabu mbali mbali vya Hadithi kama Sahih Bukhari, Sunan Tirmidhi, na Musnad Ahmad. 30

John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane

John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane SN: John Lesson 18 Page 1 John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane Read John chapter sixteen. Soma Yohana sura ya kumi na sita. 1. What "things" is Jesus referring to in these several verses? "Mambo"

More information

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013 102/3 KISWAHILI KARATASI YA TATU (FASIHI) JULAI/AGOSTI, 2013 MUDA: SAA: 2½ MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013 Hati Ya Kuhitimu Kisomo Cha Sekondari KISWAHILI

More information

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES TIP: READ ALOUD EVERY SWAHILI WORD TO PRACTICE YOUR SIGHT-READING FLUENCY. PART 1: LOCATIVES 1) Translate the following phrases a. Mimi

More information

There is one God Mungu ni mmoja 1

There is one God Mungu ni mmoja 1 There is one God Mungu ni mmoja 1 God is Mungu ni Title Kichwa Jesus is Yesu ni Genesis 1:1 "In the beginning God (Elohim) created the heavens and the earth." Mwanzo 1: 1 "Hapo mwanzo Mungu (Elohim) aliziumba

More information

Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir

Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir , 33 Abdilahi Nassir 33 Sura al-ahzaab Tafsiri na Maelezo Abdilahi Nassir Haki ya kunakili imehifadhiwa na Abdilahi Nassir, 2005 Chapa ya Kwanza 2005 Kinatangazwa na MARKAZI YA AHLUL BAYT S.L.P. 84603

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF PLENARY PROCEEDINGS, HELD AT THE PLENARY HALL, BOMAS OF KENYA ON 16.03.04 Page 1 of 9 CONSTITUTION

More information

NEW INTERNATIONAL VERSION

NEW INTERNATIONAL VERSION RUTH Swahili / English Page 1 RUTHU 1 RUTH 1 1:1 Ikawa zamani za Waamuzi walipoamua, kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja wa Bethlehemu ya Yuda, akaenda kukaa katika nchi ya Moabu, yeye na

More information

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Waliopotosha Ukweli Author(s): kh Mu tasim Sayyid

More information

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh)

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh) BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh) 8 December, 2014 Posted by Salafibayaan ClarificationsRefutations 1223 views Nauliza suali: Muheshimiwa

More information

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI)

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI) BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI) Simu 255-022-2120261-7 Ext. 331 Ofisi ya Msajili Nukushi: 255-022-2139951 SLP 9083 DAR ES SALAAM FOMU NAMBA 11 TANZANIA MAOMBI

More information

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags:

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Tawasali Tawasali At-Tawassul Author(s): Seyyid Abdul Rahim Al-Musawi [3] Publisher(s): Al Itrah Foundation [4] Kitabu

More information

Published on Al-Islam.org ( Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu

Published on Al-Islam.org (  Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu Mahari ya Damu Authors(s): Ustadh Shahid Murtadha Mutahhari [3] Translator(s): S. Muhammad Ridha Shushtary [4]

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF PLENARY PROCEEDINGS HELD AT THE PLENARY HALL AT BOMAS OF KENYA ON 26.02.04 Page 1 of 7 CONSTITUTION

More information

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU Kama unataka kujifunza zaidi njia ya Mkristo wa kweli anavyopaswa kuishi, basi ni lazima ujifunze Biblia. Ili kukusaidia; Kanise la Christadelphian Bible Mission limechapisha kijitabu kuhusu mafunzo ya

More information

Bismillah ar-rahman ar-raheem SHAHADA 1 YALIYOMO

Bismillah ar-rahman ar-raheem SHAHADA 1 YALIYOMO Bismillah ar-rahman ar-raheem SHAHADA 1 YALIYOMO Utangulizi wa mfasiri Utangulizi wa mfasiri wa lugha ya kiingereza Utangulizi wa mwandishi Nafasi ya kalima Ubora wa kalima Uchambuzi wa kisarufi wa tamko

More information

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1 Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1 1. Mujaddid wa zama zetu hizi, Imâm al-albâni alisema katika mwaka wa 1412 AH (1991 CE), ulipokuwa ni wakati baadhi yetu bado

More information

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT NANDI COUNTY ASSEMBLY 1 OFFICIAL REPORT Wednesday 11 th July, 2018 The House met at 2:30 pm [The Temporary Speaker (Hon Kipkurui Chepkwony) in the Chair] PRAYER QUORUM Hon. Temporary Speaker (Kipkurui

More information

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili Compiled by Sandy Harris Designed by Norma Hays This book is lovingly dedicated to our precious grandchildren, the joys of our hearts. It is our prayer that

More information

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania HAKIKA YA AHMADIYYA Watu wengi hawathamini ukweli. Hata hawashuhguliki kwa kuupeleleza wenyewe. Hata hivyo ukweli, hususa unohusika na Dini, ni muhimu sana kwa kila mwanadamu kwa ajili ya wokovu wake.

More information

YA AL HABBIB SAYYEID

YA AL HABBIB SAYYEID YA AL HABBIB SAYYEID . NA Yamefasiriwa kwa Kiswahili na: Al habbib Sayyeid Umar Bin Sayyeid Abdallah (Mwinyi Baraka). First addition. 03 Sept, 2005. 28 Rajab, 1426. HR. i MANAQIB YA AL-MAARUF Baada ya

More information

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume > Lifuatalo ni jibu alilotoa mtukufu mtume (S.A.W) wakati alipoulizwa na imam Ali (A.S) kuhusu

More information

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO FISHERS OF MEN MINISTRIES CHURCH NAME 2 Fishers of Men Ministries uses a Christ centered approach to transform one life at a time by feeding their body

More information

DINI JE, DINI NI MUHIMU?

DINI JE, DINI NI MUHIMU? SURA YA KWANZA DINI Hivyo, Mwislamu wa kweli ni yule ambaye hufuata mafundisho ya Uislamu wakati wote. Kama tu Waislamu wa kweli, basi lazima tufuate sheria za Ki-Islamu tukiwa ndani na nje ya nyumba zetu,

More information

Imam Mahdi katika Usunni Na Ushia

Imam Mahdi katika Usunni Na Ushia Imam Mahdi final D.Kanju chk Lubumba.qxd 7/1/2011 4:45 PM Page A Imam Mahdi katika Usunni Na Ushia Kimeandikwa na: Sayyid Abdul Rahim al-musawi na Sheikh Abdul Karim al-bahbahani Kimetarjumiwa na: Hemedi

More information

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES This Psalm is a talk between those bringing the Good News and an individual who responds and then with our great God who has been listening to this conversation; and at the end, He also wants to jump in.

More information

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO DISCIPLESHIP SERIES I FULL LIFE MINISTRY KENYA NAME 2 Purpose: Provide teachings to equip the body of Christ to become warrior disciples of Jesus Christ.

More information

Ukoo Wake Na Kunasibika Kwake:

Ukoo Wake Na Kunasibika Kwake: Ukoo Wake Na Kunasibika Kwake: Yeye ni Sheikh wa ki-salafi, kisha ni mfuasi wa riwaya na mtunzi wa vitabu vingi vya ki-islamu na vya uswahihishaji, Alî Ibn Hasan Ibn Alî Ibn Abdil-Hamîd Al-Ya fî, mnasaba

More information

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

NANDI COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT NANDI COUNTY ASSEMBLY 1 OFFICIAL REPORT Wednesday, 8 th August 2018 The House met at 2:30 pm [The Temporary Speaker (Hon. Chepkemei Clara) in the Chair] PRAYER QUORUM Temporary Speaker (Hon. Chepkemei):

More information

AHMAD AL-RAYSUNI. SWAHILI VERSION idara ya Lugha na ukalimani ya Chuo Kikuu cha waislamu cha Morogoro. IIIT Mfululizo wa Vitabu kwa Muhtasari

AHMAD AL-RAYSUNI. SWAHILI VERSION idara ya Lugha na ukalimani ya Chuo Kikuu cha waislamu cha Morogoro. IIIT Mfululizo wa Vitabu kwa Muhtasari AHMAD AL-RAYSUNI AL-SHUURA Kanuni ya Qur an ya Kufanya Uamuzi kwa Kushauriana SWAHILI VERSION idara ya Lugha na ukalimani ya Chuo Kikuu cha waislamu cha Morogoro IIIT Mfululizo wa Vitabu kwa Muhtasari

More information

Zanzibar itafutika-mwanasheria

Zanzibar itafutika-mwanasheria Hili la kadhia ya Masheikh... www.annuurpapers.co.tz au facebook:annuurpapers@yahoo.com Sauti ya Waislamu Dk. Shein hasalimiki 16 ISSN 0856-3861 Na. 1199 DHULHIJJA 1436, IJUMAA, OKTOBA 16-22, 2015 BEI

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT RHAMU

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT RHAMU CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL CONSTITUENCY, HELD AT RHAMU ON 2 JUNE 03, 2002 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, MANDERA CENTRAL

More information

NEW INTERNATIONAL VERSION

NEW INTERNATIONAL VERSION HOSEA Swahili / English Page 1 Osee 1 Hosea 1 1:1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia Hosea, mwana wa Beeri, siku za Uzia, na Yothamu, na Ahazi, na Hezekia, wafalme wa Yuda; na siku za Yeroboamu, mwana

More information

Toleo la kwanza: June, 2007 (Jamaadi Aakhar, 1428) Vitabu ii.

Toleo la kwanza: June, 2007 (Jamaadi Aakhar, 1428) Vitabu ii. . i Toleo la kwanza: June, 2007 (Jamaadi Aakhar, 1428) Vitabu 1000. First addition All rights reserved ii. No. Yaliyomo: Ukurasa. 1. Yaliyomo iii. 2. Utangulizi (Mqaddima Al Habib Syd. Omar.. v. 3. Dibaji

More information

Gazeti la kwanza la Kiislam kutolewa kwa lugha ya Kiswahili - mwaka 1936

Gazeti la kwanza la Kiislam kutolewa kwa lugha ya Kiswahili - mwaka 1936 Gazeti la kwanza la Kiislam kutolewa kwa lugha ya Kiswahili - mwaka 1936 Mapenzi ya Mungu Mapenzi kwa wote bila chuki kwa yeyote DAR ES SALAAM TANZANIA JUZU 76 No. 189 Nukuu ya Qur an Tukufu Enyi watu!

More information

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam. Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Khadija-tul-Kubra Khadija-tul-Kubra Author(s): Sayyed A. A. Razwy [3] Publisher(s): Al-Itrah Foundation [4] Maisha

More information

IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE.

IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE. IFAHAMU BIBLIA KATIKA UBORA WAKE. Na Ngowi Dennis. "*Natazamia Mbingu mpya na Nchi mpya* 1 YALIYOMO: SHUKRANI:... 5 UTANGULIZI KWA WASOMAJI WA BIBLIA!... 6 AGANO LA KALE... 7 AGANO JIPYA... 8 USOMAJI WA

More information

HALI YA UISLAMU. Maelezo ya kumsaidia Mkristo aufahamu Uislamu

HALI YA UISLAMU. Maelezo ya kumsaidia Mkristo aufahamu Uislamu HALI YA UISLAMU Maelezo ya kumsaidia Mkristo aufahamu Uislamu Kosni nondiki mondo otigo e Yala Theological Centre, PO Box 765, Yala, Kenya, kod Siaya Theological Centre, PO Box 635, Siaya. Jandiko en Jim

More information

Kuishi Maisha Tele. Katika mwanzo wa mwaka mpya, Niliwapa changamoto

Kuishi Maisha Tele. Katika mwanzo wa mwaka mpya, Niliwapa changamoto UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, JANUARI 2012 Na Rais Thomas S. Monson Kuishi Maisha Tele Katika mwanzo wa mwaka mpya, Niliwapa changamoto Watakatifu wa Siku za Mwisho kote kufanya uchunguzi muhimu wa kibinafsi

More information

2002 Version of the Basic Talk on "Using African Proverbs, Sayings, Idioms, Riddles, Stories, Fables, Play

2002 Version of the Basic Talk on Using African Proverbs, Sayings, Idioms, Riddles, Stories, Fables, Play 2002 Version of the Basic Talk on "Using African Proverbs, Sayings, Idioms, Riddles, Stories, Fables, Plays and Songs (African Oral Literature and Culture)" I pointed out to you the stars (the moon) and

More information

February 9, 2017 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 16 MOMBASA COUNTY ASSEMBLY

February 9, 2017 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 16 MOMBASA COUNTY ASSEMBLY MOMBASA COUNTY ASSEMBLY HANSARD REPORT Thursday, 9 th February, 2017 The House met at 2:45pm. (Deputy Speaker (Hon. Mswabah Rashid) in the Chair) PRAYERS Deputy Speaker (Hon. Mswabah Rashid): Members let

More information

Uwezo Kenya National Learning Assessment 2014

Uwezo Kenya National Learning Assessment 2014 Uwezo Kenya Nationa Learning Assessment TEST BOOKLET Promoting Learning in East Africa KENYA Uwezo Kenya at Twaweza, P.O. Box 13784-00800 Nairobi Te: +254 715 563 720 / +254 786 563 722 Emai: kenya@uwezo.net

More information

Rainbow of Promise Journal

Rainbow of Promise Journal Rainbow of Promise 2002 03 Journal Date: 9/24/2002 Submitted by: Paul Nichols Well, we re three days out of training and have shared in ministry with two wonderful churches thus far. We ve had our share

More information

Mashairi ya Masaibu ya Karbala

Mashairi ya Masaibu ya Karbala Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Mashairi ya Masaibu ya Karbala Mashairi ya Masaibu ya Karbala Publisher(s): Ahlul Bayt (a.s.) Assembly of Tanzania

More information

Je, Umesikia Juu Ya Kanuni Nne Za Kiroho?

Je, Umesikia Juu Ya Kanuni Nne Za Kiroho? Je, Umesikia Juu Ya Kanuni Nne Za Kiroho? Have You Heard of the Four Spiritual Laws? Just as there are physical laws that govern the physical universe, so are there spiritual laws which govern your relationship

More information

Ujasiri wa Kimaadili. Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani

Ujasiri wa Kimaadili. Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani Ujumbe wa Urais wa Kwanza, Machi 2010 Na Rais Henry B. Eyring Mshauri wa Kwanza katika Urais wa Kwanza Ujasiri wa Kimaadili Mojawapo ya madhumuni ya maisha ya duniani ni kumuonyesha Mungu kwamba tutatii

More information

Vitendawili Vya Swahili

Vitendawili Vya Swahili Vitendawili Vya Swahili Free PDF ebook Download: Vitendawili Vya Swahili Download or Read Online ebook vitendawili vya swahili in PDF Format From The Best User Guide Database Muundo wa vitendawili umejengwa

More information

NGUO-NYINGI MKOTI: MWANZISHAJI WA MJI WA NGOJI (ANGOCHE)

NGUO-NYINGI MKOTI: MWANZISHAJI WA MJI WA NGOJI (ANGOCHE) AAP 60 (1999). 121-130 NGUO-NYINGI MKOTI: MWANZISHAJI WA MJI WA NGOJI (ANGOCHE) THILO C.. SCHADEBERG The title of this paper gives three variants of what historically is the same name: Koti = the present-day

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS IJARA CONSTITUENCY AT IJARA BARAZA PARK

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS IJARA CONSTITUENCY AT IJARA BARAZA PARK CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS IJARA CONSTITUENCY AT IJARA BARAZA PARK 2 05 TH JUNE 2002 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, IJARA, HELD AT IJARA

More information

MOROGORO JARIDA LA. ISSN Toleo Na.4 Julai 2005 BODI ZA AFYA ZA WILAYA - SAUTI YA WANANCHI

MOROGORO JARIDA LA. ISSN Toleo Na.4 Julai 2005 BODI ZA AFYA ZA WILAYA - SAUTI YA WANANCHI JARIDA LA MOROGORO ISSN 0856-9517 Toleo Na.4 Julai 2005 BODI ZA AFYA ZA WILAYA - SAUTI YA WANANCHI Halmashauri zote nchini zilitakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin William Mkapa,

More information

In Search of Contact: Rhetorical Questions in the Communicative Frame of the Funeral Sermon

In Search of Contact: Rhetorical Questions in the Communicative Frame of the Funeral Sermon In Search of Contact: Rhetorical Questions in the Communicative Frame of the Funeral Sermon by Nganga Simon nganga_simon@ymail.com Department of Linguistics and Foreign Languages Moi University, Eldoret,

More information

NAIROBI CITY COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT

NAIROBI CITY COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT NCCA2014/030 NAIROBI CITY COUNTY ASSEMBLY OFFICIAL REPORT First County Assembly Second Session Thursday, 9 th October, 2014 The House met at 2.30 p.m. (Mr. Speaker in the Chair) PRAYERS Hon. Speaker(Mr.

More information

Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya

Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya Mamlaka, Majukumu na Uwajibikaji Jalida la Polisi Shirikishi MEI, 2017 HAKI NA USALAMA http://hakinausalama.org/ Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya Mamlaka, Majukumu

More information

TALKING ABOUT ONESELF TO ACT IN THE WORLD: A SWAHILI AUTOBIOGRAPHY (SHAABAN ROBERT, MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI

TALKING ABOUT ONESELF TO ACT IN THE WORLD: A SWAHILI AUTOBIOGRAPHY (SHAABAN ROBERT, MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI SWAHILI FORUM 19 (2012): 106-116 TALKING ABOUT ONESELF TO ACT IN THE WORLD: A SWAHILI AUTOBIOGRAPHY (SHAABAN ROBERT, MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI [ MY LIFE AND AFTER FIFTY YEARS ])1 XAVIER GARNIER

More information

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian ISSN: 1570-0178 Volume 2, Issue 8 (6 June 2000) The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian Introduction First Part 1 First Part 2 Second Part

More information

JUNE 4, Acts 2:1-12 and Offering...Pastor Maromy Samuel All Hail the Power of Jesus Name led by Haitian Congregation Worship Team

JUNE 4, Acts 2:1-12 and Offering...Pastor Maromy Samuel All Hail the Power of Jesus Name led by Haitian Congregation Worship Team JUNE 4, 2017 Prelude Psalm 117...Celebration Choir & Orchestra Ezekiel 36:22-27 and Welcome...Pastor Matthew Dunlap Recognition of Ordinands...Pastor Kevin Ulmet Wes Hinton, Lisa Smith, Shane Tarter Passing

More information

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian 1 sur 38 05.02.2006 0:28 Archives of Popular Swahili logo to the LPCA home page ISSN: 1570-0178 Volume 2, Issue 2 (11 November 1998) to the APS home page The history of Zaire as told and painted by Tshibumba

More information

WELCOME TO GOD S SERVICE A.C.K. ST. LUKE S PARISH UMOJA & TENA CHURCH QUOTE OF THE WEEK PRAYER OF THE DAY

WELCOME TO GOD S SERVICE A.C.K. ST. LUKE S PARISH UMOJA & TENA CHURCH QUOTE OF THE WEEK PRAYER OF THE DAY WELCOME TO GOD S SERVICE A.C.K. ST. LUKE S PARISH UMOJA & TENA CHURCH 16 th Sunday after Trinity (Jumapili ya Kumi na Sita baada ya Utatu) 12 th October 2014 Vision: To be a Transforming, Holistic Anglican

More information

UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI

UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI Muundo Thabiti Jarida la Polisi Shirikishi MEI, 2017 HAKI NA USALAMA http://hakinausalama.org/ UWAJIBIKAJI NDANI YA JESHI LA POLISI Muundo Thabiti Jarida la Polisi

More information

2

2 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 (CKRC) VERBATIM REPORT OF 40 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, WAJIR SOUTH CONSTITUENCY HELD AT SABULI-

More information

HAKIBulletin RAIS AMTEUA PROF. JUMA KUWA JAJI MKUU WA TANZANIA. Ndani: JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA

HAKIBulletin RAIS AMTEUA PROF. JUMA KUWA JAJI MKUU WA TANZANIA. Ndani: JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA HAKIBulletin JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA ISSN: 00000054 Toleo Na. 1 Julai - Septemba, 2017 RAIS AMTEUA PROF. JUMA KUWA JAJI MKUU WA TANZANIA Ndani: MAJAJI NA MAHAKIMU WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA

More information

MRADI WA METHALI (SANALASKUJA PROJEKTI)

MRADI WA METHALI (SANALASKUJA PROJEKTI) MRADI WA METHALI (SANALASKUJA PROJEKTI) Tehtävä Tehtävän nimi Oppitunnin tavoite Mitä tarvitaan? Teach the four language skills of speaking, writing, listening and reading. Familiarize with the culture

More information

No. Book Name Category Type Price 1 AFYA MARIDHAWA -1 SWAHILI SUBSCRIPTION 2, AFYA NA UZIMA SWAHILI SUBSCRIPTION 8,500.00

No. Book Name Category Type Price 1 AFYA MARIDHAWA -1 SWAHILI SUBSCRIPTION 2, AFYA NA UZIMA SWAHILI SUBSCRIPTION 8,500.00 HOME HEALTH EDUCATION SERVICE MOROGORO - TANZANIA. Tel. No: +255 764 839 051 Website: www.stuhhes.or.tz PRICE LIST FOR 2018 Date : Wednesday, 28 November 2018 Time. : 11:34:10 pm SUBSCRIPTION Swahili 1

More information

KITABU CHA MAFUNZO KWA WATOA DAWA KATIKA MADUKA YA DAWA MUHIMU

KITABU CHA MAFUNZO KWA WATOA DAWA KATIKA MADUKA YA DAWA MUHIMU JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA KITABU CHA MAFUNZO KWA WATOA DAWA KATIKA MADUKA YA DAWA MUHIMU 2007 Toleo la Tatu Kitabu hiki kimetayarishwa

More information

Was al-isrā wa al-mi rāj a bodily or spiritual journey?

Was al-isrā wa al-mi rāj a bodily or spiritual journey? Was al-isrā wa al-mi rāj a bodily or spiritual journey? The scholars of Islam classic and modern have long disputed the exact nature of the Prophet s journey to Jerusalem and the Heavens. Specifically,

More information

Yassarnal Quran English

Yassarnal Quran English Yassarnal Quran English Free PDF ebook Download: Yassarnal Quran English Download or Read Online ebook yassarnal quran english in PDF Format From The Best User Guide Database English translation by. A.Y.

More information

TAUS RETREAT NEWS LETTER # 1

TAUS RETREAT NEWS LETTER # 1 TAUS RETREAT NEWS LETTER # 1 TANZANIA ADVENTISTS IN THE UNITED STATES OF AMERICA (TAUS) ANNUAL RETREAT When: July 12-16, 2017 Where: Wisconsin Academy, N2355 Duborg Rd, Columbus, WI 53925 Who Must Attend:

More information

HAKIBulletin JAJI MKUU AWAASA WAHITIMU WA SHERIA KUJIENDELEZA KITAALUMA HALIUZWI! BENKI YA DUNIA USULUHISHI MUAFAKA MAHAKAMA MAWAKILI MAHAKAMA KUU,

HAKIBulletin JAJI MKUU AWAASA WAHITIMU WA SHERIA KUJIENDELEZA KITAALUMA HALIUZWI! BENKI YA DUNIA USULUHISHI MUAFAKA MAHAKAMA MAWAKILI MAHAKAMA KUU, HAKIBulletin JARIDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA ISSN: 00000054 Toleo Na. 2 Oktoba - Desemba, 2017 JAJI MKUU AWAASA WAHITIMU WA SHERIA KUJIENDELEZA KITAALUMA HALIUZWI! Ndani; BENKI YA DUNIA YAIPONGEZA MAHAKAMA

More information

MASHAIRI YA WAADHI "VERSES OF ADMONITION": the people of Mombasa rebuked by P J. L Frank! and Yahya Ali Omar

MASHAIRI YA WAADHI VERSES OF ADMONITION: the people of Mombasa rebuked by P J. L Frank! and Yahya Ali Omar AAP 42 (1995). 138-157 MASHAIRI YA WAADHI "VERSES OF ADMONITION": the people of Mombasa rebuked by P J. L Frank! and Yahya Ali Omar MUKH!ASARI [SUMMARY] Aliyetunga kasiga hii, Sheikh Abgallah al-husni,

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, LAGDERA CONSTITUENCY HELD AT LIBOI ON 8 TH JUNE, 2002 2 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, LAGDERA CONSTITUENCY,

More information

TUMERITHI TUWARITHISHE

TUMERITHI TUWARITHISHE TUMERITHI TUWARITHISHE 2 3 Kampeni ya kuboresha Utunzaji wa Misitu Misitu ni rasilimali ambayo ina mchango mkubwa katika maisha ya Watanzania wengi lakini matumizi mabaya ya misitu na yaliyopitiliza pamoja

More information

HOTUBA YA JAJI MKUU MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA SIKU YA SHERIA, DAR ES SALAAM, TAREHE 1 FEBRUARI, 2018

HOTUBA YA JAJI MKUU MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA SIKU YA SHERIA, DAR ES SALAAM, TAREHE 1 FEBRUARI, 2018 HOTUBA YA JAJI MKUU MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA SIKU YA SHERIA, DAR ES SALAAM, TAREHE 1 FEBRUARI, 2018 Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dr. Tulia Ackson Mwansasu,

More information

Ahadi za Serikali II. Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007

Ahadi za Serikali II. Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007 Ahadi za Serikali II Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007 Ahadi za Serikali II Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007 Ahadi za Serikali II Zimekusanywa na HakiElimu Agosti 2007 Shukrani Ahadi hizi zilikusanywa

More information

VACATION BIBLE SCHOOL VBS. Newsletter. #Rebuilding through prayer, hard work & perseverance.

VACATION BIBLE SCHOOL VBS. Newsletter. #Rebuilding through prayer, hard work & perseverance. VACATION BIBLE SCHOOL VBS 2018 Newsletter #Rebuilding through prayer, hard work & perseverance. Pre-school Week 8th - 10th August Grade 1-8 13th - 17th August Pre-school Week Word from the Children s Pastor

More information

Al-Aqidah Al-Tahawiyyah [Sharh Al-Maydani] Introduction, Part Three Monday 7pm 9pm. Course link:

Al-Aqidah Al-Tahawiyyah [Sharh Al-Maydani] Introduction, Part Three Monday 7pm 9pm. Course link: Al-Aqidah Al-Tahawiyyah [Sharh Al-Maydani] Introduction, Part Three. 16-9-2013 Monday 7pm 9pm Course link: http://www.anymeeting.com/islamiccourses1 The Text [Al-Matn] All praise is due to Allah, the Lord

More information

Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir

Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir Tafsir ibn Kathir, is a classic Tafsir (commentary of the Qur'an) by Imad ud Din Ibn Kathir. It is considered to be a summary of the earlier Tafsir al-tabari.

More information

WELCOME TO GOD S SERVICE ACK ST. LUKE`S PARISH UMOJA Theme: Endeavoring to touch the heart of God, (Matt 25:40). Kuazimia kumpendeza Mungu

WELCOME TO GOD S SERVICE ACK ST. LUKE`S PARISH UMOJA Theme: Endeavoring to touch the heart of God, (Matt 25:40). Kuazimia kumpendeza Mungu WELCOME TO GOD S SERVICE ACK ST. LUKE`S PARISH UMOJA 8 th after Trinity (Jumapili ya Nane baada ya Utatu) 26 th July 2015 Vision: To be a Transforming, Holistic Anglican Church 2015 Theme: Endeavoring

More information

Tribute to Syyeda Fatima Zahra (S.A) on the Auspicious date of her Birth

Tribute to Syyeda Fatima Zahra (S.A) on the Auspicious date of her Birth Bismillahir Rahmaanir Raheem Tribute to Syyeda Fatima Zahra (S.A) on the Auspicious date of her Birth The date of birth of Lady Fatima Zahra (S.A.) is 20th of Jamaadil-Aakhir. This year it will fall on

More information

Past Paper Questions May/June 2009 to Oct/Nov 2016

Past Paper Questions May/June 2009 to Oct/Nov 2016 Past Paper Questions May/June 2009 to Oct/Nov 2016 Paper 1 Islamiyat GCE O LEVEL & IGCSE(0493) Compiled by Tahir Ali Babar The history and importance of the Qur an The life and importance of the Prophet

More information

Defence against Disaster

Defence against Disaster Defence against Disaster in accurately determining the positions of the Companions after the death of the Prophet by Qadi Abu Bakr ibn al- Arabi with commentary by Muhibb ad-din al-khatib In the name of

More information

Cultural Considerations Tanzania Excursion

Cultural Considerations Tanzania Excursion Cultural Considerations Tanzania Excursion The Roots of Change Cultural Considerations Table of Contents Tanzania Cultural Considerations... 3 Swahili Language Key Phrases... 4 Tribes of Tanzania... 5

More information

Imam Ali ibn Abi Talib

Imam Ali ibn Abi Talib Publicado en Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Inicio > Inquiries About Shi'a Islam > Imam Ali ibn Abi Talib > Who are the Twelve Leaders? Imam Ali ibn Abi Talib The Noble

More information

Imam Ali ibn Abi Talib Hazrat Hasan ibn Ali Imam Husayn ibn Ali

Imam Ali ibn Abi Talib Hazrat Hasan ibn Ali Imam Husayn ibn Ali Imam Ali ibn Abi Talib Hazrat Hasan ibn Ali Imam Husayn ibn Ali Imam Aga Hasan Ali Shah Imam Aga Ali Shah Imam Sultan Muhammad Shah Mawlana Shah Karim al-husayni Imam-i Zaman! " # $% &" '( #) # " * + &"

More information

HOLY COMMUNION ACCORDING TO THE KENYAN RITE

HOLY COMMUNION ACCORDING TO THE KENYAN RITE HOLY COMMUNION ACCORDING TO THE KENYAN RITE HYMN The Lord be with you And also with you. The earth is the Lord s and all that is in it Let the heavens rejoice and the earth be glad. Our help is in the

More information

AND REACTION IN SWAHILI POETRY.

AND REACTION IN SWAHILI POETRY. REVOLUTION AND REACTION IN SWAHILI POETRY. M. M. MULOKOZI** Swahili poetry is that poetry, written or oral, which has been or is being produced in the Swahili language by East Africans. Swahili poetry

More information

Ezra 3 Lessons Download or Read Online ebook ezra 3 lessons in PDF Format From The Best User Guide Database

Ezra 3 Lessons Download or Read Online ebook ezra 3 lessons in PDF Format From The Best User Guide Database Ezra 3 Lessons Free PDF ebook Download: Ezra 3 Lessons Download or Read Online ebook ezra 3 lessons in PDF Format From The Best User Guide Database of Ezra (Ezra 7:28; and repeatedly in Ezra 8-9).. (also

More information

The Lord be with you And with your spirit

The Lord be with you And with your spirit There are many ways you can add a little flavour of Kagera to your service. Try using some Swahili prayers and responses, or sing some Swahili songs. It's very easy to read Swahili; it's entirely phonic,

More information

He recited verses from al-baqarah (2: 136) and Al Imran (3: 64), reports Abdullah Ibn Abbas (Muslim). Abu Bakr al-siddiq is reported to have recited a

He recited verses from al-baqarah (2: 136) and Al Imran (3: 64), reports Abdullah Ibn Abbas (Muslim). Abu Bakr al-siddiq is reported to have recited a بسم الله الرحمن الرحیم صل ى الله علیھ وسل م WHAT THE PROPHET PARTICULARLY READ OR EMPHASISED? (An extract from the world s most popular book Way to the Qur an by Khurram Murad) There are certain Surahs

More information

Mutah Discussed, comments by Salman [ sunniforum ] and Shayk Faraz Rabbani [ sunnipath ]

Mutah Discussed, comments by Salman [ sunniforum ] and Shayk Faraz Rabbani [ sunnipath ] Mutah Discussed, comments by Salman [ sunniforum ] and Shayk Faraz Rabbani [ sunnipath ] Shia s often quote: "Then as to those by whom you take pleasure give them their appointed dowers" 6:24 Ibn Mas'ud

More information

REPUBLIC OF KENYA COUNTY ASSEMBLY OF KILIFI THE HANSARD. Wednesday, 29 th March, 2017

REPUBLIC OF KENYA COUNTY ASSEMBLY OF KILIFI THE HANSARD. Wednesday, 29 th March, 2017 March 29, 2017 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 1 REPUBLIC OF KENYA COUNTY ASSEMBLY OF KILIFI THE HANSARD Wednesday, 29 th March, 2017 The House met at the County Assembly Chamber, Malindi Town, at 2.30 p.m. [The

More information

MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU SHEIKH MUZAFFAR AHMAD DURRANI

MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU SHEIKH MUZAFFAR AHMAD DURRANI äô #Ö] Ùö ç» ö $ ºÛ$ vø Úö äö #Ö] Ÿ$]ô äø ÖF ]ôÿ6? Ümû Ó ø Ö]á ô û Ï ö Ö]è ö n$ Âô û ] ø MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU SHEIKH MUZAFFAR AHMAD DURRANI 1 MAOMBI YA QUR'AN TUKUFU Mwandishi: Sheikh Muzaffar Ahmad

More information

The Noble Qur an. Medium H/B 1098pp 8.95 Product code: 1.01A. P/B 1104pp 7.95 Product code: 1.01B. The Noble Qur an

The Noble Qur an. Medium H/B 1098pp 8.95 Product code: 1.01A. P/B 1104pp 7.95 Product code: 1.01B. The Noble Qur an The Qur aan Arabic text with corresponding English meanings. A new translation of the Qur aan brought out by Saheeh International. The two mains features that distinguish this translation are (i) the authenticity

More information

Origins of Shia a. Answering-Ansar.org Articles. Revisions:

Origins of Shia a. Answering-Ansar.org Articles. Revisions: Origins of Shia a Work file: Project: origins_of_shia.pdf Answering-Ansar.org Articles Revisions: No. Date Author Description Review Info 1.0.1 13.03.2004 Answering-Ansar.org Spelling corrections & copyright

More information

Three Ways to Forgiveness

Three Ways to Forgiveness Original Title: Three Ways to Forgiveness By: Ibn Rajab al-ḥanbalī 1 Oh son of Adam, as long as you call upon me and hope in me, I will forgive you for whatever (sins) you have and I will not mind... The

More information

I. Matching. Match the letter that corresponds to the definition. Mother of the believers. One who invites to a particular belief

I. Matching. Match the letter that corresponds to the definition. Mother of the believers. One who invites to a particular belief I. Matching. Match the letter that corresponds to the definition. Mother of the believers Leader, chieftan One who invites to a particular belief Speaker, orator Military expeditions Witness, martyr One

More information

Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir

Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir Tafsir Ibn Kathir Alama Imad ud Din Ibn Kathir Tafsir ibn Kathir, is a classic Sunni Islam Tafsir (commentary of the Qur'an) by Imad ud Din Ibn Kathir. It is considered to be a summary of the earlier Tafsir

More information

Aisha Siddiqua RA she who lives. Feb 13 th 2009 Shaheen Zakaria

Aisha Siddiqua RA she who lives. Feb 13 th 2009 Shaheen Zakaria Aisha Siddiqua RA she who lives Feb 13 th 2009 Shaheen Zakaria Early Life Born in Mecca in the?4 th year of Nubuwwat Parents: Abu Bakr Siddique and Umme Rumman (RA) Since I reached the age when I could

More information

1/17/2016 Name: Please choose the best answer to the following questions:

1/17/2016 Name: Please choose the best answer to the following questions: Grade 5 Seerah Br. Muhammad Maqbool Students will be given 20 questions from this pool. Please choose the best answer to the following questions: 1. All of these statements are true about Barakah EXCEPT:

More information

What is the rule regarding Al-Tawassul through the Prophets and Saints?

What is the rule regarding Al-Tawassul through the Prophets and Saints? 1 Published by TheSunniWay. Written by Mufti Zahid Hussain Al-Tawassul What is the rule regarding Al-Tawassul through the Prophets and Saints? The rule regarding Al-Tawassul through the Prophets and Saints

More information

A brief look at the life of the one who spread Islam to the corners of the world.

A brief look at the life of the one who spread Islam to the corners of the world. Published by Abul Hasanaat Islamic Research Centre Misri Gunj, Hyderabad. 500 053 Ph No: 040-24469996 A brief look at the life of the one who spread Islam to the corners of the world. 2 Introduction: It

More information

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian 1 sur 25 05.02.2006 0:37 ISSN: 1570-0178 Volume 2, Issue 6 (8 October 1999) The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian Introduction First Session,

More information