Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir

Size: px
Start display at page:

Download "Sura al-ahzaab. Tafsiri na Maelezo. Abdilahi Nassir"

Transcription

1 , 33 Abdilahi Nassir

2 33 Sura al-ahzaab Tafsiri na Maelezo Abdilahi Nassir

3 Haki ya kunakili imehifadhiwa na Abdilahi Nassir, 2005 Chapa ya Kwanza 2005 Kinatangazwa na MARKAZI YA AHLUL BAYT S.L.P MOMBASA (KENYA) Simu: Mobile: Jalada limechorwa na: DeskTop Productions Ltd.

4 YALIYOMO Dibaji i Utangulizi wa Sura iv Vifupisho vii Ufupisho wa Vitabu Nilivyovirejelea viii Sura al-ahzaab Waislamu wasiwatwii makafiri na wanafiki Ni muhali moyo mmoja kuamini itikadi mbili zisizowafikiana Ada ya dhihaar haikubaliwi na Uislamu Mtoto aitwe kwa ubini wa babake wa kumzaa, sio wa kumlea Mtume ana haki zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao Wake wa Mtume ni mama za Waislamu Msingi wa kurithiana katika Uislamu Ahadi iliyochukuliwa kwa mitume wote Sababu ya kuchukuliwa ahadi hiyo Vita vya Makundi (Ahzaab) Mwenyezi Mungu alivyowasaidia Waislamu kwa upepo Msaada wa majeshi ya malaika Majeshi ya makafiri yaliyowazukia Waislamu Wasiwasi na wahka waliokuwa nao Waislamu Mtihani wa Mwenyezi Mungu kwa Waislamu Yaliyosemwa na wanafiki Visingizio vya wanafiki Wanafiki si watu wa kuamania Funzo kwa wanaharakati wa Kiislamu Mauti hayakimbiliki Sifa za wanafiki Muhammad (s.a.w.w.): Ruwaza njema Msimamo wa waumini wa kweli Khiana ya Banii Quraydhwa na matokeo yake Kuhusu wake wa Mtume (s.a.w.w.) Wateue moja ya mambo mawili Mafunzo matatu makubwa Adhabu yao ni mara mbili ya wengine Wao si kama wanawake wengine Wanapozungumza wasilegeze sauti zao Wakae majumbani mwao Madhara ya wanawake kutokaa majumbani Wasidhihirishe mapambo yao Baina ya jahilia ya kwanza na ya leo Waliyoandaliwa Waislamu na Mwenyezi Mungu Waumini lazima wafuate la Mwenyezi Mungu na Mtume Wake

5 Kisa cha Zayd b. Haaritha na mke wake Mtume (s.a.w.w.) anamposea Zayd Anamnasihi asimwache mke wake Alilolificha Mtume (s.a.w.w.) moyoni mwake Tuhuma dhidi ya Mtume haina mashiko Kuowa mtalaka wa mtoto wa kupanga ni halali Lengo ni kubatilisha dasturi ya kijahilia Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho Kumkumbuka Mwenyezi Mungu Sifa tano za Mtume Muhammad (s.a.w.w.) Talaka na hukumu zake Ndoa za Mtume (s.a.w.w.) na hukumu zake Aruhusiwa kuowa zaidi ya wake wanne Bila ya kutoa mahari Anaachiwa hiari ya kugawanya noba Hikima ya hukumu hizo Hakuruhusiwa kuongeza/kupunguza wake zake Nyumba za Mtume (s.a.w.w.) na adabu zake Msiziingie bila ya ruhusa Msende wakati wa kuandaa chakula Mkisha kula nendeni zenu Sababu ya kuwekwa sharia hizi Semeni na wake zake nyuma ya mapazia Ni haramu kuowa wake zake baada yake Hikima yake ni nini Wanaoruhusiwa kuonana nao Jinsi ya kumswalia Mtume (s.a.w.w.) Wanaomuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wana laana Wanawake kujivutia nguo na kujisitiri Onyo kali kwa wanafiki Kiyama kitakuja lini? Makafiri na hali yao Motoni Mayahudi walivyomtaabisha Nabii Musa (a.s.) UchaMungu na Mafanikio yake Amana iliyokataliwa na viumbe vyote ila Mwanadamu VIJALIZO I. Ahlul Bayt ni nani? Ni watu watano waliotajwa na Mtume (s.a.w.w.)? Ni wake wa Mtume (s.a.w.w.)? Ni walioharamishiwa sadaka? Funzo kubwa la aya hii II. Muhammad: Mtume wa Mwisho Lini Mtume huhitajiwa

6 Ushahidi wa Qur ani Tukufu Zaidi ya hayo Ushahidi wa Hadith za Mtume (s.a.w.w.) Ushahidi wa maneno ya maimamu Ushahidi wa komangano la maswahaba Ushahidi wa komangano la wanazuoni Ushahidi wa maneno ya Mirza Ghulam Ahmad Ushahidi wa makamusi Hujja za Makadiani na majibu yetu III. Hikima ya ndoa za Bwana Mtume (s.a.w.w.) Kipindi cha Kwanza Kipindi cha Pili Kipindi cha Tatu Kipindi cha Nne Tathmini ya Ndoa Hizo IV. Ati kweli Mtume harithiwi? Wanaoamini kwamba harithiwi Wanaoamini kwamba anarithiwa Ni kinyume na Qur ani Tukufu Ni kinyume na Hadith za Mtume (s.a.w.w.) Ni ya Bwana Abu Bakar peke yake Mitume waliotangulia pia walirithiwa Ni jitihadi ya wanazuoni Nadharia ya sawa ni ipi hapo? SHUKRANI Shukrani nyingi kwa Baraza la Ilimu ya Kiislamu (The Islamic Education Board of the World Federation of Khoja Shia Ithna-Asheri Muslim Communities) la London, Uingereza kwa kugharimia uchapaji wa kitabu hiki. Mwenyezi Mungu awalipe malipo mema, amin.

7 DIBAJI Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na swala na salamu zimshukie Mtume Muhammad na aali zake wema waliotakaswa wakatakasika. Hii ni tafsiri yangu ya tatu ya baadhi ya sura za Qur ani Tukufu. Ya kwanza ilikuwa ni ya Sura Al-Talaaq yenye tafsiri na maelezo ya aya zake. Hii niliitoa mwaka wa Ya pili ni ile ya Juzuu ya Amma ambayo, kwa kuombwa na Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa wakati huo aliyekuweko Nairobi, na ambaye aligharamia uchapaji wake, niliitoa mwaka wa Hii ilikuwa ni tafsiri ya aya peke yake; haikuwa na maelezo. Ionekanavyo, tafsiri hii imependwa sana kwa vile ambavyo, mpaka hivi sasa, ishachapishwa mara nyingi sana nisizozijua idadi yake, na kusambazwa kila mahali, khaswa vyuoni (madrasa). Zaidi ya hilo, jambo la kutia moyo ni kuona kuwa umadhihabi haukutiwa maanani sana katika kuisambaza. Hata hivyo, kwa sababu ambazo wanazijuwa wao wenyewe, baadhi ya waliojitolea kuieneza hawakupendelea kulichapa jina langu katika nuskha (nakala) walizozitoa! Hata hivyo, ni wajibu wangu kuwaombea Mwenyezi Mungu awalipe malipo mema - hapa duniani, na kesho Akhera; amin. Ya tatu ndio hii iliyo mikononi mwako. Inshallah ni nia yangu kuendelea kuandika tafsiri za sura nyengine mbalimbali pamoja na maelezo yake, popote nitakapopata wasaa; na kuwafikiwa ni kwa Mwenyezi Mungu. Kazi hii ya kufasiri Qur ani Tukufu sikuianza mwaka wa 1981 nilipoitoa tafsiri ya Sura Al-Talaaq. Nilianza kabla ya hapo katika mwaka wa 1960: baada ya Sheikh Muhammad Abdalla Ghazali (maarufu: Mwalimu Ghazali) kufariki dunia. Katika mwezi wa Ramadhani Sheikh Ghazali, aliyekuwa mmoja wa wanafunzi wakubwa wa Sheikh Al Amin bin Aly Mazrui, alikuwa na darasa mbili za tafsiri ya Qur ani Tukufu katika mji wa Mombasa. Darasa moja, baada ya swala ya adhuhuri, aliifanya Msikiti wa Mnara (maarufu: Msikiti wa Bashekhe). Wengi wa waliokihudhuria darasa hii walikuwa ni wakazi wa Mji wa Kale (Old Town) ambao, kwa maneno ya marehemu Sheikh Ghazali mwenyewe, Uislamu ulikuwa ni kabila yao! Kwa ajili hii aliruhusu maskhara na dhihaka katika suali alizokiulizwa! Ya pili, baada ya swala ya alasiri, aliifanya Msikiti wa Shibu. Wengi wa waliokihudhuria hii walikuwa ni wakazi wa mitaa ya Majengo. Hawa, Sheikh Ghazali alikisema, wamekuja kufuatia dini. Kwa hivyo hakuruhusu maskhara wala dhihaka. Kusema kweli, katika darasa hii, alikiwa mkali sana kwa yeyote aliyekifanya maskhara. Alipofariki dunia mwaka wa 1959, mwanafunzi wake mkubwa na mkono wake wa kulia i

8 (Sayyid Abdulrahman Alawy Saggaf; maarufu: Mwalimu Saggaf) alinitaka mimi nishike na kuendelea na darasa hizo. Kusema kweli, kwanza niliogopa kujitweka mzigo huo kwa sababu ya kutojiamini. Lakini baadaye, baada ya yeye kunihakikishia kuwa atakuwa na mimi kwa lolote litakalonitokea, nilikubali; nikatawakali. Hata hivyo, sikuweza kuzishika zote darasa mbili; nilishika ile ya Shibu peke yake. Niliishika darasa hiyo kuanzia 1960 hadi Nilipohamia Nairobi kwa kazi, mwaka wa 1965, niliendelea nayo huko katika mtaa wa Pumwani, ujilikanao pia kwa jina la Majengo. Hata hivyo, kwa kuwa msikitini kulikuwa na darasa ya Sheikh Ahmad Muhammad Chole iliyonitangulia kwa miaka mingi, sikuweza kuendelea na yangu huko. Badali yake nilianza kwenye Ukumbi wa Makumbusho wa mtaa huo kwa miaka miwili mitatu hivi. Baadaye, kwa ruhusa ya Sheikh Chole - yeye mwenyewe - na wazee wa mtaa, ndipo nilipohamia msikitini (Msikiti wa Riadha) ambako niliendelea mpaka mwaka wa 1990 nilipostaafu na kurejea Mombasa. Wakati huo nilikuwa nishajitokeza kuwa ni Shia. Kwa hivyo, kwa ushawishi wa viongozi (sio mashekhe) wengi wa kisunni na mashekhe wa kiwahabi, misikiti mingi ya kisunni iliogopa kunifungulia milango yao. Kwa sababu ya hili ilinilazimu kufanya darasa zangu hizo katika ukumbi wa Bilal Muslim Mission ya Kenya (Mombasa) kuanzia mwaka wa 1991 hadi Kwa kuongezeka wasikilizaji, waume kwa wake (ambao wengi wao walikuwa vijana wa kisunni), ilibidi tutafute ukumbi mkubwa zaidi. Hivyo kuanzia 1994 hadi 1996 tulihamia Ukumbi wa Wanawake wa Kiasia (Asian Women Hall). Miaka ya pekee ambayo sikuwa na darasa Kenya ni 1997 (niliposomesha Dar es Salaam) na 1999 (niliposomesha London). Mtindo wa kufanya darasa zangu hizo katika ukumbi huo usio na fungamano na Uislamu uliwakera baadhi ya wasikilizaji na wapenzi wangu, akiwamo Sheikh Ali Muhammad Mwinzagu (Kadhi wa Mombasa). Baada ya mashauriano na baadhi yao, ilipendekezwa waendewe wakuu wa Jumuiya ya Mabulushi kuombwa waturuhusu kutumia ukumbi wao ulio karibu na Msikiti wa Mbaruku. Walipoendewa na Sheikh Ali M. Mwinzagu, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo alitoa ruhusa, na Ramadhani mosi ya mwaka wa 1418H (1998) tukaanza darasa yetu katika Ukumbi wa Baluchi. Usiku wa hiyo hiyo Ramadhani mosi nikapata simu ya Sheikh Ali M. Mwinzagu kuniambia kesho yake nisende ukumbi huo kwa sababu ya kutoelewana kulikozuka baina ya viongozi wa Jumuiya hiyo kwa ajili yangu! Nami sikwenda. Lakini baadhi ya watu, kwa kutojua yaliyopita, walikwenda. Walipoona milango imefungwa walinijia, nami nikawaeleza yaliyotokea. Kati ya hao ni baadhi ya vijana wa kisunni waliopendezwa na darasa zangu, na waliokuwa na ukumbi wao katika mtaa wa Floringi. Wao walinijia na kuniomba tuendelee na darasa yetu huko. Nami, baada ya mazungumzo marefu, na baada ya kunihakikishia kuwa kilichoniuma jana leo hakinitambai, nilikubali. Ndipo tarehe tatu ya Ramadhani ya mwaka huohuo wa 1418H (1998) tulipoanza darasa yetu katika ukumbi huo unaojulikana kwa jina la Al-Amaan Social Hall. Hapo niliendelea mpaka mwaka wa 2001 nilipokata shauri ii

9 ya kutoendelea tena na tafsiri ya mdomo, bali hata na mihadhra! Badali yake nishughulike na uwandishi wa tafsiri ya Qur ani Tukufu na vitabu vyengine vya dini. Katika kuiandika tafsiri hii, mbali na vitabu nilivyovirejelea (uk. viii-xi humu), nimesaidiwa sana na mazungumzo yangu na mashekhe-swahibu zangu pamoja na wanafunzi wangu. Wote hao nawashukuru pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu awajazi majaza mema - hapa duniani na kesho Akhera. Hata hivyo, kwa ajili ya kazi kubwa ya kuutayarisha muswada wa tafsiri hii, aliyoifanya kwa kujitolea na kwa bidii kubwa, napenda kumshukuru kwa jina mmoja wa wanafunzi wangu walio karibu mno na mimi, Sayyid Ahmad Agil Jamalil Layl. Mwisho, kama mtakuwa na lolote la makosa katika tafsiri hii, basi jukumu la kosa hilo ni langu peke yangu; na kwalo ninamuomba Mwenyezi Mungu anisamehe. Lakini kama hamtakuwa na la makosa, basi wa kushukuriwa ni Mwenyezi Mungu na wote walionisaidia kwa fikra zao njema njema. Mombasa, Kenya 21 Shawwaal, Disemba, 2003 Abdilahi Nassir iii

10 UTANGULIZI WA SURA Jina Sura hii imepata jina lake la Al-Ahzaab (makundi) kutoka aya ya 20 ya sura hii. Ilipoteremshwa Kama tunavyojua, Qur ani Tukufu ina jumla ya sura 114. Sura hizo zimegawanywa mafungu mawili makubwa kwa kutegemea muda ambapo aya zake ziliteremshwa. Zile zilizoteremshwa wakati Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipokuwa bado yuko Makka (hajahamia Madina) huitwa Makkiyya (za Makka), na zile zilizoteremshwa baada ya kuhamia Madina huitwa Madaniyya (za Madina). Kwa kuwa inazungumzia matukio matatu muhimu katika historia ya Kiislamu, ambayo yote yalitokea baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuhamia Madina, sura hii huitwa Madaniyya. Matukio hayo ni yale ya Vita vya Handaki (au Makundi) vilivyokuwa katika Shawwaal (Mfungo Mosi) ya mwaka wa 5H; mashambulizi ya Banii Quraydhwa yaliyofanywa katika Dhil Qa dah (Mfungo Pili) ya huohuo mwaka wa 5H; na ndoa ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kumuowa Bi. Zaynab bt. Jahsh ambayo vilevile ilikuwa katika hiyo Dhil Qa dah ya mwaka wa 5H. Yanayozungumzwa humu Ukizitaamali khalfia za sehemu kubwa ya aya zake, utaona kwamba sura hii haikushughulika na muktadha mmoja au maudhui mamoja, bali imeshughulika na maudhui mengi mbalimbali. Mwanzo kabisa (aya ya 1-3) Bwana Mtume (s.a.w.w.) na, kwa kupitia kwake yeye, Waislamu wote wanaamrishwa na kuonywa kwamba wasiwafuate makafiri na wanafiki katika ukafiri na unafiki wao, bali wafuate yale ya Mwenyezi Mungu peke yake na wamtegemee Yeye; wasitegemee nguvu zozote nyengine. Aya tatu hizo zimetangulizwa ili ziwe ni mwongozo wa kuamulia migongano iliyotokea baina ya Uislamu na ya Ukafiri yanayoelezwa katika aya zinazofuatia. Ili kuyafafanua hayo, aya mbili zinazofuatia (ya 4-5) zinatunabihisha mtu mmoja hawezi kuwa na nyoyo mbili katika kifua kimoja hata aweze kufuata mambo mawili yanayopingana. Haiwezekani kuyaamini yanayoamrishwa na Uislamu, na wakati huohuo ukayaamini yanayolekezwa na Ukafiri. Ukifanya hivyo, hutakuwa Mwislamu tena, bali utakuwa mnafiki moja kwa moja - sifa ambayo ni mbaya zaidi kuliko ile ya kuwa kafiri! Kwa msingi huo basi, ndipo Waislamu walipowekewa ile sharia ya kubatilisha dhihaar (tiz. Kidokezo Na. 4 humu) na ile ya kutowafanya watoto wao wa kupanga kuwa sawa na watoto wao khaalisa. Yote hayo yakakhatimishwa kwa agizo la kwamba hakuna yeyote aliye na haki ya iv

11 kuwatawalia Waislamu mambo yao zaidi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ambaye Mitume wote waliomtangulia walichukua ahadi ya kumtolea bishara (aya 6-8). Kuanzia aya 9-27 vinaelezwa Vita vya Makundi (au vya Handaki). Hivi ni vita vilivyotukia mwaka wa 5H; pale makafiri wa Makka, wakishirikiana na mayahudi na wanafiki, walipounda jeshi kubwa sana kwa lengo la kuwaangamiza Waislamu na Dini yao. Mweneyezi Mungu akawapatia ushindi Waislamu kwa kupeleka upepo mkali sana na wa baridi, ulioyang oa mahema yote ya adui zao na kuzima nyoto zao. Aya zinaeleza kuhusu wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza (aya ya 28-31) inazungumzia onyo ambalo Mwenyezi Mungu alitaka Mtume (s.a.w.w.) awape wake zake waliokuwa na kero: kwamba wateuwe baina ya maisha ya dunia na pambo lake na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Nyumba ya Akhera. Kama watataka hilo la kwanza, waseme hivyo waziwazi: nao watapawa kitoka nyumba na kuachwa kwa vizuri. Na kama watataka hilo la pili, basi waambiwe kuwa Mwenyezi Mungu atawaandalia malipo makubwa. Sehemu ya pili (aya ya 32-35) inazungumzia mabadiliko ya kijamii yaliyohitajika kufanywa katika kuiunda jamii mpya ya Kiislamu. Kuhusu hili, mabadiliko yenyewe yalianzwa nyumbani mwa Mtume (s.a.w.w.) yeye menyewe; hivyo wake zake waliamrishwa waache zile dasturi na mila za jahilia ya kizamani, wakae majumbani mwao kwa hishima, na wasilegeze sauti zao wanapozungumza na wanaume. Hayo ni baada ya kuhakikishiwa kwamba wao si kama wanawake wowote wengine kwa vile wao ni wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) - lakini kwa sharti: iwapo watamcha Mwenyezi Mungu. Yeyote katika wao atakayefanya uchafu, atazidishiwa adhabu mara mbili. Na atakayemtwii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na akatenda njema Mwenyezi Mungu atampa malipo yake mara mbili na atamwandalia riziki yenye hishima. Baada ya hayo, ndipo ndoa ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Bi. Zaynab bt. Jahsh, iliyoleta vundo na mshindo mkubwa, inapozungumzwa (aya ya 36-48). Katika aya hizi unajibiwa ule upinzani wa maadui wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) dhidi ya ndoa hii; shaka, zilizokuwa zikitiwa katika nyoyo za Waislamu, zinaondolewa; Waislamu wanaelezwa hadhi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwao, anapoamua jambo; na yeye mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.) analekezwa na Mwenyezi Mungu kutojali kero na udhia wa makafiri, bali amtegemee Yeye maana Yeye peke Yake ndiye Mlinzi wa kweli. Kisha katika aya 49 sharia ya talaka inatangazwa na kutolewa maelezo zaidi ukiilinganisha na Sura 2:229, Katika aya ya sharia za ndoa, zilizowekwa makhsusi kwake, zinaelezwa. Mabadiliko ya kijamii, yaliyotajwa katika aya ya 32-35, yanapanuliwa zaidi katika aya ya Waislamu wakatazwa kuingia nyumbani kwa Mtume (s.a.w.w.) bila ya idhini yake; wafundishwa adabu za kukaa ndani ya nyumba ya Mtume (s.a.w.w.), na pia adabu ya kuzungumza na wake zake; na kwamba wake zake hawaruhusiwi kuolewa na mtu yeyote baada yake. v

12 Katika aya ya 56 Waislamu wanaelezwa jinsi Mwenyezi Mungu na malaika Wake wanavyomwenzi Bwana Mtume (s.a.w.w.), na kwamba wao nao wafanye vivyo hivyo - kwake yeye, na kwa watu wa Nyumba yake (ahlul bayt). Pia (katika aya ya 57-58) Waislamu wanakatazwa kumuudhi Mtume (s.a.w.w.), kama walivyokifanya makafiri, na kuudhiana wao kwa wao pia. Maana wanaofanya hivyo hupata laana ya Mwenyezi Mungu - hapa duniani na Akhera. Katika aya ya 59 khatua nyengine ya mabadiliko ya kijamii inachukuliwa: ya kuwaamrisha wake za Mtume (s.a.w.w.), na wake za waumini wote, wajifunike vizuri wanapotoka nje. Mwisho, kuanzia aya ya 60-73, wanafiki na wajinga wengine wanafichuliwa na kulaaniwa kwa ufisadi wao dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.), Uislamu na Waislamu kwa jumla. vi

13 VIFUPISHO Katika maandishi yaliyomo humu, baadhi ya maneno tumeyachapisha kwa ufupi. Kuwasaidia wasomaji wetu - wasiovielewa - kuvielewa vifupisho hivyo, tunaviorodhesha hapa chini pamoja na maelezo yake: a.s. alayhis/has salaam (maana yake: amani iwe juu yake) b. bin Bi. Bibi B.K. Baada ya Kristo bt. binti Bw. Bwana Dk. Daktari H Hijriya Jz. Juzuu k.m. kwa mfano k.v. kama vile k.w.k. kadhaa wa kadhaa Na. Nambari n.k. na kadhalika n.k.w.k. na kadhaa wa kadhaa n.w. na wengineo r.a. radhiyallaahu anhu/anhaa (maana yake: Mwenyezi Mungu amwelee radhi). s.a.w. swallallaahu alayhi wasallam (maana yake: Mwenyezi Mungu amrehemu na kumteremshia amani). s.a.w.w. swallallaahu alayhi wa aalihii wasallam (maana yake: Mwenyezi Mungu amrehemu na kumteremshia amani, yeye na aali zake). s.w.t. subhaanahuu wata-aalaa (maana yake: kutakasika na mawi [mabaya] na kutukuka ni Kwake). tiz. tizama uk. ukurasa vii

14 UFUPISHO WA VITABU NILIVYOVIREJELEA Baadhi ya vitabu nilivyovirejelea mara kwa mara katika tafsiri hii nimeviandika kwa ufupi katika maelezo. Vyengine nimevitaja kwa ukamilifu. Kati ya nilivyovitaja kwa ufupi ni hivi: VYA TAFSIRI YA QUR ANI TUKUFU 1. al-amthal Al-Amthal Fii Tafsiiri Kitaabillaahil Munazzal ya Sheikh Naasir Makaarim ash-shiiraazi. 2. al-barwani Tarjama ya AL MUNTAKHAB katika Tafsiri ya Qur ani Tukufu ya Sheikh Ali Muhsin al-barwani. 3. Daryabadi Holy Qur an with English Translation and Commentary ya Maulana Abdul Majid Daryabadi. 4. al-farsy Qur ani Takatifu iliyofasiriwa na Sheikh Abdullah Saleh al-farsy. 5. Ibn Kathiir Tafsiir Ibni Kathiir ya Ismail b. Umar ad-dimishqii. 6. al-kaashif Tafsiirul Kaashif ya Sheikh Muhammad Jawaad Mughniyyah. 7. Maududi The Meaning of the Quran ya Syed Abul A la Maududi. 8. Mazrui Tafsiri ya Qur ani Tukufu ya Sheikh Al Amin Bin Aly Mazrui. 9. al-miizaan Al Miizaan Fii Tafsiiril Qur aan ya Sayyid Husayn at-twabaatwabaaii. 10. ar-raazi At Tafsiirul Kabiir ya Imam Fakhruddin ar-raazi. 11. Qadiani KURANI TUKUFU Pamoja na Tafsiri na Maelezo kwa Kiswahili ya Sh. Mubarak Ahmad Ahmadi. 12. al-qurtubi Jaami u Ahkaamil Qur aan ya Muhammad bin Ahmad al-answaari al-qurtubii. 13. al-waadhih at-tafsiirul Waadhih ya Muhammad Mahmud Hijaazii. viii

15 VYA HADITH 1. Abuu Daawuud Sunan Abii Daawuud ya Abuu Daawuud Sulayman as-sajistaani. 2. Bukhari Sahih Bukhari ya Imam Muhammad bin Ismail al-bukhaarii. 3. Daarimi Sunanud Daarimii ya Abdullah bin Abdulrahman ad-daarimii. 4. Ibni Majah Sunan Ibni Majah ya Muhammad bin Yazid al-qazwiinii. 5. Imam Ahmad Musnad ya Imam Ahmad bin Hambal. 6. Muslim Sahih Muslim ya Imam Muslim bin al-hajjaj al-qushayrii. 7. Mustadrak Al-Mustadrak Alas Swahiihayni ya Muhammad bin Abdullah al-haakim an-niisaabuurii. 8. Nasaai Sunanun Nasaaii ya Ahmad bin Shuayb an-nasaaii. 9. Tirmidhi Sunanut Tirmidhii ya Muhammad bin Isa at-tirmidhii ix

16 33 SURA AL-AHZAAB Imeteremshwa Madina Ina aya 73 na makara matano Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu. 1. Ewe Mtume! 1 Mche Mwenyezi Mungu, 2 wala usiwatwii makafiri na wanafiki. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hikima. 2. Na fuata uliyoteremshiwa wahyi kutoka kwa Mola wako. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa habari ya mnayoyatenda. 3. Na mtegemee Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni wa kutegemewa. م ن اف ق ني ط ع ال ك ف ر ين و ال ا انل ب ات ق اهلل و ل ت ه ي ي ا أ ا ١ ك يم ا ح ل يم إ ن اهلل ك ن ع ا ك إ ن اهلل ك ن ب م ب ك م ن ر إ ل وح ا ي و ات ب ع م ا ٢ ب ري ل ون خ م ت ع ف ب اهلل و ك يل ٣ اهلل و ك و ت و ك ع 1 Maneno yaliyomo katika aya hii, na yale yaliyomo katika aya mbili zinazofuatia, yanasemezewa Mtume Muhammad (s.a.w.w.); ndipo yakaanza na Ewe Mtume! Hata hivyo, hivi si kusema kwamba aliyekusudiwa kwa maneno hayo ni yeye peke yake; hasha! Bali amekusudiwa yeye na Waislamu wote kwa jumla, kama inavyoeleweka kwa maneno...mwingi wa habari ya mnayoyatenda... yaliyomo katika hiyo aya ya pili. 2 Hapa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) na, kupitia kwake yeye, Waislamu kwa jumla wanaamrishwa wamche Mwenyezi Mungu wala wasiwatwii makafiri na wanafiki. Hiyo ni amri inayotoka kwa Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa kila lenye maslaha na Waislamu, asiyehukumu isipokuwa kwa lenye hikima. Katika kueleza sababu ya kuteremshwa aya hii, wanazuoni wametaja sababu mbalimbali, zote takriban zikitaja maudhui mamoja - nayo ni haya: Baada ya Vita vya Uhud (3 Hijriya) Abuu Sufyaan, na wakubwa wengine wa makafiri na washirikina, waliomba na wakapawa amani na Mtume (s.a.w.w.); wakaingia Madina. Baada ya kuingia Madina, wao na Abdallah b. Ubayy na jamaa zake wengine wakamwendea Mtume (s.a.w.w.), wakamwambia: Ewe Muhammad! Usiwataje miungu yetu - Laata, Uzzaa na Manaata - kwa uovu. Na sema kuwa wana uwezo wa kuwasamehe wanaowaabudu, nasi tutakuacha wewe na Mola wako. Hilo likamhuzunisha sana Mtume (s.a.w.w.). Umar b. al-khattwaab akasema: Turuhusu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, tuwauwe. Mtume (s.a.w.w.) akasema: Mimi nimewapa amani hawa. Kisha akaamrisha watolewe Madina. Ndipo iliposhuka aya hii kumwamrisha Mtume s.a.w.w. asiyasikilize mashauri kama hayo. 1

17 JUZUU YA Mwenyezi Mungu hakumjaalia mtu yeyote kuwa na nyoyo mbili ndani ya mwili wake. 3 Wala hakuwafanya wake zenu - ambao mnailinganisha migongo yao na migongo ya mama zenu - kuwa ni mama zenu. 4 Wala hakuwafanya watoto wenu wa kupanga kuwa ni watoto wenu khaswa. 5 Hayo ni maneno ya vinywa vyenu tu. 6 Na Mwenyezi Mungu ndiye anayesema kweli, na Yeye ndiye anayeongoza Njia. AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA و ف ه و م ا ج ع ل ب ني ف ج ن ق ل ل م ع ل اهلل ل ر ج م ا ج ا ات ك م و م ه م ه ن أ ك م الل ئ ت ظ اه ر ون م ن و اج أ ز ل ك م ق و ل ك م ن اء ك م ذ ب ع ي اء ك م أ د ج ع ل أ ف و اه ك م و اهلل ي ق ول ال ب أ د ي الس ب يل ٤ ه و ي ق و ه 3 Maneno haya yana lengo la kutufunza kwamba ni muhali moyo mmoja kuamini itikadi mbili zisizowafikiana au rai mbili zinazopingana. Hivyo, kama kutakuwa na rai mbili zinazopingana bila shaka zitakuwamo katika nyoyo mbili, sio moyo mmoja. Na kwa kuwa mtu mmoja hawezi kuwa na nyoyo mbili ndani yake, ndiyo vivyo hivyo: hawezi kuamini kwa wakati mmoja vitu viwili vinavyopingana. Baadhi ya wanazuoni wamesema kwamba maneno haya yamekuja kama utangulizi wa yale yanayofuatia - ya dhihaar na ya mtoto wa kupanga. Maana katika dhihaar, mtu humfanya mke wake kama mamake; na katika mtoto wa kupanga, mtu humfanya mtoto huyo kama mtoto wake halisi (wa kumzaa)! Na hivyo sivyo! Mke hawi ni mama, kama ambavyo mtoto wa kupanga hawi mtoto halisi wa mtu. Hao ni watu wawili tafauti wenye hadhi mbalimbali. Kwa hivyo hawawezi kuwa na hadhi moja katika moyo mmoja ila mtu awe na nyoyo mbili; na Mwenyezi Mungu hakumjaalia hilo. Pia tunaweza tukasema kwamba maneno hayo yanatufafanulia zaidi yale ya kutowatwii makafiri na wanafiki, yaliyomo katika aya ya kwanza hapo juu, na yale ya kufuata wahyi wa Mwenyezi Mungu, yaliyomo katika aya ya pili. Mtu hawezi kufuata ya Mwenyezi Mungu, na wakati huohuo akawa anawatwii makafiri na wanafiki. Imani mbili hizo, zinazopingana, haziwezi zikakaa katika moyo mmoja. Zitahitajia nyoyo mbili ambazo hakuna binadamu mwenye nazo. 4 Kabla ya Uislamu Waarabu walikuwa na ada ya mtu, anapotaka kumtaliki mke wake, kumwambia: Wewe kwangu ni kama mgongo wa mamangu au: Mgongo wako kwangu ni kama mgongo wa mamangu. Na papo hapo talaka huwa ishapita! Ada hii, ambayo hujulikana kwa jina la dhihaar katika sharia ya Kiislamu, haikubaliwi na Uislamu. Kusema kweli, yeyote anayemwambia mke wake hivyo, huwa - kwa sharia ya Kiislamu - hana haki ya kumkurubia mke wake huyo mpaka atoe kafara. Akitoa kafara, na asimwendee mke wake, basi mke huyo ana haki ya kumwendea kadhi ambaye atamwamrisha bwana huyo amwache mke wake huyo kwa mujibu wa sharia za Kiislamu, au atoe kafara na waendelee na maisha yao ya ndoa. Kwa maelezo zaidi ya jambo hili, tizama Sura 58: Hii nayo ni ada nyengine iliyokuwako kabla ya Uislamu. Nayo ilikuwa hivi: Mtu alikichukua mtoto ambaye si wake wa kumzaa, akamfanya ni wake khaswa. Akampa nasaba yake na haki zote ambazo mtoto wa kumzaa anazo kwa babake halisi; ikawa wanarithiana, na mke wa mtoto huyo kutoweza kuolewa na baba huyo - kama mtoto huyo atamwacha - na kinyume chake. Kwa maneno haya katika aya hii, ada hii imepigwa marufuku. 6 Hilo la kuwaita watoto wa kupanga kwa ubini wenu ni maneno yanayotoka vinywani mwenu tu. Hayabadilishi ukweli hata chembe. Ukweli ni huu anaousema Mwenyezi Mungu - kuwa si watoto wenu halisi. 2

18 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA 5. Waiteni kwa baba zao. Hilo ni adilifu وا م ل ع ق س ط ع ند اهلل ف إ ن ل م ت وه م ل ب ائ ه م ه و أ اد ع zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. 7 Na س mkiwa hamwajui baba zao, basi ni ndugu ي ال ك م و ل و ك م ف ادل ين و م ان و آب اء ه م ف إ خ ل ي ك م ج ن اح ف يم ا أ خ ط أ ت م ب ه و ل ك ن م ا ت ع م د ت zenu katika Dini, na rafiki zenu. 8 Wala ع hamna lawama kwa mliyoyakosea, lakini lawama mnayo kwa yale yaliyofanywa ا ٥ ح يم ا ر ور ف ق ل و ب ك م و ك ن اهلل غ makusudi na nyoyo zenu. 9 Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. 7 Hivyo waiteni watoto hao kwa ubini wa baba zao waliowazaa, hata kama si Waislamu. Maana kufanya hivyo ndio uadilifu kwa Mwenyezi Mungu. Maneno Hilo ni adilifu zaidi... katika aya hii hayamaanishi kwamba kuwaita watoto hao kwa ubini wa baba zao wa kuwalea ni uadilifu, lakini kuwaita kwa ubini wa baba zao wa kuwazaa ni uadilifu zaidi; hasha. Huo ni aina ya msemo tu unaotumiwa katika hali fulani. Ni kama vile kusema mathalan: Ni bora mtu kutahadhari asijitie katika hatari. Hilo halimaanishi kwamba kujitia hatarini ni jambo zuri, lakini kutahadhari ni bora; hasha! Muradi hapo ni kulinganisha lililo zuri na baya tu. Kutokana na aya hii, ni kosa vilevile kuwanyima watu wanaosilimu ubini wa baba zao waliowazaa - hata kama wao hawakufuata watoto wao hao katika Uislamu - na kuwaita kwa ubini wa wale waliowasilimisha. La sawa, baada ya kumpa jina la Kiislamu mtu aliyesilimu, ni kumwacha aendelee kutumia ubini wa babake wa kumzaa - kwa jina lilelile analoiumia lisilokuwa la Kiislamu. 8 Kutowajua baba zao hakuwapi nyinyi haki ya kuwaita kwa majina ya mababa wengine, bali waiteni kama ndugu zenu katika Dini au rafiki zenu. Neno la Kiarabu katika aya hii, tulilolifasiri kama rafiki zenu, ni mawaaliikum. Na neno hilo ni wingi wa neno mawlaa. Wanazuoni wa Tafsir hulifasiri neno mawlaa kwa maana mbalimbali. Wengine hulifasiri kwa maana ya rafiki au swahibu. Na wengine hulifasiri kwa maana ya mtumwa aliyeachwa huru; maana baadhi ya hao watoto wa kupanga walikuwa ni watumwa walionunuliwa na kuachwa huru. Kwa kuwa bwana zao waliowamiliki walikuwa wakiwapenda sana, walikuwa wakiwachukulia kama watoto wao. Hivyo muradi wa neno mawlaa hapa ni wale watumwa walioachwa huru ambao, kwa sababu ya muamala mzuri waliofanyiwa na waliokuwa bwana zao, walipendelea kuendelea na uhusiano wao. Mfano mzuri ni ule wa Zayd b. Haaritha. Yeye alikiitwa Zayd b. Muhammad baada ya kuachwa huru na Bwana Mtume (s.a.w.w.). Lakini mara tu iliposhuka aya hii hapo juu, Bwana Mtume (s.a.w.w.) akamwambia: Wewe ni Zayd b. Haaritha. Na watu baada ya hapo wakawa humwita Zayd, mawlaa Rasulillahi. Mfano mwengine ni wa Salim aliyekuwa mtumwa wa Abuu Hudhayfa. Yeye alikiitwa kwa ubini wa aliyekuwa bwana wake baada ya kuachwa huru. Lakini baada ya kuteremshwa aya hii akaitwa Salim mawlaa Abii Hudhayfa. 9 Mkiwa mtamwita mtu kwa jina la asiyekuwa babake wa kumzaa, kwa kudhania kuwa ndiye babake, au kwa ajili ya mazowea, au kwa kutelezwa na ulimi, basi hapo hamtakuwa na makosa. Mwenyezi Mungu atawasamehe. Lakini mkiwa mtafanya hivyo kwa makusudi, basi hapo mtakuwa mmefanya kosa, na mtaadhibiwa kwalo. Amesema Bwana Mtume (s.a.w.w.): Umma wangu wamesamehewa kwa walifanyalo kwa makosa, kwa kusahau, walilotenzwa nguvu kulifanya, wasilolijua, wasiloliweza ila kwa mashaka, na lililowadharurikia (al-kaashif). 3

19 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ه ات ه م 6. Mtume ana haki zaidi kwa waumini kuliko م و اج ه أ و أ ز س ه م نف ؤ م ن ني م ن أ انل ب أ و ل ب ال م waliyonayo wao juu ya nafsi zao. 10 Na wake zake ni mama zao. 11 Na jamaa wana haki و ل ب ب ع ض ف ك ت اب اهلل م ن ه م أ ض ع ام ب ح و ال ر و أ ول zaidi wao kwa wao katika Kitabu cha ائ ك م ل وا إ ل أ و ل ع ف ن ت ر ين إ ل أ Mwenyezi Mungu kuliko waumini wengine اج ه م ؤ م ن ني و ال ال م ا na wahamiaji, 12 ila muwe mnawafanyia ٦ ك ت اب م س طور م ع ر و ف ا ك ن ذ ل ك ف ال wema marafiki zenu. 13 Haya yamekwisha andikwa Kitabuni. 10 Mtume (s.a.w.w.) ana haki zaidi kwa waumini kuliko nafsi zao katika kila kitu - katika mambo ya kidunia na ya kiakhera. Hivyo ni wajibu juu yao kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.) kuliko asiyekuwa wao - hata nafsi zao. Na hukumu yake (Bwana Mtume (s.a.w.w.)) iwe ndiyo yenye nguvu juu yao kuliko hukumu yao. Na haki yake iwe ndiyo yenye kuthubutu zaidi kwao kuliko haki zao, nafsi zao ziwe mhanga kwa ajili yake, na miili yao iwe ni kinga yake dhidi ya kila shari. Na kila aliloliamrisha au alilolikataza wawe ni wenye kulipokea kwa kuliamini, kwa kuwa ni uwongozi na mwongozo kwao, ili wafuzu hapa duniani na Akhera... (al-waadhih). Hilo, kwa yeyote mwenye fahamu zake, haliwi ni ajabu. Maana Bwana Mtume (s.a.w.w.) ni ma suum (hafanyi dhambi wala hakosei) na ni wakili wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.). Hafikirii wala haamui jambo lisilo na maslaha na jamii au mtu; wala hafuati matamanio yake abadan. Hili limeelezwa wazi katika Sura 53:3. Vilevile, katika aya ya 36 ya Sura hii, Mwenyezi Mungu anatwambia: Haiwi kwa muumini mwanamume wala muumini mwanamke, Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanapoamua jambo, kuwa na hiari... Na katika Hadith tunaambiwa: Haamini mmoja wenu mpaka matamanio yake yawe ni yenye kufuata niliyoyaleta. (Bukhari). Pia: Ninaapa kwa ambaye nafsi yangu i mkononi Mwake! Haamini mmoja wenu mpaka niwe ninapendeza zaidi kwake kuliko nafsi yake, watoto wake na watu wote. (Bukhari). Hali kadhalika: Hakuna muumini ila mimi ndimi mwenye haki zaidi juu yake kuliko mtu yeyote duniani na Akhera. (Bukhari). 11 Umama huu si wa kuzaa; ni wa hishima na kuwatukuza tu. Kama vile ambavyo Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ni baba wa kiroho wa waumini, ndivyo hivyohivyo walivyo wake zake, ni mama zao wa kiroho. Kutokana na hilo, Mwenyezi Mungu amewaharamishia waumini kuwaoa mabibi hao baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuwaacha au kufariki dunia (tiz. aya ya 53 humu). Lakini hakuwafanyia hivyo watoto wao. Wao wanaweza kuowana nao. 12 Kama inavyojulikana katika historia, Waislamu walihama Makka kukimbia mateso waliyokuwa wakiteswa na makafiri wa huko. Walikimbilia Madina ambako walipokelewa vizuri na ndugu zao, Waislamu wa huko, waliojitolea kushirikiana nao kwa kila walichokuwa nacho. (Sura 59:9). Kwa kuwa hali ya Waislamu wa Madina ilikuwa karibu kama ile ya ndugu zao wa Makka - ya kupigwa vita na jamaa zao waliokuwa makafiri - Bwana Mtume (s.a.w.w.) alijenga udugu baina ya Waislamu wa Makka (muhaajiruun) na wale wa Madina (answaar); wakawa ndugu hata wa kurithiana. Hata hivyo mpango huu, tangu mwanzo haukukusudiwa uwe wa kudumu. Ulikuwa ni wa muda tu. Uislamu ulipopata nguvu, na wapinzani wengi kusilimu, Mwenyezi Mungu aliuondoa mpango huo kwa aya hii; ikawa msingi wa kurithiana si wa dini peke yake, bali na ujamaa na udugu wa damu pia. Na huu ndio muradi wa maneno ya aya hii hapo juu. 13 Kuondolewa mpango wa mirathi kwa msingi wa udugu wa kidini peke yake, na kuongezwa msingi wa ujamaa na udugu wa damu, hakumaanishi kwamba Mwislamu hana tena nafasi ya kumtendea wema asiyekuwa ndugu wa damu; hasha, bali bado anayo nafasi hiyo. Anaweza, akipenda, kumwachia urathi 4

20 JUZUU YA Na kumbuka tulipochukua ahadi kwa mitume na kwako wewe, na kwa Nuhu na Ibrahimu na Musa na Isa mwana wa Mariamu; na tulichukua kwao ahadi ngumu Ili Mwenyezi Mungu awaulize wakweli 15 juu ya ukweli wao. Na amewaandalia makafiri adhabu yenye kutia uchungu. AL-AHZAAB 33 asiyekuwa ndugu/jamaa yake wa damu, hata kama si Mwislamu. Lakini kwa sharti. Na sharti yenyewe ni kwamba atakachousia kisizidi thuluthi moja ya tarka yake yote. Na huo ndio muradi wa maneno ila muwe mnawafanyia wema marafiki zenu hapo juu. Kama mtu huyo hakuacha wasia wa aina.hiyo, basi tarka yake yote itarithiwa na hao jamaa zake kwa mujibu wa sharia za mirathi. 14 Ni ahadi gani hiyo iliyochukuliwa kwa mitume wote hao? Hapa haikutasuliwa. Lakini tunapoitaamali aya nyengine ya Qur ani, ambapo ahadi ya mitume imetajwa, tunaweza tukaielewa ni ahadi ipi hiyo. Aya yenyewe ni hii: Na pale Mwenyezi Mungu alipochukua ahadi ya mitume kwamba: Nikishawapa Kitabu na hikima, kisha akawajia Mtume mwenye kuwafikiana na mlichonacho, ni juu yenu mumwamini na mumnusuru. Akawambia: Jee, mmekubali na mmechukua ahadi Yangu kwa hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema Mwenyezi Mungu: Shuhudieni, na Mimi pamoja nanyi ni katika wenye kushuhudia (Sura 3:81). Kutokana na aya hiyo basi, tunaona kwamba ahadi ambayo Mwenyezi Mungu aliichukua kwa mitume wote waliomtangulia Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ni kwamba atakapokuja yeye ambaye wito wake utakubaliana na wito wao - itawalazimu wamwamini na kumsaidia. Mitume hao wakalikubali hilo na kuwajulisha wafuasi wao kama ipasavyo (k.m. Sura 61:6). Mbali na kuichukua ahadi hiyo kwa mitume, Mwenyezi Mungu aliichukua hata kwa wafuasi wao, kama ilivyo wazi katika Sura 3:187, kwa mfano. Na hilo limethubutu hata katika Biblia (tiz. Kumbukumbu 18:17-19 na Yohana 16:7-14). 15 Hapa Mwenyezi Mungu anaeleza kwamba alituma mitume akachukua ahadi kwao ili awaulize wakweli juu ya ukweli wao... Lakini wakweli hao ni kina nani? Kwa mujibu wa aya nyengine za Qur ani (Sura 49:15), wakweli ni wale ambao wamemwamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, kisha wakawa hawakufanya shaka kabisa, na wakapigana jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao... na (Sura 59:8) wale mafakiri wahamiaji waliotolewa majumbani mwao na mali yao kwa ajili ya kutafuta fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na radhi Zake, na wanamnusuru Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Hao ndio wale wanaoelezwa, katika aya ya 23 ya Sura hii, kuwa ni watu waliotimiza waliyoahidiana na Mwenyezi Mungu. Kwa maneno mengine, muradi wa wakweli katika aya hii ni wale ambao wamethibitisha ukweli wao na imani yao katika nyanja za kuihami Dini ya Mwenyezi Mungu, wakapigana jihadi na kusimama imara mbele ya matatizo yaliyowakabili kwa kuzitoa mhanga roho zao na mali yao. Na jee, hilo watakaloulizwa na Mwenyezi Mungu ni lipi? Na wapi? Kwa dhahiri ya aya hii, na maelezo tuliyoyaeleza hapa, wataulizwa suala hiyo Siku ya Kiyama. Na watakaloulizwa ni: Jee waliithibitisha imani yao hiyo kwa vitendo? Na pia katika midani; walipigana jihadi kwa mali yao na nafsi zao? 5 UTLU MAA UHIYA ا م ن انل ب ي ن ذ خ و إ ذ أ و ع يس وس و إ ب ر اه يم و م يث اق ا غ ل يظا ٧ م وح م و م نك و م ن ن ه ني م يث اق م ه ا م ن ن ذ خ م و أ ي ر اب ن م ا ٨ ل م ا أ اب ذ د ل ل ك ف ر ين ع و أ ع ل الص اد ق ني ع ن ص د ق ه م ي سأ ل

21 JUZUU YA Enyi mlioamini! Zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu zilizo juu yenu pale mlipojiwa na majeshi, 16 nasi tukayapelekea upepo 17 na majeshi ambayo hamkuyaona. 18 Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona mnayoyatenda. AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ا ال ين آم ن وا اذ ك ر وا ن ع م ة اهلل ع ل ي ك م ه ي ي ا أ س ل ن ا ع ل ي ه م ر حي ا و ج ن ود ا ل م ر ك م ج ن ود ف أ اء ت إ ذ ج ا ٩ ص ري ون ب ل م ع ا ت ا و ك ن اهلل ب م ه ت ر و 10. Walipowajia nyinyi kutoka juu yenu, na kutoka chini yenu; 19 na macho yalipokodoka, na nyoyo zikapanda kooni, nanyi mkamdhania Mwenyezi Mungu kila dhana. 20 ن ف و ق ك م و م ن أ س ف ل م نك م و إ ذ م م اء وك إ ذ ج ن اج ر و ت ظ ن ون ب ص ار و ب ل غ ت ال ق ل وب ال ت ال ز اغ ا ١٠ ب اهلل الظ ن ون 16 Majeshi haya ni yale yaliyowazukia Waislamu katika vita vijulikanavyo katika historia kwa jina la Vita vya Makundi au Vita vya Handaki vilivyopiganwa katika mwaka wa 5 Hijriya. Makundi hayo yalikuwa ni muungano wa makabila mbalimbali ya Kiarabu na ya Kiyahudi yenye lengo moja tu: la kuwaangamiza Waislamu na Dini yao. Jumla majeshi hayo yalikuwa na watu baina ya 10,000 na 12,000. Waislamu walikuwa kama 3,000 hivi. Kuanzia aya hii mpaka ile ya 27 tunaelezwa habari ya vita hivyo. 17 Upepo huu ni ule uliopiga majeshi ya makafiri. Ulikuwa mkali sana na wa baridi, na uliyang oa mahema yote ya makafiri na kuzima nyoto zao. Sir William Muir, katika kitabu chake kiitwacho Life of Muhammad (uk ) aliieleza hivi hali hiyo: Chakula cha farasi kilipatikana kwa shida kubwa; vyakula vya watu vikawa vinakwenda vikipungua, na ngamia na farasi wakawa hufa kila siku kwa idadi kubwa. Wakiwa wamechoka na roho kuingia maji, usiku wenye baridi na tufani uliwaingilia. Upepo na mvua ikaipiga vibaya vibaya kambi yao isiyo na kinga. Tufani ikazidi na kuwa kimbunga. Nyoto zao zikazima, mahema yao yakang oka, vyombo vya kupikia na vifaa vyengine vikatupiliwa mbali. Akiwa anasikia baridi na asiye na furaha, Abuu Sufyaan ghafla aliamua kuondoka papo hapo. Aliwaita wakubwa wa majeshi yake haraka haraka, akawajuza uamuzi wake: Vunja kambi, alisema, na ondokeni. Mimi, kwa upande wangu, ninaondoka. Kumaliza maneno haya, alimrukia ngamia wake (haraka yake, tunaambiwa, ilikuwa kubwa mno) hali mguu wake wa mbele haujafunguliwa kigogoni, akaongoza njia. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu alivyowasaidia Waislamu kwa upepo. 18 Majeshi hayo yalikuwa ni ya malaika. Hata hivyo, wao hawakushika silaha na kushiriki katika vita isipokuwa tu kujiunga kwao na majeshi ya Waislamu kuliwatia khofu makafiri na kuwapa moyo Waislamu. Hilo la msaada wa malaika kwa Waislamu limetajwa pia katika Sura 3: Majeshi hayo ya makafiri yaliwazukia Waislamu kutoka kila upande. Huo ndio muradi wa kutoka juu yenu, na kutoka chini yenu katika aya hii. Mayahudi wa kabila la Banii Nadhiir na Banii Qaynuuqaa walitokea kaskazini. Kutoka mashariki, yalishuka makabila ya Ghatafaan - Banii Sulaym, Fazaarah, Murrah, Ashja, Sa d, Asad na wengineo. Na kutoka kusini walishuka makureshi na jeshi kubwa la rafiki zao. 20 Maneno haya yanaelezea wasiwasi na wahka waliokuwa nao Waislamu baada ya kuzingirwa na majeshi ya makafiri waliokuwa na silaha na vifaa bora vya vita kuliko wao, idadi kubwa (zaidi ya mara tatu) ya wapiganaji wao, mbali uadui wa wanafiki na Mayahudi wengine waliokuwa miongoni mwao. Hali hii, ya kutokuwako vita wala amani, iliendelea kwa muda wa zaidi ya siku ishirini na tano. Baadhi ya wafasiri wa Qur ani huona ugumu kuyanasibisha maneno haya na Waislamu. Wao huona 6

22 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA 11. Hapo ndipo waumini walipojaribiwa, na wakatikiswa mtikiso mkali Na kumbuka waliposema wanafiki, na wale wenye maradhi katika nyoyo zao: Mwenyezi Mungu na Mtume Wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. 22 ت ل ه ن ال ك اب ول ال ق و إ ذ ي ز ال ش د يدا ١١ وا ز ل ز ل ل ؤ م ن ون و ز ال م ر ض وب ه م م ن اف ق ون و ال ين ف ق ل م ا ١٢ ر ور إ ل غ س ول اهلل و ر ا م ا و ع دن kwamba yanawaelekea zaidi wanafiki. Lakini tunapozingatia kwamba aya hii imeanza kwa Enyi mlioamini, na kwamba wahka waliokuwa nao Waislamu ulikuwa ni wasiwasi wa kishetwani tu wala sio imani yao - ambao si hasha kuwapata waumini, khaswa wanapokuwa dhaifu wa imani au wapya na Uislamu wao, na wamekabiliwa na hali ngumu kama hiyo - tutaona kwamba inawezekana kuwa Waislamu ndio waliokusudiwa hapo, kama ilivyoelezwa hali kama hiyo katika Sura 3: Hali hiyo, iliyowakuta Waislamu walipokuwa wamezingirwa hivyo na makafiri, ilikuwa ni mtihani wa Mwenyezi Mungu kwao. Waliachwa katika hali kama hiyo kwa siku nyingi hivyo, ili kuwajaribu: watasimama imara au watatepetea? Na hivi ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowajaribu wote wale wanaodai kwamba wanamwamini, kama inavyoelezwa katika aya nyengine za Qur ani zikiwamo: i) Mnadhani kwamba mtaingia Peponi bila ya kujiwa na mfano wa yaliyowajia wale waliopita kabla yenu? Iliwapata wao shida na madhara, na wakatikiswa hata Mtume na walioamini pamoja naye wakasema: Lini itakuja nusura ya Mwenyezi Mungu? Jueni kuwa nusura ya Mwenyezi Mungu iko karibu (Sura 2:214). ii) Jee! Mnadhani kwamba mtaingia Peponi na hali Mwenyezi Mungu hajawajulisha wale waliopigana jihadi miongoni mwenu, na hajawajulisha wenye kusubiri? (Sura 3:142). iii) Jee! Wanadhani watu kwamba wataachwa kwa kuwa wanasema: Tumeamini. Nao hawatajaribiwa? Hakika tuliwajaribu waliokuwa kabla yao, na kwa yakini Mwenyezi Mungu atawajulisha walio wakweli na atawajulisha walio waongo (Sura 29:2-3). 22 Katika hali ngumu ya wasiwasi kama ile iliyowakabili Waislamu pale walipokuwa wamezingirwa katika Vita vya Handaki, hapana budi kufuchuka yaliyokuwamo nyoyoni mwa waliokuwako. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, kama inavyoelezwa katika aya hii na inayofuatia. Wale wanafiki na waliokuwa na imani dhaifu walirudi nyuma, wakajaribu kuwavunja moyo Waislamu wenye imani thabiti kwa kusema Mwenyezi Mungu na Mtume Wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. Kuielewa ni ahadi gani hiyo aliyoitoa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake inatubidi turejee kwenye historia ili tuone mambo yalivyokuwa. Nayo ni hivi: Waislamu walipopata habari kwamba makafiri wa Makka, wakishirikiana na Mayahudi na rafiki zao wengine, waliungana na kuimda jeshi kubwa sana ili kuishambulia Madina na kuwaangamiza Waislamu; na kwa kuelewa kwamba wao walikuwa wachache sana wakilinganishwa na adui zao, walishauriana na Bwana Mtume (s.a.w.w.) kutafuta njia bora ya kujihami. Salmaan al-faarisii akatoa shauri la kuchimbwa handaki ambalo lilichimbwa kwa ujima wa Waislamu wote, akiwamo mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.). Walipokuwa wanachimba handaki hilo, Waislamu walipambana na mwamba uliowashinda kuuvunja! Wakampelekea habari Bwana Mtume (s.a.w.w.), naye papo hapo akafika pale palipokuwako huo mwamba. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akachukua sururu. Akaupiga ule mwamba kwa nguvu. Cheche zikatoka. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akasema kwa sauti: Allahu Akbar! (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa!) Akaupiga tena. Tena cheche zikatoka, na tena akasema kwa sauti: Allahu Akbar! Akaupiga mara ya tatu; na tena cheche zikatoka. Na kwa mara ya tatu akasema kwa sauti: Allahu Akbar! Ule mwamba ukawa vipande vipande. Maswahaba wakamuuliza Bwana 7

23 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ث ب ل م ق ام ل ك م 13. Na kumbuka kundi moja miongoni ه ل ي ا أ ه م ي ن ت طائ ف ة م و إ ذ ق ال mwao liliposema: Enyi watu wa Yathrib! 23 Hamna pa kukaa. Basi rudini. 24 Na ه م انل ب ي ق ول ون إ ن ن ت أ ذ ن ف ر يق م س ف ا ر ج ع و ا و ي ا kundi jengine miongoni mwao likamuomba ١٣ ة إ ن ي ر يد ون إ ل ف ر ار ر و ا ه ب ع ر ة و م و ن ا ع ب ي وت ruhusa Mtume kwa kusema: Hakika nyumba zetu ni tupu, hali hazikuwa tupu. Walilolitaka ni kukimbia tu. 25 Mtume (s.a.w.w.) yote waliyoyaona na kwa nini, mara zote tatu, alipiga takbiri? Bwana Mtume (s.a.w.w.) akaeleza: Mara tatu nimeupiga mwamba huu kwa sururu hii, na mara tatu nimefunuliwa utukufu wa Uislamu wa siku zijazo. Katika cheche za kwanza niliziona kasri za Sham (Syria) za Dola ya Warumi. Nikapawa funguo zake. Mara ya pili nikaziona kasri zinazong aa za Ufursi (Iran), na nikapawa funguo za Dola ya Wafursi. Mara ya tatu niliyaona malango ya San aa, na nikapawa.ftinguo za Ufalme wa Yaman. Hizi ni ahadi za Mwenyezi Mungu. Basi pokeeni bishara njema. Hivyo, kwa bishara hizo, Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.) waliwaahidi Waislamu kwamba watazishinda dola hizo, zilizokuwa kubwa sana zama zao, na kuzitawala. Lakini wanafiki na wale waliokuwa dhaifu wa imani - kuona ukubwa na nguvu za jeshi la makafiri dhidi ya lile la Waislamu siku hiyo - walivunjika nguvu, na wakawa wanavunjana nguvu kwa kuambiana maneno yaliyomo katika aya hii. Linganisha maneno hayo, na ya aya mbili zinazofuatia, na yale ya Waislamu wenye imani thabiti yaliyotajwa katika aya ya 22 humu. 23 Yathrib ni jina la zamani la mji wa Madina, kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kuhamia huko. 24 Hili ni kundi jengine la wanafiki. Wao nao, kwa kutumia kisingizio cha wingi na nguvu za jeshi la makafiri, walijaribu kuwavunja moyo na kuwatisha Waislamu kwa kuwambia kwamba wasiwe na tamaa ya kulishinda jeshi la makafiri; hivyo bora waache kupigana nao na warudi mjini! Hapa tunaweza kuswawiri athari ya propaganda kama hiyo juu ya wale dhaifu wa imani waliokuwamo katika jeshi la Waislamu. Ikumbukwe kwamba katika jeshi kubwa hilo la makafiri, mbali na kuwa na watu wengi waliokuwa na uzoevu wa vita, lilikuwa na wanafarasi 300 na jumla ya ngamia 2,500 waliobeba vyakula. Wakati huo, Waislamu walipokuwa wamehusuriwa ndani ya Madina kwa muda wote huo wa zaidi ya wiki tatu, ilikuwa hakuingii kitu Madina wala hakitoki. 25 Hili nalo ni kundi jengine la wanafiki lililokuwamo ndani ya jeshi la Waislamu. Wao walitumia kisingizio cha khiana iliyofanywa na kabila la Kiyahudi la Banii Quraydhwa dhidi ya Waislamu. Kuelewa ubaya na uzito wa khiana hiyo, inatubidi tuitizame jiografia ya mji wa Madina ilivyokuwa wakati wa vita hivyo. Kusini ya Madina kulikuwa na mabustani mengi. Kwa hivyo haikuwezekana kuushambulia mji huo kutoka upande huo. Upande wa mashariki kulikuwa na majabali ambayo jeshi kubwa kama hilo la makafiri lisingeweza kupita. Na vivyo hivyo ndivyo ilivyokuwa upande wa kusini-magharibi. Kwa hivyo haikuwezekana kuishambulia Madina ila kutokea kaskazini (ima kutokea upande wa mashariki wa Mlima Uhud au magharibi yake). Na upande huo kulikuwa kushachimbwa handaki. Hivyo makafiri walikuwa wamebakiwa na shauri moja tu; nalo ni kulichochea lile kabila la Kiyahudi la Banii Quraydhwa, lililokuwa na maskani yao sehemu ya kusini-mashariki ya Madina, lifanye uaswi. Kwa kuwa Waislamu walikuwa wamefanya mkataba nao - kwamba endapo Madina itashambuliwa, wao wataungana na Waislamu kuihami - Waislamu hawakuchukua hatua zozote za ulinzi upande huo. 8

24 JUZUU YA Na lau wangeliingiliwa kwa pande zote, kisha wakatakiwa kufanya khiana, wangeliifanya. Na wasingelikaa ila kidogo tu. 26 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ه م م ن أ ق ط ار ه ا ث م س ئ ل وا ال ف ت ن ة ي ل خ ل ت ع و ل و د ا ١٤ س ري ا إ ل ي ث وا ب ه ب ل ا ت ا و م ه و لت 15. Na hakika walikuwa wameshamwahidi Mwenyezi Mungu kabla yake, kwamba hawatageuza migongo yao. 27 Na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuulizwa. ار ب ل ون ال د و ب ل ل ي وا اهلل م ن ق د وا عه ن و ل ق د ك ه د اهلل م س ئ ول ١٥ و ك ن ع Badali yake walizipeleka hata familia zao huko kupata hifadhi katika ngome zilizokuwako huko. Makafiri waliutambua udhaifu huu. Kwa hivyo walimtuma Huyayy b. Akhtab, kiongozi wa Kiyahudi wa kabila la Banii Nadhiir, ende kwa jamaa zao, Banii Quraydhwa, na kuwashawishi wavunje ule mkataba waliofanyiana na Mtume Muhammad (s.a.w.w.), na waingie vitani. Mwanzo Banii Quraydhwa walilikataa shauri hilo kwa hujja kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) hajavunja mkataba wao, bali ameutekeleza kikamilifu. Lakini baada ya kushikiliwa mno na huyo Huyayy, Uyahudi wao ulikuja juu, wakauvunja mkataba na kufanya khiana! Habari ya khiana hii ilipowafikia Waislamu iliwagutusha na kuwahangaisha, maana walitambua kwamba wamezungukwa, na mji wao umo hatarini upande ambao haukuwa na ulinzi, na ambako wameziacha familia zao katika ngome za huko kupata hifadhi. Hapo ndipo wanafiki walipopata nafasi ya kujaribu kuwamsha roho Waislamu kwa maneno yaliyotajwa katika aya hii: ya nyumba zao kuwa tupu, hali hazikuwa tupu! Yote hayo yaliyosemwa na makundi ya wanafiki hao yalikuwa ni propaganda na njama tu za kutaka kukimbia vita na kusababisha Waislamu kushindwa. Lakini Mwenyezi Mungu hakusimama nao! 26 Wanafiki, na watu wenye imani dhaifu kama hao waliotajwa katika aya hapo juu, siku zote si watu wa kuamania. Ni watu ambao, kama Mwenyezi Mungu anavyotueleza hapa, lau watafuatwa na washawishiwe kuufanyia khiana Uislamu (kwa kutoka na kurudi ukafirini, au kuupiga vita), bila shaka watalifanya hilo wala hawatasitasita. Hapa pana funzo kwa wana-harakati wa Kiislamu; nalo ni: kila harakati lazima iwe na watu aina ya waliotajwa katika aya ya 13-15, ya 18-20, na humu. Hivyo wasihadaiwe na kila anayeitwa/anayejiita mwana-harakati, bali wamweke katika mizani ya aya kama hizo na kumwamili vipasavyo. 27 Watu hao, walioelezwa udhaifu wao wa imani katika aya iliyotangulia, walipombai Bwana Mtume (s.a.w.w.) kabla ya Vita vya Handaki, waliapa na kuahidi kwamba watasimama naye bega kwa bega, na watamnusuru wala hawatamkimbia. Vipi basi, sasa watakuwa tayari kuivunja ahadi hiyo? Jee, hawajui kwamba kesho Akhera wataulizwa ahadi waliyoitoa? 9

25 JUZUU YA Sema: Kukimbia hakutawafaa kitu; ikiwa mnakimbia kifo au kuuwawa. Na hata hivyo hamtastareheshwa ila kidogo tu Sema: Ni nani ambaye anaweza kuwalinda na Mwenyezi Mungu pindi akiwatakia uovu au akiwatakia rehema? Wala hawatapata mlinzi wala msaidizi asiyekuwa Mwenyezi Mungu. 29 AL-AHZAAB 33 KARA LA PILI UTLU MAA UHIYA ل ت ق و ال ت أ و م م م ن ال ت ع ك م ال ف ر ار إ ن ف ر ر نف ق ل ل ن ي ع ون إ ل ق ل يل ١٦ ت م و إ ذ ا ل ت ك ص م ا ال ي ي ع ن ذ ق ل م ة و ل ي ح ر اد ب ك م ر س وء ا أ و أ ا ١٧ ص ري ا و ل ن اهلل و ل ر اد ب ك م م م ن اهلل إ ن أ ون ن د م م ه د ون ل 18. Kwa hakika Mwenyezi Mungu anawajua miongoni mwenu wanaowazuilia na wanaowambia ndugu zao: Njooni kwetu! Wala hawaingii vitani ila kidogo tu. 30 ق ني م نك م و ال ق ائ ل ني ل خ و ان ه م و ع م إ ل ق ل يل ١٨ م اهلل ال ل ع ق د ي س ت ون ال أ أ ن ا و ل ي ه ل م إ ل 28 Ewe Muhammad! Wambie hao wanafiki wanaotaka kuvikimbia vita kwa kuogopa kufa, kwamba kukimbia kwao hakutawafaa kitu. Maana mauti hayakimbiliki; popote mtu alipo yatamfikia (Sura 4:78) - iwe ni kitandani, iwe ni vitani - bora tu ajali yake iwe ishafika (Sura 7:34). Na kama ajali yake haijafika, basi ataendelea kubaki hai - lakini kwa muda mfupi tu; halafu lazima atakufa. Hapo wanafiki watiwe Motoni, na mashahidi watiwe Peponi. Amesema Imam Alii (a.s.): Naapa kwa ambaye nafsi yangu i mkononi Mwake! Dharba elfu za panga ni khafifu zaidi kwangu kuliko kufa godoroni. 29 Ewe Muhammad! Wambie tena hao wanafiki: Ni nani kati yao anayeweza kujikinga na analotaka Mola? Hawajui kwamba kukimbia kwao hakuwafai kitu? Mwenyezi Mungu akiwatakia uovu, utawapata tu: hata wawe majumbani mwao. Na akiwatakia rehema, itawafikia hata wawe vitani. Basi kukimbia huko ni kwa nini? Jee, wanaye mlinzi au msaidizi asiyekuwa Mwenyezi Mungu? 30 Hii ni aina nyengine ya wanafiki waliokuwa wakiwashawishi Waislamu wamwachilie mbali Mtume (s.a.w.w.) Wakisema: Ya nini kwenda vitani na kujitia mashakani? Njooni kwetu mle raha kama tunavyoila sisi! Na kwa kawaida watu kama hao, uadui wao unapogunduliwa, hujifanya wanajitolea kupigana - lakini kidogo tu. Inaelezwa katika riwaya kwamba swahaba mmoja wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliondoka kwenye midani ya vita na kwenda mjini Madina kwa dharura. Akamwona ndugu yake ameweka mikate, nyama za kuchoma, na vinywaji. Akamuuliza: Wewe umo katika hali hii; unakula raha na Mtume wa Mwenyezi Mungu ameshughulika na vita, yu katikati ya vyembe na panga? Yule nduguye akamjibu: Ewe mjinga! Kaa uwe na sisi hapa. Naapa kwa ambaye Muhammad huapa Kwaye! Hatarudi kutoka kondo ya safari hii! Na jeshi kubwa hili, lililoungana kumwangamiza, halitamwacha hai Muhammad wala swahaba zake! Yeye naye akamjibu: Unasema uwongo! Ninaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu; nitamwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.), nimjulishe uliyoyasema. Akenda kwa Mtume (s.a.w.w.), akamwambia. Ndipo iliposhuka aya hii. (al-amthal). Watu kama hao hupatikana zama zote. 10

26 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA أ ي ت ه م ي نظ ر ون 19. Wana choyo juu yenu. 31 Lakini khofu ف ر ا ج اء ال و ك م ف إ ذ ي ل أ ش ح ة ع ikija utawaona wanakutizama na macho ت yao yanazunguka kama ambaye amezimia و م ه م ن ال ي ل ع ش ل ي ي غ ي ن ه م ك ع د ور أ ت إ ل ك kwa mauti. 32 Lakini khofu inapoondoka ع ة ش ح اد أ س ن ة ح د ل م ب أ وك ق ف س ل و ه ب ال ف إ ذ ا ذ و ك ن wanawaudhi kwa ndimi kali, na wanaifanyia choyo kheri. 33 Hao hawakuamini, kwa hivyo ب ط اهلل أ ع م ال ه م ح م ن وا ف أ ؤ ري أ ول ئ ك ل م ي ال Mwenyezi Mungu amezipomosha amali zao. ا ١٩ س ري اهلل ي ذ ل ك ع Na hayo, kwa Mwenyezi Mungu, ni mepesi Katika aya hii Mwenyezi Mungu anatufafanulia zaidi sifa za wanafiki hao, na kwa kweli sifa za wanafiki wowote - wa mahali popote na zama zozote. Sifa ya kwanza ni hiyo ya uchoyo. Wao huwa choyo - si wa mali tu, bali hata nguvu zao, wakati wao, akili zao; sikwambii kuingia vitani na kuzitoa mhanga roho zao! Hawako tayari kuusaidia Ukweli, wala kushirikiana na wanaoutetea, kwa njia yoyote ile. 32 Sifa nyengine ya wanafiki ni uwoga wanapokabiliwa na hatari. Kwa kuwa wao huwa hawajauonja utamu wa imani ya kweli, na hawajakuwa na mategemeo madhubuti katika maisha yao, basi hushindwa kuzimiliki nafsi wakati wa hatari na misukosuko. Kama aya hii inavyoeleza hapo juu, utawaona wanakutizama na macho yao yanazunguka kama ambaye amezimia kwa mauti. Sheikh Ali Muhsin al-barwani, katika kukieleza kipande hiki cha aya hii, anasema: Aya hii tukufu inaashiria ukweli wa kisayansi ambao ulikuwa haukujulikana namna yake wakati wa kuteremka Qur ani Tukufu. Ukweli huo ni kuwa jicho wakati wa kukurubia mauti au wakati wa khofu huzunguka. Na katika sababu za hayo ni kuwa kwa shida ya khofu utambuzi hutoweka, ikawa mtu hajitambui. Vituo vya navo zisiotambua katika ubongo hupoteza mizani yake, basi huwa huyo mwenye khofu kama mfano wa mwenye kuzimia kwa kukaribia kufa, jicho lake huzunguka na mboni ya jicho hupanuka, na hubaki katika hali ya kukodoa macho mpaka kufa. (al-barwani). 33 Sifa ya tatu ya wanafiki hudhihiri wakati wa amani au ushindi. Kama vile walivyokifanyia ubakhili walichonacho - wakati wa vita - ndivyo wanavyozifanyia ubakhili ngawira zilizopatikana - baada ya vita! Hunoa ndimi zao kuonyesha kwamba wao pia walishiriki katika vita, kwa njia moja au nyengine, na hivyo wana haki ya kupata sehemu ya ngawira zilizopatikana. 34 Hapa Mwenyezi Mungu anatoa hukumu ya watu kama hao: kwa kuwa wao hawakuamini isipokuwa walidhihirisha imani kufichia ukafiri wao tu; na kwa kuwa walijiunga na jeshi la Waislamu kinafiki na kwa kujionyesha tu, Mwenyezi Mungu amezipomosha (amezibatilisha) amali zao zimekuwa kazi bure (Sura 25:23) kwa sababu hazikufanywa kwa ajili Yake. Na hayo, kwa Mwenyezi Mungu, ni mepesi. Kama alivyosema Bwana Mtume (s.a.w.w.) katika Hadith yake moja: Yoyote yule ambaye kuhama kwake ni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, basi kuhama kwake ni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na ambaye kuhama kwake ni ili aipate dunia, au mwanamke wa kumuowa, basi kuhama kwake ni kwa hilo alilolihamia. (al-kaashif). 11

27 JUZUU YA Wanadhani yale makundi ya maadui hayajaondoka. Na lau yaja hayo makundi, watatamani wangekuwa jangwani pamoja na mabedui, wakiuliza habari zenu. Na lau wangelikuwa pamoja nanyi, wasingelipigana ila kidogo tu Hakika nyinyi mna ruwaza njema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu 36 - kwa mwenye kumtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi. 37 AL-AHZAAB Mwenyezi Mungu anaendelea kuufuchua uadui uliokuwamo nyoyoni mwa wanafiki. 12 UTLU MAA UHIYA Kama tulivyoona chini ya maelezo Na.17 humu, majeshi ya makafiri yalirejea kwao baada ya kupambana na vituko vya Mwenyezi Mungu. Lakini, kwa ajili ya nia mbovu walizokuwa wamezificha nyoyoni mwao, wanafiki wa Madina walishindwa kuliamini hilo. Walitamani lau yangekuwa hayakuondoka; na hilo ndilo lililowapitia ndotoni mwao, kwa sababu walikatikiwa kuwa wataweza kuwaangamiza Waislamu na Mtume wao! Lau itokee kwamba majeshi hayo yameshindwa, lakini yarudi tena Madina baada ya kujiandaa upya, basi wanafiki watatamani wasingekuwa na Waislamu ndani ya Madina, bali wangekuwa jangwani pamaja na mabedui wakiuliza, kwa mbali tu, yaliyowapata Waislamu! Na lau ingetokea wawe ndani ya Madina, hivyo walazimike kushiriki katika vita, basi wasingelipigana ila kidogo tu. 36 Kutokana na jinsi wanafiki na wale dhaifu wa imani walivyokuwa katika vita vya Handaki, kama tulivyoona mpaka hapa, Mwenyezi Mungu anawawekea Bwana Mtume (s.a.w.w.) kama mfano bora wa kuigwa. Katika vita hivi hakukuwa na shughuli wala shida yoyote iliyowapata Waislamu ambayo yeye aliihepa. Ikiwa ni handaki, yeye naye alishiriki katika kulichimba. Ikiwa ni njaa, yeye naye ilimpata kama ilivyowapata wafuasi wake - mpaka ikambidi ajifunge jiwe tumboni kupunguza athari yake! Wakati walipokuwa wamezingirwa na makafiri, hata mara moja hakuondoka kwenye midani, wala hakurudi nyuma hata hatua moja. Baada ya Banii Quraydhwa kufanya khiana yao, si familia za Waislamu wengine tu zilizokuwa zimekabiliwa na hatari, bali na yake pia! Hata hivyo, alipofanya mipango ya kuwalinda na kuwahifadhi, hakufanya mipango maalumu na tafauti kwa familia yake. Wote aliwaamili sawa. Daima alikuwa mstari wa mbele katika kujitolea kwa lolote lile alilowambia wafuasi wake wajitolee. Kwa hivyo yeyote yule anayedai kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni mtume wake, inataka aige mifano yake hiyo. Wala yeye hakuwa ruwaza njema katika Vita vya Handaki peke yake, bali katika hali zote. Maisha yake yote - aliyoyasema na aliyoyatenda - ndio mfano bora wa kuigwa. Kwa Mwislamu, hakuna mfano bora zaidi ya yeye. 37 Hapa tunaelezwa sifa za wale ambao wataweza kufaidika kwa ruwaza ya Mtume (s.a.w.w.). Kwanza, ni wale wenye tamaa ya rehema na fadhila za Mwenyezi Mungu. أ حز اب ل م ي ذ هب وا و إ ن ي حي س ب ون ال وا د و اب ي ز ت ال ح و و ل م نب ائ ك ل ون ع ن أ سأ ر اب ي اد ون ف ال ع م ب ه ن ل و أ وا إ ل ق ل يل ٢٠ ل ا ق ات م م وا ف يك ك ن م ن ك ن س ن ة ل و ة ح س ول اهلل أ س ك م ف ر ل ق د ك ن ل ا ٢١ ث ري ك ر اهلل ك م ال خ ر و ذ و اهلل و ال و ج ي ر Pili, wakawa wanaiamini Siku ya Mwisho: kwamba siku hiyo watu watalipwa mema kwa kiasi ambacho wamemfuata Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kama ruwaza yao. Tatu, wakawa wanamtaja na kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, sio kwa tukizi au mara moja moja tu. Baadhi ya wafasiri wanasema kuwa muradi wa kumkumbuka Mwenyezi Mungu hapa ni kuswali swala tano za faradhi. (al-kaashif).

28 JUZUU YA Na waumini walipoyaona makundi, walisema: Haya ndiyo aliyotuahidi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wamesema kweli. Na hayo hayakuwazidishia ila imani na utwiifu. 38 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ى ال أ ا ر و ل م ز ؤ م ن ون ال ح م و ص د ق اهلل و ر سول اهلل و ر سول ا ٢٢ س ل يم و ت ا ا و ع دن ا م ذ وا ه اب ق ال ا ان م إ ل إ يم ه اد و م ا ز 23. Miongoni mwa waumini wako watu waliotimiza waliyoahidiana na Mwenyezi Mungu. Baadhi yao wamekwisha kufa, na baadhi wanangojea; wala hawakubadilisha ahadi yao hata kidogo Ili Mwenyezi Mungu awalipe wakweli kwa ukweli wao, na awaadhibu wanafiki, akipenda, au apokee toba yao. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. 40 ه ي ل وا اهلل ع د ه ا ع ق وا م د ؤ م ن ني ر ج ال ص م م ن ال وا د ل ا ب ن ي نت ظ ر و م م م ه ب ه و م ن ن ن ق ض م م ف م ن ه د يل ٢٣ ت ب م ن اف ق ني إ ن ذ ب ال ع ز ي اهلل الص اد ق ني ب ص د ق ه م و ي ل ج ا ٢٤ ح يم ا ر ور ف ي ه م إ ن اهلل ك ن غ ل ش اء أ و ي ت وب ع Watu wowote wasio na sifa zilizotajwa hapo juu, au wenye kinyume cha sifa hizo, hawawezi kufaidika na ruwaza hiyo kwa sababu hawatakuwa wanamfuata kikamilifu. 38 Baada ya Mwenyezi Mungu kutupa picha ya wanafiki na wale wenye nyoyo dhaifu katika vita hivi, sasa anatueleza msimamo wa waumini wa kweli: kwamba wao, kinyume cha wanafiki (tiz. aya ya 12 humu), hawakuwa na shaka na ahadi ya Mwenyezi Mungu bali waliiamini kikwelikweli. Mara tu walipouona wingi wa jeshi la makafiri, na hatari iliyowakabili pale walipokuwa washazingirwa, waliikumbuka nusura waliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu katika Sura 2:214. Hilo likawazidishia imani na utwiifu badali ya uwoga na uaswi. Na huo ndio msimamo wa kila mwenye imani ya kweli. Shida, mitikiso, maafa - yote hayo hayampunguzii imani yake bali humzidishia kwa kuikumbuka ahadi ya Mwenyezi Mungu kwamba hatamwacha bila ya kumfanyia mtihani wa dai lake kwamba yeye ni muumini (Sura 29: 2-3). 39 Aya hii inatufahamisha kwamba hakuna zama ambayo hukosa waumini wa kweli waliotimiza waliyoahidiana na Mwenyezi Mungu. Kuna ambao wamekwisha kufa. Kuna na ambao wanangojea wakati wao ufike. Wala hakuna la kuwarudisha nyuma. Hao ndio wanaojulikana kama mashahidi. Kwa wakati iliposhuka aya hii, wanazuoni wa Tafsir wanasema kwamba muradi wa ambao wamekwisha kufa ni wale waliokufa mashahidi katika vita vilivyotangulia vya Badri na Uhud - k.v. Hamza b. Abdil Muttwalib, Anas b. an-nadhiir na wengineo; na muradi wa ambao wanangojea ni wote wale waliokufa katika vita vilivyofuatia viwili hivyo, vikiwamo vya Handaki, na pia wale waliopoteza roho zao katika njia ya Mwenyezi Mungu - tangu siku hizo hadi mwisho wa dunia. 40 Ili Mwenyezi Mungu awalipe waumini malipo mema, kwa ukweli wao, na awaadhibu wanafiki kwa unafiki wao, au awasamehe iwapo wataomba maghfira. Yote hayo yamo mikononi Mwake, maana yeye ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. 13

29 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA 25. Na wale waliokufura, Mwenyezi Mungu ف ري ا و ك وا خ ن ال م ي ظ ه م ل ي ر وا ب غ ف و ر د اهلل ال ين ك aliwaradisha nyuma na ghadhabu yao; ا hawakupata kheri yoyote. 41 Na Mwenyezi ٢٥ ز يز ا ع ق ت ال و كن اهلل ق و ي م ن ني ال ؤ م ال Mungu amewakifia waumini vita. 42 Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mshindi. 26. Na akawateremsha wale waliowasaidia maadui katika Watu wa Kitabu kutoka katika ngome zao; na akatia khofu katika nyoyo zao. 43 Baadhi yao mkawa mnawauwa, na 41 Muradi wa wale waliokufuru katika aya hii ni yale majeshi ya makafiri yaliyokuja na lengo la kuuangamiza Uislamu katika Vita vya Handaki. Yalirudi kwao na hasira kwa kutopata ushindi wowote. 42 Mwenyezi Mungu, kwa nguvu Zake, aliwatoshea Waislamu mapambano yao na makafiri. Alikuja akavumisha pepo kali lililowatia kikuli makafiri, wakatafutana wasionane. Pakawa hapana haja tena ya kupigana. Ndipo waliporudi makwao na mitungi yao mitupu. Kwa kweli Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mshindi. 43 Katika aya hii na inayofuatia, Qur ani inasimulia habari za Banii Quraydhwa - khiana yao na matokeo yake. Ili kuzielewa vizuri aya mbili hizi, inatubidi turejee kwenye historia japo kwa ufupi: Madina, wakati huo, kulikuwa na makabila matatu maarufu ya Kiyahudi: Banii Quraydhwa, Banii Nadhiir na Banii Qaynuuqaa. Makabila haya yalipatana na Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwamba hayatawasaidia adui zake wala hayatawafanyia upelelezi, na wataishi na Waislamu kwa amani. Lakini Banii Qaynuuqaa walivunja ahadi yao katika mwaka wa 2 Hijriya, na Banii Nadhiir wakaivunja yao katika mwaka wa 4 Hijriya - kwa nyudhuru mbalimbali - na kushikilia kupambana na Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hata hivyo upinzani wao mwisho ulishindwa, hivyo wakafukuzwa Madina: Banii Qaynuuqaa wakenda Sham, na baadhi ya Banii Nadhiir wakenda Khaybar na wengine wakenda Sham. Kwa hivyo Banii Quraydhwa peke yao ndio waliokuwa wamebaki Madina ilipofikia mwaka wa 5 Hijriya, palipozuka Vita vya Handaki. Na kama tulivyodokeza chini ya maelezo Na. 25 hapo juu, na wao nao pia wakavunja ahadi yao katika vita hivyo. Waliwasiliana na makafiri, wakafuta panga zao kupigana na Waislamu. Baada ya kwisha Vita vya Handaki, na majeshi ya makafiri kurudi nyuma, Bwana Mtume (s.a.w.w.), kwa mujibu wa riwaya (mapokezi) ya Kiislamu, alirudi nyumbani kwake, akavua silaha zake na kwenda kuoga. Jibril, malaika wa Mwenyezi Mungu, akamshukia kwa amri ya Mwenyezi Mungu, akamwambia: Kwa nini umebwaga silaha na hali malaika hawa hapa wamejiandaa kupigana? Lazima uende sasa kwa Banii Quraydhwa umalize mambo yao. Kwa kweli, hakukuwa na fursa bora ya kumalizana na Banii Quraydhwa kuliko hii. Maana Waislamu walikuwa bado wamo katika vuguvugu la ushindi, hali Banii Quraydhwa walikuwa katika maumivu na uchungu wa kushindwa. Khofu kubwa ilikuwa imewavaa, hali rafiki zao - yale makabila ya Kiarabu yaliyokuja Madina kuwashambulia Waislamu - walikuwa taabani, hawana nguvu, mabega yamewashuka. Walikuwa wako njiani wanarudi makwao, nyuso hawawezi kuziinua kwa fadheha iliyowapata; hawana wa kuwakinga wala kuwatetea. Hapo ndipo mtangazaji mmoja wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipowanadia Waislamu wawaendee Banii Quraydhwa kabla hawajaswali alasiri. Na hapohapo Waislamu wakajiandaa kwa haraka kwenda vitani; na kabla ya jua kutwa wakawa washazizingira ngome zote za Banii Quraydhwa (al-amthal). Mzingiro huo uliendelea kwa siku 25. Walipojiona wamo katika hatari ya kuangamia, walimwomba Bwana 14 ك ت اب م ن ل ال ه م م ن أ ر وه و أ نز ل ال ين ظاه وب ه م الر ع ب ف ر يق ا ت ق ت ل ون ف ف ق ل ص ي اص يه م و ق ذ ا ٢٦ س ون ف ر يق و ت أ

30 JUZUU YA 21 wengine mnawateka. 44 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA 27. Na akawarithisha nyinyi ardhi yao, majumba yao na mali zao, na ardhi ambayo hamjapata kuikanyaga. 45 Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu. ض ا ل م ر ه م و أ ال و م ه م و أ ار ه م و د ي ض ر ك م أ ث ر و أ و ء ق د ير ا ٢٧ ك ش ت ط ئ و ه ا و ك ن اهلل ع Mtume (s.a.w.w.) - kwa hiari yao wenyewe - wahukumiwe na Sa d b. Muaadh, aliyekuwa mkubwa wa kabila la Awsi waliokuwa marafiki wa Banii Quraydhwa. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akamwita Sa d akamwambia: Hawa wametaka kuhukumiwa na wewe kwa hiari zao. Basi hukumu kwa upendalo. Sa d akauliza: Na hukumu yangu itafuatwa? Mtume (s.a.w.w.) akajibu: Ndio! Sa d akahukumu kwamba wanaume wao walioshiriki vitani wauliwe, mali yao yagawanywe, watoto wao na wanawake wao wachukuliwe mateka, na majumba yao yachukuliwe na muhaajiruun (Waislamu wa kutoka Makka), sio answaar (Waislamu wa Madina), kwa sababu answaar wanayo majumba yao; muhaajiruun hawana. (al-kaashif). Muradi wa Watu wa Kitabu waliotolewa katika ngome zao, katika aya hii, ni hao Mayahudi wa Banii Quraydhwa tulioieleza habari yao hapo juu. 44 Waliuliwa, na wengine wakachukuliwa mateka kwa hukumu ya Sa d b. Muaadh waliyoiomba na kuikubali wao wenyewe! Wala Sa d hapo hakuleta hukumu ya kichwa chake ila alihukumu kama Taureti, kitabu cha Mayahudi, inavyosema hadi hii leo: Utakaposongea karibu ya mji kwenda kupigana juu yake, ndipo utakapowapigia ukelele wa amani. Itakuwa utakapokujibu kwa amani, na kukufungulia, ndipo watu wote watakaoonekana humo watakufanyia kazi ya shokoa, na kukutumikia. Na kwamba hautaki kufanya amani nawe, lakini utafanya vita juu yako, ndipo uuhusuru; na Bwana, Mungu wako, autiapo mkononi mwako, mpige kila mume aliyemo kwa makali ya upanga; lakini wanawake na watoto, na wanyama wa mji, na vilivyo mjini vyote, navyo ni nyara zake zote, uvitwae viwe mateka kwako; nawe utakula nyara za adui zako alizokupa Bwana, Mungu wako. (Kumbukumbu 20:10-14). Hata hivyo, hukumu hiyo ya Sa d haikuwa kali hivyo ukiilinganisha na ile ya Kumbukumbu 13:15-16 inayosema:...hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga. Na nyara zake zote uzikusanyie katikati ya njia yake; na uuteketeze kwa moto, na nyara zake zote, kuwe sadaka kamili ya kuteketezwa kwa Bwana, Mungu wako; nao utakuwa magofu milele; usijengwe tena. Hii inaamrisha wauliwe watu wote wa mji huo, bila ya kuacha wanawake wala watoto, kisha mji wote uteketezwe, pamoja na vyote vilivyomo humo, mpaka uwe magofu milele: usijengwe tena! Lakini Waislamu hawakufanya hivyo. Ikumbukwe kwamba kitendo walichokifanya Banii Quraydhwa, hata kwa sharia za nchi za kisasa za zama zetu, ni cha ukhaini mkubwa ambacho adhabu yake ni mtu kunyongwa. 45 Wanazuoni wa Tafsir wamekhitalifiana hapa kuhusu ni ipi hiyo ardhi ambayo hamjapata kuikanyaga. Wengine wamesema ni ardhi ya Khaybar. Wengine wasema ni ya Makka. Bali wengine wemesema ni ardhi za Urumi na Ufarisi (Iran). Na wengine wemesema kwamba hiyo ni ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Waislamu, ya ardhi zote na miji yote itakayoingia mikononi mwao - tangu siku hiyo mpaka Siku ya Kiyama. Na hilo si muhali kwa Mwenyezi Mungu. Maana Yeye ni Mwenye uwezo juu ya kila kila kitu. 15

31 JUZUU YA 21 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA ي اة 28. Ewe Mtume! Wambie wake zako: Ikiwa ت ر د ن ال نت إ ن ك اج ك و ا انل ب ق ل ل ز ه ي ي ا أ nyinyi mnataka maisha ya dunia na pambo ح ك ن lake, basi njooni niwape kitoka nyumba na س ك ن و أ ع ت م ال ني أ ت ع ا ف ت ه ي ا و ز ين ادل ن niwaache mwachano mzuri. 46 س اح ا ج يل ٢٨ 46 Kuanzia aya hii mpaka aya ya 34 - isipokuwa kipande cha mwisho cha aya ya 33 - ya Sura hii ni mambo yanayohusu wake za Bwana Mtume (s.a.w.w.). Baada ya Vita vya Badri na vya Handaki, na baada ya kuwahusuru Banii Quraydhwa na kuwatoa Madina, Waislamu walipata ngawira na mateka mengi. Hivyo hali yao ya kiuchumi ilitengenea sana. Mapato hayo yaliathiri Waislamu kwa jumla wakiwamo, miongoni mwao, wakeze Bwana Mtume (s.a.w.w.). Baada ya kuona hali ya Waislamu ilivyotengenea, na yao kuwa palepale - maana Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliendelea kuishi vilevile kimaskini - wake za Bwana Mtume (s.a.w.w.) walianza kumtaradhia masurufu zaidi. Jambo hili Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakulipendelea, bali lilimhuzunisha sana kiasi cha kwamba alijitenga nao, na hata swahaba zake, kwa muda hivi. Ndipo Mwenyezi Mungu alipoteremsha aya mbili hizi - hii na inayofuatia kumwambia Bwana Mtume (s.a.w.w.) awateuze wake zake moja ya mambo mawili: ama wateue maisha ya dunia na pambo lake, au wamteue Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Nyumba ya Akhera. Kama watateua hilo la kwanza, ambalo muradi wake ni kuteua maisha ya fakhari na anasa, basi hawataweza kuendelea kuwa wake za Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w.w. maana watakuwa wamevunja miko ya kuwa katika Nyumba hiyo, kama tutakavyoona hapa chini. Hivyo, kwa sababu hiyo, Bwana Mtume s.a.w.w. atakuwa yu tayari kuwaacha (kutokana nao) kwa vizuri na kuwapa kitoka nyumba chao. Lakini kama watateua hilo la pili, la Mwenyezi Mungu na Mtume Wake..., basi watabaki kuwa wake zake na kuwa miongoni mwa watenda njema ambao Mwenyezi Mungu amewaandalia malipo makubwa. Hata hivyo, kitendo hiki cha Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuwa tayari kuwaacha wakeze kama watateua maisha ya dunia na pambo lake, hakimaanishi kwamba Uislamu hauwaruhusu Waislamu kula vizuri, kuvaa vizuri, na kuishi vizuri kwa raha na starehe; la! Uislamu haukatazi hilo (Sura 7:32). Bali kitendo hicho kilikusudiwa kufunua zaidi tu maana ya kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni ruwaza njema kwa waumini: kwamba sio awe hivyo yeye peke yake, bali ni lazima aila yake vilevile iwe ni ruwaza kwa aila zote, na wake zake wawe ni viongozi wa wanawake wote waumini mpaka Siku ya Kiyama. Mtume (s.a.w.w.) hakuwa ni mfalme wala mtawala wa kuwa na upande maalumu (wa nyumba yake) kwa ajili ya wanawake na kuwamiminia mapambo ya thamani na majohari. Yeye alikuwa kiongozi aliyeamua kuishi maisha ya kawaida, kwa hiari yake mwenyewe. Wakati ambapo Waislamu walitajirika kwa mali na ngawira walizopata, yeye alikuwa akikaa mwezi mzima na nyumbani kwake hakufuki moshi; meko yamelala paka! Aliishi hivyo pamoja na sadaka zote, hiba zote, na hidaya zote zilizokuwa zikipitia mkononi mwake! Yote hayo ni kwa ajili ya kutaka kuzitukukia starehe za maisha ya dunia, na kuyapendelea yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu (Fii Dhwilaalil Qur aan). Na hivyo ndivyo aiivyotaka wake zake pia, maadamu wamo ndani ya nyumba yake, wawe. Hapa (katika kuzieleza aya mbili hizi: ya 28 na 29) pana mafunzo matatu makubwa: i) kwamba wake za Bwana Mtume (s.a.w.w.), na kwa kweli wake wa Mtume yeyote yule, ni binadamu; si malaika. Kwa hivyo wao huweza kufanya lolote lifanywalo na wengine. Kutokana na hilo basi, kitendo chao - cha kumkera Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwa kutaka kuzidishiwa masurufu yao - kionekane kama kitendo cha kawaida tu cha wake wowote kwa waume zao; si kizushi. Hivyo yaliyomo katika aya mbili hizi hapo juu yasionekane kwamba ni raddi kwao, bali ni maelekezo ya vipi wawe, kama wake wa kiongozi ambaye ni ruwaza njema kwa wafuasi wake wote, katika maisha yao. ii) japokuwa wanaosemezwa hapa ni wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), lakini yaliyomo katika aya hizo, 16

32 JUZUU YA Na ikiwa mnamtaka Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Nyumba ya Akhera, basi Mwenyezi Mungu amewaandalia watenda njema, miongoni mwenu, malipo makubwa. 30. Enyi wake wa Mtume! Yeyote kati yenu atakayefanya uchafu dhahiri, atazidishiwa adhabu mara mbili. 47 Na hilo, kwa Mwenyezi Mungu, ni jepesi. 48 AL-AHZAAB 33 UTLU MAA UHIYA و ادل ار ال خ ر ة ف إ ن اهلل ر د ن اهلل و ر سول ت و إ ن ك نت ا ٢٩ ظ يم ر ا ع ج س ن ات م نك ن أ ح م أ ع د ل ل ي ا ن س اء انل ب ف ل ه ي ضاع ا ٣٠ س ري ي ن ة ب ي ة م اح ش ت م نك ن ب ف أ م ن ي اهلل ني و ك ن ذ ل ك ع ف ذ اب ض ع ع ا ال na natija yake, inawachanganya wao na wasiokuwa wao - khaswa viongozi: wawe ni wa kidini ama kidunia. Suali hapa ni: wataishi maisha ya kawaida kama wanavyoishi wafuasi wao; au watatumia nyadhifa zao na vyeo vyao kujistareheshea wao na familia zao huku wafuasi wao wakiwa katika shida na mashaka? iii) aya hizi vilevile ni majibu tosha kwa wale maadui wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) wanaodai kwamba aliowa wake wengi kwa sababu za kijinsia. Hivi kweli mtu anayependa kustarehe na wanawake atawambia wateue baina ya maisha ya raha na talaka, kama alivyofanya yeye? Si kila mtu anajua kwamba yeyote anayependa wanawake hujaribu kuwashawishi na kuwavutia kwa kila aina ya anasa na mambo ya fakhari? Vipi Bwana Mtume (s.a.w.w.) atakuwa anataka kuwa na wanawake hali wakati huohuo nyumbani kwake hakufuki moshi hata kwa mwezi mzima? Na sio kwamba hali imekuwa hivyo kwa kukosa cha kupika, bali kwa kutaka tu kutotawaliwa na matamanio ya kidunia! Anayependa wake kweli hufanya hivyo? 47 Muradi wa neno faahishah katika aya hii, ambalo tumelifasiri kwa neno uchafu, ni maasia ya aina yoyote. Hivyo Mwenyezi Mungu hapa anawambia wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwamba yeyote katika wao atakayemuasi Mwenyezi Mungu, basi adhabu yake itakuwa kawili. Kwa nini ikawa hivyo Imekuwa hivyo kwa sababu ya hadhi walizokuwa nazo. Kwanza, wao wanakaa katika majumba ambamo humo huteremka wahyi wa Mwenyezi Mungu, na ndiyo makao makuu ya Utume. Pili, kwa sababu ya saa zote kuwa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), walikuwa na fursa ya kwanza ya kujifunza mambo ya Kiislamu kuliko watu wengine wote. Tatu, kwa sababu hiyohiyo ya kuwa na Bwana Mtume (s.a.w.w.) watu walikuwa wakiwatizama wao, na yote waliyokuwa wakiyafanya, kama ruwaza kwao. Kutokana na hayo, kwa hivyo, athari ya mwendo wa watu kama hao na tabia zao haziwi juu yao peke yao, bali vilevile juu ya jamii wanayoishi nayo. Hivyo huweza kuiathiri jamii kwa wema au kwa uovu (al-amthal). Ndipo thawabu zao na adhabu zao zikawekwa kawili kawili. 48 Yaani, enyi wake wa Mtume! Msidhani kuwa la kuwaadhibu nyinyi ni zito kwa Mwenyezi Mungu. Wala msidhani kwamba, la nyinyi kuwa wake wa Mtume, litamzuia Yeye kuwaadhibu. Hasha! Hishima yenu iko palepale kama wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Lakini mkiasi, mtaadhibiwa. Tizama pia aya ya 32 na maelezo yake yanayofuatia hapa chini. 17

33 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 KARA LA TATU WAMAN YAQNUT 31. Na yeyote katika nyinyi atakayemtwii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na akatenda njema, tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki yenye hishima. 32. Enyi wake wa Mtume! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine kama mtamcha Mwenyezi Mungu. 49 Basi msilegeze sauti zenu, asije akaingia tamaa mwenye maradhi moyoni mwake. 50 Na ال ا م ل ص ع ول و ت س ق ن ت م نك ن هلل و ر و م ن ي ا ٣١ ر يم ق ا ك ا ر ز ه ا ل ن ت د ني و أ ع ت ر ا م ر ه ج ا أ ت ه ن ؤ ت ي ق د م ن الن ساء إ ن ات ح أ ك ي ا ن ساء انل ب ل ست ن ر ض و ق ل ل ف ي طم ع ال ي ف ق ل ب ه م و ق ضع ن ب ال ف ل ت ر وف ا ٣٢ ع ق و ل م 49 Enyi wake wa Mtume! Kwa hishima yake (s.a.w.w.), nyinyi si kama wanawake wengine. Nyinyi mko juu. Lakini kwa sharti. Sharti yenyewe ni mumche Mwenyezi Mungu. Mkifanya hivyo, mtaipata hadhi hiyo. Kinyume chake, hamtakuwa na fungamano lolote na Bwana Mtume (s.a.w.w.) - kama ilivyokuwa kwa mke wa Nabii Nuhu (a.s.) na mke wa Nabii Lutwi (a.s.) (Sura 66: 10). Na huu ndio msimamo wa dini ya Kiislamu. Mkuruba wa aina yoyote na watu wema, usiokuwa na amali njema, haumfai kitu mtu (Sura 23:101). Na Bwana Mtume (s.a.w.w.) amelikiri hilo kwa Hadith kama zifuatazo: Imepokewa kwamba wakati mmoja Bwana Mtume (s.a.w.w.) alinadi: Ewe Fatma binti Muhammad! Ewe Swafia binti Abdil Muttwalib! Enyi Banii Abdil Muttwalib! Sitawafaa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Niombeni, katika mali yangu, mnachotaka. (Muslim). Katika riwaya nyengine imepokewa kwamba alinadi: Enyi Makureshi mlio hapa! Jiokoeni na Moto! Enyi Banii Ka b mlio hapa! Jiokoeni na Moto! Enyi Banii Haashim mlioko hapa! Jiokoeni na Moto! Enyi Banii Abdil Muttwalib mlioko hapa! Jiokoeni na Moto. Ewe Fatma binti Muhammad! Jiokoe na Moto. Maana mimi, ninaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu, sitawafaa kitu mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kwamba nitaendelea na ujamaa wangu nanyi (Muslim na Tirmidhi). 50 Mnapozungumza na wanaume msiwalegezee sauti bali zungumzeni nao kwa sauti ya kawaida isiyowatia mshawasha. Maana wale ambao ni wagonjwa wa maradhi ya jinsia ni rahisi sana kutekeka kwa sauti kama hiyo. Ukweli wa maneno haya ya Mwenyezi Mungu umewadhihirikia hata wataalamu wa saikolojia wa hizi zama zetu. Kwa mfano, katika uk. 61 wa Psychology of Sex cha Havelock Ellis, imeandikwa: Mlio wa sauti, utamu wake na nguvu zake, wembamba wake au unene wake, usafi wake au ukali wake mara nyingi, kwa haraka isiyo ya kawaida, hulazimisha mapenzi ya ghafla... Mvuto mkubwa wa sauti hudhihirishwa na idadi kubwa ya wanawake wanaoshikwa na mahaba ya kuwapenda waimbaji. (Daryabadi) Ikumbukwe kwamba amri hiyo, ya kutolegeza sauti wakati wanapozungumza na wanaume, wanaambiwa wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) mama za waumini - ambao hakuna kumbukumbu yoyote ya wao kukosewa adabu na maswahaba. Tena imeteremshwa katika zama za Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliyekuwa amezungukwa na swahaba wema. Na pamoja na yote hayo Mwenyezi Mungu, kwa kujua hatari ya sauti ya mwanamke kwa mwanamume, amewazuia wake za Mtume Wake wasilegeze sauti zao. Kefu leo ambapo tumekabiliwa na kila aina ya fitna! Sayyid Abul A la Maududi, katika Tafsiri yake ya Kiingereza chini ya aya hii, anasema hivi: 18

34 JUZUU YA 22 semeni maneno mema. 51 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 33. Na kaeni majumbani mwenu, 52 wala msidhihirishe mapambo yenu kama yalivyokuwa yakidhihirishwa katika jahilia Sasa hebu fikiri: Wakati ambapo Uislamu haumruhusu mwanamke kuzungumza na wanaume wengine kwa sauti laini na tamu, bali hata unamharamishia kutoa sauti yake mbele ya wanaume wengine bila ya dharura, jee utamruhusu atokeze juu ya jukwaa na kuimba, kucheza, kurembusha macho na kujitamanisha? Jee, utamruhusu aimbe nyimbo za mapenzi redioni na kuwatia shauku watu kwa nyimbo tamu zilizojaa fikra pujufu? Jee, utamkubalia acheze duri za wake na wapenzi wa watu wengine katika tamthilia? Au wanawake wafanywe wanahewa na wafunzwe maalumu kuwavutia na kuwashawishi abiria? Au watembelee vilabu na kuhudhuria dhifa na mikusanyiko ya starehe wakiwa wamejirembua kikamilifu, na kuchanganyika ovyo na wanaume, na kufanyiana nao maskhara na kustarehe? Utamaduni huu unatokana na Qur ani ipi? Maana katika Qur ani iliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu hamna kidokezo chochote cha kukubalika utamaduni wa aina hii. 51 Hapo juu wanawake wameamrishwa wasilegeze sauti wanapozungumza na wanaume. Sasa wanaamrishwa wateue hata ya kuzungumza nao. Yaani mazungumzo yao na wanaume yawe ni ya maneno mema. Muradi wa maneno mema hapa ni yale mazungumzo ambayo hayatampatia shetwani nafasi ya kuingia kati na kuleta ufisadi wake. 52 Hii ndiyo amri ya Mwenyezi Mungu kwa wanawake: kwamba wakae majumbani mwao; wasitoke ovyo ovyo bila ya dharura. Nyumba zao ziwe ndiyo makao yao makuu. Kusema hivi hakumaanishi kwamba mwanamke haruhusiwi kabisa kutoka nyumbani; la. Anaruhusiwa; lakini kwa dharura. Hata hivyo, dharura yenyewe isiachiliwe hadi ikaugeuza huu mpango wa Mwenyezi Mungu; ikawa mwanamke huyo anautumia wakati wake mwingi nje kuliko ndani ya nyumba yake. Baadhi ya watu hutoa hujja kwamba, kwa maisha yalivyo magumu siku hizi, ni vigumu kwa wanawake kukaa majumbani na kutotoka kwenda kutafuta kazi. i) ni kweli, maisha ni magumu siku hizi. Lakini hilo halikuletwa na amri ya Mwenyezi Mungu ya wanawake kukaa majumbani. Zaidi limeletwa na wanaume kutupa jukumu lao la kusimamia wanawake - wawe ni wake zao, mama zao, au dada zao - kwa mahitaji yao ya kimaisha kama ilivyoamrishwa na Mwenyezi Mungu (Sura 4:34). ii) Uislamu hauzuii wanawake kutoka majumbani na kwenda nje kufanya kazi. Unalosema ni kwamba hilo liwe ni kwa dharura tu; isiwe ndio mtindo. Na hata hivyo, kazi zenyewe ziwe ni zile ambazo hazitawapelekea wanawake hao kupoteza ile hadhi yao kama wanawake wa Kiislamu. K.m. wanaweza wakawa madaktari/ wakunga wa watoto wadogo/wasichana, wapishi wa kuajiriwa majumbani/mahotelini bora tu wafanye hivyo kwa kuchunga sharia nyengine za Kiislamu, washonaji nguo za kike - au hata za kiume - bora tu wawe hawakumpima wao huyo mwanamume, na kadhalika. iii) Wengi wa wanawake wanaofanya kazi nje hawana pato kubwa hivyo la kutosha kuendeshea maisha yao. Wanachopata ni sitara ya mbuzi tu kukalia mkia wake! Na hata hicho kichache wakipatacho huishia kugawanyiana na watumishi wanaowaajiri kuwafanyia kazi zao za nyumbani, ambazo huwa ni tabu kwao kuzifanya wanaporudi kutoka kazini! Kwa hili bila shaka tunaweza kuwalaumu wale wanaume waliokimbia jukumu lao la kuwatizama mama zao na dada zao hata ikabidi dada zao wabeheneke kuwatafutia tonge mama zao na, pengine, hata hao kaka zao! iv) Mbali na kutopata mishahara ya kutosha, mara nyingi hatuzingatii hasara kubwa inayopata jamii kwa mwanamke kutokaa nyumbani. 19 اه ل ي ة ال ول ب ج ال ن ت ب ج ي وت ك ن و ل ت و ق ر ن ف ب س ول ن اهلل و ر ط ع ك ة و أ ن الص ل ة و آت ني الز و أ ق م

35 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ya kizamani. 53 Na simamisheni swala, na toeni zaka, na mtwiini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. 54 Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi Watu wa Nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa. 55 Kwa mfano, mama anayetoka kazini, taabani kwa pirika pirika za kazi, hawezi kuipa nyumba haki yake kama mke nyumbani. Hawezi kuwapa watoto wake haki yao na kuwatizama na kuwalea vifaavyo. Unapoyatizama majumba ya wanawake wafanyakazi utaona kwamba mazingira yake hayana tafauti na yale ya hoteli na maloji! Nyumba, kuwa nyumba kweli, harufu yake hainukii ila ipulizwe na mke; kite chake hakienei ila kitawaliwe na mama. Na mwanamke, au mke, au mama anayemaliza wakati wake wote, na juhudi zake zote, nguvu zake zote za kiroho katika kazi hataleta katika nyumba isipokuwa mapresha, machofu na hangaiko tu (Fii Dhwilaalil Qur aan). Mbali malezi yasiyo ya Kiislamu, tunayowaachia watoto wetu kuinukia nayo, kwa mamama kwenda kazini na watoto wao kuwa mikononi mwa manasi na mamedi wasiokuwa Waislamu! Jee, hupata tukaiswawiri hasara inayorundikika kwa umma wa Kiislamu baada ya watoto hao kukua? Watu wengine, katika kutetea wanawake kutoka majumbani, hutoa hujja ya Bibi Aisha, mmoja wa wake za Bwana Mtume (s.a.w.w.), pale aliposhiriki katika Vita vya Ngamia (mwaka wa 36 Hijriya) kumpinga Imam Alii (a.s.). Lakini watu wanaotoa hujja hii, anasema Sayyid Abul A la Maududi kalika Tafsir yake ya Kiingereza, labda hawajui maoni ya Bibi Aisha, yeye mwenyewe, yalikuwaje juu ya jambo hili. Abdallah bin Ahmad bin Hanbal amesimulia katika Zawaid az-zuhd yake, na Ibn Mundhir, Ibn Abii Shayba na Ibn Sa d katika vitabu vyao, ile Hadith kutoka kwa Masruq inayosema kwamba Bibi Aisha alipokuwa akisoma Qur ani na kufikia aya hu (wa qarna fii buyuutikunna) alikianza kulia bila ya hiari mpaka mtandio wake ukaroa (kwa machozi), maana aya hii ilikimkumbusha kosa alilolifanya katika Vita vya Ngamia. 53 Kama tulivyokwisha kuona hapo juu, amri ya wanawake kukaa nyumbani, haimaanishi kwamba hawaruhusiwi kutoka nje asilan. La! Wanaruhusiwa, lakini pale tu panapokuwa na dharura. Hata hivyo, wanapotoka wanaamrishwa wasiyadhihirishe mapambo yao kama yalivyokuwa yakidhihirishwa katika jahilia ya kizamani. Nini muradi wa kudhihirisha mapambo kama yalivyokuwa yakidhihirishwa katika jahilia ya kizamani? Mujaahid amesema: Mwanamke alikitoka na kupita katikati ya wanaume. Hiyo ndiyo tabarrujul jaahiliyyah. Qataada amesema: Walikuwa na mwendo wa kumshawishi mtu na kumvutia. Mwenyezi Mungu akakataza hilo. Muqaatil b. Hiyyaan amesema: Tabarruj ni kwamba alikuwa akiweka mtandio juu ya kichwa chake, na asiufunge. Hivyo akaonyesha mikufu yake, vipuli vyake na shingo yake. Vyote hivyyo vikawa vinaonekana. Hiyo ndiyo tabarruj. (Ibn Kathiir). Na nini muradi wa jahilia ya kizamani? Lililo wazi iu kwamba hayo ni yale maovu vote yaliyokuwa yakifanywa na Waarabu, bali na watu wa ulimwengu mzima, kabla ya Uislamu (Maududi). Wala jahilia si kipinai cha zama maalumu, bali ni hali maalumu ya kijamii yenye mitizamo maalumu ya maisha. Na huwezekana kupatikana hali hii na mtizamo huu katika zama zozote na mahali popote. Ikawa ni dalili ya jahilia vyovyote ilivyo. (Fii Dhwilaalil Qur aan). Hivyo tunapoilinganisha hiyo jahilia ya kwanza na hii ya zama zetu tutaweza kuona jinsi tulivyopia hatua! Kama wanawake walikuwa wakidhihirisha mapambo yao katika zama za jahilia na kuvua mitandio yao kwa 20 ت س أ ه ل ال ي ج نك م الر ا ي ر يد الل ه ل ذ ه ب ع إ ن م ا ٣٣ ر ك م ت طه ري و ي طه

36 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 34. Na kumbukeni yanayosomwa majumbani mwenu katika aya za Mwenyezi Mungu na hikima. 56 Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya siri, Mwingi wa habari. 57 namna ambayo ilikidhihirisha sehemu za vifua yyao, shjngo zao, vidani vyao na vipuli vyao, basi katika zama zetu kuna vilabu vya watu kukaa uchi kama waliyyozaliwa na mama zao - na mifano yavyo ni maarufu Uingereza - na fedheha zifanywazo kwenye mabichi na mabwawa ya kuogelea, bali hata mwahali mwa watu wote na hadharani barabarani, kalamu huteshewa kuyataja. Kama katika jahilia (ya kwanza) malaya walikuwa na alama zao, walipokuwa wakipandisha bendera zao juu ya majumba yao ili kuwaita watu wawaendee, basi katika jahilia ya karne yetu watu hupeleka mambo na matakwa yao katika uwanja huu kupitia kwenye magazeti maalumu - mambo ya fedheha na ambayo kalamu huogopa kuyataja. Na jahilia hii ya Waarabu ni bora mara mia kuliko jahilia ya leo (al-amthal). Hapa ninakumbuka maneno yaliyosemwa na mwenzetu mmoja tulipokwenda Uingereza kwa mara ya kwanza katika mwaka wa Yeye alipoyaona maasia ya siku hizo, ambayo si chochote ukiyalinganisha na ya leo, alisema: Nina hakika lau Abuu Jahl atafufuka, Jeo na aje huku, basi bila ya, shaka atakuwa mwanafunzi wa maasia kwa watu hawa! 54 Baadhi ya watu hutoa hujja kwamba hizi amri zilizomo humu, kuanzia aya ya 28, zimekusudiwa wakeze Bwana Mtume peke yao kwa sababu ndio wanaosemezwa na Mwenyezi Mungu. Lakini amri hii ya kusimamisha swala, kutoa zaka, na kumtwii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake inaivunja hujja hiyo; maana haiwahusu wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) peke yao bali Waislamu woie. Hivyo amiri zilizomo humu haziwahusu wakeze Mtume peke yao bali wanawake wote. Kutajwa wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) hapo ni kiasi cha kutilia mkazo tu. Ni sawa na mtu kumwambia mwanachuoni: Wewe ni mwanachuoni. Basi usiseme uwongo. Hili halimaanishi kwamba uwongo unaruhusiwa kwa wafu wengine, ila linamaanisha kwamba inahitajia mwanachuoni akiogope zaidi kitendo hicho. 55 Kipande hiki cha aya hii kina mabishano makubwa - khaswa kuhusu muradi wa neno ahlul bayt (watu wa Nyumba ya Mtume) - baina ya wale wanaoamini kwamba, baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kufariki dunia, waliofaa kushika uwongozi wa Waislamu ni hao ahlul bayt (Shia), na wale wasioikubali imani ihiyo (Sunni na wengineo). Hivyo, kwa maelezo zaidi, soma Kijalizo 1 (uk. 46) humu. 56 Neno wadhkurna, katika aya hii, kwa kawaida lina maana mbili: kumbukeni na tajeni. Kwa maana ya kwanza, aya hii itakuwa na maana ya: Enyi wake wa Mtume! Msiyasahau hayo anayoteremshiwa Mtume (Wahyi) katika majumba yenu na hikima anazozitoa yeye kinywani mwake. Mjue kwamba jukumu lenu ni kubwa. Kwa hivyo msiteleze, mkaacha vitendo vya kijahilia vikaonekana katika majumba yenu. Kwa maana ya pili, itakuwa na maana ya: Enyi wake wa Mtume! Watajieni watu yote mnayoyasikia - ya wahyi anaoteremshiwa Mtume katika majumba yenu, na maelezo (sunna) yake ya wahyi huo yaliyojaa hikima. Maana nyinyi, kwa kuwa na Mtume wakati mwingi, mna fursa ya kujifunza mengi kwake. Hivyo watajieni (wafunzeni) na wengine. Pia, katika aya hii, vitu viwili vimetajwa: (i) aya za Mwenyezi Mungu; na (ii) hikima. Aya za Mwenyezi Mungu ni hizi aya za Qur ani Tukufu. Na hikima ni yale maneno ya (Hadith za) Bwana Mtume (s.a.w.w.) yaliyojaa hikima na ambayo, kwa kweli, ni kielelezo bora cha hiyo Qur ani (Sura 16:44). 57 Neno latwiifan, katika aya hii, vilevile lina maana mbili: Mjuzi wa mambo ya siri na Mpole. Tukilifasiri kwa maana hiyo ya kwanza itakuwa: Mwenyezi Mungu anazijua siri zenu na nia zenu, na hata yale ambayo yamefichika katika vifua vyenu na mabongo yenu ambayo nyinyi wenyewe hamna habari nayo. Tukilifasiri kwa maana hiyo ya pili itakuwa: Mwenyezi Mungu ni Mpole kwenu na Mwenye kuwarehemu sana. 21 ي وت ك ن م ن ف ب و اذ ك ر ن م ا ي ت ل ا ٣٤ ب ري ا خ ط يف إ ن اهلل ك ن ل ة ك م آي ات اهلل و ال

37 JUZUU YA Hakika Waislamu 58 wanaume na Waislamu wanawake, na waumini 59 wanaume na waumini wanawake, na watwiifu 60 wanaume na watwiifu wanawake, na wa-kweli 61 wanaume, na wa-kweli wanawake, na wanaosubiri 62 wanaume na wanaosubiri wanawake, na wanyenyekevu 63 wanaume na wanyenyekevu wanawake, na watoa-sadaka 64 wanaume na watoa-sadaka wanawake, na wanaume wanaofunga 65 na wanawake wanaofunga, na wanaume wanaozihifadhi tupu zao 66 na wanawake AL-AHZAAB WAMAN YAQNUT م ن ات ؤ م م ن ني و ال ؤ م ات و ال س ل م م س ل م ني و ال م إ ن ال ان ت ات و الص اد ق ني و الص اد ق ات ق ان ت ني و ال و ال ق ات ع ني و ال اش ع و الص اب ر ين و الصاب ر ات و ال اش م ت ص د ق ات و الص و ال م ت ص د ق ني و ال ات ائ م ني و الص ائ م و ال اف ظ ني ف ر وج ه م و ال ا ٣٥ ظ يم ر ا ع ج غ ف ر ة و أ م م ه ع د اهلل ل و ال اك ر ات أ ا ث ري اك ر ين اهلل ك اف ظ ات و ال 58 Waislamu ni wale ambao wameukubali Uislamu kuwa mwendo wao wa maisha, wameamua kuufuata katika maisha yao wala hawana nia ya kuupinga. Kwa maneno mengine, wamesalimu amri kikamilifu kwa Mwenyezi Mungu. 59 Waumini ni wale ambao utwiifu wao si wa juu juu tu au wa kukosa budi, bali huamini kwamba msingi wa uwongozi wa Kiislamu ni ukweli, na kwamba njia iliyoonyeshwa na Qur ani na Bwana Mtume (s.a.w.w.) ndiyo njia ya haki na iliyonyoka ambayo, ikifuatwa, ndiyo pekee inayoleta ufanifu wa kweli. Baadhi ya wafasiri huchukulia kuwa neno Islam lina maana moja na neno Iman. Lakini, kwa kweli, sivyo; kama Sura 49:14 inavyotufunulia. Hata Imam Ja far as-swaadiq (a.s.) amelifunua zaidi hilo katika riwaya hii: Mmoja wa maswahaba wake alimuuliza kuhusu Islam na Iman. Jee, ni tafauti? Imam (a.s.) akajibu: Iman imechanganya Uislamu, lakini Uislamu haukuchanganya Iman. Yule mtu akaomba afunuliwe zaidi. Imam (a.s.) akasema: Uislamu ni kushuhudia kwamba hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu, na kumsadikisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.). Kwawo damu zimehifadhiwa, ndoa na mirathi hupita, na watu hufuata dhahiri yake. Iman ni uwongofu na yaliyothubutu katika nyoyo, na amali iliyodhihiri kwayo. (Usuul al-kaafi) Na Bwana Mtume (s.a.w.w.) amesema: Haamini mmoja wenu mpaka matamanio yake yafuate niliyoyaleta. 60 Watwiifu ni wale ambao utwiifu wao umeandamana na unyenyekevu. Ni wale ambao utwiifu wao unatokana na imani kamili. Sio wale wanaoamini kuwa amri na makatazo ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.) ni haki, halafu wakatenda kinyume chayo. 61 Wa-kweli ni wale ambao wa hivyo kwa maneno yao na vitendo vyao, na muamala wao. Hawasemi uwongo. Hawahadai. Hawapunji. Hawasemi kwa ndimi zao lisilokuwamo nyoyoni mwao. Amesema Bwana Mtume (s.a.w.w.): Imani ya mja haiwi imara mpaka unyoke moyo wake; na moyo wake haunyoki mpaka unyoke ulimi wake. 62 Wanaosubiri ni wale wanaovumilia wanapokabiliwa na shida, hatari, vikwazo, na hasara kwa kufuata njia ya Haki iliyofundishwa na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.). Ni wale wanaopigana na matamanio ya nafsi zao, wasiyaachie kuwatawala. 63 Wanyenyekevu ni wale wanaojielewa vizuri kuwa wao, kama binadamu wenzao, ni waja wa Mwenyezi Mungu. Hawana cheo chochote zaidi ya hicho cha uja. Kwa hivyo hawana jeuri wala mtwazo wala kiburi kwa wengine. 64 Watoa-sadaka ni wale wanaozitoa hizo sadaka kwa ajili ya Mwenyezi Mungu: kusaidia maskini, mayatima, wagonjwa, vilema, wasiojiweza, na lolote ambalo litaipeleka mbele Dini ya Mwenyezi Mungu. 65 Wanaofunga ni wale wanaofunga saumu ya faradhi (ya Ramadhan) na za sunna ambazo humpa mtu mazoezi mazuri ya kuidhibiti nafsi yake na kutukukia yale matamanio yote ya kinyama yaliyo ndani ya nafsi ya binadamu. 66 Wanaozihifadhi tupu zao sio wale wanaojizuia kuzini tu, bali pia wale wasiokaa uchi kama wanavyofanya

38 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT wanaozihifadhi tupu zao, na wanaume wanaomkumbuka Mwenyezi Mungu 67 kwa wingi na wanawake wanaomkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi - Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na malipo makubwa Haiwi kwa muumini mwanamume wala muumini mwanamke, Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanapoamua jambo, kuwa na hiari. Na yeyote mwenye kumwasi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, basi amepotea upotevu ulio wazi. 69 ر ا م أ ا ق ض اهلل و ر سول م ن ة إ ذ ؤ و ل م م ن ؤ و م ا ك ن ل م م ر ه م و م ن ي ع ص اهلل ري ة م ن أ ن ي ك ون ل ه م ال أ ب ين ا ٣٦ ق د ض ل ض ل ل م ف و ر سول watu wengi wa zama zetu. Wala kukaa uchi sio maana yake ni kukaa bila nguo mwilini tu. Hata kuvaa nguo nyembamba inayoonyesha rangi ya mwili, au kuvaa nguo ya kubana inayodhihirisha umbo lake, pia ni kukaa uchi. Watu wa aina hiyo huwa hawamo katika wanaozihifadhi tupu zao. 67 Wanaomkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi ni wale wanaomkumbuka na kumtaja katika kila hali iwe wamesimama, wameketi au wamelala kwa mbavu zao (Sura 3:191) - na kila wakati - iwe ni asubuhi ama jioni (Sura 76:25). Wanamkumbuka wakati wa furaha na wakati wa huzuni, wakati wa shida na wakati wa raha, wakati wa maudhiko na wakati wa furaha, wakati wa uzima na wakati wa ugonjwa, na wakati wa ujana na wakati wa ukongwe. 68 Aya hii imekariri mara kumi kwamba wanawake wanaweza kuwa na sifa njema zilizotajwa humu kama wanavyoweza wanaume. Hili linaonyesha kwamba, kwa mujibu wa Qur ani, wanaume na wanawake ni sawa kiroho. Amesema Mwenyezi Mungu (Sura 16:97): Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa malipo yao kwa bora ya waliyokuwa wakiyatenda. 69 Karibu wanazuoni wote wa Tafsir wamekomangana kwamba aya hii iliteremshwa kuhusu ndoa ya Zaynab binti Jahsh na Zayd b. Haaritha. Zaynab binti Jahsh alikuwa binti ya Umayma binti Abdil Muttwalib, shangazi lake Bwana Mtume (s.a.w.w.). Na Zayd b. Haaritha alikuwa mtumwa wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) ambaye, baada ya kumwacha huru, alijulikana kama Zayd b. Muhammad. Lakini baada ya kuzuiliwa ada hiyo, ya mtu kumwita huru lake kwa ubini wake (tiz. aya 4-5 humu pamoja na maelezo yake), alirudi kuitwa kwa jina la babake mzazi. Bwana huyu alikuwa Mwislamu madhubuti na swahaba mwenye hishima kubwa. Aliwahi hata kuwa mmoja wa viongozi wa jeshi la Waislamu katika Vita vya Mu tah (8 Hijriya) ambapo alikufa shahidi. Alipotaka kumwoza Zayd, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alimwendea Abdallah b. Jahsh, kakake Zaynab bt. Jahsh, kumposea Zaynab. Mwanzo Zaynab alidhani kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) alitaka yeye kuowa. Kwa hivyo alifurahi, na akakubali. Lakini alipotambua kwamba anamposea Zayd, alibadilika akakataa. Na kaka yake pia akakataa. Ndipo Mwenyezi Mungu alipoiteremsha aya hii kumuonya Zaynab na kakake kwamba, kama Waislamu, hawana uwezo wa kupinga uamuzi wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Kama watafanya hivyo watakuwa wamemwasi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na hivyo wamepotea upotevu ulio wazi. Kusikia hayo, waliukubali uposo wa Bwana Mtume (s.a.w.w.); na Zayd b. Haaritha akamuowa Zaynab bt. Jahsh. Japokuwa aya hii ilishuka mintarafu ya ndoa ya Zayd na Zaynab bt. Jahsh, lakini amri iliyomo humo inahusu Waislamu wote wa zama zote na nchi zote. Hilo limewekwa wazi katika aya kadha wa kadha za Qur ani Tukufu, kama vile: Na ni nani mwenye dini bora kuliko mwenye kuisalimisha nafsi yake kwa Mwenyezi Mungu, na akawa ni 23

39 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 37. Na kumbuka pale ulipomwambia yule ه ي ل م ت ع ع ن ه و أ ي ل ع م اهلل ع ق ول ل ل ي أ ن و إ ذ ت ambaye Mwenyezi Mungu alimneemesha, nawe ukamneemesha: 70 Shikamana na م س ك اهلل و ت ف ف ن ف س ك أ ع ل ي ك ز و ج ك و ات ق mkeyo, na mche Mwenyezi Mungu. 71 اه ن ت ش ح ق أ و اهلل أ د يه و ت ش انل اس ب م ا اهلل م Ukaficha nafsini mwako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, 72 na ل ي ك ون ن ه ا و ط ر ا ز و ج ن اك ه ا ل ك ي د م ز ا ق ض ف ل م ukacha watu hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kutenda mema... (Sura 4:125). Naapa kwa Mola wako! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye hakimu wao katika wanayozozania, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utakayotoa, na wasalimu amri kabisa kabisa (Sura 4:65). Hakika neno la waumini, wanapoitwa kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake ili ahukumu baina yao, ni kusema: Tumesikia na tumetwii. Na hao ndio wenye kufaulu. (Sura 24:51). 70 Huyu ni Zayd b. Haaritha. Mwenyezi Mungu alimneemesha kwa kumjaalia kuwa Mwislamu na swahaba wa Mtume Wake (s.a.w.w.). Na Mtume (s.a.w.w.) alimneemesha kwa kumwacha huru, kumlea na kumfunza na kumwoza Zaynab bt. Jahsh. 71 Haya ndiyo maneno ambayo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alimwambia Zayd pale aliposhikilia kutaka kumtaliki mkewe. Na ilikuwa hivi: Baada ya kuowana, ilidhihiri kwamba ndoa yao ilikuwa zaidi ni ya miili yao. Tabia zao hazikuowana. Kwa hivyo ikawa ndoa hiyo haishi khasama. Ndipo Zayd akawa huenda kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) mara kwa mara kumshitakia na kumtaka shauri; na Bwana Mtume (s.a.w.w.) akawa humwambia asubiri, asifanye haraka kuacha. Huo ndio muradi wa: Shikamana na mkeyo, na mche Mwenyezi Mungu. 72 Kama tulivyoona katika aya ya 4, na katika maelezo Na. 5 humu, Mwenyezi Mungu aliiondoa ile dasturi iliyokuwa imeenea Bara Arabu, ya kumfanya mtoto wa kupanga kama mtoto halisi. Na kuzidi kulithibitisha hilo, alikuwa ameshapanga kwamba Zayd atamwacha mkewe na Bwana Mtume (s.a.w.w.) atamuowa baada ya kwisha eda yake ili, kama ilivyo katika aya hiyo hapo juu (na tiz. maelezo Na. 74), isiwe tabu kwa waumini kuowa wake wa watoto wao wa kupanga watakapokuwa wamekwisha haja nao. Na Bwana Mtume (s.a.w.w.) akadokezwa hilo na Mwenyezi Mungu. Lakini Zayd alipokuwa akimwendea na kumshtakia matatizo yake na mkewe, Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakumfunukia kwa hilo. Badali yake alilificha nafsini mwake, hali Mwenyezi Mungu alikuwa ameshapanga kulidhihirisha, na akalidhihirisha. Baadhi ya maadui wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) wametumia maneno haya yaliyomo katika aya hii kumkashifia Bwana Mtume (s.a.w.w.). Wanasema kwamba siku moja Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikwenda nyumbani kwa Zaynab. Kwa kuwa mlango wake ulikuwa umeshindikwa tu, alimwona vizuri na palepale akapagawa na uzuri wake! Zayd alipolijua hili, alimwacha, halafu Mtume (s.a.w.w.) akamuowa!! Kwa kweli, tuhuma hii haina mashiko. Tukumbuke kwamba Zaynab alikuwa binti ya shangazi lake Bwana Mtume (s.a.w.w.). Kwa hivyo hakuwa mgeni naye. Alikimjua tangu Zaynab ni mtoto. Kisha Bwana Mtume (s.a.w.w.), yeye mwenyewe, ndiye aliyekwenda kumposea Zayd. Na kama Zaynab alikuwa mzuri hivyo, basi hayumkini kwamba Mtume (s.a.w.w.) alikuwa halijui hilo. Pia, Zaynab hakumtaka Zayd bali alimkataa kweupe. Yeye akipenda kuwa mke wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hata pale Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipopeleka uposo wa Zayd, Zaynab na kakake walifurahi kwa kudhania kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa amekwenda kujiposea mwenyewe. Yeye alikubali kuolewa na Zayd pale tu iliposhuka aya ya 36 ya Sura hii. Basi kama mambo yalikuwa hivi, ni jambo gani lililomzuia Bwana Mtume (s.a.w.w.) kumuowa tangu yu mwanamwali bikra, akangojea mpaka akawa mke mkuu? Bila shaka tuhuma hii ni ovyo mno; yeyote mwenye akili timamu hatasita kuikataa. 24

40 JUZUU YA 22 aliye na haki zaidi ya kuchiwa. 73 Basi Zayd alipokwisha haja naye, tulikuoza wewe ili isiwe tabu kwa waumini kuowa wake wa watoto wao wa kupanga watakapokuwa wamekwisha haja nao. 74 Na amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kutekelezwa. 75 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ا و ا ق ض د ع ي ائ ه م إ ذ و اج أ ز ؤ م ن ني ح ر ج ف أ م ال ع ع ول ٣٧ ف م ر اهلل م م ن ه ن و طر ا و ك ن أ 38. Hapana lawama kwa Mtume kufanya ambalo amebainishiwa hukumu yake na Mwenyezi Mungu. 76 Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu kwa waliopita zamani. 77 Na amri ya Mwenyezi Mungu ni kadara س ن ة اهلل ل ا ف ر ض ر ج ف يم انل ب م ن ح م ا ك ن ع ا ر م ر اهلل ق د ب ل و ك ن أ ا م ن ق و ل اهلل ف ال ين خ ا ٣٨ م ق دور 73 Unachelea watu kukusema kwamba umemuowa mtalaka wa mtoto wako wa kupanga, kwa kuwa kitendo hicho ni aibu kubwa kwa mujibu wa mila zao, hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kuogopewa? Hapa Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama binadamu yeyote yule katika hali kama hiyo, alikuwa na wasiwasi wa watu watasemaje pindi yeye atakapomuowa Zaynab. Si watu watasema kwamba amemuowa mkwe wake? Lakini Mwenyezi Mungu alikuwa anataka kuiondoa dasturi hiyo ya kijahilia, ndipo akampa yeye jukumu hilo. Kwa hivyo hapana cha ati ati. Lazima afanye analolitaka Mwenyezi Mungu, watu wapende wasipende! 74 Hapa inaelezwa khaswa sababu ya Mwenyezi Mungu kushikilia Bwana Mtume (s.a.w.w.) amuowe mtalaka wa mtoto wake wa kupanga; nayo ni: isiwe tabu kwa waumini kuowa wake wa watoto wao wa kupanga. Yaani Mwenyezi Mungu anataka kuiondoa dasturi hiyo ya kijahilia, na amependelea jambo hilo lianzwe kufanywa na yeye mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.); tena ndani ya nyumba yao wenyewe ili hilo liwe mfano kwa wengine. Neno tulikuoza wewe katika aya hii linafahamisha wazi kwamba ndoa hiyo ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Zaynab bt. Jahsh ilikuwa ni kwa amri ya Mwenyezi Mungu; haikuwa ni chaguo lake wala la Zaynab. Na hii ni hujja nyengine ya kuwajibia wale wanaotuhumu kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) alimuowa Zaynab kwa kuvutiwa na uzuri wake (tiz. maelezo Na. 72 hapo juu). Hata yeye mwenyewe Bibi Zaynab alikuwa akijifakhiri mbele za wake wengine wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwa kusema: Nyinyi mmeozwa na watu wenu. Mimi nimeozwa na Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni (al-kaamil). 75 Yaani lolote lile analotaka Mwenyezi Mungu liwe, lazima liwe; halina kinga wala kafara. Na hivyo ndivyo ndoa ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Bibi Zaynab bt. Jahsh ilivyokuwa. 76 Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemwamrisha Mtume Wake (s.a.w.w.) amuowe mtalaka wa mtoto wake wa kupanga ili kuibatilisha ile dasturi ya kijahilia. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akatwii amri hiyo. Kwa hivyo hapana ila wala aibu hapo, kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) wala mtu mwengine, kufanya jambo hilo maadamu Mwenyezi Mungu amelihalalisha hata watu wasemeje. Aya hii ina funzo kubwa kwa viongozi - khaswa wa kidini: kwamba wasisikilize maneno ya watu katika kutekeleza amri za Mwenyezi Mungu; wala wasichunge siasa wala dasturi na mila zisizo za sawa zinazopingwa na Mwenyezi Mungu. Watekeleze amri za Mwenyezi Mungu bila ya kuogopa kulaumiwa (Sura 5:54) wala kukejeliwa. Maana haiwezekani kuwaridhisha watu wote. Wengine, kusema kweli, hawaridhiki mpaka wafuatwe wao (Sura 2: 120). 77 Muradi wa waliopita zamani hapa ni Mitume wa Mwenyezi Mungu waliotangulia ambao wanaendelea 25

41 JUZUU YA 22 iliyokwisha kadiriwa. 78 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 39. Ambao walikifikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na kumwogopa Yeye, wala hawamwogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu. 79 Na Mwenyezi Mungu ndiye anayetosha kuhisabu Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu, 81 bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu 82 na Mwisho wa Mitume. 83 Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. 84 kutajwa katika aya inayofuatia. Hivyo anaambiwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) hapa: Sio peke yako unayepata tabu hii kwa kuondoa mila iliyozoewa na kuota mizizi. Hata wale Mitume wenzako waliokutangulia, pia walipambana na tabu kama hiyo popote walipojaribu kuzing oa ada mbovu. 78 Yaani mipango ya Mwenyezi Mungu haiendi ovyo ovyo au sabahalala. Hupangwa kwa hikima na ujuzi na mizani - tangu mwanzo mpaka mwisho. Na lazima iwe vile alivyopanga Yeye. Hakuna cha kuizuia wala wa kuizuia. Hiyo ndiyo maana ya kadara iliyokwisha kadiriwa. 79 Hawa ni hao mitume wa Mwenyezi Mungu waliopita zamani, kama ilivyotajwa katika aya kabla ya hii. Wao waliwafikishia watu wao kila walilotumwa na Mwenyezi Mungu kulifikisha na, katika kuitekeleza kazi yao hiyo, hawakimwogopa yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu. Na hivyo, ewe Muhammad, ndivyo inavyotakikana uwe. Usiogope yeyote wala chochote katika kutekeleza ujumbe wako. 80 Fanya kazi yako, na hisabu mwachie Mwenyezi Mungu. Yeye anazihifadhi kazi zako na juhudi zako zote, na atakulipa mema kwazo; kama ambavyo anayahifadhi maneno yote machafu na kashfa zilizoenezwa na maadui ili aje awahisabu Siku ya Malipo na kuwaadhibu kwayo. Siku hiyo hakuna kitakachomponyoka Mwenyezi Mungu (Sura 18:49). Kila mtu atapawa kitabu cha hisabu yake akisome yeye mwenyewe (Sura 17:14). 81 Aya hii ni ya mwisho katika kueleza mambo yanayohusiana na ndoa ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Bibi Zaynab bt. Jahsh. Na ni jawabu fupi ya yale yaliyokuwa yakipingwa na adui za Bwana Mtume (s.a.w.w.): Jambo la kwanza walilokuwa wakilipinga ni Mtume kumuowa mkwe wake nalhali, kwa sharia yake, ni haramu mtu kumuowa mtalaka wa mwanawe. Hilo limejibiwa kwa maneno haya katika aya hii: Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu...; si Zayd wala mwenginewe. Zayd hakuwa mtoto wake wa kumzaa. Alikuwa mtoto wake wa kupanga. Lakini hilo limeshabatilishwa na Mwenyezi Mungu (tiz. aya ya 37 hapo juu). 82 Jambo la pili walilokuwa wakilipinga ni kitendo hicho kufanywa na Mtume, yeye mwenyewe. Wao wakisema : Hata kama mtoto wa kupanga si mtoto wake halisi, hapakuwa na haja ya yeye kumuowa mtalaka wa mtoto wake huyo. Hilo nalo limejibiwa kwa maneno:...bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu... ambaye ni wajibu wake kuongoza upinzani wowote dhidi ya mambo yasiyopendwa na Mwenyezi Mungu. Na tunapozingatia uzito wa kadhia yenyewe na jinsi ilivyokuwa imeshaota mizizi, na uzito wa wahusika wake, ni nani zaidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) angelifaa kujitokeza kuikomesha ada ya kijahilia kama hiyo? 83 Isitoshe! Mbali na kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, vile vile ni Mwisho wa Mitume yote. Hapana tena Mtume, wala wahyi, baada yake. Kwa hivyo imebidi awaachie umma wake turathi ya yote wanayoyahitajia mpaka Siku ya Kiyama; na ndivyo alivyofanya. Japokuwa Waislamu wote, wa madhehebu yote na zama zote, wanaamini kwamba Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho, na kwamba yeyote asiyeamini hivyo ni kafiri, lakini kuna baadhi ya watu wanaojulikana kama Makadiani au Mirzai au Wa-Ahmadiyya wanaokataa hilo. Kwa yanayosemwa na hao, na majibu yetu, soma Kijalizo II (uk. 57) humu. 84 Anajua mahitaji ya watu wote, wa jinsi zote, nyakati zote, mazingira yote, hali zote - tangu mwanzo wa dunia hadi mwisho wake. Kwa hivyo, kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kama Mtume wa Mwisho, amewawekea sharia ya mwisho - na misingi yake mikuu - ya kuswarifia yote mnayoyahitajia maishani mwenu. 26 ن ه و ل ي ش و ن و غ ون ر س الت اهلل و ي ش ب ل ال ين ي ف ب اهلل ح س يب ا ٣٩ أ ح دا إ ل اهلل و ك ن ر ج ال ك م و ل ك ن ر س ول د م ح ا أ ب م ا ك ن م م د أ ا ٤٠ ل يم ء ع اهلل و خ ات م انل ب ي ني و ك ن اهلل ب ك ل ش

42 JUZUU YA Enyi mlioamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi. 42. Na mtakaseni asubuhi na jioni Yeye ndiye anayewarehemu nyinyi, na malaika Wake pia, 86 ili awatoe vizani na kuwatia katika nuru. 87 Naye ni Mwenye kuwarehemu waumini Maamkizi yao siku watakayokutana naye 89 yatakuwa: Amani. 90 Na amewaandalia malipo yenye hishima. AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ا ٤١ ث ري ر ا ك ر وا اهلل ذ ك ك ن وا اذ ا ال ين آم ه ي ي ا أ ص يل ٤٢ ر ة و أ ك ح وه ب و س ب ن ي ك م و م ل ئ ك ت ه ل خ ر ج كم م ل ع ه و ال ي ي ص ل ا ٤٣ ح يم ؤ م ن ني ر م و ك ن ب ال ات إ ل انل ور م الظ ل ا ٤٤ ر يم ر ا ك ج ه م أ ع د ل ن ه س ل م و أ و ق ل و م ي ت ي ت ه م ي 85 Kwa maelezo zaidi, ya aya hii na iliyotangulia, tiz. maelezo Na. 67 humu. 86 Haya ni matokeo ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na kumtakasa. Kana kwamba Mwenyezi Mungu anawambia wale wanaofanya hivyo kuwa Yeye daima huwarehemu na kuwasamehe, kama ambavyo malaika nao - kwa upande wao - siku zote huwaombea wao rehema na maghfira Kwake. Na kwa rehema hiyo pazia la giza huondoka, na nyoyo zao na roho zao hujaa nuru ya ilimu, hikima, imani na ucha-mungu. Aya hii ni bishara kubwa kwa kila mwenye kufuata njia ya Haki: kwamba kuna mvuto wa nguvu kutoka upande wa Mwenye kupendwa (Mwenyezi Mungu) unaomvutia mwenye kupenda (binadamu) upande Wake ili juhudi za mwenye kupenda huyo, aliye muhitaji, ziishie mahali maalumu, zisipotee bure (al-amthal). 87 Na hii ndiyo rehema khaswa: ya kuwatoa waumini kwenye viza vya hamu na ghamu, vya matamanio na wasiwasi wa Shetwani, na kuwatia katika nuru ya yakini, utulivu wa moyo na kutotawaliwa na nafsi. Maana kama si kwa rehema za Mwenyezi Mimgu, isingewezekana kuifuata njia ya kutuongozea Kwake ambayo imejaa mizunguko na mipindopindo. 88 Rehema yenyewe ndiyo hiyo tuliyoitaja hapo juu. 89 Katika kueleza maana ya kukutana na Mwenyezi Mungu siku hiyo, Imam Fakhr ar-raazi amesema hivi katika Tafsir yake: Binadamu mara nyingi hughafilika na Mwenyezi Mungu katika ulimwengu huu kwa sababu ya kuzama katika mambo ya kimada na ya kwenda mbio kutafuta maisha. Lakini siku hiyo yeye mzima atamlekea Mola wa viumbe vyote kwa sababu yote yale yanayoshughulisha fikra zake hatakuwa nayo. Na hii ndiyo maana ya kukutana na Mwenyezi Mungu. (ar-raazi). Kutokana na maelezo hayo ni wazi kwamba kukutana na Mwenyezi Mungu kulikotajwa katika aya hii sio kukutana naye kimwili. Hilo si jambo linalowezekana, maana Mwenyezi Mungu hana mwili wala hali za kimwili. Kukutana huko ni kukutana naye kwa jicho la moyo maana siku hiyo mapazia yataondolewa, utukufu wa Mwenyezi Mungu na dalili Zake zote zidhihiri kwa wingi zaidi kuliko wakati wowote uliopita, na binadamu afikie daraja ya kuona kwa batini yake na moyo wake na, kutokana na uonaji wa aina hiyo, kila mtu atapata daraja inayolingana na kiasi cha ujuzi wake na amali zake njema alizozifanya hapa duniani. (al-amthal). 90 Ni nani atakayetoa salamu hiyo? Kutokana na aya nyengine za Qur ani inawezekana ikawa: i) ni Mwenyewe Mwenyezi Mungu ndiye atakayewaamkia waumini hivyo, kama ilivyotajwa katika Sura 36:58. ii) ni Malaika wa Mwenyezi Mungu, kama ilivyoelezwa katika Sura 16:32. iii) ni waumini ndio watakaoamkiana hivyo, wao kwa wao, kama ilivyoelezwa katika Sura 10:10. 27

43 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 45. Ewe Mtume! Hakika Sisi tumekutuma ير ا ٤٥ ذ uwe shahidi 91 na mtoa habari njema na ش ا و ن ب ر سل ن اك ش اه دا و م ا انل ب إ ن ا أ ه ي ي ا أ muonyaji Katika aya hii, na ile inayofuatia, Mwenyezi Mungu anamtaja Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwa sifa tano. Ya kwanza ni hii ya yeye kuwa ni shahidi. Ni shahidi kwa ulimi wake kwa kuwafikishia watu yote yale aliyotumwa na Mwenyezi Mungu, bila ya kuacha chochote. Ni shahidi kwa vitendo vyake kwa kuwa ruwaza njema wa yote yale aliyoyafikisha. Ni shahidi kesho Akhera katika Mahakama ya Mwenyezi Mungu kwamba, bila ya kufanya khiana yoyote, amefikisha ujumbe aliopawa, kwa ulimi wake na vitendo vyake. Qur ani inatueleza mahali pengine, ikisema na yeye Mtume (s.a.w.w.): Basi watakuwaje pindi tutakapowaletea kila umma shahidi wao, na wewe tutakuleta kuwa shahidi juu ya hawa? (Sura 4:41). Katika kuieleza aya hii, Sheikh al-amin b. Aly Mazrui amesema hivi katika Mjallada wa Pili wa Tafsir yake: Imepokewa kuwa siku moja Mtume (s.a.w.) alimwamrisha Bwana Abdallah bin Mas uud amsomee Qur ani; akamsomea. Hata alipofika katika aya hii, Mtume (s.a.w.) akatokwa ni matozi, na akamwambia Bwana Abdallah: Basi yatosha! Alilia Mtume (s.a.w.) kwa kukumbuka siku atakayosimamishwa mbele za watu wote kuwashuhudilia umma wake, wema wao na waovu wao, akihisi kama mtu atakayesimamishwa mbele za hakimu ili kutoa ushahidi wa uovu wa mwanawe ili apate adhibiwa kwa uovu wake. Basi ewe ndugu yangu Islamu! Ikiwa Mtume (s.a.w.) amelia kwa kufanywa shahidi juu ya umma wake kwa kite alicho nacho juu yao, jee wewe mwenye kushuhudiliwa umejizingatia hali utakayokuwa siku hiyo? Umejieka tayari na kujiandaa kwa amali za kheri ili siku hiyo usiwe miongoni mwa watakao dhurika na kuadhibiwa kwa ushahidi utakaotolewa ni Mtume (s.a.w.)? (Mazrui). 92 Sifa ya pili na ya tatu ni ya yeye kuwa ni mtoa habari njema na muonyaji. Ni mtoa habari njema, kwa waumini wote, ya malipo ya Mwenyezi Mungu yasiyo na ukomo, ya amani na furaha ya milele. Na ni muonyaji, kwa makafiri na wanafiki na watenda maovu wote, wa adhabu kali ya Mwenyezi Mungu. Katika Qur ani Tukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.), na Mitume wengine pia, wamesifiwa kwa sifa mbili hizi kwa mara zisizopungua 17. Hii ni kuonyesha umuhimu wa misingi miwili hii, bishara na onyo, kama wasila wa kutekelezea Ujumbe. Kwa kawaida, binadamu huwa na msukumo mkubwa zaidi wa kufanya mema pindi anaposhajiishwa, kama ambavyo hujizuia zaidi kufanya maovu pindi anapotishwa. Kushajiisha peke yake hakutoshi kumsukuma mtu kufanya wema, iwapo patakosekana cha kumzuia kufanya maovu. Pengine kielelezo kizuri cha hili ni Wakristo ambao kufanya maasia kwao ni jambo la kawaida. Hili hutokana na ile itikadi yao ya ukombozi: kwamba Yesu Kristo alijitoa mhanga ili wafuasi wake wasamehewe dhambi zao; au pia kwa itikadi yao kwamba maaskofu wao wana uwezo wa kuwafutia dhambi zao kwa njia mbalimbali, k.v. kuwapa hati za kusamehewa. Bila shaka watu wenye itikadi kama hizo huwa rahisi sana kwao kufanya maasia. Hili huonekana pia miongoni mwa Waislamu wanaoielewa vibaya itikadi ya uombezi wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwa kuamini kwamba madhambi yoyote atakayoyafanya Mwislamu, hata yawe makubwa vipi, hatatiwa Motoni kwa sababu Bwana Mtume (s.a.w.w.) atamshufaia, Waislamu wengi waonekana kutojali kufanya maasia! Kutokana na maelezo yetu hapo juu ni wazi kwamba, ili binadamu anyoke, anahitajia yote mawili: kutiwa tamaa na kutishwa; lakini kwa kiwango adilifu. Lau atatiwa tamaa mno, huenda akawa hajali kufanya lolote. Na lau atatishwa mno, huenda akakata tamaa, na shauku ya kufanya wema ikamtoka! Ili kumwezesha binadamu awe na mizani nzuri ya kuendeshea maisha yake, Mwenyezi Mungu alimtuma Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kama mtoa habari njema na, wakati huo huo, muonyaji. 28

44 JUZUU YA Na mlingania watu kwa Mwenyezi Mungu, 93 kwa idhini Yake, 94 na taa ing azayo. 95 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ن ه و س و د اع ي ا إ ل اهلل ب إ ذ ا ٤٦ ن ري ا م اج 47. Na wape habari njema waumini ya kwamba wana fadhila kubwa itokayo kwa Mwenyezi Mungu. 96 ش و ب ا ٤٧ ب ري م م ن اهلل ف ض ل ك ه ؤ م ن ني ب أ ن ل ال م 93 Hii ndiyo sifa ya nne ya Bwana Mtume (s.a.w.w.): kwamba anapolingania watu, huwalingania kwa Mwenyezi Mungu; sio dunia, wala utukufu, wala uzalendo, wala ubora wa kijahilia, wala ngawira, wala ufalme au cheo. 94 Wala hafanyi hivyo kwa kuzua yake mwenyewe. Hasha! Hufanya hivyo kwa amri ya Mwenyezi Mungu na idhini Yake. Lau angezua yake mwenyewe, Mwenyezi Mungu asingemwachilia (Sura 69:44-46). 95 Hii ndiyo sifa yake ya tano. Yeye si taa tu, bali ni taa ing azayo; yaani inayotoa nuru au mwangaza. Neno la Kiarabu, tulilolifasiri kwa taa hapa, ni siraaj. Neno hili, katika Qur ani Tukufu, limetumiwa mara nne. Mara tatu katika hizo limetumiliwa jua. Jua, kama inavyojulikana, mwangaza wake unatokana na loo lenyewe, hauupati kutoka sayari nyengine, kama mwezi mathalan. Na vivyo hivyo ndivyo alivyo Bwana Mtume (s.a.w.w.). Yeye ni taa inayotoa mwangaza unaoondoa viza vyote vya ujinga, ushirikina, na ukafiri. Lakini kama ambavyo kipofu hafaidiki kwa mwangaza wa jua, na kama ambavyo popo hujikinga nao kwa sababu ya macho yake kutoweza kuuhimili, ndivyo hivyo hivyo walivyo vipofu wa nyoyo, wakaidi na wenye chuki. Wao abadan hawafaidiki wala hawatafaidika kwa nuru hii, kama Abuu Jahl na mfano wake. Walikitia vidole vyao masikioni mwao ili wasisikie sauti ya Qur ani na utamu wake! Daima giza huleta khofu na jitimai; na nuru huleta utulivu na raha. Hivyo wevi na majambazi hutumia giza la usiku kuvunjia majumba na kunyakulia wanachokipata. Na wanyama wawindaji aghalabu hutoka mapangoni mwao wakati wa usiku panapokuwa giza. Mwangaza ndio msingi wa ukuaji wa miti, na matunda kuiva. Kwa ufupi, nishati zote za uhai hupatikana kwa mwangaza. Na hivyo ndivyo alivyo Bwana Mtume (s.a.w.w.). Kuwako yeye ndio msingi wa umakinifu na utulivu, na wevi wa dini na imani kukimbia, na vilevile wa mwitu wanaozidhuru na kuzidhulumu jamii zao. Huleta umakinifu wa nyoyo, na ukuaji wa roho ya imani na tabia njema. Kwa ufupi, ni msingi wa uhai na harakati. Na historia ya maisha yake ni ushahidi hai wa hilo (al-amthal). 96 Ni fadhila gani hiyo, iliyo kubwa, ambayo waumini wanabashiriwa kuwa wataipata kwa Mwenyezi Mungu? Fadhila hiyo ni ile ya Mwenyezi Mungu kuwalipa waumini malipo makubwa kuliko ya wema walioufanya, kama inavyoelezwa katika aya nyengine za Qur ani: i) Yeyote atakayefanya wema, atalipwa mfano wake mara kumi... (Sura 6:160). ii) Mfano wa ambao hutoa mali yao katika njia ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa punje iliyotoa mashuke saba, katika kila shuke mkawa na punje mia. Na Mwenyezi Mungu humzidishia anayemtaka... (Sura 2:261). Na zaidi ya hayo: iii) Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika hayo yanayofurahisha macho... (Sura 32:17). Hivyo, ni shida kwa muumini kujua, au hata kuswawiri, ukubwa wa fadhila aliyowekewa na Mola wake! 29

45 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 48. Wala usiwatwii makafiri na wanafiki, 97 و ك ع اه م و ت ذ م ن اف ق ني و د ع أ ط ع ال ك ف ر ين و ال و ل ت wala usijali udhia wao. 98 Nawe mtegemee Mwenyezi Mungu. 99 Na Mwenyezi Mungu اهلل و ك ف ب اهلل و ك يل ٤٨ anatosha kuwa Mlinzi. 49. Enyi mlioamini! Mkiwaowa wanawake ا ال ين آم ن وا إ ذ ا ن ك ح ت م ال م ؤ م ن ات ث م ه ي ي ا أ waumini, 100 kisha mkawaacha kabla ya kuwaingilia, 101 basi hamna eda juu yao ن ت م س وه ن ف م ا ل ك م ع ل ي ه ن ل أ ب وه ن م ن ق ت م ط ل ق 97 Kwa mara ya pili katika Sura hii Bwana Mtume (s.a.w.w.) anaambiwa maneno haya. Mara ya kwanza ni katika aya ya kwanza kabisa. Kama inavyojulikana katika historia, makafiri na wanafiki walijaribu sana kumshawishi Bwana Mtume (s.a.w.w.) awache kazi aliyopawa na Mwenyezi Mungu. Mara walimtaka asiwataje masanamu yao kwa ubaya. Mara wakamwambia Turuhusu tumwabudu Mola wako mwaka mmoja, na wewe uabudu miungu yetu mwaka mwengine! Mara nyengine wakasema: Tupe muhula mwaka mmoja tuendelee na dini yetu. Kisha tukuamini wewe. Pia waliwahi kumwambia: Waweke kando hawa waumini mafukara na maskini ili sisi - matajiri wenye vyeo - tuungane nawe. Na hata ufalme, mali na wanawake wazuri wazuri - walijaribu kumhonga! Yote hayo yalikuwa ni njama na hila za kuuzuia Uislamu usienee, na mizizi ya ukafiri na unafiki ising olewe. Na lau kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) angelionyesha ulaini au angelimili kupatana nao kwa mojawapo ya waliyoyataka, bila shaka zile nguzo za mapinduzi ya Kiislamu zingeporomoka, na juhudi zote za Bwana Mtume (s.a.w.w.) zisingekuwa na natija yoyote (al-amthal). Hiyo ndiyo sababu ya Mwenyezi Mungu kumwambia Bwana Mtume (s.a.w.w.) na, kupitia kwake, Waislamu wote kwamba wasiwatwii makafiri na wanafiki. 98 Mbali na kumtaradhia na kumbembeleza Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama tulivyoona hapo juu, makafiri na wanafiki - walipokata tamaa ya kukubaliwa maombi yao - walianza kumfanyia adha yeye, na Waislamu kwa jumla. Adha yenyewe ilikuwa ni ya kila aina. Mara waliwabeza. Mara waliwatukana na kuwakejeli na kuwakashifu. Mara nyengine waliwapiga na kuwatesa, na kujaribu kuwauwa. Hata kuwatenga na kuwasusia Waislamu wasiwe na maingiliano ya aina yoyote na wao, pia waliwafanyia. Yote hayo, anaambiwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) asiyajali; yaani asiyaache yakamshughulisha mno mpaka akawa hana nafasi ya kuifanya ile kazi kubwa aliyopawa na Mwenyezi Mungu ya kuwalingania watu, kama tulivyoieleza chini ya maelezo Na. 93. Hapa pana funzo zuri kwa viongozi wa dini: kwamba wasipoteze wakati wao kulipiza visasi kwa matusi au maovu wanayofanyiwa. Maana kadri ambavyo watautumia wakati wao kupambana na mambo hayo, ndiyo kadri ambayo maadui watafurahi kwa kujua kwamba lengo lao, la kuwakengeua na ujumbe wao, limefaulu. 99 La kufanya, katika hali kama hiyo tuliyoieleza hapo juu, baada ya kuchukua hatua za lazima, ni kumtegemea Mwenyezi Mungu. Na hivyo ndivyo alivyofanya Bwana Mtume (s.a.w.w.) pamoja na swahaba zake. Walipambana na upinzani wa makafiri kiume; hawakuteteleka hata chembe. Na uwezo huo waliupata kwa sababu walimtegemea Mwenyezi Mungu Mlinzi, naye akawalinda na kuwanusuru. 100 Baada ya Mwenyezi Mungu kuzungumza na Bwana Mtume (s.a.w.w.) katika aya nne zilizopita, sasa anarudi kuzungumza na waumini. Kwa kusema: Mkiwaowa wanawake waumini... hapa haimaanishi kwamba Waislamu hawaruhusiwi kuowa wanawake wasio waumini; la. Kwa mujibu wa Sura 5:5 Waislamu wanaruhusiwa kuowa wanawake wa Waliopawa Kitabu, yaani Wakristo na Mayahuhdi. Lakini ni bora kwao kuowa wanawake wa Kiislamu kuliko hao wa Kikristo na Kiyahudi. 101 Neno la Kiarabu katika aya hii, tulilolifasiri kwa kuwaingilia, ni tamassuuhunna. Maana ya neno hili, kwa lugha ya kawaida, ni kugusa. Hivyo, lau tutaifasiri aya hii neno kwa neno, itakuwa:... kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa... Lakini, kwa tafsiri hii, hatutaweza kuielewa aya hii vile ilivyokusudiwa kwa Kiarabu. Maana neno tamassuuhunna katika aya hii limetumiwa kistiara, sio kilugha ya kawaida. Ndio tukalifasiri 30

46 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT mtakayoihisabu. 102 Hivyo wapeni cha س احا ع وه ن و س ح وه ن ت م ا ف ه ون ت د ع ة ت م ن ع د kuwaliwaza, 103 na waacheni kwa njia nzuri. 104 ج يل ٤٩ 50. Ewe Mtume! Hakika Sisi tumekuhalalishia wewe wake zako ambao umewapa mahari yao, 105 na uliowamiliki kwa mkono wako wa kulia و اج ك الل ت آت ي ت ز ن ا ل ك أ ل ل ح ا انل ب إ ن ا أ ه ي ي ا أ ج ور ه ن و م ا م ل ك ت ي م ين ك م م ا أ ف اء اهلل ع ل ي ك أ ن ات ن ات خ ال ك و ب م ات ك و ب ن ات ع م ك و ب و ب ن ات ع kwa kuwaingilia - neno ambalo vilevile, katika lugha ya Kiswahili, hutumiwa kistiara kwa maana ya kuonana nao au kufanya nao kitendo. Hivyo aya hii, kwa lugha nyengine, itakuwa na maana:... kabla ya kufanya nao kitendo cha kike na kiume. Mwenyezi Mungu ametumia lugha ya stiara hapa ili kuepuka kutumia neno lake halisi ambalo, katika mazungumzo ya watu wowote wastaarabu, huonekana kuwa ni neno la kihimi au la kishenzi. Hata tafsiri yake ya Kiswahili, tuliyoitumia hapa, ni ya stiara. Hatukuweza kutumia neno lake halisi la Kiswahili. 102 Kwa sharia ya Kiislamu, wanawake wanapoachwa na waume zao, huwalazimu eda ya kuachwa, kama ilivyoelezwa katika Sura 2:228. Lakini hilo huwa ni iwapo waume zao waliwahi kuwaingilia kabla ya kuwaacha. Kama hawakuwahi kuwaingilia, basi hawatakaa eda, bali wataweza hata kuolewa na waume wengine mara tu baada ya kuachwa. Hilo ndilo linalosemwa na aya hii. 103 Katika Sura 2:237 Mwenyezi Mungu anawambia waume kwamba iwapo watawaacha wake zao kabla ya kuwaingilia lakini baada ya kuwakadiria mahari, itawalazimu kuwapa nusu ya mahari waliyowakadiria. Kama wamewaacha wake zao hao kabla ya kuwaingilia na kabla ya kuwakadiria mahari, kwa mujibu wa Sura 2:236 huwa hawana lazima ya kulipa chochote katika mahari. Lakini itawalazimu kuwapa cha kuwaliwaza. Wala hicho cha kuwaliwaza, hakina kima maalumu, bali kinategemea uwezo wa mume: aliye mweza kwa kadri yake, na aliye maskini kwa kadri yake (Sura 2:236). 104 Hili ndilo lile lile linalohimizwa katika Sura 2:229 na linalokaririwa wakati wa kufunga ndoa: la kuowana kwa wema na kuachana kwa wema. Waume, katika aya hii, wanahimizwa kwamba wanapowaacha wake zao wawaache kiungwana na kwa hishima. Isiwe ni mambo ya kutukanana na kukashifiana, au kutoleana aibu zilizositirika. Huo ndio muradi wa waacheni kwa njia nzuri katika aya hii. 105 Iliposhuka aya hii Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na wake wanne: Bibi Sawda bt. Zam ah ambaye alimuowa katika mwaka wa 3 H; Bibi Aisha bt. Abu Bakar ambaye alimuowa miaka mitatu kabla ya kuhamia Madina, lakini akamwingilia katika mwaka wa 1 H; Bibi Hafswa bt. Umar ambaye alimuowa katika mwaka wa 3 H; na Bibi Hindu bt. Abii Umayya (Ummu Salama) aliyemuowa katika mwaka wa 4 H. Hao ni wanne ambao ndicho kiwango kikubwa na cha mwisho anachoruhusiwa Mwislamu yeyote kuowa na kuwa nao kwa wakati mmoja (Sura 4:3), baada ya kuwalipa mahari. Halafu katika mwaka wa 5 H, akamuowa Bibi Zaynab bt. Jahsh ambaye kisa chake kimetajwa humu (aya ya 37). Hili likawapa fursa nzuri adui zake kueneza sumu kwamba Muhammad (s.a.w.w.) amewazuia wafuasi wake kuowa wake zaidi ya wanne, lakini yeye mwenyewe ameowa wa tano. Ndipo Mwenyezi Mungu alipoteremsha aya hii kuwahakikishia Waislamu kuwa Yeye (s.w.t.) ndiye aliyemhalalishia Mtume Wake (s.a.w.w.) kuowa zaidi ya wane. Ndoa hizi, za wake wengi alioruhusiwa Bwana Mtume (s.a.w.w.), zimewapa wapinzani wake hadi hii leo nafasi ya kumshambulia na kumwita mpenda wake! Bila shaka hili ni kwa kushindwa na kutotaka kuelewa hikima ya kuruhusiwa ndoa hizo. Kwa maelezo zaidi, tiz. Kijalizo III (uk. 90 humu). 31

47 JUZUU YA 22 katika uliopawa na Mwenyezi Mungu, 106 na mabinti ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako, na mabinti wa dada za mamako waliohama pamoja nawe, 107 na mwanamke muumini akijitoa mwenyewe kwa Mtume, ikiwa Mtume anataka kumuowa. 108 Hili ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine. 109 Sisi tunajua tuliyowafaridhia wao, kuhusu wake zao na wale waliomilikiwa na mikono AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT خ ال ت ك الل ت ه اج ر ن م ع ك و ام ر أ ة م ؤ م ن ة إ ن و ه ب ت س ت نك ح ه ا خ ال ص ة ل ك ر اد انل ب أ ن ي ب إ ن أ ا ل لن ن ف سه ي ه م ف ل ا ف ر ضن ا ع ن ا م ل م ؤ م ن ني ق د ع م م ن د ون ال ي ل ي ك ون ع ل ي ك ه م ل ك ان م ي ك ت أ ل ا م أ ز و اج ه م و م 106 Mbali ya hao wake watano, ambao tayari alikuwa anao, Mwenyezi Mungu vilevile alimhalalishia wajakazi aliowashika mateka katika vita vya jihadi. Hao ndio muradi wa uliowamiliki kwa mkono wako wa kulia katika uliopawa na Mwenyezi Mungu katika aya hii. Wajakazi hao, kwa kauli ya baadhi ya wanazuoni wa Tafsir, ni: Bibi Maria Mkibti aliyepawa hidaya na Maqauqis wa Misri; Bibi Rayhana bt. Sham un aliyeshikwa mateka katika mashambulizi dhidi ya Banii Quraydhwa; Bibi Juwayriya bt. al-haarith aliyeshikwa mateka katika mashambulizi dhidi ya Banii Mustwaliq; na Bibi Swafia bt. Huyayy b. Akhtab aliyeshikwa mateka Khaybar. Watatu kati ya hao Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwanza aliwaacha huru, ndipo kisha akawaowa. Lakini kuhusu Bibi Maria Mkibti hakuna ushahidi kuwa alifanyiwa kama hao wenzake watatu. Lielewekalo ni kwamba alitiwa usuriani. 107 Pia alihalalishiwa kuwaowa na hao. Lakini kwa sharti: wawe wamehama (hijra) pamoja naye. Muradi wa mabinti ami zako, na mabinti wa shangazi zako ni wanawake wa Kikureshi; na muradi wa mabinti wa wajomba zako, na mabinti wa dada za mamako ni wanawake wa kabila la Banii Zuhra, kabila la mamake Bwana Mtume (s.a.w.w.) (al-miizaan). Miongoni mwa wake zake katika kundi hili ni: Bibi Zaynab bt. Jahsh aliyekuwa binti ya shangazi lake, Umayma bt. Abdil Muttwalib, na Bibi Armala bt. Abii Sufyaan (Ummu Habiba). 108 Aina nyengine ya wanawake aliohalalishiwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuwaowa ni wale ambao, kwa ridhaa yao wenyewe na bila ya kutaka mahari, wamejitoa hiba kuolewa na yeye - kama atataka kuwaowa. Kuhusu hawa, kuna khitilafu baina ya wanazuoni. Baadhi yao, k.v. Ibn Abbas na wanazuoni wengine wa Tafsir, wanasema kuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakuowa mwanamke yeyote kwa namna hiyo. Hiyo ni ruhusa tu aliyopawa ambayo hakuitumia. Wengine wasema: La! Aliowa. Na hutaja majina ya wanawake watatu au wanne aliowaowa kwa namna hiyo. Nao ni: Maymuna bt. al-haarith, Zaynab bt. Khuzayma. Hawa wawili walikuwa ni answaar. Na mwanamke mmoja wa kabila la Banii Asad aliyekuwa akiitwa Ummu Sharik bt. Jabir, na Khawla bt. Haakim (al-amthal). Bila shaka mabibi hao hawakuwa na tamaa yoyote kwa kutaka kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.) bila ya mahari isipokuwa kupata fakhari ya kiroho ya kuwa wake wa Mtume au mama za waumini. 109 Hii ya kuowa mke bila ya kutoa mahari ni ruhusa aliyopawa Bwana Mtume (s.a.w.w.) peke yake. Mtu mwengine yeyote haruhusiwi kufanya hivyo, kwa sharia ya Kiislamu. Na hata kama mahari hayakutajwa wakati wa kufunga ndoa, itabidi mahari ya kufanana yatolewe. Na hayo ni yale mahari ambayo, kwa kawaida, hulipwa mwanamke mwenye sifa na tabia kama za huyo aliyeolewa bila ya kutajiwa mahari, katika mji ambako ndoa hiyo imefanyika. Aya hii pia inatufahamisha kwamba kuna amri maalumu ambazo zinamhusu Bwana Mtume (s.a.w.w.) peke 32 ا ٥٠ ح يم ا ر ور ف ح ر ج و ك ن اهلل غ

48 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT yao ya kulia, ili isiwe dhiki juu yako. 110 Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. KARA LA NNE 51. Unaweza kumwakhirisha umtakaye katika wao, na umsongeze kwako umtakaye. 111 Na umtakaye miongoni mwa uliowatenga, basi si vibaya kumsongeza kwako. Kufanya hivi kutapelekea yaburudike macho yao, wala wasihuzunike, na wawe radhi juu ya kila unachowapa wao wote. 112 Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole. 113 ه ن و ت ن ت شاء م ن ج م ت ر ل ت ف ل ج ن اح ز ي ت م م ن ع اب ت غ ت ق و اهلل ي ع ل م م ا ف ق ل وب ك م ن ن ت شاء و م ك م و ي إ ل ؤ أ ن د ذ ل ك أ ع ل ي ك ن ن ت ه ن ك ه ي ا آت ر ض ني ب م ي ن ه ن و ل حي ز ن و ي ع ر أ ا ٥١ ل يم ا ح ل يم و ك ن اهلل ع yake kuzifuata, sio Waislamu wengine. K.m. ni haramu yeye na jamaa zake kupokea sadaka; lakini si haramu kwa Waislamu wengine kufanya hivyo. Kuowa wake zaidi ya wanne, na kuwa nao wote kwa wakati mmoja, ni halali kwake, lakini si halali kwa Waislamu wengine. Yeye ameruhusiwa kumuowa mwanamke aliyejitoa hiba, bila ya mahari; lakini Mwislamu yeyote hamhusiwi hilo. Wake zake, baada ya yeye kufariki dunia, ni haramu kuolewa na yeyote. Lakini sio hivyo kwa wake wa Waislamu wengine, na kadhalika. Baadhi ya wanazuoni, katika sharia ambazo ni makhsusi kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.), hutaja ile ya mirathi: kwamba yeye harithiwi, kinyume cha watu wengine! Lakini hilo halina hujja madhubuti. Kwa maelezo zaidi, tiz. Kijalizo IV (uk. 98 hurnu). 110 Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ndiye anayejua sharia alizowawekea Waislamu za ndoa: za kutoa masumfu, mahari, kutokuwa na zaidi ya wake wanne kwa wakati mmoja, na za kuwa na wajakazi, na kadhalika. Na ndiye anayejua alizomwekea Bwana Mtume (s.a.w.w.) makhsusi. Na sababu yake ni kwamba asiwe na dhiki wala tabu. Kwa maelezo zaidi tiz. Kijalizo III (uk. 90 humu). 111 Katika maelezo Na. 46 ya aya 28 na 29 ya Sura hii, tuliona jinsi wake wa Mtume (s.a.w.w.) walivyokuwa wakimkera kuhusu masurufu yao kila siku, na jinsi Mwenyezi Mungu alivyomteremshia Bwana Mtume (s.a.w.w.) aya mbili hizo kuwateuza baina ya maisha ya dunia na pambo lake na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Nyumba ya Akhera. Wakaambiwa kinagaubaga kwamba kama watateua hilo la kwanza, basi itabidi Bwana Mtume (s.a.w.w.) awaache. Kama watateua hilo la pili, basi itawabidi waishi naye maisha yayo hayo ya kawaida. Wakeze wakateua hilo la pili. Zaidi ya hilo, wake hao pia walikuwa wana mashindano baina yao kuhusu noba zao, yaani vipi Bwana Mtume (s.a.w.w.) agawanye wakati wake baina yao. Japokuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) alijitahidi kadri alivyoweza kufanya uadilifu baina yao, mabibi hao waliendelea kuzozana. Ndipo Mwenyezi Mungu alipoteremsha aya hii kumwachia Bwana Mtume (s.a.w.w.) uhuru wa kugawanya wakati wake baina ya wake zake vile anavyotaka yeye: aache kulala kwa amtakaye, na alale kwa amtakaye. Na huo ndio muradi wa: Unaweza kumwakhirisha umtakaye katika wao, na umsongeze kwako umtakaye katika aya hii. Hata hivyo, pamoja na kupawa ruhusa hiyo na Mwenyezi Mungu, Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliendelea kuwafanyia uadilifu wakeze. Hakumpendelea yeyote bali aliwalalia wote kwa noba zao, isipokuwa ilipotokea dharura ya kutofanya hivyo. 112 Ilipotokea dharura ya kutomlalia mke wake fulani, aliruhusiwa kufanya hivyo. Lakini ilipotokea kutaka kumlalia yule ambaye hakumlalia, anaambiwa hapa kwamba si vibaya kumlalia. Maana kufanya hivyo 33

49 JUZUU YA Hawakuhalalikii wewe wanawake wengine baada ya hawa, wala kuwabadilisha kwa wake wengine 114 ingawa uzuri wao AL-AHZAAB 33 kutapelekea yaburudike macho yao (wafurahi), wala wasihuzunike, na wawe radhi juu ya kila unachowapa wao wote. 113 Makusudio ya nyoyoni mwenu hapa ni nyoyo za wake wa Mtume (s.a.w.w.) na watu wengine kwa jumla. Hivyo aya hii inawafahamisha wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anajua hukumu gani wameridhika nayo, kwa hivyo wameikunjulia nyoyo zao, na hukumu gani hawakuridhika nayo, kwa hivyo hawakuifurahia. Hali kadhalika aya hii inawafahamisha watu wengine, wasiokuwa wakeze Mtume (s.a.w.w.), kwamba Mwenyezi Mungu anazijua shaka zozote walizonazo nyoyoni mwao kuhusu unyumba wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama ambavyo anawajua wale walioridhika na hukumu Zake. Na kila mmoja atamlipa vifaavyo, maana Yeye ni Mjuzi, Mpole. Kwa hukumu zilizotajwa katika aya hii ya 51 yote, baadhi ya watu hudai kwamba Mwenyezi Mungu (Mwenyezi Mungu apishe mbali) amempendelea Bwana Mtume (s.a.w.w.) hapa na kuwanyima wake zake haki zao! Lakini tunapozingatia hadhi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.), upinzani aliokipambana nao, na kila aina ya vitimbi, ndipo tutakapoweza kuelewa hikima ya hukumu hizo. Na hapa chini tunajaribu kueleza japo kwa ufupi: Kiongozi yeyote mkubwa aghalabu huwa hana wakati mwingi wa kufikiria maisha yake ya kinyumbani, seuze Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliyekuwa amekabiliwa na wakati mgumu sana. Makafiri walikuwa wakimlia njama na kumpangia kila aina ya vitimbi - kwa ndani na kwa nje. Kwa hivyo alihitajia sana kuwa na utulivu mwingi katika maisha yake ya kinyumbani ili apate umakinifu wa kuyatatua yale matatizo yaliyokuwa yamemzunguka pande zote. Katika kipindi kigumu na nyeti kama kile kilichomkabili Bwana Mtume (s.a.w.w.) wakati huo, ilikuwa ni hatari kubwa kwake yeye, na kwa umma wote kwa jumla, kuwa na migogoro yoyote ya kinyumbani inayohanikiza moyo wake au fikra zake. Hilo ni zaidi pindi tunapotambua kwamba wake zake hawakuwa ni wake wa nyumbani tu, bali walikuwa ni wendani wake katika kuutekeleza na kuutendea kazi Ujumbe wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.). Hivyo khitilafu zozote baina ya wake zake, mizozo yoyote ya kike iliyokuwa ikizuka baina yao - ambayo ni kawaida kuzuka baina ya wake wenza - ilileta migongano ndani ya Nyumba ya Mtume (s.a.w.w.) iliyokishughulisha mno bongo lake. Hapo ndipo Mwenyezi Mungu alipomteremshia sharia nyengine makhsusi - yake yeye peke yake - iliyotuliza mizozo hiyo na kumpa yeye umakinifu wa kushughulikia kazi zake muhimu za kiutume; nayo ni hii iliyomo katika aya hii: Unaweza kumwakhirisha umtakaye katika wao, na umsongeze kwako umtakaye... Sote tunajua kwamba sharia ya Kiislamu kuhusu wake wengi inalazimisha wagawanyiwe nyakati zao kwa uadilifu. Mume akilala kwa mmoja siku moja, ni lazima alale kwa wa pili siku ya pili. Maana hakuna tafauti wala khitilafu baina ya wake katika hili. Lakini sharia hii ilimvua Bwana Mtume (s.a.w.w.) na jukumu hilo; ikawa si lazima kwake kuwagawanyia siku wake zake. Na hilo lilitokana na hali maalumu aliyokuwa akiishi, na migogoro na misukosuko iliyokuwa imemzunguka pande zote - khaswa pale alipokuwako Madina, ambako ndiko alikoanza kuwa na wake wengi, na ambako karibu kila mwezi alikuwa amekabiliwa na vita vya aina moja au nyengine. Hivyo kwa kuondolewa jukumu la kuwagawanyia siku wake zake, aliweza kufanya vile alivyotaka. Hata hivyo, historia inatueleza kwamba, kadri alivyoweza, alikuwa akiwagawanyia siku zao kwa uadilifu. 114 Katika aya ya 28 na 29 ya Sura hii, tumeona yale ambayo Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliamrishwa na Mwenyezi Mungu awateuze wake zake. Nao wakamteua Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Nyumba ya Akhera. Kwa maneno mengine, waliteua kuishi maisha ya kawaida yasiyo ya fakhari, tafauti na maisha ya wake wa maswahaba wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). 34 WAMAN YAQNUT ن ت ب ه ن م ن ب د ل ع د و ل أ س اء م ن ب ل حي ل ل ك الن ك ت ي م ين ك ل ا م ن ه ن إ ل م س ج ب ك ح ع و اج و ل و أ أ ز

50 JUZUU YA 22 utakupendeza, 115 isipokuwa yule aliyemilikiwa na mkono wako wa kulia. 116 Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu. AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ق يب ا ٥٢ ء ر ك ش و ك ن اهلل ع 53. Enyi mlioamini! Msiingie nyumba za Mtume ila mpawe ruhusa 117 kwenda kula, sio mngojee chakula kiive. Lakini mtakapoitwa, انل ب إ ل أ ن ي ؤ ذ ن وا ب ي وت ن وا ل ت د خل ا ال ين آم ه ي ي ا أ ري ن اظ ر ين إ ن اه و ل ك ن إ ذ ا د ع يت م ام غ ل ك م إ ل ط ع Katika aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamwekea Bwana Mtume (s.a.w.w.) sharia nyengine makhsusi kwake yeye tu: kwamba baada ya wake zako kuteua kubaki na wewe, basi huruhusiwi tena kuongeza wake wengine, wala kuwaacha hao na kuowa wanawake wengine mahali pao. Yaani usizidishe ulionao, wala usiwabadilishe. Sharia hii, kama tunavyojua, hawakuwekewa Waislamu wengine. Aliwekewa Bwana Mtume (s.a.w.w.) peke yake. Na bila shaka ina hikima na falsafa yake. Tunapoisoma historia, tunaona kwamba watu na makabila mbalimbali yalikuwa yakikimbizana kutaka Bwana Mtume (s.a.w.w.) aowe wanawake wao. Wengine walikuwa wa tayari hata kujitoa hiba: waolewe na Bwana Mtume (s.a.w.w.) bila ya kulipwa mahari wala sharti lolote! Bila shaka Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliowa hao aliowaowa, kama tulivyoeleza katika Kijalizo III (uk. 90) humu, kwa lengo la kijamii na la kisiasa: la kutatua matatizo fulani. Hata hivyo tayari hao aliokuwa nao walikuwa washakuwa wengi. Jee, aongeze wengine? Makabila mengine, ambayo yalikuwa bado hayajaolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), yalipendelea hivyo; yakitaka angalau na wao wapate ukwe wake. Lakini kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) angelimridhia kila aliyetaka - hata kama ni kumuowa tu bila ya kumwingilia, hilo nalo lingeleta matatizo mengine. Maana mambo yakizidi mno, huwa ni mno. Hivyo Mwenyezi Mrmgu Mwenye hikima akateremsha aya hii ili kuzuia matatizo ambayo yangelitokea lau asingemwekea Mtume Wake kikwazo hicho. 115 Baadhi ya watu walikijaribu kumshawishi Bwana Mtume (s.a.w.w.) aongeze wake kwa kisingizio kwamba alionao ni wake wakuu au si wazuri wa sura. Hivyo aongeze walio bikra au wazuri wa sura. Lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamwambia Bwana Mtume (s.a.w.w.) hapa kwamba asiongeze wala asibadilishe ingawa uzuri wao utakupendeza! 116 Hiyo amri ya kutoongeza wake aliokuwa nao ilihusu wale waungwana tu, sio wale waliomilikiwa na mkono wako wa kulia, yaani wajakazi. Hao aliruhusiwa kuowa idadi aitakayo, ila hakuitumia tu ruhusa hiyo. Wanawake waungwana waliwekewa kikomo kwa sababu baadhi yao ndio waliokuwa wakimkera Bwana Mtume (s.a.w.w.). 117 Kabla ya Uislamu, katika siku za jahilia, Waarabu hawakuwa na dasturi ya kubisha hodi walipokitaka kuingia nyumba ya mtu! Walikuwa wakijivurumiza tu mpaka ndani, bila ya kuomba ruhusa - hata kama ni nyumbani kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.)! Hivyo, kwa aya hii, waumini wanakatazwa kufanya hivyo. Wanaambiwa ni lazima waombe ruhusa kuingia - iwe ni kwa ajili ya ziara tu au ni kwa ajili ya kwenda kula. Amri hii, ya kutoingia nyumba ya mtu bila ya idhini yake, ilianza na nyumba ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwanza. Halafu, kama ilivyoelezwa katika Sura 24:27, ilichanganya nyumba zote - za Mtume (s.a.w.w.) na zisizokuwa za Mtume (s.a.w.w.). 35

51 JUZUU YA 22 basi ingieni. 118 Na mkisha kula, tawanyikeni, wala msiweke mazungumzo. 119 Hakika hayo yanamuudhi Mtume, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa jambo la haki. 120 Na mnapowauliza wakeze haja, basi waulizeni nyuma ya mapazia. 121 Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo AL-AHZAAB ن س ني ل د يث وا و ل م ست أ ف ي س م نك م و اهلل ل WAMAN YAQNUT ش ا طع م ت م ف انت وا ف إ ذ ل ف اد خ ذ ي انل ب ؤ ل ك م ك ن ي ي ت ح إ ن ذ ن م وه ل م و إ ذ ا سأ ق ي م ن ال ي س ت ح وب ك ل و ر اء ح جاب ذ ل ك م أ طه ر ل ق وه ن م ن ل ت اع ف اسأ ا م و ق ل وب ه ن و م س ول اهلل و ل أ ن ت نك ح وا أ ز و اج ه وا ر ذ ؤ ن ت م أ ك ك ن ل 118 Hii ni dasturi nyengine ya kijahilia waliyokuwa nayo Waarabu: ya mtu kwenda nyumbani kwa rafiki yake, au mtu tu anayemjua, wakati wa kula ili apate kula - japokuwa hakualikwa! Au ende wakati chakula kinapikwa, ajiweke kungojea kiive ili naye ajipatie angalau tonge! Yote hayo yanakatazwa na Mwenyezi Mungu. Linalotakikana ni watu wende kula nyumba za watu wengine pale tu wanapokuwa wamealikwa. Amri hii, kama ile iliyotangulia hapo juu, haimhusu Bwana Mtume (s.a.w.w.) peke yake bali Waislamu wote. Imeanzia nyumbani kwake kama kigezo tu. 119 Mnapokuwa mmealikwa kula, na mmekwisha kula basi msiendelee kukaa na kupiga soga. Tokeni na mwende zenu - isipokuwa kama mwenyeji wenu amewaomba mkae. Amri hii inatiliwa mkazo zaidi inapokuwa ni nyumba ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) ambaye haitakiwi kumshughulisha na mambo ambayo yatamwasa kutekeleza wajibu wake wa kiutume. 120 Sababu kubwa ya kuwekwa sharia hizi ni ili Bwana Mtume (s.a.w.w.) asighasike. Maana hayo yaliyokuwa yakifanywa na watu, kabla ya kuwekwa sharia hizi, yalikuwa yanamuudhi Mtume, isipokuwa alikuwa hawezi kusema; anawastahi hao wageni wake. Lakini kwa jambo kama hilo, la haki, Mwenyezi Mungu hastahi: Hulieleza kweupe! Kuhusu aya hii Anas b. Malik, aliyekuwa mtumishi makhsusi wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), ana yafuatayo ya kutueleza: Mtume (s.a.w.w.) aliniamuru niwaalike chakula swahaba zake. Nikawaalika. Wakawa huja makundi makundi, wanakula na kutoka. Mpaka nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Hakubaki mtu ambaye sikumwalika. Akaamrisha liondolewe kanda la chakula. Likaondolewa, na watu wakenda zao isipokuwa watu watatu. Wao walibaki katika nyumba ya Mtume (s.a.w.w.), wameshughulika na mazungumzo. Mtume (s.a.w.w.) alipoona mazungumzo yao yamekuwa marefu, aliondoka. Nami nikaondoka naye; ili hwenda watu nao wakaondoka kwenda makazini mwao. Aliondoka akenda mpaka kwa Bibi Aisha. Kisha akarejea mara nyengine, nami niko naye. Nikawaona watu wa vilevile, wamekaa. Ikateremshwa aya hii, nami nikawafahamisha jinsi ya kuamiliana katika masuala haya. (al-amthal). 121 Ni ada ya watu wote ulimwenguni, tangu kale hadi leo, wanapotokewa na haja ya kitu chochote, kwenda kwa jirani zao kukiazima. Na hivyo ndivyo walivyokuwa Waarabu pia zama za Bwana Mtume (s.a.w.w.). Walikuwa wakenda nyumbani kwake, kwa wake zake, kwa haja zao; na wakati huo walikiweza kuonana nao uso kwa uso. Kwa kuwa jambo hilo, la kuwaona wake za Bwana Mtume (s.a.w.w.) hivyo, halikuwa jambo zuri, ndipo Mwenyezi Mungu alipoteremsha aya hii kuwambia watu kwamba wanapokuwa na haja kwa wake za Mtume (s.a.w.w.), basi wawaulize nyuma ya pazia au nyuma ya mlango; wasionane nao uso kwa uso. Aya hii ndiyo inayojulikana kama aya ya hijabu. Lakini hijabu hapa ina maana ya pazia, sio mtandio au kitambaa cha kichwa, kama inavyojulikana hii leo. Wakati huo, iliposhuka aya hii, neno hijab halikijulikana kwa maana hii ya leo. Hivyo baada ya kushuka aya hii, mapazia yalitungikwa milangoni mwa nyumba za wake wa Mtume (s.a.w.w.) na, kwa kuwafuata wao, nyumba za Waislamu wote kwa jumla.

52 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT zao. 122 Wala haiwafalii nyinyi kumuudhi ا ٥٣ ظ يم ب دا إ ن ذ ل ك م ك ن ع ند اهلل ع د ه أ م ن ب ع Mtume wa Mwenyezi Mungu, wala kuwaowa wake zake baada yake kabisa. Hakika jambo hili ni dhambi kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mkidhihirisha chochote kile, au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu Hapana ubaya kwao kuonana na baba zao, wala watoto wao, wala ndugu zao, wala watoto wa ndugu zao wa kiume, wala watoto wa ndugu zao wa kike, wala wanawake wenzi wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao 122 Hilo la wanaume kuzungumza na wake wa Mtume (s.a.w.w.) nyuma ya pazia linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao. Suali hapa ni: Kama wake wa Mtume (s.a.w.w.) na maswahaba ni hivyo, jee sisi wa leo? Si ndio zaidi tutahadhari kuchanganyika ovyo wanaume na wanawake? Mwalimu wetu wa chuoni, Sheikh Muhammad Ahmad Matano, alikuwa na maneno yake ya nasaha aliyokuwa akipenda sana kutukariria. Nayo ni haya: Mwenyezi Mungu ndiye aliyemuumba mwanamume, na ndiye aliyemuumba mwanamke. Yeye ndiye anayejua ametia chuma gani kwa mwanamume, na sumaku gani kwa mwanamke; ndipo akaonya kwamba wawili hao wasiachwe kukaribiana maana lazima watavutana. Sasa! Twendapo tukapuuza onyo hilo, ndio tunajiona sisi tuna akili zaidi kuliko Yeye? 123 Hii ni hukumu nyengine ambayo ni makhsusi kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.): kwamba wake zake ni haramu kuolewa na yeyote baada yake. Lakini sio hivyo kwa wake wa watu wengine. Kwa mujibu wa Tafsir zao, miongoni mwa nyengine, Imam Fakhr ar-raazi na al-qurtubi wamesema kwamba aya hii iliteremshwa pale Twalha b. Ubaydullaah at-taymi aliposema: Muhammad (s.a.w.w.) atakapokufa, nitamuowa Aisha. Tukiizingatia hukumu hii, tutaona kuwa nayo pia ina hikima zake: Moja: ni kwamba, kama tulivyoona katika sababu ya kuteremshwa aya hii, baadhi ya watu walikuwa wameazimia kuwaowa wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), baada ya yeye kufariki dunia, kama njia mojawapo ya kumlipa kisasi na kutia doa utakatifu wake. Pili: lau kama ingeliruhusiwa wake wa Mtume (s.a.w.w.) waolewe na watu wengine, baada ya yeye kufariki dunia, maadui wa Uislamu wangelipata fursa nzuri ya kuukoroga. Maana, kwa kuwaowa mabibi watukufu hao, wangeliweza kueneza uwongo na unafiki mwingi kwa kudai kwamba wameyapata hayo kwa wake zao waliokuwa chemchemu za ilimu ya Waislamu kwa kusadifu kutangulia kuwa wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hivyo Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa ya siri na ya dhahiri, aliliwahi jambo hili kabla ya kutukia; akapitisha hukumu hiyo. Kwa sababu hii, kama historia inavyoshuhudia, ndio wake wa Mtume (s.a.w.w.) wakaweza, baada yake, kuishi kwa adabu na hishima kama mama za waumini. 124 Chochote mlichokipanga, cha kumuudhia Mtume (s.a.w.w.) - iwe mmekidhihirisha kwa ndimi zenu, au mmekificha nyoyoni mwenu - msidhani kwamba Mwenyezi Mungu hakijui. Anayajua yote hayo vizuri sana, na kila mmoja wenu atalipwa kwa mujibu wa aliyoyafanya. 37 وه ف إ ن اهلل ك ن ب ك ل ش ء ئ ا أ و ت ف ي وا ش د إ ن ت ب ا ٥٤ ع ل يم ب ن ائ ه ن و ل إ خ و ان ه ن ي ه ن ف آب ائ ه ن و ل أ ل ل ج ن اح ع ات ه ن و ل ن س ائ ه ن و ل ن اء أ خو ب ان ه ن و ل أ ن اء إ خو ب و ل أ ك ه ن و ات ق ني اهلل إ ن اهلل ك ن ع ان م ي ك ت أ ل م ا م

53 JUZUU YA 22 ya kulia. 125 Na mcheni Mwenyezi Mungu, enyi wanawake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushuhudia kila kitu Hakika Mwenyezi Mungu na malaika Wake wanamswalia Mtume. Enyi mlioamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu. 127 AL-AHZAAB WAMAN YAQNUT ء ش ه يد ا ٥٥ ش ا ال ين ه ي انل ب ي ا أ إ ن اهلل و م لئ ك ت ه ي ص ل ون ع ا ٥٦ وا ت سل يم م ه و سل ي ل آم ن وا صل وا ع 125 Baada ya Mwenyezi Mungu kuwaamrisha wanaume wasiwaombe haja wake za Mtume (s.a.w.w.) isipokuwa nyuma ya mapazia, katika aya hii wamevuliwa watu maalumu katika hukumu hiyo. Hao hapana ubaya kwao kuonana nao. Baadhi ya wanazuoni wa Tafsir wamesema kwamba baba za wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) na watoto wao na aila zao, baada ya kushuka aya ya 53 hapo juu, walimuuliza: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Na sisi pia tuzungumze nao nyuma ya mapazia? Ndipo ilipoteremshwa aya hii (al-amthal). Amri kama hii pia wameteremshiwa wanawake wa Kiislamu kwa jumla. Tiz. Sura 24: Wanawake wanaosemezwa katika aya hii hapa ni wake wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Wao ndio waliokusudiwa kwa amri hiyo ya kumcha Mwenyezi Mungu hapa, ingawa amri hiyo huchanganya watu wote - wake kwa waume - maana ucha-mungu ndio msingi mkubwa wa kuzitwiia amri za Mwenyezi Mungu na kuepukia makatazo Yake. 127 Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.), katika aya zilizotangulia, kutueleza ilivyo wajibu wetu kumtukuza na kumhishimu Mtume Muhammad (s.a.w.w.), na kutomuudhi, katika aya hii kwanza anatuelezea mapenzi Yake na ya malaika Wake kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.), na kisha anawaamrisha waumini nao wampende na kumtukuza. Muradi wa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kumswalia Mtume (s.a.w.w.) ni kuridhika naye na kumrehemu; muradi wa malaika kumswalia yeye ni kumsifu kwa kila jema; na muradi wa waumini kumswalia ni kumwombea rehema. Hivyo, kwa lugha nyengine, aya hii inasema hivi: Hakika Mwenyezi Mungu ameridhika na Mtume Wake, na humrehemu wakati wote; Malaika nao, kwa upande wao, saa zote humwombea rehema kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo nanyi, enyi waumini, msiache kumuombea rehema na kumsalimu kwa salamu. Lakini ni vipi khaswa kumswalia Mtume? Hilo aliulizwa yeye mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.) na akajibu hivi: Semeni Allaahumma swalli alaa Muhammadin wa alaa aali Muhammad, kamaa swallayta alaa Ibraahiima wa alaa aali Ibraahiima, innaka Hamiidun Majiid. Allaahumma baarik alaa Muhammadin wa alaa aali Muhammad, kama baarakta alaa Ibraahiima wa alaa aali Ibraahiima, innaka Hamiidun Majiid. Kutokana na Hadith hiyo hapo juu, ambayo imepokewa kwa maswahaba mbalimbali k.v. Ibn Abbas, Twalha, Abuu Said al Khudhri, Abuu Hureira, Abuu Mas uud al-answaari, Burayda, Ibn Mas uud, Imam Alii (a.s.) na wengineo, ndiyo baadhi ya Waislamu (Mashia) wakawa humswalia Mtume, popote anapotajwa, kwa kusema: Allaahumma swalli alaa Muhammadin wa ( alaa) aali Muhammad au Swallallahu alayhi wa aalihii wa sallam. Hata hivyo ni jambo la kuhuzunisha kuona kuwa Waislamu wengi sana (Sunni na wengineo) hawafanyi hivyo. Wao hutosheka na kumswalia Mtume (s.a.w.w.) peke yake bila ya kumchanganya na aali zake, kwa kusema Allahumma swalli alaa Muhammad au Swallallaahu alayhi wasallam tu! Na hilo limekatazwa khaswa na mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.), katika Hadith iliyotajwa na Ibn Hajar katika kitabu chake kinachoitwa As Swawaaiqul Muhriqah. Amesema kwamba imepokewa kuwa Mtume (s.a.w.w.) alisema: Msiniswalie swala kigutu. Maswahaba wakamuuliza: Ni ipi swala kigutu? Akajibu: Ni kusema Allaahumma swalli alaa Muhammad, mkasimama. Bali semeni: Allaahumma swalli alaa Muhammadin wa aali Muhammad. Kwa ajili hii ndiyo nasi, katika Tafsir yetu hii na maandishi yetu mengine, tukawa tunatumia (s.a.w.w.) - sio (s.a.w.) - tunapomtaja Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hiyo (s.a.w.w.) ni kifupisho cha swala sahihi ya kumswalia Bwana Mtume (s.a.w.w.); na (s.a.w.) ni kifupisho cha hiyo swala kigutu!

54 JUZUU YA Hakika wale ambao humuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu yenye kufedhehi Na wale ambao huwaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya kosa lolote, bila shaka wamebeba dhulma kubwa na dhambi zilizo wazi. 129 AL-AHZAAB WAMAN YAQNUT ي ا ن ه م اهلل ف ادلن ع ل ذ ون اهلل و ر سول ؤ إ ن ال ين ي ه ين ا ٥٧ ا م اب ذ ه م ع ع د ل و ال خ ر ة و أ ت سب وا ري م ا اك م ن ات ب غ ؤ م ؤ م ن ني و ال م ذ ون ال ؤ و ال ين ي ب ين ا ٥٨ ا م م ا و إ ث ت ان ه وا ب ل ت م د اح ف ق Hali kadhalika imehimizwa sana kwamba tusichoke wala tusione choyo kumswalia Mtume (s.a.w.w.) popote anapotajwa maana yeye mwenyewe (s.a.w.w.) amesema: Bakhili ni yule ambaye ninapotajwa mbele zake, haniswalii (Imam Ahmad). Mbali zile Hadith zinazotueleza fadhila zake: Bora ya watu kwangu Siku ya Kiyama ni aliye mwingi mno wa kuniswalia (Tirmidhi). Mwenye kuniswalia mimi mara moja, Mwenyezi Mungu humswalia yeye, kwa swalayake hiyo, mara kumi (Muslim, Abuu Daawuud, Tirmidhi). Mwenye kuniswalia mimi swala moja, Mwenyezi Mungu humswalia yeye swala kumi na (pia) humfutia makosa kumi (lmam Ahmad). Katika maelezo ya aya hii, wanazuoni wengi wa Tafsir wa Kisunni wamesema kwamba haifai kumswalia yoyote asiyekuwa Mtume (s.a.w.w.) kwa swala hiyo, na hata kwa kusema alayhis salaam (a.s.)! Hili bila shaka limelengewa Mashia ambao popote wanapowataja maimamu wao 12 na Bibi Fatma (a.s.) huwasalimu hivyo. Lakini la kushangaza hapa ni kwamba tunapoisoma Sahih Bukhari, ambacho ndicho kitabu sahihi mno baada ya Qur ani kwa wanazuoni hao na wafuasi wao, tunaona kwamba maneno alayhis/ alayhas salaam yametumiwa baada ya kutaja majina ya watukufu hao, k.v. Imam Alii (a.s.), Bibi Fatma (a.s.), Imam Hasan b. Alii (a.s.), Imam Husein b. Alii (a.s.)!! 128 Makusudio ya kumuudhi Mwenyezi Mungu hapa ni kumshirikisha na kitu, kumnasibisha na kisichokuwa laiki Yake, kumsingizia la uwongo, kutofuata amri Zake. Na makusudio ya kumuudhi Mtume Wake ni kumtaja kwa lisilokuwa laiki yake, kumshambulia, kutomfuata, kumzulia uwongo, na kuwaudhi watu wa Nyumba yake (ahlul bayt). Basi wale wanaofanya mambo kama hayo huwa wamemuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.); hivyo hulaaniwa na Mwenyezi Mungu hapa duniani na Akhera na pia, huko Akhera, amewaandalia adhabu yenye kufedhehi. Na maana ya kulaaniwa ni kutengwa au kuwekwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu. Amesema Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuhusu binti yake, Fatma (a.s.): Fatma ni sehemu yangu mimi. Anayemghadhibisha yeye basi amenighadhibisha mimi (Bukhari). Pia amesema: Fatma ni sehemu yangu mimi. Hunighasi linalomghasi, na huniudhi linalomuudhi (Muslim). 129 Neno la Kiarabu katika aya hii, tulilolifasiri kwa neno dhulma kubwa, ni buhtaanan. Neno hili kwa kawaida lina maana ya uwongo au kumsingizia uwongo mtu, au kukashifu. Historia inatujulisha kwamba siku hizo, katika mji wa Madina, kulikuwa na watu waliokuwa hawana kazi isipokuwa kueneza uvumi na uwongo dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Waislamu wote kwa jumla. Watu hao, ambao wengi wao walikuwa wanafiki, ndio wanaoonywa kuwa kitendo chao hicho ni dhulma kubwa na dhambi zilizo wazi. Jambo hili limeelezwa vizuri na Bwana Mtume (s.a.w.w.), katika Hadith iliyopokewa na Abuu Daawuud na Tirmidhi, pale alipoulizwa ni nini ghiibat (kusengenya). Akajibu: Ni kumtaja nduguyo kwa njia ya kumtweza. Akaulizwa: Jee, kama huyo ndugu yangu analo kweli jambo hilo? Mtume (s.a.w.w.) akajibu: Kama analo kweli jambo hilo, basi umemsengenya. Kama hana, basi umemkashifu.

55 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ز و اج ك و ب ن ات ك و ن س اء ال م ؤ م ن ني 59. Ewe Mtume! Wambie wake zako na binti ا انل ب ق ل ل ه ي ي ا أ zako, na wake za waumini, wajiteremshie ع ر ف ن nguo zao. Hilo ni karibu zaidi kuweza ن ي أ ن د ي ه ن م ن ج ل ب يب ه ن ذ ل ك أ ل ي د ن ني ع kujulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye ا ٥٩ ح يم ا ر ور ف ف ل ي ؤ ذ ي ن و ك ن اهلل غ kurehemu. 130 KARA LA TANO 60. Kama wanafiki, na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha kufanya hivyo, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu. 131 ر ض وب ه م م ن اف ق ون و ال ين ف ق ل م نت ه ال ل ئ ل م ي ك ب ه م ث م ل ي او ر ون ك ن ر ي د ين ة نل غ م ج ف ون ف ال ر و ال م ف يه ا إ ل ق ل يل ٦٠ Pia imepokewa kwa Imam Alii b. Musa ar-ridhaa (a.s.) kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) amesema: Yeyote anayemkashifu muumini mwanamume au mwanamke, au anayemsema kwa asilokuwa nalo, basi Mwenyezi Mungu aliyetukuka atamsimamisha Siku ya Kiyama juu ya kilima cha moto, mpaka atoke katika yale aliyomsingizia (Bihaarul Anwaar). 130 Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.), katika aya zilizopita, kukataza watu wasimuudhi Bwana Mtume (s.a.w.w.) na waumini, katika aya hii anamwamrisha Mtume Wake (s.a.w.w.) awambie wake zake na binti zake, na wake za waumini wajifunike vizuri wanapotoka nje. Amri hii ilikuwa ni moja ya mbinu za kufungia nafasi iliyokuwa ikitumiwa kuwaudhia Waislamu na Mtume wao. Siku hizo, wanawake wa Kiislamu walikuwa wakenda msikitini kuswali nyuma ya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Walipokuwa wakenda kuswali magharibi na ishaa, baadhi ya vijana wakora walikuwa wakikaa njiani na kuwaudhi kwa maskhara na uchokozi wa kuwakosea adabu. Ndipo ikateremshwa aya hii kuwaamrisha wajiteremshie nguo zao ili wasijulikane wasije wakaudhiwa (al-amthal). Neno la Kiarabu katika aya hii, tulilolifasiri kwa nguo zao, ni jalaabiibihinna. Neno hili ni wingi wa neno jilbaab ambalo lina maana ya mtandio na ukaya au nguo ndefu kuliko mtandio inayofunika kichwa, shingo na kifua au kanzu pana ya kupwaya mwili (al-amthal). Na muradi wa wajiteremshie nguo zao katika aya hii ni: wajivutie nguo zao ili ziwe ni sitara yao, wasiziache ovyo zikadhirihisha miili yao. Kuhusu aya hii, na maana za neno jilbaab tulizozitaja hapo juu, kuna makindano baina ya wanazuoni kuhusu uso: ufunikwe pia, au usifunikwe? Baadhi yao wasema lazima ufunikwe, na wengine wasema si lazima. Kwa kuwa, kabla ya kushuka amri hii, wanawake wa Kiislamu hawakuwa wakijihifadhi hivyo, walikuwa na wasiwasi wa hilo. Hivyo Mwenyezi Mungu anawadokeza hapa kwamba, kwa kuwa hali yao kabla ya aya hii ilitokaua na kutojua, atawasamehe maana Yeye ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. Lakini wasirudie tena kutoka bila ya kujisitiri kisharia. 131 Muradi wa wanafiki ni wale wanaoficha ukafiri wao na kudhihirisha Uislamu; wenye maradhi nyoyoni mwao ni wale wenye imani dhaifu; na wanaoeneza fitna ni kundi kati ya wanafiki lililokuwa likieneza uvumi dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na waumini. 40

56 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 61. Wamelaaniwa! Popote waonekanapo na ق ت يل ٦١ وا ت ل وا و ق ت kabisa. wakamatwe na kuuliwa خ ذ وا أ ق ف ا ث ن م ي ع ون ني أ م ل Hii ni ada ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika ada ya Mwenyezi Mungu Watu wanakuuliza kuhusu Kiyama. Sema: Ujuzi wake u kwa Mwenyezi Mungu peke Yake, na ni kipi kitakachokujuza Kiyama ni lini? Hwenda Kiyama kikawa ki karibu. 134 Watu hao - yote makundi matatu - walikuwako Madina. Walikuwa na dasturi ya kueneza kila aina ya uvumi dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Kwa mfano, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipokuwa amekwenda vitani, huku nyuma walikuwa wakivumisha kuwa ameuliwa! Au ameshikwa mateka! Hilo lilikuwa likiwaathiri mno wale Waislamu ambao walibaki nyuma ambao, kwa sababu moja au nyengine, hawakwenda vitani. Pia walikijaribu kuwavunja moyo na kuwatisha Waislamu kwa kuwatangazia kuwa kuna jeshi litakuja kuwahujumu, au Madina ilikuwa imehusuriwa na maadui, na kadhalika. Watu hao, katika aya hii, wanaonywa vikali kwamba, kama hawataacha kufanya hivyo, basi adhabu yao wao na wanaowasikiliza itakuwa ni kuuliwa au kutolewa mji. Wala mbinu hii ya kujaribu kuuvunja Uislamu na kumkashifu Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwa kueneza uvumi na uwongo haijakoma hadi hii leo bali, kwa kupata vifaa vya kisasa, imekomaa. Ndiyo hii inayoitwa vita vya kisaikolojia au propaganda. Kwa kutumia vifaa vya kisasa kama magazeti na vitabu, maredio na televisheni na sinema, tepu na video na kaseti zake, kompyuta na kadhalika, wapiiizani wa Uislamu wameweza kueneza sumu yao dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Uislamu kwa jumla, na kuyahozi mabongo hata ya Waislamu wenyewe. Jambo la kuhuzunisha, hata hivyo, ni kuona Waislamu na dola zao, pamoja na utajiri mkubwa walionao, jinsi ambavyo hawakabiliani na hujuma hizo wala hawaonekani kuwa na mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa sumu hiyo haitawaathiri Waislamu na wasio Waislamu ambao wanapenda kuujua Uislamu. 132 Hii ndiyo adhabu ya watu hao; kuuliwa - popote waonekanapo! Wao ni kama kiungo kiovu kinachohatarisha mwili mzima; kisipokatwa, mwili utapotea. 133 Muradi wa ada ya Mwenyezi Mungu hapa ni sharia Yake. Yaani ni sharia ya Mwenyezi Mungu watu waovu kama hao kuuliwa. Wala sharia hiyo haianzi leo. Ilikuwako kwa wale waliopita zamani, iko na sasa, na itaendelea kuwako milele. Wala haitabadilika. 134 Katika aya zilizopita tuliona zile njama zilizokuwa zikipangwa na wanafiki na watu waovu, pamoja na uvumi waliokuwa wakiueneza, dhidi ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) khaswa na Uisiamu kwa jumla. Lengo kubwa la njama hizo liiikuwa ni kuichafua imani ya waumini, khaswa wale waliokuwa dhaifu wayo, au kupanda mbegu za shaka katika nyoyo zao. Moja ya mbinu walizozitumia katika njama zao hizo ni suali hili lililotajwa katika aya hii: Hicho Kiyama kitakuja lini? Kwa vile Bwana Mtume (s.a.w.w.) mara nyingi, khaswa pale walipokikanusha aliyokuwa akiwaeleza, alikiwaonya kuhusu Siku ya Kiyama, ambayo hawalikiiamini, wanafiki walikiliuliza suali hilo ama kwa stihizai au kwa nia ya kutia watu shaka. Hivyo Mwenyezi Mungu anamtuma Bwana Mtume (s.a.w.w.) awajibu kwamba anayejua siku hiyo itakuwa lini ni Mwenyezi Mungu peke Yake. Hakuna yeyote mwengine anayejua - hata Mitume na Malaika pia. 41 ة اهلل د ل سن س ن ة اهلل ف ال ين خ ل و ا م ن ق ب ل و ل ن ت د يل ٦٢ ت ب ا ع ند اهلل ه م ا ع ل م ة ق ل إ ن الساع ل ك انل اس ع ن ي سأ ك ون ق ر يب ا ٦٣ ع ل الساع ة ت د ر يك ل و م ا ي

57 JUZUU YA Hakika Mwenyezi Mungu amewalaani makafiri, 135 na amewaandalia Moto unaowaka kwa nguvu. 65. Watakaa humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru. 66. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtwii Mwenyezi Mungu na tungelimtwii Mtume! Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatwii bwana zetu na wakubwa wetu, nao wakatupoteza njia. 137 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ا ٦٤ ه م سع ري ع د ل ع ن ال ك ف ر ين و أ إ ن اهلل ل ا ٦٥ ص ري ا و ل ن د ون و ل ب دا ل ي ا أ خ ادل ين ف يه طع ن ا اهلل ن ا أ ا ل ت ول ون ي ق ه م ف انل ار ي ق ل ب و جوه ي و م ت ن ا الر س ول ٦٦ و أ طع ا ض ل ون ا ف أ ب اء ن ن ا و ك ت ن ا س اد ط ع ا أ ن ا إ ن ب و ق ال وا ر الس ب يل ٦٧ Hwenda kikawa ki karibu. Kwa hivyo ni lazima tujiandae nacho. Na hii ndiyo siri na hikima kubwa ya Mwenyezi Mungu kutomwachia yeyote asiyekuwa Yeye kujua kitakuwa lini. Lau tungelikuwa tunajua kitakuwa lini, bila shaka tungelikuwa na mfumo mwengine katika maisha yetu na uhai wetu. Hata hivyo, inafaa tukurnbuke kwamba, mbali na hicho Kiyama kikubwa ambapo sote kwa jumla - na kwa wakati mmoja - tutaifariki dunia hii, kila mmoja wetu ana kiyama chake kidogo; nacho ni pale anapokata roho. Na hicho pia hakuna anayekijua kitakuwa lini! Ile kuwa kinaweza kikawa wakati wowote ndiyo maana ya kuwa ki karibu. Mahali pengine katika hii Qur ani (Sura 7:187) Mwenyezi Mungu ameeleza hivi: Wanakuuliza kuhusu Kiyama: lini kitakuwa? Sema: Ujuzi wake uko kwa Mola wangu. Hakuna atakayekidhihirisha kwa wakati wake ila Yeye. Ni kizito katika mbingu na ardhi. Hakitawajia isipokuwa kwa ghafla! Wanakuuiiza kana kwamba wewe una pupa kukijua. Sema: Ujuzi wake u kwa Mwenyezi Mungu. Lakini wengi wa watu hawajui. 135 Kulaaniwa na Mwenyezi Mungu ni kuwekwa kando/mbali na rehema Yake. 136 Watasema maneno hayo kwa majuto. Watatamani siku hiyo lau wangelikuwa wamemtwii Mwenyezi Mungu (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.w.). Lakini ifaeni! Majuto ni mjukuu! Hali hii ya majuto imeelezwa pia katika aya nyengine (Sura 25:27-29): Siku ambayo dhalimu atajiuma mikono yake kwa majuto, aseme: Laiti ningelishika njia ya sawa pamoja na Mtume! Ee ole wangu! Laiti nisingemfanya fulani kuwa rafiki! Kwa hakika alinipoteza nikauacha Ukumbusho baada ya kunijilia; na kweli Shetwani ni khaini kwa mwanaadamu. 137 Siku hiyo ya Kiyama, watakapoiona hiyo adhabu waliyoonywa hapa duniani kuwa itawapata na wakaikanusha, wale makafiri na maasi wengine watasema maneno haya yaliyomo katika aya hii. Muradi wa bwana zetu hapa ni wale maraisi wa nchi; na wakubwa wetu ni wale wanaoziendesha idara za nchi chini ya udhamini wa hao mabwana ambao huzingatiwa kuwa ni washauri na wasaidizi wao. Kana kwamba wanasema: Sisi tuliuweka utwii wa mabwana mahali pa utwii wa Mwenyezi Mungu, na utwii wa wakubwa mahali pa utwii wa Mitume (al-amthal). 42

58 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT 68. Mola wetu! Wape wao adhabu mara ا ٦٨ ب ري ن ا ك ع ه م ل ن ع و ال mbili, 138 na walaani laana kubwa. اب ذ ع ني م ن ال ف ن ا آت ه م ض ع ر ب 69. Enyi mlioamini! Msiwe kama wale waliomtaabisha Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtakasa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye hishima mbele ya Mwenyezi Mungu Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni maneno ya sawa Atawatengenezea amali zenu kuwasamehe dhambi zenu. 141 Na yeyote 138 Kwa nini adhabu mara mbili? ه ف ب أ وس ا م و وا كل ين آذ ن وا ل ت كون ا ال ين آم ه ي ي ا أ ا ٦٩ وا و ك ن ع ند اهلل و ج يه ا ق ال اهلل م م وا ق و ل س د يدا ٧٠ وا اهلل و ق ول ق ن وا ات ا ال ين آم ه ي ي ا أ Moja ni kwa sababu wao wenyewe walikuwa wamepotea. Na ya pili ni kwa sababu waliwapoteza na wengine. Lakini katika Sura 7:38 Mwenyezi Mungu anawajibu watu hao kwamba kila mmoja wao - waliopoteza na waliopotezwa - atapata adhabu mara mbili! Basi ni vipi? Ya waliopoteza wenzi wao, tumeshaona hapo juu kwa nini waadhibiwe mara mbili. Jee, hawa waliopotezwa; kwa nini? Wao wataadhibiwa mara mbili kwa sababu: Mosi: ni kwa sababu ya kujiachilia kupotea. Na pili: ni kwa sababu ya kuwasaidia na kuwaunga mkono madhalimu waliowapoteza. Maana madhalimu peke yao, hata wawe na nguvu vipi, hawawezi kuendelea na upotofu wao. Lazima wapate msaada wa wafuasi wao ndipo upotofu wao ushamiri. Kwa maneno mengine, mkubwa hawezi kuwa mkubwa kama hana wadogo. Kama wote ni wakubwa, yeye atakuwa mkubwa wa nani? 139 Waliomtaabisha Musa, waliokusudiwa hapa, ni wana wa Israeli (Mayahudi). Wao walimsumbua kwa kumsingizia mambo ambayo hakuwa nayo, kama inavyoelezwa katika Biblia: Kutoka 5:20-21, 14:11-12, 16:2-3, 17:3-4; na Hesabu 11:1-5, 14:1-10, 16 (Sura yote), na 20:1-5. Mwenyezi Mungu, katika aya hii, anawaonya Waislamu wasimfanyie Mtume Muhammad (s.a.w.w.) vile Mayahudi walivyomfanyia Mtume Musa (a.s.). Wakifanya hivyo, basi wawe tayari kupatwa na yale yaliyowapata Mayahudi. Wakati mmoja Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa akiwagawanyia watu vitu. Mtu mmoja akasema: Katika ugawanyaji huu, Muhammad hakutaka radhi ya Mwenyezi Mimgu wala Akhera! Bwana Mtume (s.a.w.w.) uso ukamwiva, Akasema: Mwenyezi Mimgu amrehemu Musa. Aliudhiwa zaidi kuliko hivi; akasubiri (Musnad Ahmad, Tirmidhi, na Abuu Daawuud). 140 Makusudio ya maneno ya sawa hapa ni maneno ya haki na ukweli bila ya kuficha kitu, hata kama ni juu ya nafsi yako. Katika Tafsir ya ad-durrul Manthuur ya Imam as-suyuutwi mna Hadith isemayo kuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) halikipanda mimbarini ila alikisoma aya hii na iliyofuatia. 141 Hayo ndiyo matokeo ya ucha-mungu: amali hutengenea, na dhambi husamehewa. و م ن ع م ال ك م و ي غ ف ر ل ك م ذ ن وب ك م ي ص ل ح ل ك م أ ا ٧١ ظ يم ا ع ز ق د ف از ف و ف ي ط ع اهلل و ر سول Pia tiz. Sura 65:5. 43

59 JUZUU YA 22 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT atakayemtwii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, bila shaka amefanikiwa mafanikio makubwa Hakika Sisi tuliikadimisha amana kwa mbingu na ardhi na milima; na vyote hivyo vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini Mwanaadamu akaichukua. Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake, na washirikina wanaume na washirikina ب ال او ات و ال ر ض و ال السم ة ع ان إ ن ا ع ر ضن ا ال م نس ان إ ن ه ا ال ه ا و ح ل ه ق ن م ن ا و أ شف ن ه ن حي م ل ف أ ب ني أ ه ول ٧٢ ا ج وم ك ن ظل ش ك ني م ات و ال ن اف ق م م ن اف ق ني و ال ب اهلل ال ذ ل ع م ن ات ؤ م ؤ م ن ني و ال م ال ش ك ت و ي ت وب اهلل ع و ال م Kwa kweli ucha-mungu ndio nguzo na msingi wa kutengenea ulimi, na ndio chemchemu ya neno la kweli. Na neno la kweli ni moja ya vitenda-kazi vyenye athari katika kutengenea amali, kama ambavyo kutengenea amali ndiyo sababu ya kusamehewa dhambi (Sura 11114). Wanazuoni wa akhlaaq (tabia njema) wanasema: Ulimi ndicho kiungo cha mwili chenye baraka kushinda vyote, na ndicho chombo chenye athari kubwa kuliko vyote, katika utwiifu, uwongofu na usuluhifu. Na wakati huohuo ndicho kiungo chenye hatari kuliko vyote. Hata husemwa kwamba maasia makubwa karibu thalathini hutokana na kiungo kidogo hiki. Bwana Mtume (s.a.w.w.) amesema: Imani ya mja haiwi imara mpaka unyoke moyo wake, na moyo wake haimyoki ila unyoke ulimi wake. (Bihaarul Anwaar). Katika hadith nyengine iliyopokewa kwa Imam as-sajjaad (a.s.) inasema: Ulimi wa mwanaadamu kila siku huvikabili viungo vyake, ukaviuliza: Mmeamkaje? Navyo vikajibu, Vyema, kama utatuacha. Kisha vikaongeza: Halla halla na sisi! Vikamtaradhia na kumwambia: Sisi hupata thawabu kwawe, na huadhibiwa kwawe. (Bihaarul Anwaar). 142 Atafuzu hapa duniani kwa kufanikiwa na kuwa na sera nzuri, na Akhera kwa kunali radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu Zake. 143 Mwenyezi Mungu alipoviumba viumbe Vyake - mbingu, ardhi, milima, Mwanaadamu, na vyenginevyo - alivipa amana viitekeleze. Amana hiyo ilikuwa ni: kila kiumbe kiwe na hiari na uhuru wa kufanya kinalotaka muradi tu kiwe tayari kulipwa kwa mujibu wa vitendo vyake - mema kwa mema, na maovu kwa maovu. Viumbe vyote vikakataa kuichukua amana hiyo - sio kwa jeuri na kiburi kama alivyofanya Iblis (Sura 2:24), bali kwa kuliogopa jukumu lake, kama ilivyoelezwa katika aya hii. Vilipendelea zaidi kutokuwa na hiari hiyo ili vipate kutwii matakwa ya Mwenyezi Mungu tu. Mwanaadamu peke yake, kati ya viumbe vyote, ndiye aliyekubali kuichukua amana hiyo! Tunapoitaamali aya hii tutatambua kwamba viumbe kama mbingu, ardhi na majabali - vilivyotajwa hapa - vina aina ya maarifa ya kiuungu. Humtaja Mwenyezi Mungu na kumtakasa (Sura 17:44), humnyenyekea na kumsujudia (Sura 16:49) isipokuwa kwamba havifanyi hayo kwa hiari bali kwa kuwa na maumbile yavyo na kwa kutenzwa nguvu (Sura 13:15). Kwa ajili hii viumbe hivyo havina ile daraja ya ukamilifu na utukufu iliyofikiwa na Mwanaadamu. Mwanaadamu pekee, kati ya viumbe vyote, ndiye ambaye hana ukomo wa kupanda kwake na kushuka kwake. Ikitegemea anavyoichukua amana hiyo anaweza, kwa kuitekeleza kama anavyotaka Mola wake, akafikia daraja ya muqarrabun (waliokaribishwa kwa Mwenyezi Mungu - Sura 56:11) kama ambavyo anaweza pia, kwa kuikhini, akashuka na kuwa asfala saafiliin (chini ya walio chini -Sura 95:5). 44

60 JUZUU YA 22 wanawake; na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. 144 AL-AHZAAB 33 WAMAN YAQNUT ا ٧٣ ح يم ا ر ور ف و ك ن اهلل غ 144 Matokeo ya Mwanaadamu kukubali kuichukua amana hiyo - ya kuachiwa hiari na uhuru wa kufanya wanalotaka - ni kupatikana miongoni mwao wale ambao watayakataa ya Mwenyezi Mungu, au wale ambao watadhihirisha imani na kuficha ukafiri wao (wanafiki) ambao, katika aya iliyotangulia, ndio wanaoitwa dhalimu wakubwa; au watapatikana wale wanaokataa kumpwekesha Mwenyezi Mungu (washirikina) ambao wameitwa wajinga sana. Kwa kuwa wameamua wenyewe kuwa hivyo, Mwenyezi Mungu atawaadhibu. Ama wale ambao watamtwii Mola wao (waumini); hao Mwenyezi Mungu anawapa matumaini ya kupokelewa toba yao na kusamehewa dhambi zao. Mwenyezi Mungu atujaalie kuwa miongoni mwao; amin. 45

61 KIJALIZO I AHLUL BAYT NI NANI? Mwenyezi Mungu, kama inavyojulikana, ndiye aliyetuumba sisi binadamu na viumbe vyengine vyote. Kwa upande wetu sisi binadamu, baada ya kututengeneza na kutupulizia roho, alitupa viungo masikio, macho na nyoyo vya kuhisia na kudirikia mambo (Sura 32:9). Kisha akatwamrisha tuvitumie. Ndipo ikawa, katika Qur ani Tukufu, popote panapohitajiwa kutumia viungo hivyo, huulizwa: Jee! Hamtafakari (Sura 6:50)? Jee! Hamfahamu (Sura 23:80)? Jee! Hamsikii (Sura 28:71)? Jee! Hamwoni (Sura 51:21)? Na tukaonywa kwamba, kama hatutavitumia viungo hivyo kama ilivyokusudiwa, basi tutakuwa kama wanyama; bali tutakuwa wapotofu zaidi (Sura 7:179)! Hata hivyo, kwa kuwa akili zetu haziko sawa (kila mtu ana yake), na kwa kuwa matumizi yetu ya hivyo viungo vyengine hutafautiana, Mwenyezi Mungu anatwambia kwamba hatutaacha kukhitalifiana kwa sababu hivyo ndivyo alivyotuumba (Sura 11: ). Lakini panapotokea khitilafu yoyote baina yetu, na tukawa tunataka uamuzi wa haki na wa mwisho, basi tuirejeze khitilafu yetu hiyo kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) na kwa Mtume (s.a.w.w.) (Sura 4:59). Kuirejeza khitilafu kwa Mwenyezi Mungu maana yake ni: tuitizame Qur ani Tukufu inavyosema, tuifuate. Kama hatukuupata utatuzi humo, basi tuutafute katika sunna za Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Na hiyo ndiyo maana ya kuirejeza khitilafu yetu kwa Mtume (s.a.w.w.). Maana kazi ya kutufafanulia sisi Qur ani Tukufu aliachiwa yeye (Sura 16:64). Na mara tu tukishajua Mtume (s.a.w.w.) amesemaje, basi ni lazima tumfuate (Sura 59:7). Hapo huwa hatuna tena hiari kabisa (Sura 33:36). Baada ya utangulizi huu mfupi, hebu sasa tutizame tafauti zilizoko kuhusu tafsiri ya neno hili ahlul bayt lililomo katika sura hii tuliyoifasiri katika kitabu hiki (Sura 33:33), pamoja na hujja zinazotolewa na wafasiri wazo, ili tuweze kuamua ni tafsiri ipi kati ya hizo iliyo sahihi kwa mujibu wa misingi ya Sura 4:59 iliyoelezwa hapo juu. Ni watu watano waliotajwa na Mtume (s.a.w.w.)? Tafsiri ya kwanza ni ile inayosema kwamba makusudio ya ahlul bayt waliotajwa katika aya ya 33 ya sura hii ni: Alii na mke wake, Fatma, na watoto wao, Hasan na Husein, pamoja na Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Tafsiri hii ndiyo iliyoelezwa na yeye mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w.w.) katika Hadith zake sahihi na mutawaatir 1 zilizonukuliwa katika vitabu kadha wa kadha vya Tafsir, 2 chini ya aya hii, na vya Hadith. 3 Moja ya Hadith hizo ni ile inayosema kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.), yeye mwenyewe, 1 Hadith mutawaatir ni ambayo imepokewa kwa watu wengi sana kiasi cha kwamba ni muhali wote kukomangana kusema uwongo. 2 K.v. Tafsir Twabari, Durrul Manthuur ya Suyuutwi, Kash-shaaf ya Zamakhshari, Tafsir Ibn Kathiir, Tafsir Qurtubi na nyenginezo. 3 K.v. Sahih Muslim, Sunan Tirmidhi, Musnad ya Ahmad b. Hambal, Mustadrak ya Haakim, Mu jamus Swaghiir ya Twabarani, na vyenginevyo. 46

62 ndiye aliyesema kwamba aya hii iliteremshwa kwa ajili ya watu watano: mimi, Alii, Fatma, Hasan na Husein. Hayo yamo katika Tafsir kadhaa 4 na vitabu kadhaa vya Hadith. 5 Hadith ya pili ni ile iliyopokewa kwa Bibi Ummu Salama, mke wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Yeye amesema kwamba aya hii iliteremshwa nyumbani mwake. Ilipoteremshwa, Mtume (s.a.w.w.) alimwita Alii, Fatma, Hasan, na Husein. Kisha akawafunika guo lake, pamoja na yeye mwenyewe. Halafu akatoa mkono wake na kuulekeza mbinguni huku akisema: Ewe Mola! Hawa ndio ahlul bayt wangu. Basi waondolee uchafu na uwatakase kabisa kabisa. Kusikia na kuona hivi, Bibi Ummu Salama akasema na huku analiinua lile guo kutaka kuingia: Na mimi niko pamoja nanyi, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mtume akambwekura lile guo (kumzuia asiingie) na kumwambia: Wewe umo katika kheri. Hii nayo pia imetajwa katika Tafsir 6 na vitabu mbalimbali vya Hadith. 7 Hadith ya tatu ni ile iliyopokewa kwa Bibi Aisha, mke mwengine wa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Yeye amesimulia kwamba ilipoteremshwa aya hii, Mtume (s.a.w.w.) alijifunika hilo guo lake pamoja na Alii, Fatma, Hasan na Husein. Kisha akaisoma aya hii. Hayo pia yanapatikana katika vitabu mbalimbali. 8 Isitoshe! Imepokewa pia kwamba Mtume (s.a.w.w.), alipokuwa akenda msikitini kuswali alfajiri, alikuwa akipita nyumba ya Bibi Fatma (a.s.) huku akilingana: Swalaa! Swalaa! enyi ahlul bayt! Kisha akisoma aya hii. Hilo, kwa riwaya ya Anas b. Malik, alilifanya kwa miezi sita; na kwa riwaya ya Ibn Abbas, miezi sabaa. 9 Hivyo, kwa mujibu wa Hadith sahihi za Bwana Mtume (s.a.w.w.), ambazo sizo zote tulizozitaja hapa, ahlul bayt waliotajwa katika aya hii, kwa wakati huo ambao Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa bado yungali hai, 10 ni hao watu watano tu: Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Alii b. Abii Twaalib (a.s.), Bibi Fatma (a.s.), Hasan (a.s.), na Husein (a.s.). Ni wake wa Mtume (s.a.w.w.)? Tafsiri ya pili ni ile isemayo kwamba muradi wa ahlul bayt katika aya hii ni: wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). 11 Na hujja za wanaoshikilia tafsiri hiyo ni kwamba: 4 K.v. Tafsirul Khaazin, Tafsir Fakhrur Raazi, Fat hul Qadiir ya Shawkaani, Fat hul Bayaan ya Swaadiq Hasan Khan, na nyenginezo. 5 K.v. Mishkaatul Maswaabiih, Maswaabiihus Sunnah ya Baghawi, na vilivyotajwa Na. 3 hapo juu isipokuwa cha mwisho. 6 K.v. Tafsir Twabari, Tafsir Ibn Kathiir, Durrul Manthuur ya Suyuutwi, Fat hul Qadiir ya Shawkaani, na Fat hul Bayaan ya Swaadiq Hasan Khan. 7 Sunan Tirmidhi, Siratun Nabawiyyah ya Zayn Dahlaan, Dhakhaairul Uqba ya Twabari, Usudul Ghaabah ya Ibn Athir. 8 Fat hul Qadiir ya Shawkaani, Fat hul Bayaan ya Swaadiq Hasan Khan, Sahih Muslim, Mustadrak ya Haakim, Dhakhaairul Uqba ya Twabari, na vyenginevyo. 9 Sunan Tirmidhi, Mustadrak ya Haakim, Musnad ya Ahmad b. Hambal, Majma uz Zawaaid ya Haithami, Kalimatul Gharraa ya Imam Abdulhusein Sharafuddin. 10 Baada ya Mtume (s.a.w.w.) kufariki dunia, na kwa mujibu wa Hadith zake mutawaatir, jumla ya ahlul bayt ni 14 : ni hao watano na 9 wengine katika kizazi cha Imam Husein (a.s.). 11 Tafsiri hii ndiyo inayoshikiliwa sana na wale mashekhe wanaoipinga ile tafsiri ya kwanza, ya kuwa ni watu watano, tuliyokwisha kuieleza hapo juu. 47

63 (i) neno ahlul bayt kwa kawaida hutumiwa kwa maana ya mke au wake ; na hivyo ndivyo lilivyotumiwa, kwa mfano, katika Sura 11:73 na 28:12. (ii) aya hii ya 33 ya sura hii, imekuja baina ya aya ya 27 mpaka ya 34 zinazozungumzia wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Basi vipi aya hiyo, iliyoko katikati ya hizo nyengine, iwe haizungumzii wake wa Mtume (s.a.w.w.)? (iii) kuna Hadith zilizopokewa kwa Ibn Abbas na Urwa b. Zubayr zinazoeleza kwamba muradi wa ahlul bayt katika aya hii ni wake wa Mtume (s.a.w.w.). Na hivyo pia ndivyo alivyosema Ikrima na Muqaatil b. Sulaymaan. Lakini ukizitaamali vizuri hujja hizo utaziona kwamba hazina mashiko kwa sababu zifuatazo: (i) Ni kweli neno ahlul bayt limo katika Sura 11:73 ambayo Kiswahili chake ni: Jee! Unastaajabia amri ya Mwenyezi Mungu? Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka Zake ziko juu yenu, enyi watu wa Nyumba (ya Nabii Ibrahimu)... Na ni kweli neno hilo limo katika Sura 28:12 ambayo Kiswahili chake ni: Na tukamharamishia (Musa) wanyonyeshaji tangu mwanzo. Basi (dadake) akasema: Jee! Niwaonyeshe (nyinyi) watu wa Nyumba watakaowalelea nyinyi (huyu mtoto)...? Lakini si kweli kwamba, katika aya mbili hizo, neno ahlul bayt limekuja kwa maana ya mke au wake tu wa mtu yeyote. Ukweli ni kwamba, katika Sura 11:73, neno hilo limekuja kwa maana ya mke wa Nabii Ibrahimu pamoja na yeye mwenyewe (a.s.) kama inavyoelezwa na wanazuoni wa Tafsir. 12 Na katika Sura 28:12 limekuja kwa maana ya mamake Nabii Musa (a.s.), sio kwa maana ya mke wa babake (Musa) wala Firauni! Lakini hata kama neno hilo, katika hizo aya mbili tulizozitaja hapo juu, lingekuwa limekuja kwa maana ya mke au wake wa mtume yeyote yule, hilo lisingekuwa ni thibitisho kwamba, na katika aya hii ya 33 ya hii sura ya al-ahzaab vilevile, limekusudiwa wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Maana tunapozitaamali aya kadhaa za Qur ani, tunaona kwamba neno fulani linapokuja kwa maana fulani katika aya moja, si lazima lije kwa maana hiyohiyo katika aya nyengine. Kwa mfano neno an-naas (kwa wingi), lililokuja kama mara 240 hivi katika Qur ani Tukufu, kwa kawaida maana yake ni watu. Lakini katika mwanzo wa Sura 3: halikuja kwa maana hiyo, bali kwa maana ya mtu (mmoja)! Na mtu mwenyewe alikiitwa Nuaym b. Mas uud. 14 Yeye ndiye aliyewatisha Waislamu, kama aya inavyosema, kwa kuwambia kwamba watu (yaani makafiri) wamewakusanyikia. Muradi wa neno an-naas hapo, katika aya hiyo, ni mtu mmoja badali ya watu wengi, kama ilivyo dhahiri ya neno lenyewe, kwa sababu ya kujulikana sababu ya kuteremshwa 15 aya hiyo. 12 Tiz. Ahlul Bayt Fil Kitaabi Was Sunnah cha as-sayyid Amir Muhammad al-kaadhwiimi al-qazwiini, uk Tafsiri yake ni: Ambao waliambiwa na watu: Hakika watu wamewakusanyikia nyinyi; basi waogopeni! Hayo yakawazidishia Imani, wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosha, naye ni Mbora wa kutegemewa. 14 Tiz. Kash-Shaaf ya Zamakhshari; Tafsiri ya Jalaleni; Fat hul Qadiir ya Shawkaani, Tafsir Qurtubi, Tafsir Fakhrir Raazi. 15 Aya nyingi za Qur ani ziliteremshwa maalumu kuelezea au kufafanulia tukio maalumu. Hiyo ndiyo inayojulikana kuwa ndiyo sababu ya kuteremshwa (sababun nuzuul) aya hiyo. 48

64 Mfano mwengine ni wa neno nisaa-anaa (wanawake wetu) katika Sura 3: Kwa kawaida neno nisaa (kwa wingi) lina maana ya wake au wanawake. Lakini katika aya hiyo neno hili, ambalo limetajwa mara zisizopungua 59 katika Qur ani Tukufu, halikuja kwa maana hizo bali limekusudiwa mwanamke (mmoja) tu; naye ni Bibi Fatma (a.s.), binti ya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Japokuwa iliposhuka aya hiyo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa tayari anao wake zake, na japokuwa neno hilo limekuja kwa maana ya wake wa Mtume katika aya nyengine (k.m. Sura 33:30 na 32), lakini muradi wa neno hilo katika hiyo Sura 3:61 sio wanawake (kwa wingi), wala wake wa watu fulani, wala wake wa Mtume (s.a.w.w.). Muradi wake ni mwanamke maalumu, naye ni Bibi Fatma (a.s.), kwa sababu hivyo ndivyo alivyotueleza Mtume Muhammad (s.a.w.w.). 17 Kutokana na maelezo mafupi haya, tunaelewa kwamba neno fulani katika Qur ani Tukufu linaweza likaja kwa maana tafauti kabisa na ile ya kawaida ama kwa kutokana na sababu ya kuteremshwa aya hiyo, au kutokana na ufunuo wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) wa aya hiyo. Na hivyo ndivyo tulivyoupata muradi wa neno ahlul bayt katika hiyo aya ya 33 kwamba ni hao watu wane na yeye mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.). Wake zake hawamo! Juu ya hayo, kwa mujibu wa nahau (sarufi) ya Kiarabu, dhamiri ankum iliyomo katika aya hii (ya 33) haitumiki kwa wanawake peke yao. Hutumika kwa wanaume peke yao, au wanaume pamoja na wanawake. Kwa hujja hii kwa hivyo, haiwezekani kuwa aya hii imekusudiwa wake wa Mtume (s.a.w.w.). Kama ingekuwa hivyo, bila shaka ingetumiwa ankunna (dhamiri ya wanawake peke yao) badali ya hiyo ya ankum. (ii) Ni kweli aya ya 33 ya sura hii imekuja baina ya aya ya 27 mpaka ya 34 zinazozungumzia wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Lakini hilo halimaanishi kwamba aya hiyo ni lazima izungumzie lile lililozungumziwa na aya zilizoitangulia aya hiyo (aya ya 27-32) na ile iliyofuatia (aya ya 34). Tunapozitaamali baadhi ya aya za Qur ani Tukufu, tunaona kwamba huwezekana katikati ya aya moja mkawa na kifungu cha maneno kisicholingamana na maneno yaliyokitangulia na yaliyokifuatia. Mfano mzuri wa hilo ni Sura 5:3 isemayo: Mmeharamishiwa nyamafu na damu na nyama ya nguruwe, na kilichochinjwa si kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kilichokufa kwa kusongeka koo, na kilichokufa kwa kupigwa, na kilichokufa kwa kuanguka, na kilichokufa kwa kupigwa pembe (na mwengine), na kilicholiwa na mnyama (kikafa) ila mkiwahi kukichinja kabla hakijafa. Na (pia mmeharamishiwa) kilichochinjwa panapofanyiwa ibada isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu. Na (ni haramu kwenu) kutaka kujua siri kwa kuagua kwa mabao. Hayo yote ni maasi. Leo waliokufuru wamekata tamaa na dini yenu. Basi msiwaogope, bali niogopani Mimi. Leo nimewakamilishia nyinyi dini yenu, na kuwatimizia neema Yangu, na kuwapendelea Uislamu uwe dini yenu. Na mwenye kudharurika kwa njaa, pasi na kulekea kwenye dhambi (akala hivi vilivyoharamishwa), hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu. 16 Tafsiri yake ni: Basi watakaokuhuji katika haya baada ya kukufikilia ujuzi huu wambie: Njooni tuwete watoto wetu na watoto wenu, na wanawake wetu na wanawake wenu, na sisi wenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo. 17 Tiz. Kash-shaaf ya Zamakhshari; Fat hul Qadiir ya Shawkaani; Tafsir Qurtubi, Tafsir Ibn Kathiir, Tafsir Twabari. 49

65 Katika aya hiyo utaona kwamba, katikati ya vifungu vinavyozungumzia vilivyoharamishwa kuliwa, mna kifungu kinachozungumzia kukamilishwa dini (tulichokichapa kwa italiki). Sasa kimaudhui, vinahusiana vipi vifungu hivyo? Hilo linatufahamisha kwamba, katika Qur ani Tukufu, hupatikana aya, au kifungu cha maneno katika aya, kinachozungumzia maudhui tafauti na yale ya aya au vifungu vya aya vilivyokizunguka. Hili ni kwa sababu ya kwamba aya zote za Qur ani zilipangwa hivi na Mtume Muhammad (s.a.w.w.) mwenyewe; na alipozipanga, hakuzipanga kwa mtiririko wa kihistoria. Kwa hivyo mtu anaweza kuziona aya, katika sura moja au kara moja au aya hiyo hiyo moja, ambazo ziliteremshwa nyakati mbalimbali. Zaidi ya hayo, sio kwamba wake wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) hawakutajwa katika Qur ani Tukufu; la! Wametajwa, lakini si kwa jina la ahlul bayt. Mara sabaa wametajwa kwa jina la azwaaj, 18 na mara mbili kwa jina la nisaa an-nabiy. 19 Basi kwa nini, na katika aya hii tunayoijadili, wasitajwe kwa jina mojalo ya hayo mawili khaswa kwa hivi ambavyo, baina ya aya ya 28 na 34 ya sura hii hii ya al-ahzaab, jina la azwaaj limetajwa mara moja (aya ya 28), na jina nisaa an-nabiy limetajwa mara mbili (aya ya 30 na 32)? Hili ni kuonyesha kwamba neno ahlul bayt katika aya ya 33 halina maana ya wake wa Mtume. (iii) Kuhusu Hadith zilizopokewa kwa Ibn Abbas na Urwa b. Zubayr, kwamba muradi wa ahlul bayt katika aya hii ni wake wa Mtume (s.a.w.w.), maelezo yetu ni kama ifuatavyo: Riwaya ya Ibn Abbas imetajwa na Imam al-waahidii katika kitabu chake, Asbaabun Nuzuul; nayo haikubaliki kwa sababu nne: Kwanza: ni kwamba katika sanad 20 ya riwaya hiyo mna watu kama Swalih b. Musa wanaojulikana katika fani ya Hadith, kama matrukiin. 21 Watu kama hao Hadith zao hazishikwi. Katika Miizanul I tidaal ya adh-dhahabii, chini ya harufo ya swad, riwaya za mtu huyo zimeelezwa kuwa ni dhaifo, si kitu, wala haziandikwi Hadith zake, munkar, nyingi ya riwaya anazozisimulia hazifoatwi na yeyote. Pili: riwaya hiyo inapingana na riwaya nyengine ya Ibn Abbas yuyo huyo ambayo ni muttafaqun alayhi, 22 Riwaya hiyo inasema hivi: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) kwamba Mwenyezi Mungu amewagawanya viumbe (Vyake) vigawanyo viwili: akaniweka mimi katika kigawanyo kilicho bora yavyo...kisha akayafanya makabila ni majumba; akaniweka mimi katika bora ya majumba. Ndilo neno Lake (Mwenyezi Mungu) (s.w.t.): Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafo, enyi watu wa Nyumba (ya Mtume), na kuwatakasa kabisa kabisa. Kwa hivyo hatuwezi kuiacha riwaya hii yenye nguvu, tukaishika hiyo isiyotegemeka. Tatu: riwaya hiyo inapingana na zile riwaya tulizozitaja huko nyuma (uk ), ambazo ni mutawaatir, zinazoonyesha kwamba ahlul bayt waliokusudiwa katika aya hii ni wale 18 Katika Sura 33:6, 28, 50, 53, 59 na Sura 66:1 na Sura 33:30 na Sanad ni ile silsila (orodha) ya watu ambao Hadith fulani imepokewa kwao. 21 Matrukiin ni wale wasimulizi wa Hadith wanaotuhumiwa kuwa ni waongo. 22 muttafaqun alayhi ni ile Hadith ambayo Bukhari na Muslim wamekomangana kuwa ni sahihi. 50

66 watu watano watakatifo (akiwamo Bwana Mtume (s.a.w.w.)) wala sio wake zake. Kwa hivyo hatuwezi kuiacha riwaya mutawaatir kwa riwaya dhaifo. Lazima tuikatae dhaifo. Pia tusiisahau ile riwaya ya Ibn Abbas yuyo huyo, tuliyoitaja katika uk. 47 humu, kwamba kwa miezi sabaa Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikipita nyumba ya Bibi Fatma (a.s.) kila alfajiri huku akilingana: Swalaa! Swalaa! enyi ahlul bayt! Kisha akisoma aya hii tunayoijadili. Nne: riwaya hii ni mawquuf 23 hali hizo riwaya zake nyengine ni marfuu. 24 Hivyo hatuwezi kuiacha Hadith marfuu kwa mawquuf. Ama ya Urwa b. Zubayr; nayo pia haikubaliki kwa sababu tatu: Kwanza: riwaya yake, kama ile ya Ibn Abbas hapo juu, ni mawquuf. Kwa hivyo haikubaliki. Pili: Urwa alikijulikana kwamba alikuwa ni adui wa Alii, Fatma, Hasan na Husein (a.s.). Pia akituhumiwa kwa kumvutia fadhila khalati yake, Bibi Aisha. Kwa hivyo riwaya yake juu ya jambo hili haiaminiki wala haitegemeki. Tatu: riwaya hiyo, kama ile ya Ibn Abbas hapo juu, inapingana na zile riwaya mutawaatir zisemazo kwamba ahlul bayt katika aya hii tunayoijadili ni wale watano tuliowataja huko nyuma (uk ). Ama kuhusu Ikrima; huyu maneno yake hayafai kushikwa kwa sababu, kwa kauli za wanazuoni wa Hadith, mtu huyu alikuwa mwongo. Isitoshe; mtu huyu alikuwa na uadui mkubwa na Imam Alii (a.s.) na wanawe, kwa hivyo hatarajiwi kuwapendelea wao kheri. Alikuwa katika khawaarij. 25 Kwa mfano, inasimuliwa na Abdallah b. Haarith kwamba siku moja aliingia nyumbani kwa Alii b. Abdallah b. Abbas, akamkuta Ikrima amefungwa kwa kamba. Akamwambia Alii: Humchi Mwenyezi Mungu wewe? Alii akamjibu: Khabithi huyu anamsingizia babangu uwongo. Angalia anavyoitwa khabithi hapo! Hali kadhalika inasimuliwa na Yaziid b. Zanaad kwamba siku moja aliingia kwa Alii b. Abdallah b. Mas uud akamkuta Ikrima amefungwa kwenye mlango... Akamuuliza: Ni vipi hivi? Alii akamjibu: Huyu anamsingizia babangu uwongo. Haya! Huyo ndiye Ikrima. Anawasingizia maswahaba Ibn Abbas na Abdallah b. Mas uud uwongo! Mtu kama huyo ni wa kuaminiwa anayoyasema? Kuhusu Muqaatil b. Sulaymaan; yeye naye, kama Ikrima, alikuwa adui wa Imam Alii (a.s.), 23 Mawquuf ni ile riwaya ambayo sanad yake huishia kwa swahaba au maswahaba, haiendelei mbele. 24 Marfuu ni ile riwaya ambayo sanad yake huishia kwa Bwana Mtume (s.a.w.w.). 25 Khawaarij ni wale watu waliompinga na kupigana vita na Imam Alii (a.s.) kwa sababu ya kufanyiana suluhu na Muaawiya b. Abii Sufyaan. 51

67 mwongo na jasiri. Pia inajulikana kwamba alikuwa murjiah 26 na mushabbih. 27 Zaidi ya hayo, inavyoelezwa na Ibn Khalikaan katika kitabu chake, Wafayaatul A ayaan. Muqaatil alikuwa akipokea kwa Mayahudi na Manasara ilimu ya Qur ani inayokubaliana na vitabu vyao, na alikuwa mushabbih aliyekimshabihisha Mwenyezi Mimgu na viumbe! Kwa maelezo mafupi haya mbali ya mengi tuliyoyaacha ni muhali kwa mtu yeyote kuyashika maneno ya watu wawili hao. Kwa hivyo tafsiri yao, ya ahlul bayt kuwa ni wake wa Mtume, haikubaliki. Kwa wale wanaojua Kiarabu, wanaotaka kujua zaidi uwongo wa watu wawili hao, na mengine mengi, nawasome hiyo Wafayaatul A ayaan ya Ibn Khalikaan, Miizanul I tidaal ya adh-dhahabii, na Mu jamul Udabaa na vitabu vyengine vya rijaal 28 chini ya majina yao. Watayaona ya kuyaona! Ni walioharamishiwa sadaka? Wengine husema kwamba makusudio ya ahlul bayt katika aya hii ni wale walioharamishiwa sadaka, yaani Banuu Haashim wote. Na ushahidi wao wanaoutoa ni ule wa Hadith iliyopokewa kwa Zayd b. Arqam iliyomo katika Baabu Fadhaaili Alii katika Sahih Muslim (Kwa Kiengereza ni Hadith Na katika uk Vol. IV ). Katika Hadith hiyo, alipoulizwa ni nani ahlul bayt wake? Wake zake? Zayd b. Arqam alijibu: La! Naapa kwa Mwenyezi Mungu! Mwanamke hukaa na mwanamume (kama mke wake) kwa muda fulani; kisha humtaliki, naye akarejea kwa wazazi wake na watu wake. Ahlul bayt ni yeye mwenyewe na jamaa zake (wanaohusiana naye kwa damu) walioharamishiwa sadaka. Hayo ndiyo maelezo ya Zayd b. Arqam. Lakini tunapoitizama hiyo Hadith ya Sahih Muslim tutaona kwamba maana ya ahlul bayt aliyoulizwa Zayd sio ile iliyomo katika aya tunayoijadili, bali ni ile iliyomo katika Hadith ya vizito viwili. 29 Kama angeliulizwa ile iliyomo katika hii aya tunayoijadili bila shaka yoyote angelijibu vilivyo sawa, kama walivyofanya kina Abuu Said al-khudrii, Mujaahid, Oataada na wengineo. Wala asingeliisahau Hadithul Kisaa 30 kama ambavyo asingeliipinga tafsiri ya Bwana Mtume 26 Murjiah ni wale watu wanaofuata madhihabi yanayosema kwamba maadamu mtu anayo Imani, basi hatadhurika kwa dhambi zozote atakazofanya - hata ziwe kubwa vipi; na kwamba maadamu mtu ni kafiri, basi hatanufaika kwa njema zozote atakazofanya - hata ziwe kubwa vipi. Wao husema yoyote anayefanya dhambi kubwa kubwa asihukumiwe kuwa yu kafiri isipokuwa hukumu yake iakhirishwe mpaka kesho Siku ya Kiyama. 27 Mushabbih ni yule anayemfananisha Mwenyezi Mungu na viumbe - kwa sifa au vitendo. 28 Vitabu vya rijaal ni vile vinavyoeleza habari za wapokezi wa Hadith ambazo kwazo mtu huweza kujua yupi kati yao ni wa kutegemeka au la. 29 Hadith hiyo inasema hivi:...enyi Watu! Hakika mimi ni binadamu; nami nataraji (hivi karibuni) kujiwa na mjumbe (malaika wa mauti) wa Mola wangu na kuitika (mwito Wake). Kwa hivyo ninawaachia nyinyi vizito viwili: cha kwanza ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu chenye uwongozi na mwangaza. Basi shikamaneni na Kitabu cha Mwenyezi Mungu...na watu wa Nyumba yangu (ahlu baytii). Ninawakumbusha nyinyi watu wa Nyumba yangu. Ninawakumbusha nyinyi watu wa Nyumba yangu. Ninawakumbusha nyinyi watu wa Nyumba yangu. 30 Hadith hiyo inasema hivi: Aya hii Hakika Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu ahlul bayt, na kuwatakasa kabisa kabisa ilishuka katika nyumba ya Ummu Salama. Mtume (s.a.w.w.) akamwita Fatma, Hasan na Husein; akawafunika guo. Na Alii, akiwa nyuma ya mgongo wake, pia alimfunika lile guo. Kisha akasema: Hawa ni ahlu baytii (watu wa Nyumba yangu); basi uwaondolee uchafu na uwatakase kabisa kabisa. Ummu Salama akasema: Na mimi ni pamoja nao, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! (Mtume) akajibu: Wewe kaa hapo hapo ulipo. Wewe ni kheri kwangu. 52

68 (s.a.w.w.) 31 tuliyoiona mwanzo wa maelezo haya (uk. 46). Vyovyote viwavyo, ni muhimu tuelewe kwamba hii Hadith ya Zayd b. Arqam, iliyonukuliwa katika Sahih Muslim, iko nje ya maudhui yetu. Kwa hivyo ushahidi wake hausimami. Pili: hata kama tutakubali kwamba aliyoyasema Zayd katika Hadith hiyo ni tafsiri ya aya tunayoijadili, bila shaka hiyo itakuwa ni tafsiri yake kwa maoni yake binafsi. Si tafsiri aliyoinukuu kutoka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Na kwa kuwa tafsiri hiyo inapingana na ile ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) tuliyokwisha kuiona hapo juu, bila shaka hatuwezi kuikubali. Jee! Tuache la Mtume, tushike lisilo la Mtume?! Funzo kubwa la aya hii Katika aya hii (ya 33 ya sura hii), neno tulilolifasiri kwa uchafu ni rijs. Neno hili, katika Qur ani Tukufu, limetumiwa mara 10 kuelezea vitu au mambo mbalimbali. Kwa mfano, katika Sura 5:90 pombe, kamari, kuabudu masanamu na kupiga ramli vimeitwa rijs. Katika Sura 6:145, nyamafu au damu inayomwagika au nyama ya nguruwe pia imeitwa rijs. Hali kadhalika, katika Sura 22:30 masanamu na neno la uwongo pia limeitwa hivyo. Katika Sura 9:95 na 125, neno hilo limetumiwa kuelezea unafiki na wanafiki, kama ambavyo katika Sura 10:100 limetumiwa kuelezea ukafiri/makafiri. Neno hili pia limetumiwa kwa maana ya adhabu ya Mwenyezi Mungu katika Sura 6:125 na Sura 7:71. Kwa ajili ya matumizi ya neno hilo kuelezea vitu, hali ya vitendo mbalimbali ndipo mabingwa wa lugha ya Kiarabu wakalifasiri neno hilo kuwa ni uchafu 32 au uchafu wowote. Pia hutumiwa kuelezea la haramu, kitendo kiovu, adhabu, laana, ukafiri...na kitendo chochote kichafu. 33 Kwa hivyo tunaposoma katika aya hii kwamba Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea rijs watu wa Nyumba ya Mtume (Ahlul bayt) (s.a.w.w.), maana yake ni kwamba anataka kuwaondolea kila aina ya uchafu uliotajwa hapo juu na ulio kama huo, ambao haukutajwa. Kwa maneno mengine, Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea kila la dhambi, awafanye watakatifu. Lakini hayo matakwa yaliyotajwa katika aya hii, ambayo Mwenyezi Mungu anawatakia ahlul bayt, ni yapi? Kujibu suala hili, itatubidi tuelewe aina zilizoko za matakwa ya Mwenyezi Mungu, ndipo tujue hii iliyotajwa katika aya hii ni ipi. Matakwa ya Mwenyezi Mungu yako aina mbili. Moja inaitwa iraadah tashrii iyyah (matakwa ya kisharia); na nyengine iraadah tak-wiiniyyah (matakwa ya kimaumbile). Muradi wa matakwa ya kisharia ni zile amri za Mwenyezi Mungu na makatazo Yake. Kwa mfano, Mwenyezi Mungu anataka sisi tuswali, tufunge, tuhiji, tule vya halali, tuseme kweli, na kadhalika; na anatukataza kuzini, kuiba, kusema uwongo, kulewa, na kadhalika. Haya ndio matakwa ya kisharia ambayo, ukiyataamali, utayaona yana fungamano na vitendo vyetu sisi binadamu, sio vitendo vya Mwenyezi Mungu (s.w.t.). Yaani hiari ni yetu: kuyafuata matakwa hayo au kuyakataa. Lakini vyovyote vile tutakavyoamua, havitamdhuru Mwenyezi Mungu chochote; wala hayatayatia ila matakwa Yake. 31 Kuwa ni hao watu wane pamoja na mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.). 32 Pia tizama tarjuma ya neno hilo katika Tafsir ya Sheikh Abdullah Saleh al-farsy na ya Sheikh Alii Muhsin al-barwani. 33 Tiz, Tafsir Twabari katika maelezo ya aya hiyo. 53

69 Ama matakwa ya kimaumbile ; haya ni yale yenye fungamano na Mwenyezi Mungu: ya kutaka kuleta (kuumba) kitu na kukipa umbo lake. Matakwa ya aina hiyo kabisa hayapitwi na lile lililokusudiwa isipokuwa huwa vilevile anavyotaka Mwenyewe Mwenyezi Mungu; kama inavyoelezwa katika Sura 36:82 kwamba: Hakika amri Yake, anapotaka jambo, ni kuliambia: Kuwa likawa. Sasa, baada ya kuzielewa aina za matakwa ya Mwenyezi Mungu hapo juu, ni wazi kwamba haiwezekani kuwa matakwa aliyowatakia ahlul bayt katika aya hii, ni yale ya kisharia. Na hilo ni kwa sababu zifuatazo: Kwanza ni kwamba, kwa kawaida, matakwa ya kisharia hayawahusu ahlul bayt peke yao, bali huwahusu Waislamu wote. Kwa mfano, amri ya Mwenyezi Mungu ya kuswali na kuhiji, au kutozini na kutoiba, haiwahusu ahlul bayt peke yao bali ni kwa Waislamu wote. Pili ni kwamba matakwa hayo sio kuwa hayaowani na dhahiri ya aya hii tu bali, kwa vyovyote vile, hayaowani hata na zile Hadith tulizotangulia kuzitaja humu. Maana tunapozitizama Hadith hizo kwa makini, tunaziona kwamba zinazungumzia fadhila kubwa na hiba maalumu inayowahusu ahlul bayt peke yao. Tatu ni kwamba uchafu uliotajwa katika aya hii sio ule wa dhahiri tu, bali ni ishara ya machafu yote ya kiroho (ya batini). Kwa hivyo sio uchafu wa shirki, ukafiri na vitendo visivyoambatana na murua, na mfano wa hayo tu, bali ni uchafu wa dhambi zote, maasia yote na maovu yote ya kiimani, ya kiakhlaqi na ya kimatendo. 34 Kwa hivyo, ni lazima yawe matakwa hayo ni ya kimaumbile. Na hili ni kwa sababu zifuatazo: Kwanza ni kwamba aya hii imeanza kwa neno innamaa ambalo, katika nahau (sarufi) ya Kiarabu, hujulikana kama adaatu haswrin (chombo cha kuzingira). Neno hili, linapotumiwa katika sentensi, hulihakikisha lililothubutu baada yake na kulikataa ambalo halikuthubutu. Kwa mfano, unaposema kwa Kiarabu: Innamaa laka indii shilnun (Hakika, yako wewe ni shilingi kwangu) au innamaa fid daari Zaydun (Hakika aliyeko nyumbani ni Zayd) maana yake huwa ni: Huna kwangu mimi isipokuwa shilingi tu; au: Hamna yeyote nyumbani isipokuwa Zayd. Ndipo ikawa wafasiri wetu wa jadi wa Kiswahili, kwa sababu ya kutotaka kuikhini maana ya neno hili, hulifasiri kwa maneno: hakika, si jambo jengine. Kwa hivyo, kwa kulitumia neno innamaa mwanzo wa aya, Mwenyezi Mungu anatufahamisha kwamba yanayofuatia neno hilo ni yale anayowatakia watu maalumu; sio wote. Pili: hilo la kuwakusudia watu maalumu limethubutu kwa kuwataja kwa jina khaswakhaswa: yaani ahlul bayt. Tatu: limethubutu tena kwa kukokoteza kwamba analolitaka ni kuwaondolea nyinyi (mliotajwa humu, yaani ahlul bayt) na kuwatakasa... Nne: neno rijs katika aya hii limeunganishwa na al likiwa al-rijsu. Sasa, kwa mujibu wa nahau ya Kiarabu, hiyo huitwa laamul jinsi (lamu ya jinsi) ambayo, inapounganishwa na jina 34 Tiz. al-amthal ya Sheikh Makaarim ash-shiiraazii, Jz. 13, uk

70 (noun) lolote, humaanisha jinsi yoyote ya jina hilo. Hivyo, katika aya hii, Mwenyezi Mungu anasema kwamba anataka kuwaondolea ahlul bayt (sio watu wote) kila aina ya uchafu, au uchafu wowote... Kwa hujja nne tulizozitaja hapo juu, tumeona kwamba aliyoyataka Mwenyezi Mungu katika aya hii hakuwatakia watu wote. Kwa hivyo matakwa Yake humu hayawezi yakawa ni ya kisharia, maana hayo ndiyo anayowatakia watu wote k.v. kuswali, kufunga, na kadhalika. Matakwa aliyoyataka katika aya hii ni ya watu maalumu aliowaainia ahlul bayt; na hata matakwa yenyewe pia ni maalumu kuwaondolea aina zote za uchafu: ambayo si daraja wanayoipata watu wote. Kwa hivyo matakwa haya ni lazima yawe ni ya kimaumbile. Inaposemwa hivi baadhi ya watu huelewa vibaya: kwamba ahlul bayt hawawezi kufanya maovu wala madhambi! Hivyo sivyo kabisa. Lilivyo ndivyo ni kwamba wanaweza kufanya hayo maovu au madhambi lakini, kwa daraja waliyonayo, hawafanyi. Pengine hili tutalielewa vizuri kwa mifano miwili mitatu hii. Mfano wa kwanza ni wa daktari; yeye akitaka kunywa maji yenye vidudu vya maradhi anaweza. Lakini hanywi. Kwa nini? Kwa sababu ya yakini aliyonayo, inayotokana na ujuzi wake, ya kupata madhara yanayoweza kuhatarisha maisha yake. Pili: mtu yeyote mwenye akili yake timamu anaweza kubwakia kaa la moto, akitaka, maana anayo hiari hiyo. Lakini habwakii. Kwa nini? Kwa sababu ya yakini aliyonayo, inayotokana na akili yake kuwa kamili (sio punguani), ya kuweza kuuunguza mdomo wake na kupoteza maisha yake. Basi na vivyo hivyo ndivyo walivyo ahlul bayt. Wao, kama binadamu wote, wanaweza kufanya dhambi lau watajiamulia kufanya hivyo, kwa sababu wanayo hiari ya kufanya hivyo. Lakini hawafanyi. Kwa nini? Kwa sababu ya kilele cha yakini walichokifikia, kinachotokana na ujuzi wao mkubwa ambao binadamu wengine hawana, cha kujua matokeo mabaya ya kufanya madhambi au maovu yoyote. Kama vile inavyosemwa kwa mawalii na wacha-mungu wengine, kuwa hasanaatul abraar sayyiaatul muqarrabiin (mema ya watu wema ni maovu ya wenye kukaribishwa), 35 basi kwa ahlul bayt ni zaidi. Hili la ahlul bayt kuwa hawafanyi dhambi wala kosa si uzushi. Ni ukweli ambao u wazi mno tunapozitaamali baadhi ya Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama ile ya vizito viwili na ya safina ya Nuhu miongoni mwa nyingi. Katika Hadith ya vizito viwili, 36 Bwana Mtume (s.a.w.w.) anatuhakikishia kwamba hatuwezi kupotea baada yake kama tutavifuata vitu viwili: Kitabu cha Mwenyezi Mungu (Qur ani Tukufu) na ahlul bayt. Na kwamba vitu viwili hivi havitatengana mpaka kesho Akhera. Tunapotaamali Hadith hii tutaona kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) ameiweka Qur ani Tukufu sambamba na ahlul bayt. Ili tuongoke, ni lazima tushikamane na vyote viwili; 35 Haya ni maneno yanayopigiwa mfano wacha-mungu ambao, kwa kawaida hujiepusha na mambo ambayo, japokuwa kwa watu wengine huwa si dhambi wala kosa, kwao wao - kwa kile kiwango walichofikia cha ucha-mungu wao - huona ni dhambi au kosa! Kwa hivyo huamua kutoyafanya. 36 Tiz. kidokezo Na. 29 hapo juu. 55

71 kushikamana na kimoja, na kukiacha chenginejhaitatufaa kitu kwa sababu vyoo vyenyewe havitaachana mpaka kesho Akhera. Sasa, kama ambavyo Qur ani huwaongoza watu kwenye yale yaliyonyoka, yasiyo na kombo (Sura 17:9); na kama vile ambavyo haina la batili (Sura 41:42); na kama vile ambavyo imehifadhiwa na kila aina ya kosa na ila (Sura 15:9), ndivyo vivyo hivyo walivyo ahlul bayt. Kama sio hivyo, basi pana maana gani ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuviweka sambamba? Kama hivyo ndivyo, basi vipi Qur ani itakuwa na sifa hizo na wao wawe, kinyume na Qur ani, wanafanya dhambi na makosa? Hivi kweli watu wanaweza kutopotea, kama alivyotuahidi Bwana Mtume (s.a.w.w.) katika Hadith hii, kwa kuwafuata watu wanaofanya madhambi au makosa?! Katika Hadith ya safina ya Nuhu, 37 Bwana Mtume (s.a.w.w.) amewafananisha ahlul bayt na ile safina ya Nabii Nuhu (Sura 11:36-48). Hivyo ni kusema kwamba, kama vile ambavyo wale waliomfuata Nabii Nuhu (a.s.) waliokoka kwa kuipanda safina yake, ndivyo vivyo hivyo watakavyookoka wale watakaowafuata ahlul bayt. Na kama ambavyo wale waliomwasi Nabii Nuhu (a.s.) (akiwamo mtoto wake) walighariki baharini, ndivyo vivyo hivyo watakavyoghariki wale watakaowaasi ahlul bayt. Tafauti ya pekee ni kwamba wale wa Nabii Nuhu (a.s.) walighariki baharini, hali hawa wanaowaasi ahlul bayt wataghariki Motoni! Ikiwa ni hivyo basi, jee inaingia akilini kwamba wanaoasi (wanaofanya madhambi) watagharikishwa (watatiwa Motoni) kwa kuwaasi wanaoasi? Bila shaka, la! Ndiyo tukasema kwamba moja ya sifa za ahlul bayt ni kwamba hawafanyi dhambi wala hawakosi. Kama si hivyo, amri ya kuwafuata wao itawapa vipi wafuasi wao utulivu wa moyo kwamba wataokoka na adhabu ya Mwenyezi Mungu? Juu ya hayo Bwana Mtume (s.a.w.w.), katika kutuhimiza tushikamane na ahlul bayt, katika riwaya ya Twabarani, 38 ametuonya: Basi msiwatangulie, mtaangamia; wala msibaki nyuma nao, pia mtaangamia. Wala msiwafunze, maana wao wanajua zaidi. Yaani baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.), tusijiweke wala tusimweke yeyote mbele ya ahlul bayt, wala tusiache kuyafuata ya ahlul bayt tukafuata ya wowote wasiokuwa wao. Maana hakuna yeyote anayejua zaidi yao. Kwa kumalizia makala haya, hebu tujiulize: Jee! Sifa hizi walizopawa ahlul bayt, kama tulivyoziona katika Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.) tulizozitaja hapo juu, kweli wanazo wake zake? Au wanazo kila mtu katika Banii Haashim? Au wanazo watu maalumu? Bila shaka wanazo watu maalumu, kama alivyotufahamisha yeye mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Na hao ndio ahlul bayt. 37 Hadith hiyo inasema hivi: Mfano wa watu wa nyumbani kwangu (ahlu baytii) ni mfano wa safina ya Nuhu. Aliyeipanda aliokoka, na aliyebaki nyuma (asiipande), alighariki. 38 Riwaya hiyo imetajwa katika vitabu k.w.k., kama vile Durrul Manthuur ya Suyuutwi, Majma uz Zawaaid, Kanzul Ummaal, Usudul Ghaaba, na vyenginevyo. 56

72 KIJALIZO II MUHAMMAD: MTUME WA MWISHO Jee! Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho? Majibu ni; Ndiyo! Hivi ndivyo wanavyoamini Waislamu wote wa zama zote na madhihabi yote. Kwao wao, yeyote anayeamini kinyume cha hivyo huwa ni kafiri; si Mwislamu. Lakini kuna wanaoamini kwamba Muhammad (s.a.w.w.) si Mtume wa mwisho! Kwao wao inawezekana kuja, na kweli ameshakuja, mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Hawa wanajulikana kama Makadiani na Mabahai. Makadiani wanaamini kwamba Mirza Ghulam Ahmad ndiye mtume huyo. Yeye alizaliwa mahali paitwapo Qadian huko Bara Hindi katika mwaka 1839 au 1840 B.K. Akafariki dunia katika mwaka 1908 B.K. Mabahai, kwa upande wao, wanaamini kwamba Mirza Alii Muhammad Shirazi ndiye mwakilishi wa kikwelikweli wa mitume wote waliotangulia. 1 Yeye alizaliwa mji uitwao Shiraz huko Iran katika mwaka 1820 B.K. Akahukumiwa kunyongwa, na kunyongwa 2 mjini Tabriz, hukohuko Iran, katika mwaka 1850 B.K. Katika kijalizo hiki, hata hivyo, hatutashughulika na imani ya Mabahai kwa sababu wao, mpaka dakika hii, hawajajitangaza mno. Zaidi tutashughulika na imani ya Makadiani ambao wana historia ndefu zaidi huku Afrika ya Mashariki na ambao, kwa kiasi kikubwa, wamezieneza fikra zao kwa maandishi, khaswakhaswa kwa kuichapisha tafsiri yao ya Kiswahili ya Qur ani Tukufu katika mwaka 1953 B.K. Kwanza tutatoa zile hujja ambazo Waislamu huzitegemea kuthubutishia kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho. Kama Mwenyezi Mungu anavyotaka (Sura 4:59), tutazitoa hujja hizo katika Qur ani Tukufu na Hadith za Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Pia tutatoa hujja kwa maneno ya maimamu (a.s.), maswahaba (r.a.), wanazuoni wa karne mbalimbali, makamusi ya Kiarabu, na hata kwa maneno ya Mirza Ghulam Ahmad Qadiani mwenyewe! Mwisho kabisa tutazijibu moja moja zile hujja ambazo Makadiani wamezitoa, chini ya maelezo ya Sura 33:40 katika tafsiri yao ya Kiswahili ya Qur ani Tukufu, kutilia nguvu imani yao. Lini Mtume huhitajiwa Lakini kabla ya kufanya hivyo, ni muhimu tuelewe lini Mtume huhitajiwa. Na hilo ni baada ya kutambua kwamba utume si kitu kipatikanacho kwa kukiomba au kukifanyia kazi. Ni 1 Hiyo ni moja tu ya itikadi zao. Zaidi ya hilo wanaamini kwamba Uyahudi, Ukristo na Uislamu - zote hizo zinakutana katika Ubahai, na kwamba hazina hitilafu baina yao. Pia wanaamini kwamba Mwenyezi Mungu ameingia ndani ya huyo kiongozi wao, na yeye ameingia ndani ya Mwenyezi Mungu; na itikadi nyingi nyengine zisizokuwa za Kiislamu. 2 Aliuliwa kwa sababu aliritadi. Japokuwa baadaye alitubu, baada ya kushindwa katika mjadala na wanazuoni huko Tabriz, toba yake haikukubaliwa na wanazuoni hao. Waliishuku. 57

73 cheo ambacho Mwenyezi Mungu, Yeye Mwenyewe, humtunukia anayemtaka (Sura 6:124 na 28:68). Tunapoisoma Qur ani Tukufu, na kujaribu kutafuta ni wakati gani khaswa ambapo Mwenyezi Mungu aliona haja ya kutuma Mitume Yake, tutaona kwamba ni nyakati nne: 1. Ni wakati ambapo watu huwa hawajapatapo kupelekewa mtume, wala kufikiwa na ujumbe wa mtume aliyepelekwa kwa watu wengine. 2. Ni wakati ambapo mafunzo ya mtume aliyetangulia huwa yameshasahauliwa, au yamepotolewa na kuharibiwa, kiasi cha kwamba haiwezekani tena kuyajua au kuyatendea kazi katika maisha yetu ya kawaida. 3. Ni wakati ambapo watu huwa pengine hawakuupata ujumbe na uwongozi kamili kwa mtume aliyetangulia; kwa hivyo huwa panahitajiwa mitume zaidi kuukamilisha ujumbe na uwongozi huo. 4. Ni wakati ambapo mtume mmoja huwa anahitajia msaada wa mtume mwengine katika kuutekeleza ujumbe wake. Hizo ndizo nyakati ambapo huwako haja ya kuletwa mtume/mitume. Lakini tunapoisoma Qur ani kwa makini tutaona kwamba, baada ya kuletwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), nyakati/hali hizo haziko. Hebu tuitizame Qur ani inavyosema. Ushahidi wa Qur ani Tukufu Kwa ushahidi wa aya za Qur ani ambazo tutazidondoa hapa chini, hali zote nne zilizotajwa hapo juu, hazisimami. Kwa hivyo hapana haja ya kuja mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwanza tayari sisi tulioko huku Afrika ya Mashariki, na watu wengine wote duniani, tunaye mtume wetu; naye ni Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Yeye, japokuwa alikuwa ni Mwarabu, ametumwa kwetu sote Waarabu na tusio Waarabu. Hivyo ndivyo inavyotueleza Qur ani Tukufu katika Sura 7:158; 21:107; 25:1 na 34:28. Hilo, hata wao Makadiani wanalikubali. Kwa mfano, katika maelezo yao ya Sura 7:158 (ambayo kwa hisabu yao ni Sura 7:159) wameandika hivi: Aya hii inaonyesha madai ya namna ya pekee ambayo hajapata kuyatamka Nabii ye yote kabla ya Mtume s.a.w. Hapa Mtume s.a.w. anaambiwa atangaze kuwa yeye ni Mtume kwa watu wote wa duniani. Wala Mtume Muhammad (s.a.w.w.) hakutumwa kwa watu wote wa duniani wa zama zake tu, bali wa zama zote mpaka Siku ya Kiyama. Hilo li wazi tunapoisoma Qur ani Tukufu (Sura 62:3) na tunapoikumbuka Khutba ya Mwisho ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) pale alipowambia maswahaba waliokimsikiliza: Yule aliyepo (hapa) naaufikishe (ujumbe huu) kwa ambaye hayupo. Kwa hivyo kwa kuwa tayari sisi tunaye mtume wetu, hatuna haja ya mtume mwengine, isipokuwa labda kama ujumbe aliotuletea umesahauliwa, au umepotolewa na kuharibiwa (tiz. hali na. 2 hapo juu). Lakini hilo nalo, alhamdulillahi, halipo kama ushahidi wa pili wa Qur ani unavyotubainishia: 58

74 Pili ni kwamba ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) haujasahauliwa, wala haujapotolewa wala kuharibiwa. Ukweli ni kwamba, tunapoisoma Qur ani (Sura 56:77-78; 85:21-22; 15:9 na 41:42), tunaona jinsi Mwenyezi Mungu alivyochukua ahadi ya kuuhifadhi ujumbe huo na ila zote hizo hifadhi ambayo hata wao Makadiani wanaikiri. Kwa mfano, katika maelezo ya Sura 56:77-78 (ambazo katika msahafu wao ni aya 78-79) Makadiani wamesema hivi: Aya hizi zimeeleza sifa tatu za Kurani:...(2) Mafundisho ya Kurani yatahifadhiwa na yatadumu bila kubadilika... Na chini ya maelezo yao ya Sura 41:42 (ambayo kwa msahafu wao ni aya ya 43) wameandika hivi: Dunia na iendelee namna gani katika science na maarifa haitaweza kubatilisha fundisho lolote la Kurani kuwa ni sahihi. Na majira yapinduke na yageuke namna gani haitawezekana kubadilisha maneno ya Kurani kwa maneno yoyote mengineyo. Sura hii imeanza na sifa ya Mwenyezi Mungu Hafiidh (Mhifadhi) na hapa imeonyeshwa ya kuwa Kurani imehifadhiwa katika kila hali. Mwisho, chini ya maelezo yao ya Sura 15:9 (ambayo kwao wao ni aya ya 10) wameandika: Ahadi ya kuihifadhi Kurani imetimia barabara, na hata kama kusiwe na dalili nyingine, hii tu inatosha kuhakikisha kuwa Kitabu hiki kimetoka kwa Mwenyezi Mungu. Kutobadilika kwa Kurani toka imeteremshwa kwa Mtume s.a.w. ni jambo linalokubaliwa hata na waipinzao dini ya Kiislamu... Lakini Kurani Takatifu ni kitabu kilichohifadhiwa kabisa, kisicho mageuzi, mazidisho wala mapunguzi, kama wanavyokiri hata maadui wa Uislamu. Na ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kuwa Kurani italindwa imethibitika. Kama ujumbe wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) umehifadhiwa na Mwenyezi Mungu jinsi hiyo iliyoelezwa na Qur ani Tukufu na kukiriwa hata na Makadiani wao wenyewe, basi huyo mtume atakayekuja baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) atatuletea ujumbe gani mwengine utakaoshinda ule wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.)? Bila shaka hawezi, ila kama tutadai kwamba japokuwa ujumbe huo kweli umehifadhiwa, lakini haukukamilika! Kwa hivyo pana haja ya kuja mtume mwengine kuukamilisha (tiz. hali na. 3 hapo juu). Na hilo pia halikubaliki, kama ushahidi wa tatu wa Qur ani unavyotuekea wazi: Tatu ni kwamba Mwenyezi Mungu ametuhakikishia kwamba ujumbe huu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) umekamilika. Hivyo ndivyo tunavyosoma katika Qur ani Tukufu (Sura 5:3):... Leo nimewakamilishia nyinyi dini yenu, na nimewatimizia neema Yangu na nimewapendelea Uislamu uwe dini yenu... Katika maelezo yao ya aya hii (ambayo kwa hisabu yao ni aya ya 4) katika ukurasa 198 wa tafsiri yao, Makadiani wamesema hivi: Tangazo hili la Mwenyezi Mungu ni lenye maana sana. Kurani ni Sheria ya kwanza na ya mwisho inayodai kuwa kamilifu. Vitabu vya zamani havingeweza kusema hayo kwa kuwa vilikusudiwa kwa mataifa fulani na nyakati maalumu. Taureti na Injili vilikuwa na nuru na mwongozo (Sura 5:35, 47), lakini vikachanganywa 59

75 na maneno ya watu, vikatanguliwa na Kurani. Injili yenyewe inaahidi kufika kwa mtume mwingine ambaye atawaongoza watu kwenye haki yote (Yohana 16:12-13). Sasa, kama Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ametumwa kuja kuikamilisha dini hii; na kama yeye ndiye ambaye atawaongoza watu kwenye haki yote, kama ilivyonukuliwa Injili hapo juu na kuthubutishwa na Qur ani Tukufu (Sura 17:81), basi huyo mtume atakayekuja baada yake atatuletea ujumbe gani au haki ipi nyengine? Jee! Baada ya ujumbe uliokwisha kamilishwa, pana nafasi ya ujumbe mwengine? Na jee! Baada ya haki yote kutufikia, huyo mtume mpya atatuletea haki ipi nyengine? Labda hao wanaodai kwamba inawezekana kuja mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) waseme kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alihitajia msaada wa mtume mwengine katika kutekeleza ujumbe wake (tiz. hali na. 4 hapo juu), kama Nabii Musa (a.s.) alivyoomba asaidiwe na Nabii Harun (a.s.)! Na hilo linatuleta kwenye ushahidi wetu wane: Nne ni kwamba ni kweli kwamba Nabii Musa (a.s.) aliomba asaidiwe na Mwenyezi Mungu kwa kupelekewa Nabii Harun (a.s.). Hilo tunalisoma katika Qur ani Tukufii (Sura 20:29-34; 26:12-13 na 28:34). Lakini tunapoisoma Qur ani hiyohiyo, hatuoni mahali popote ambapo Mtume Muhammad (s.a.w.w.) aliomba msaada kama huo. Kama pako, basi ni wapi? Sura gani na aya ya ngapi? Pili: tukumbuke kwamba Nabii Musa (a.s.) aliomba msaada huo alipokuwa angali hai. Baada ya yeye kufa, msaada huo usingelikuwa na maana. Hali kadhalika, na Muhammad naye; kama alihitajiamsaada kama huo, Mwenyezi Mungu angelimpatia wakati wa uhai wake. Asingelingojea mpaka baada ya miaka 1300-na; khaswa kwa vile ambavyo, katika karne za mwanzo mwanzo baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kutawafu, kulitokea mambo mabaya sana na machafu sana katika historia ya Uislamu. Tatu: ili kututhubutishia kwamba hapatatokea tena haja ya mtume mwengine baada yake yeye, Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alimwambia Imam Alii b. Abii Twaalib (a.s.) katika Hadith ijulikanayo kama Hadithul manzilah: Wewe kwangu mimi una cheo cha Harun kwa Musa isipokuwa kwamba hakuna mtume baada yangu. Kwa maneno haya Bwana Mtume (s.a.w.w.) alimhakikishia Imam Alii (a.s.) kwamba alikuwa ni msaada wake kama Harun (a.s.) alivyokuwa msaada wa Musa (a.s.). Tafauti yao ni kwamba Harun (a.s.) alikuwa ni mtume hali Alii (a.s.) hakuwa mtume. Kwa nini? Kwa sababu laa nabiyya ba dii (hakuna mtume baada yangu). Kwa maneno mengine: lau ingewezekana kuwako mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), angelikuwa Imam Alii (a.s.). Hadith hii ni mutawaatir. Inapatikana katika vitabu vikubwa vikubwa k.v. Sahih Bukhari, Sunan Ibni Maajah, Musnad Ahmad, Mustadrak ya Haakim, al-iswaabah ya Ibn Hajar, na vingi vyenginevyo. Zaidi ya hayo Kwa hujja tulizozitoa hapo juu, ninatumai kwamba msomaji wetu atabainikiwa kwamba ni 60

76 muhali kuja mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Hata hivyo tumebakiwa na hujja nyengine mbili za Qur ani Tukufu ambazo bora tuzijadili kabla ya kutizama ushahidi wa Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hujja hizo ni: Tunapoisoma Qur ani kwa uangalifu, tunaona kwamba Mwenyezi Mungu anapozungumzia lazima ya kuamini mitume, hutaja ile lazima ya kuamini mitume waliotumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) (min qablika), sio baada yake (min ba dika). Tizama kwa mfano, Sura 4:60; 12:109; 13:38; 30:47; 39:65; 40:78; 42:3 na nyengine kama hizo. Hili ni kuonyesha kwamba hakuna mtume atakayekuja baada yake. Hata hivyo, ili kuwazongazonga watu kuhusu jambo hili, na ili kupata nafasi ya kumpenyezea mtume wao, Makadiani wameifasiri Sura 2:4 (ambayo kwao wao ni 2:5) katika Tafsir yao hivi: Na ambao wanaamini yaliyoteremshwa kwako, na yaliyoteremshwa kabla yako, nao wana yakini na yale yatakayokuja baadaye. Hapo, neno la Kiarabu wabil aakhirati katika aya hiyo, wao wamelifasiri kwa na yale yatakayokuja baadaye badali ya kulifasiri kwa na Akhera, kama wanavyofanya wafasiri wote wasiokuwa wao. Lakini kwa kweli tafsiri hiyo, tukiitaamali vizuri, tutaiona kwamba si sahihi kwa sababu zifuatazo: 1. Kwa mujibu wa Qur ani Tukufu (kama tulivyokwishaona hapo juu), Hadith za Mtume Muhammad (s.a.w.w.) na komangano la wanazuoni wote wa Kiislamu (kama tutakavyoona hapa chini), Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho; hakuna mtume yeyote mwengine baada yake. 2. Hakuna mwanachuoni yeyote wa Kiislamu wa zama zozote aliyelifasiri neno aakhirati katika aya hiyo kwa yale yatakayokuja baadaye. Wote wamelifasiri neno hilo kwa Akhera. 3. Katika Qur ani Tukufu, mna aya mbili nyengine ambamo maneno aakhirati na yuuqinuun yameandamana. Hizi ni Sura 27:3 na 31:4. Katika hizo, ile ya Sura 31:4 imefuatiwa na aya yenye maneno sawasawa na yale yanayofuatia aya hii tunayoijadili. Na pamoja na hayo, neno aakhirati katika aya hizo hawalifasiri kwa yale yatakayokuja baadaye, katika tafsiri yao ya Qur ani Tukufu, bali wanalifasiri sawasawa kwa wana yakini na Akhera. Hivyo ni wazi kwamba, katika aya hii tunayoijadili, neno aakhirati wameipotoa tafsiri yake kwa maaribu yao wenyewe. 4. Kwa mujibu wa Qur ani Tukufu (Sura 2:213 na 57:25), Mitume wote wameteremshiwa Vitabu na Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo, kama Mirza Ghulam Ahmad ni mtume wa Mwenyezi Mungu, kitabu chake alichoteremshiwa yeye ni kipi khaswa kwa hivi ambavyo wafuasi wake wanaeleza kwamba ni lazima tuwe na yakini na yale yatakayokuja baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.)? Na kitabu hicho kimetuletea yapi mapya yasiyokuwamo ndani ya Qur ani? 5. Kwa uwongofu wa Binadamu, kuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho ndiyo 61

77 misingi mikubwa ambayo Qur ani inashuhudia kwa kutukariria mara zisizopungua 26. Hata wao Makadiani wanalitambua hilo kwa kusema chini ya maelezo ya Sura 2:62 (ambayo kwao ni 2:63) ya tafsiri yao (uk. 22): Hapa Mwenyezi Mungu ametaja nguzo kubwa mbili, ya kwanza na ya mwisho, na nguzo zingine zote za Uislamu zinaingia ndani yake. Yaani mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho lazima ataamini Mitume wote, na Vitabu vyote na Malaika na Uwezo wa Mwenyezi Mungu. Hapa tunauliza: Kama tutaikubali tafsiri ya Makadiani ya neno aakhirati katika aya hiyo, si tutakuwa tumeiondoa hiyo nguzo ya mwisho? 6. Tunaposoma Sura 4:136 tunamwona Mwenyezi Mungu anavyosema na sisi kwa maneno haya: Enyi mlioamini! Mwaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na Kitabu ambacho amemteremshia Mtume Wake (Qur ani) na Vitabu alivyoviteremsha kabla. Na mwenye kumkufuru Mwenyezi Mungu na Malaika Wake na Vitabu Vyake, na Mitume Wake na Siku ya Mwisho, basi amepotea upotevu wa mbali. Hivyo, kama Mwenyezi Mungu anataka sisi tuamini ya mtume atakayekuja baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), kwa nini katika aya hii amekomea na Vitabu alivyoviteremsha kabla (ya Mtume Muhammad), asiendelee na kutaja Kitabu au Vitabu vitakavyokuja baadaye? Huo ni ushahidi wazi kwamba, baada ya hayo aliyoteremshiwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) (maa unzila ilayka) na yaliyoteremshwa kabla yake (wamaa unzila min qablika), hakuna mengine ya kuteremshwa baadaye. Ya Muhammad (s.a.w.w.) ndiyo ya mwisho. 7. Na hii aya ya 40 ya sura hii ya al-ahzaab ambamo ndani yake mna neno khaataman nabiyyiin. Neno hili, katika aya hii, wafasiri wote wa Kiislamu, kama tutakavyoona hapa chini, wamelifasiri kwa maana ya Mwisho wa Mitume. Makadiani peke yao ndio ambao wameikataa tafsiri hiyo. Wao hulifasiri neno hilo kwa Muhuri wa Manabii. Halafu hutoa maelezo chungu nzima ya kuvungavunga watu, kwa kutoa maana mbalimbali za neno khaatam (tiz. uk wa Tafsir yao), ambayo tutayajibu tutakapoyajadili mwisho wa kijalizo hiki. Kwa hivi sasa lilo muhimu ni tuelewe tu, japo kwa ufupi, kwamba hakuna mtu anayekataa kuwa neno khaatam linazo hizo maana walizozitaja wao katika maelezo yao. Lakini, kama tulivyoona tulipojadili maana ya neno ahlul bayt katika Kijalizo I humu (uk. 46), si kila neno mara zote huja kwa maana yoyote ya neno hilo katika lugha. Kwa kaida ya lugha zote, kila neno huja kwa maana inayowafikiana na fuo la maneno (context/siyaaq) lilimotumika; na iwapo ni katika Qur ani Tukufu, basi kipaumbele cha kwanza huwa ni tafsiri ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwa sababu hakuna anayejua maana ya aya za Qur ani kumshinda yeye. Kwa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), katika Hadith zake chungu nzima (kama 62

78 tutakavyoona sasa hivi hapa chini) ameeleza kuwa yeye ni mwisho wa mitume, ndipo Waislamu wote waliposhikilia kuwa neno khaataman nabiyyiin katika aya hiyo lina maana hiyo. Kulipa maana yoyote nyengine, kama wanavyofanya Makadiani, itakuwa ni kwenda kinyume na Bwana Mtume (s.a.w.w.) jambo ambalo halifanywi na Mwislamu wa kweli. Sasa tumsikilize Bwana Mtume (s.a.w.w.) anavyotwambia. Ushahidi wa Hadith za Mtume (s.a.w.w.) Hadith za Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kuhusu jambo hili ni nyingi sana. Hapa chini tumeziteua chache tu kuonyesha kwamba hata yeye mwenyewe Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikijitambua kuwa alikuwa Mtume wa Mwisho. 1. Ni ile Hadith ya cheo cha Imam Alii (a.s.) kwa Mtume (s.a.w.w.) kuwa kama cha Nabii Haran (a.s.) kwa Nabii Musa (a.s.) isipokuwa hakuna mtume baada yangu. Hadith hii tushaijadili humu (uk. 60); itizame. 2. Imepokewa kwa Abuu Hureira kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: Mfano wangu mimi na mfano wa Mitume kabla yangu ni kama mfano wa mtu aliyejenga jengo, akalitengeneza na kulipamba vizuri isipokuwa mahali pa jiwe moja kipembeni. Watu wakawa hulizunguka na kupendezwa na uzuri wake, huku wanasema: Kwa nini halikuwekwa jiwe hapa? Basi mimi ndiye jiwe hilo, na mimi ndiye khaatamun nabiyyiin. (Bukhari, Muslim, Tirmidhi, Musnad Ahmad). 3 Jee! Tunataka ushahidi gani zaidi ya huo kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho? Kama jengo limejengwa, ikawa bado mahali pa jiwe moja tu kukamilika. Muhammad (s.a.w.w.) akaja akawa ndiye hilo jiwe lililobaki. Jee! Akishaingia hapo penye nafasi, ipo tena nafasi ya jiwe jengine? Jee! Katika Hadith hii tukisema kuwa khaatamun nabiyyiin maana yake ni Mtume wa Mwisho kama ambavyo jiwe lililobaki pale kipembeni lilikuwa ndilo jiwe la mwisho la jengo lile, tutakuwa tumekosea? 3. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Hakika ujumbe (risaala) na utume (unabii) umekatika (umekoma). Kwa hivyo hakuna mjumbe baada yangu wala nabii. (Tirmidhi na Imam Ahmad). 4. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Hakika Mwenyezi Mungu hakutuma mtume ila aliwatahadharisha umma wake na Dajjaal. 4 Na mimi ni mwisho 3 Katika Sahih Muslim mna Hadith nne kama hiyo. Katika riwaya ya mwisho kati ya hizo, mna maneno haya: Basi nikaja, nikawakhatimisha mitume. Imam Tirmidhi naye ameitaja Hadith hii kwa maneno yayo hayo tuliyoyanukuu katika matini ya kijalizo hiki. Abuu Daawuud at-twayaalisii, katika Musnad yake, ametaja Hadith iliyopokewa kwa Jaabir h. Abdillahi ambayo mwisho wake mna neno hili la Mtume (s.a.w.w.): Mitume wakatiwa ukomo kwa mimi. Kadhalika, Imam Ahmad ametoa Hadith k.w.k. kwa maana iliyotajwa katika matini, japokuwa maneno yake yanakhitalifiana kidogo. Hadith hizo zimepokewa kwa Ubayy b. Ka b, Abuu Said al-khudhrii na Abuu Hureira. 4 Dajjaal ni mtu mwongo. 63

79 (aakhir) wa mitume, na nyinyi ni mwisho wa nyumati. Naye (huyo Dajjaal) atatoka miongoni mwenu. (Ibn Maajah). Angalia katika Hadith hii; Mtume (s.a.w.w.) ametumia neno aakhir badali ya khaatamil anbiyaa. Jee, neno hilo lina maana gani nyengine isiyokuwa mwisho? Hata mtu wa kawaida, anayejua Kiswahili vizuri, anajua kuwa akhiri maana yake ni mwisho. Kwa hivyo kama Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alikijua kuwa khaatamun nabiyiin haina maana ya mwisho wa mitume, kwa nini akasema kuwa yeye ni aakhirul anbiyaa? Na umma wa Muhammad (s.a.w.w.), kati ya nyumati za Mitume wote waliomtangulia, umeitwa mwisho wa nyumati kwa kuwa hakutakuwa na umma wa mtume mwengine yeyote baada yake kwa vile yeye ni Mtume wa Mwisho. Kwa hivyo umma wake nao ni wa mwisho. 5. Thawbaan amesema kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema:... kutatokeza waongo 30 katika umma wangu. Kila mmoja kati yao atadai kuwa yu mtume hali mimi ndimi Mtume wa Mwisho; hakuna mtume baada yangu. (Abuu Daawuud). Jee! Tunataka maneno gani wazi zaidi kuliko hayo? Kuwa katika huu umma wa Muhammad (s.a.w.w.) (na mtume wa Makadiani alikidai yu katika umma huu!) kutatokea watu wapatao 30 watakaojidaia utume. Wote hao watakuwa waongo kwa kuwa hakuna mtume baada yake. Yeye ndiye Mtume wa mwisho. 6. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Hakuna mtume baada yangu, wala umma baada ya umma wangu. (Bayhaqii na Twabarani). Jee! Lugha hiyo ina ugumu wowote? 7. Mtume (s.a.w.w.) amesema: Wana wa Israeli walikiongozwa na Mitume. Kila mtume mmoja akifariki, mtume mwengine akifuatia nyuma yake. Hata hivyo, hakuna mtume baada yangu; kutakuwako makhalifa tu. (Bukhari). 8. Mtume (s.a.w.w.) amesema; Mimi ni Muhammad. Mimi n Ahmad. Mimi ni mfutaji; ukafiri utafutwa kwa ajili yangu. 5 Mimi ni mkusanyaji; watu watakusanywa baada yangu. 6 Na mimi ni wa mwisho (al- aaqib) ambaye baada yake hakuna mtume. (Bukhari, Muslim, Tirmidhi, Muwatta, al-mustadrak). 9. Abdulrahman b. Jubayr amesema kwamba alimsikia Abdallah b. Amr b. al-aas akisema: Siku moja Mtume (s.a.w.w.) alitutokea kana kwamba anatuaga. Akasema: Mimi ni Muhammad, Mtume asiyejua kusoma wala kuandika (ummiy), mara tatu, wala hakuna mtume baada yangu. (Musnad Ahmad). 5 Maana yake: Kwa kuja mimi ukafiri utafutwa. 6 Maana yake: Watu watakusanywa huko Akhera, Siku ya Kukusanywa Watu, baada ya mimi kuja. 64

80 10. Mtume (s.a.w.w.) amesema: Mimi ni mtu wa kwanza kuumbwa, na wa mwisho kupawa utume. (Mishkaatul Maswaabiih, at-twabaqaatul Kubraa). 11. Mtume (s.a.w.w.) amesema: Mimi ni mwisho (aakhir) wa Mitume, na msikiti wangu ni mwisho wa misikiti. (Muslim). Hadith hii haimaanishi kwamba, baada ya ule msikiti wa Madina alioujenga Mtume Muhammad (s.a.w.w.), hakutajengwa tena msikiti wowote duniani baada yake; hasha! Maana ya Hadith hii ni kwamba, kwa vile Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho, hakuna mtume mwengine atakayekuja baada yake, basi na msikiti wake ni wa mwisho kujengwa na mtume yeyote. Na hili li wazi katika Hadith nyengine isemayo: 12. Mtume (s.a.w.w.) amesema: Mimi ni mwisho wa Mitume, na msikiti wangu ni mwisho wa misikiti ya Mitume. (Kanzul Ummaal). Yaani, kama ambavyo hakuna mtume baada ya Muhammad (s.a.w.w.), hali kadhalika hakutakuwa na msikiti wa Mtume yeyote baada yake. 13. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Nimefadhilishwa juu ya Mitume kwa mambo sita: Nimepawa maneno fasihi (jawaamiul kalim); 7 nimeokolewa kwa khofu; 8 nimehalalishiwa ngawira; nimefanyiwa ardhi kuwa msikiti kwangu, na tohara; 9 nimetumwa kwa viumbe vyote; 10 na Mitume (wote) wametiwa mwisho (khutima) kwa mimi. (Muslim, Tirmidhi na Ibn Maajah) 14. Imepokewa kwa Bibi Aisha, mke wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Hakuna utume (nubuwwat) baada yangu isipokuwa mubash-sharaat. (Maswahaba) wakauliza: Mubash-sharaat ni nini, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: Ni ndoto (ru yaa) ya kweli. (Musnad Ahmad). Kwa Hadith hii Bwana Mtume (s.a.w.w.) anatufahamisha kwamba hakutakuwa na wahyi tena baada yake. Kubwa litakalokuwako ni ilhamu (ufunuo) ambayo itakuwa kwa namna ya ndoto ya kweli. 15. Mtume (s.a.w.w.) amesema; Enyi watu! Kwa hakika hakuna mtume baada yangu, wala sunna baada ya sunna yangu. Yeyote atakayedai hilo, basi kwa dai lake hilo na uzushi (bid ah) wake huo ataingia Motoni. Muuweni. Na atakayemfuata, naye pia ataingia Motoni... (Wasaailush Shii ah). 16. Imepokewa kwa Abii Umaama kwamba Mtume s.a.w.w alisema: Enyi watu! Hakika hakuna mtume baada yangu, wala umma baada yenu. Zindukeni! Mwabuduni Mola wenu... (Wasaailush Shii ah). 7 Haya ni maneno machache yaliyojaa maana na hikima. 8 Yaani, nimepawa ushindi dhidi ya adui zangu kwa wao kuingiwa na khofu ya mimi na wafuasi wangu. 9 Yaani katika sharia ya Muhammad (s.a.w.w.) swala inaweza kuswaliwa popote juu ya ardhi, si lazima msikitini; na mchanga unaweza kutumiwa badali ya maji kujitwahirishia (tayammum). 10 Tiz. Sura 2:107 na 25:1. 65

81 17. Imepokewa kwa Abuu Ja far Muhammad b. Alii 11 (a.s.) kwamba alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alihiji kutoka Madina akaeleza kisa cha Ghadir Khum 12 na khutba ya Mtume hapo akasema: Ninaapa kwa Mwenyezi Mungu! Manabii na Mitume (mursaluun) wa mwanzo walinitolea bishara mimi. Na mimi ni mwisho wa Manabii na Mitume, na ni hujja 13 juu ya viumbe vyote vilivyoko mbinguni na ardhini. Yeyote mwenye shaka na hili, basi huyo ni kafiri wa ukafiri wa jahilia ya kwanza. 14 Na yeyote mwenye shaka na neno langu hili, basi atakuwa ametilia shaka yote. Na mwenye kutilia shaka hayo, basi huyo yu Motoni. (al-ihtijaaj na Mustadrakul Wasaail). Mara nyengine, wale wanaokataa kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho hujaribu kupambanua baina ya unabii na urasuul! Hudai kwamba kilichokoma ni urasuli (utume wa kuleta sharia) sio unabii. Lakini Bwana Mtume (s.a.w.w.), katika Hadith hii, analibatilisha dai lao hilo kwa kusema yeye ni mwisho wa nabiyyiin na mursaliin. Pia tizama Hadith Na. 3 hapo juu. 18. Imepokewa kwa Alii b. Hilaal kwamba babake alisema: Niliingia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) naye yu katika ile hali aliyofia. Nikamkuta Fatma yu kichwani kwake analia kwa sauti kubwa. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) akamwinulia kichwa chake, akasema:...sisi ahlul bayt Mwenyezi Mungu aliyetukuka ametupa mambo sabaa ambayo hajampa yeyote kabla yetu, wala hatampa yeyote baada yetu. Mimi ni Mwisho wa Mitume na Mbora (akram) wa Mitume... (Kashful Ghummah). Makadiani, katika kukataa kwao kuwa neno khaatam lina maana ya mwisho, hudai kwamba lina maana ya mbora. Kama ni hivyo, mbona katika Hadith hii Bwana Mtume (s.a.w.w.) amesema kuwa yeye ni khaatamun nabiyyiin na akramun nabiyyiin? Ina maana yeye ni mbora wa mitume na mbora wa mitume? Vyalekea hivyo? Kama havilekei na kweli havilekei basi neno akram hapo lifasiriweje? Mpaka hapa tumeshaona jinsi Mtume Muhammad (s.a.w.w.), katika Hadith zake 15 tulizozinukuu hapo juu, alivyotufasiria neno khaataman nabiyyiin kwa hakuna mtume baada yangu, ujumbe na utume umekatika, na mimi ni mwisho (aakhir) wa mitume. Lakini, pamoja na hayo, Makadiani hushikilia kwamba, kwa maneno hayo, hakukusudia kusema kuwa yeye ni mtume wa mwisho au hakuna mtume atakayekuja baada yake! Hivi ni kweli kwamba aliposema kuwa hakuna mtume baada yake alimaanisha yuko mtume baada yake? Au aliposema ujumbe na utume umekatika (umekoma) alimaanisha utaendelea? Vipi mnahukumu? (Sura 10:35) 11 Huyu ni al-baaqir (a.s.), Imam wa tano. 12 Ghadir Khum ni mahali ambapo Bwana Mtume (s.a.w.w.), baada ya hijja yake ya mwisho, alisimama na kuwahutubia maswahaba, akawatangazia kwamba kama ambavyo yeye ni mawlaa (mtawalia mambo) wa Waislamu, basi vivyo hivyo ndivyo Alii awe kwao. 13 Ni hujja kwa viumbe vyote kwa kuwa, kwa kuletwa yeye, watu hawatakuwa tena na hujja ya kumwasia Mwenyezi Mungu. 14 Ukafiri huo ni ule wa kabla ya kuja Uislamu. 15 Na hizi sizo zote; nyengine tumeziacha. 66

82 Ushahidi wa Maneno ya Maimamu Kabla ya kufariki dunia, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alituachia maimamu 12 katika ahlul bayt. 16 Akatuusia kwamba, kama tunataka tusipotee, basi tushikamane na wao; maana wao na Qur ani Tukufu kabisa hawatatengana mpaka kesho Akhera. 17 Pia akatwambia kwamba, kwa kushikamana na maimamu hao, tutakuwa kama watu wa Nabii Nuhu waliopanda safina yake. Tutaokoka na adhabu ya Mwenyezi Mungu kama walivyookoka wao. 18 Kwa hivyo, hebu sasa tuangalie maimamu hao wamesema nini kuhusu khaataman nabiyyiin: 1. Imam Alii b. Abii Twaalib (a.s.), 19 katika khutba yake Na. 133 katika Nahjul Balaaghah, 20 amesema hivi:...alimtuma (Muhammad (s.a.w.w.)) baada ya kipindi kirefu cha Mitume kupita, na watu kuzozana. Akawatia ukomo (faqaffaa) Mitume kwaye, akaukhatimisha na wahyi kwaye Pia amenukuliwa, katika kitabu kiitwacho al-ihtijaaj cha Abuu Mansuur: Ahmad b. Alii at-twabrisii, 21 kuwa alisema: Ama Mtume wa Mwenyezi Mungu, yeye ni khaatamun nabiyyiin: hakuna nabii baada yake wala mjumbe (rasuul). Na, kwa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu (yaani Mtume Muhammad (s.a.w.w.)), Mitume wametiwa ukomo (khutima) mpaka Siku ya Kiyama. 3. Imepokewa kwa Asmaa bt. Umays kwamba Bibi Fatma (a.s.) 22 alimhadithia: Nilipochukua mimba ya Hasan 23 na kumzaa, Mtume (s.a.w.w.) alikuja... Kisha akashuka Jibril na kusema: Ewe Muhammad! Mwenyezi Mungu aliyetukuka anakutolea salamu na anasema: Alii kwako ana cheo cha Harun kwa Musa, lakini hakuna mtume baada yako. Mwite mtoto wako huyu kwa jina la mtoto wa Harun... ( Uyuunu Akhbaarir Ridhaa). 4. Imam Hasan b. Alii b. Abii Twaalib (a.s.) amesema: Walikuja watu kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) wakasema: Wewe unadai kwamba u Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kwamba wewe unaletewa wahyi kama vile ambavyo Mwenyezi Mungu alimpelekea wahyi Musa b. Imraan. Mtume akanyamaza kwa muda, kisha akasema: Ndiyo! Mimi ni bwana wa watoto wa Adam, wala (sisemi hilo kwa) fakhari. Na mimi ni Mwisho wa Mitume na kiongozi wa wacha-mungu, na ni Mtume wa Bwana wa viumbe vyote... (al-burhaan) 5. Imepokewa kwa al-a mash kwamba Husein b. Alii (a.s.) 24 alisema: Niambie ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Jee, kutakuwa na mtume baada yako? Akajibu: La! Mimi ni 16 Hayo yamo katika Sahih Bukhari, Sahih Muslim, Sunan Tirmidhi, Musnad Ahmad, na vyenginevyo. 17 Tiz. kidokezo Na. 29 chini ya Kijalizo I humu. 18 Tiz. kidokezo Na. 37 chini ya Kijalizo I humu. 19 Huyu ndiye Imam wa kwanza. 20 Hiki ni kitabu kilichokusanya khutba zake na barua zake zilizojaa hikima. Ni muhimu Mwislamu kuwa nacho na kukisoma. 21 Huyu ni kati ya wanazuoni wakubwa wa kame ya 6 ya Kiislamu. 22 Huyu ni binti ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) aliyekuwa mke wa Imam Alii (a.s.). Ni miongoni mwa ahlul bayt (tiz. Kijalizo I). 23 Huyu ni mtoto wa Imam Alii (a.s.), kuzaa na Bibi Fatma (a.s.). Yeye ndiye Imam wa pili baada ya babake. 24 Huyu ni Imam wa tatu. Ni mdogo wake Imam Hasan (a.s.) aliyetajwa Na. 23 hapo juu. 67

83 Mwisho wa Mitume. Lakini baada yangu kutakuwa na maimamu wenye kusimamisha uadilifu; idadi yao ni (kama ile) ya wakubwa (nuqabaa) 25 wa wana wa Israeli... (Ithbaatul Hudaat na Manaaqibu Aali Abii Twaalib). 6. Imepokewa Hadith kwa Abuu Ja far (a.s.) 26 kwamba: Mwenyezi Mungu, kwa Kitabu chenu hiki (Qur ani), amevitia ukomo vitabu (vyote); na kwa Mtume wenu (Muhammad (s.a.w.w.)), amewatia ukomo Mitume (wote). (al-kaafi). 7. Ismail b. Jaabir amesema kwamba alimsikia Abuu Abdillahi Ja far b. Muhammad as-swaadiq (a.s.) 27 akisema: Hakika Mwenyezi Mungu aliyetukuka alimtuma Muhammad (s.a.w.w.), akawatilia ukomo (khatama) Mitume kwaye; kwa hivyo hakuna mtume baada yake. Akamteremshia Kitabu (Qur ani), akavitia ukomo vitabu vyote kwacho; kwa hivyo hakuna kitabu baada yacho. Humo amehalalisha halali, akaharamisha haramu. Hivyo, halali yake ni halali mpaka Siku ya Kiyama, na haramu yake ni haramu mpaka Siku ya Kiyama... (al-miizaan). 8. Imepokewa kwa Ayyuub b. al-hurr kwamba alimsikia Abuu Abdillahi (a.s.) 28 akisema: Hakika Mwenyezi Mungu amewatia ukomo mitume kwa Mtume wenu (Muhammad (s.a.w.w.)); kwa hivyo hakuna mtume baada yake abadan. Akavitia ukomo vitabu kwa Kitabu chenu (Qur ani); kwa hivyo hakuna kitabu baada yake abadan. Na akateremsha humo maelezo (tib-yaana) ya kila kitu... (al-waafii). 9. Imam Alii b. Musa ar-ridhaa (a.s.) 29 amesema, katika Hadith ya kuusifu Uimamu na Imam: (Uimamu) u mikononi mwa watoto wa Alii peke yao mpaka Siku ya Kiyama, maana hakuna mtume baada ya Muhammad (s.a.w.w.)... (Uyuunu Akhbaarir Ridhaa). 10. Imepokewa kwamba katika baadhi ya dua za Imam Muhammad b. Alii al-jawwaad (a.s.) 30 ni hii: Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu ya mambo, Mkubwa wa dalili, Mbora wa utawala. Atakalo Mwenyezi Mungu huwa, na asilolitaka haliwi. Ninashuhudia kwamba Nuhu ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwamba Ibrahimu ni kipenzi cha Mwenyezi Mungu, kwamba Musa ni mzungumzi (kaliim) wa Mwenyezi Mungu na ni mnong ona naye (najjiihi), kwamba Isa b. Mariamu ni roho ya Mwenyezi Mungu na neno Lake amani imshukie yeye na wote pamoja na kwamba Muhammad (s.a.w.w.) ni Mwisho wa Mitume, hakuna mtume baada yake. (Bihaarul Anwaar). Hayo basi ni baadhi tu ya yaliyopokewa kwa baadhi ya hao maimamu 12. Mengi sana tumeyaacha kwa kuchelea kuyarefusha mambo. Na yote ni ushahidi tosha kwamba, kwao wao pia, Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alikuwa ni Mtume wa mwisho; hakuna mtume baada yake. 25 Wakubwa hao, kama maimamu aliotuachia Bwana Mtume (s.a.w.w.), walikuwa 12. (tiz. Sura 5:12). 26 Huyu ni Muhammad b. Alii al-baaqir (a.s.), Imam wa tano. 27 Huyu ni Imam wa sita. 28 Huyu ni yeye yeye Imam Ja far as-swaadiq (a.s.), Imam wa sita. 29 Huyu ni Imam wa nane. 30 Huyu ni Imam wa tisia. 68

84 Sasa tuangalie ushahidi wa komangano la maswahaba:. Ushahidi wa Komangano la Maswahaba Tunaposoma historia, tunaona kwamba maswahaba wote walikomangana katika kuwapiga vita wale waliodai kuwa ni mitume, na wale waliowakubali pia. Mfano mzuri ni wa yule aliyekiitwa Musaylima Mwongo. Yeye hakukataa kuwa Muhammad (s.a.w.w.) alikuwa Mtume, isipokuwa alidai tu kuwa alikuwa Mtume mwenzake. Kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kufariki dunia, aliwahi kumwandikia: Kutoka kwa Musaylima, yende kwa Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu: Amani iwe juu yako. Inataka ujue kuwa nimefanywa mshirika wako katika kazi ya utume. (Twabari, Jz. 2, uk Chapa ya Misri). Zaidi ya hayo, Twabari amesimulia kwamba katika mwadhini chini ya Musaylima, maneno: Ash-hadu anna Muhammadar Rasuulul Laah yalikitamkwa vilevile. Hata hivyo, alihukumiwa kuwa kafiri, akapigwa na vita. Historia inathubutisha pia kwamba Banuu Haniifa walimwamini kwa insafi, na walifahamishwa kwamba Muhammad (s.a.w.w.), yeye mwenyewe, alimfanya mshirika wake katika Utume. Na hilo ni kwa sababu mtu mmoja, aliyekuwa amejifimza Qur ani Madina, aliwaendea hao Banii Haniifa na kuwasomea baadhi ya aya kwa kuwahadaa kwamba ameteremshiwa Musaylima. Lakini, pamoja na yote hayo, maswahaba hawakuutambua Uislamu wao, bali waliwatokea na kuwapiga vita. Wala haiwezi kudaiwa kwamba maswahaba hawakuwapiga vita kwa kuritadi kwao, bali waliwapiga vita kwa uaswi wao dhidi ya dola ya Kiislamu. Maana, kwa mujibu wa sharia ya Kiislamu, vita wanapopigwa waasi wa Kiislamu, mateka wao hawafanywi watumwa wala wajakazi. Bali hata dhimmiy 31 hawawezi kufanywa hivyo. Lakini maswahaba walipotoka kupigana na Musaylima na wafuasi wake, na Khalifa Abu Bakar akatangaza wachomwe moto na kuuwawa, na wanawake wao na watoto wao wafanywe wajakazi na watumwa, na wasikubaliwe lolote isipokuwa Uislamu, walifanywa hivyo. Ndipo Alii b. Abii Twaalib (a.s.) alipompata yule mjakazi aliyemzalia mtoto wake, Muhammad bin Hanafiyya. (al-bidaayah wan Nihaayah, Jz. 6, uk. 316, 325). Kwa hivyo, ni wazi kwamba jinai ambayo maswahaba walitoka ili kupigana na Banii Haniifa kwayo, haikuwa ni jinai ya uaswi. Ilikuwa ni kwa sababu mmoja katika wao alidai utume, na wengine wakamwamini. Na haya yote yalitokea mara tu baada ya kutawafu Mtume (s.a.w.w.), chini ya uwongozi wa Abu Bakar, na kwa komangano la maswahaba wote. Yumkini hakuna mfano wazi zaidi ya huo wa komangano la maswahaba Dhimmiy ni Nasara au Yahudi anayekaa katika daarul Islam (nchi ya Kiislamu), na aliyefanyiana ahadi ya kulindwa na dola hiyo. 32 Sehemu kubwa ya ushahidi huu, na unaofuatia, nimeunukuu kutoka Maa Hiyal Qaadiyaaniyyah cha Abul A laa al-mawdudi, uk

85 Ushahidi wa Komangano la Wanazuoni Sasa tutizame yale yaliyosemwa na wanazuoni mbalimbali, wa madhihabi mbalimbali, katika kame mbalimbali: 1. Imam Abuu Haniifa ( H): Katika zama zake, mtu mmoja alidai utume. Akasema: Nipeni muda ili niwaletee dalili za utume wangu. Abuu Haniifa akasema: Yeyote atakayetaka dalili kwake, atakuwa amekufuru, kwa sababu Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) amesema: Hakuna mtume baada yangu. (Manaaqib al-imaamil A dham Abii Haniifa, Ibn Ahmad al-makki, Jz. 1, uk Chapa ya Hyderabad, 1321H). 2. Ibn Jariir Twabari ( H), katika Tafsir yake ya Qur ani (Jz. 22, uk. 12), ameeleza maana ya Sura 33:40 hivi: Lakini yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Mitume ambaye ameutia ukomo (khatama) utume na kuupiga muhuri (twaba a alayhaa). Kwa hivyo hautafunguliwa kwa yeyote baada yake mpaka Kiyama kisimame. 3. Imam Twahaawi ( H), katika kueleza imani za maimamu waliotangulia, khaswa Imam Abuu Haniifa, Abuu Yusuf na Muhammad (Mwenyezi Mungu awarehemu), amesema: Kwamba yeye (Muhammad (s.a.w.w.)) ni Mwisho wa Mitume, kiongozi wa wacha-mungu, bwana wa Mitume na kipenzi cha Bwana wa viumbe vyote. Dai lolote la utume baada yake ni upotofu (ghawan) na (kuabudu) matamanio. (Sharhut Twahaawiyah, Daarul Ma arif, Misri, uk. 15, 87, 96, 97, 100, 102). 4. Allaamah Ibn Hazm al-andaluusi ( H) ameandika: Na kwa hakika wahyi umekatika (umekoma) tangu alipokufa Mtume (s.a.w.w.). Na ushahidi wa hilo ni kwamba wahyi hauwi isipokuwa kwa Mtume, hali Mwenyezi Mungu aliyetukuka amesema: Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Mitume. (al-muhallaa, Jz. 1, uk. 26). 5. Imam Ghazali ( H) amesema: Umma (wa Kiislamu) umekomangana kwamba, kwa neno hili: laa nabiyya ba dii (hakuna mtume baada yangu), Mtume (s.a.w.w.) hakukusudia lolote isipokuwa hili: kwamba hakutakuwa na nabii baada yake abadan, wala hakutakuwa na mtume (rasuul) baada yake abadan. Wala halina maana wala taawili yoyote nyengine. Na yeyote anayelikanusha hili, huwa amekanusha komangano la wanazuoni. (al-iqtiswaadfil I tiqaad, Misri, uk. 114) 6. Muhyis Sunnah al-baghawi (510H), katika Tafsiri yake ya Qur ani iitwayo Ma alimut Tanziil (Jz. 3, uk. 158), amesema: Mwenyezi Mungu ameukhatimisha utume kwaye; kwa hivyo yeye ni wa mwisho wao... Na imepokewa kwa Ibn Abbas kwamba Mwenyezi Mungu aliyetukuka (katika aya hii) amehukumu kwamba hakuna mtume baada yake. 7. Allaamah Zamakhshari ( H) amesema katika Tafsiri yake iitwayo al-kash-shaaf (Jz. 2, uk. 215): Ukiuliza: Vipi (Muhammad) atakuwa Mwisho wa Mitume hali (inaaminiwa kwamba) Isa atashuka siku za mwisho kabla ya Kiyama? Nitajibu: Maana ya (Muhammad) kuwa ni Mwisho wa Mitume ni kwamba hatapawa utume yeyote 70

86 baada yake. Ama Isa; yeye ni katika waliopawa utume kabla yake. Na atakaposhuka, atashuka kama mfuasi wa sharia ya Muhammad atakayeswali kwa kulekea kibla chake (al-ka bah) kama yeyote katika umma wake. 8. Qadhi Iyaadh (544H) amesema katika kitabu chake kiitwacho ash Shifaa (Jz. 2, uk ): Yeyote anayejidaia utume, au anayejawizisha kwamba mtu anaweza kuuchuma, au kuifikia daraja yake kwa utakatifu wa moyo, kama wanavyosema mafilosofa na masufi; hali kadhalika yeyote katika wao anayedai kwamba anateremshiwa wahyi, japo asidai kuwa yu mtume...basi hao wote ni makafiri wenye kumkadhibisha Mtume (s.a.w.w.), kwa sababu yeye (s.a.w.w.) ametupasha habari kwamba ni Mwisho wa Mitume, hakuna mtume baada yake. Pia ametupa habari kutoka kwa Mwenyezi Mungu aliyetukuka kwamba yeye ni Mtume wa mwisho, na kwamba ametumwa kwa watu wote; na umma wote umekomangana kuwa maneno haya hayana maana yoyote zaidi ya haya yaliyo dhahiri. Kwa hivyo hapana shaka yoyote kwamba watu kama hao ni makafiri wote, kwa komangano la wanazuoni na kwa Hadith. 9. Allaamah Shihristani (548H) naye ameandika, katika Jz. 3, uk. 249 wa kitabu chake kiitwacho al-milal wan Nihal: Kadhalika, anayesema kwamba, baada ya Muhammad (s.a.w.w.), kuna mtume asiyekuwa Isa mwana wa Mariamu (a.s.); mtu kama huyo, hakuna watu wawili wanaokhitaliflana kwamba yu kafiri. 10. Imam Raazi ( H), katika kuieleza aya ya khaataman nabiyyiin, amesema hivi: Sababu ya kusema wakhaataman nabiyyiin ni hii: Kwamba kama mtume, ambaye baada yake atakuja mtume mwengine, ataacha kutoa nasaha yoyote au maelezo, basi yule atakayekuja baada yake atayatoa. Lakini yule ambaye hakuna mtume baada yake, huwa na huruma zaidi na umma wake, na kuwapa maongozi, maana yeye huwa ni kama mzazi kwa mtoto wake ambaye hana yeyote mwengine wa kumtizama (baada yake) isipokuwa yeye. (at Tafsiirul Kabiir, Jz. 6, uk. 581). 11. Allaamah al-baydhwaawi (685H) ameandika katika Tafsiri yake iitwayo Anwaarut Tanziil: Yaani (Muhammad) ni wa mwisho wao (aakhiruhum) aliyewatilia ukomo au waliotiwa ukomo kwaye. Wala kushuka kwa Isa baada yake hakupingi hilo, kwa sababu atakapokuja Isa, atakuwa mfuasi wa dini yake (yaani Muhammad). (Jz. 4, uk. 164). 12. Allaamah Hafidhud Din an-nasafii (710H) amesema katika uk. 471 wa Tafsiri yake iitwayo Madaarikut Tanziil: Maana ya wakhaataman nabiyyiin ni wa mwisho wao (aakhiruhum). Yaani hakuna yeyote atakayepawa utume baada yake. Kuhusu Isa; yeye ni katika waliopawa utume kabla yake, na atakaposhuka, atashuka kama mfuasi wa sharia ya Muhammad (s.a.w.w.), na kama mmoja wa umma wake. 13. Allaamah Alaaud Din al-baghdaadii (725H) amesema katika uk wa Tafsiri yake iitwayo al-khaazin: Wakhaataman nabiyyiin; Mwenyezi Mungu ameutia ukomo utume kwaye, kwa hivyo hakuna utume baada yake, wala pamoja naye... Wakaanal Laahu bikulli shay-in aliimaa: yaani imeingia katika ujuzi Wake kwamba hakuna mtume baada yake. 71

87 14. Allaamah Ibn Kathiir ad-dimishqii (774H) ameandika katika Tafsiri yake (uk. 493 wa Jz. 3): Hivyo, aya hii ni nassi ya kwamba hakuna nabii baada yake. Na kama hakuna nabii baada yake, basi hapana rasuul (mtume) pia; maana daraja ya utume ni akhasi kuliko daraja ya unabii. Hivyo, kila mtume ni nabii, lakini si kila nabii ni mtume (rasuul). 15. Allaamah Jalaalud Din as-suyuutwii (911H) amesema katika Tafsiri yake iitwayo Jalaalayn (uk. 768): Wakaanal Laahu bikulli shay-in aliimaa: Anajua kwamba hakuna mtume baada yake; na atakaposhuka Isa, atahukumu kwa sharia yake (Muhammad s.a.w.w). 16. Allaamah Ibn Nujaym (970H) ameandika katika uk. 179 wa kitabu chake kiitwacho Kitaabul Ashbaah wan Nadhaair: Kama mtu haamini kwamba Muhammad (s.a.w.w.) ni Mwisho (aakhir) wa Mitume, basi huyo si Mwislamu, maana hili ni katika dhwaruuriyyaat (mambo ya kimsingi ambayo kuyajua na kuyaamini ni msingi wa Imani). 17. Mulla Alii Qaarii (1016H) amesema katika uk. 202 wa kitabu chake kiitwacho Sharhul Fiqhil Akbar: Kudai utume baada ya Mtume wetu (s.a.w.w.) ni ukafiri kwa komangano la wanazuoni wote. 18. Sheikh Ismail al-haqqii (1137H), katika kueleza maana ya wakhaataman nabiyyiin, amesema hivi katika uk. 188 wa Jz. 22 ya Tafsiri yake iitwayo Ruuhul Bayaan: Aaswim 33 amesema neno khaatam, kwa kuitia fataha tee, itakuwa na maana ya muhuri unaotumiwa kupigia muhuri vitu. Na kwa neno hili (aya hii itamaanisha kuwa) yeye (Muhammad (s.a.w.w.)) ni wa mwisho wao (aakhiruhum) ambaye kwaye wametiwa ukomo (mitume wote)... Waliobaki wamelisoma neno hili kwa kuitia kasra tee (yaani khaatim) kwa maana ya anayepiga muhuri. Kwa njia hii, wanazuoni wa umma wake wanamrithi yeye (s.a.w.w.) upande wa walaya 34 tu, kwa vile ambavyo urathi wa utume umekatika kwa yeye kuwa mwisho wake. Wala hili la yeye kuwa Mwisho wa Mitume halipingani na kuja Nabii Isa baada yake, kwa sababu maana ya yeye kuwa khaataman nabiyyiin ni kwamba hatapawa utume yeyote baada yake; kama alivyomwambia Alii: Wewe kwangu una daraja ya Harun kwa Musa isipokuwa kwamba hakuna mtume baada yangu. Isa ni kati ya waliopawa utume kabla yake; na atakapokuja, atakuja kama mfuasi wa sharia ya Muhammad (s.a.w.w.), atakayeswali kwa kulekea kibla chake, kama yeyote katika umma wake. Hatateremshiwa wahyi wala hatatoa hukumu, bali atakuwa Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu tu (s.a.w.w.)... Kwa hivyo, yeyote anayesema kuwa kuna mtume mwengine baada ya Mtume wetu, atakuwa ni kafiri, kwa sababu atakuwa ameikataa nguzo kubwa ya Imani. Hali kadhalika, aliye na shaka na hilo, naye pia atakuwa ni kafiri, maana haki imeshapambanuliwa na upotofu. Na dai la yeyote kuwa yu mtume baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) si lolote isipokuwa udanganyifu tu. 19. Kwa mujibu wa al-fataawaa Aalamgiirii (uk. 263 wa Jz. 2), ambazo ni fatwa za wanazuoni 33 Huyu ni mmoja wa maqurraa (wataalamu wakubwa wa usomaji wa Qur ani). 34 Yaani uendeshaji wa mambo ya Waislamu. 72

88 wakubwa wakubwa wa Bara Hindi katika kame ya 12 ya Kiislamu, kwa amri ya Mfalme Aurangzeb Aalamgiir: Kama mtu haamini kwamba Muhammad (s.a.w.w.) ni mwisho wa Mitume (aakhirul anbiyaa), basi huyo si Mwislamu; na kama atadai kuwa yeye ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu au nabii, atakuwa kafiri. 20. Allaamah Shawkaani (1255H), katika Tafsiri yake iitwayo Fat-hul Qadiir (Jz. 4, uk. 275), amesema: Wengi (jumhuur) wa wanazuoni wameisoma khaatim kwa tee kasra; lakini Aaswim ameisoma kwa tee fat-ha (khaatam). Kwa kisomo cha kwanza, itakuwa na maana ya kuwa (Muhammad) aliwakhatimisha, yaani alikuja mwisho wao (jaa-a aakhiruhum). Kwa kisomo cha pili, itakuwa na maana ya kuwa alikuwa kama muhuri kwao ambao, kwawo, (mitume) walipigwa na, kwa yeye kuwa miongoni mwao, walipambika. 21. Allaamah al-aluusi (1270H), katika uk. 32 wa Tafsiri yake iitwayo Ruuhul Ma ani, amesema hivi: Neno nabii ni pana zaidi (a- ammu) kuliko rasuul. Kwa hivyo, kwa kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni khaatamun nabiyyiin ni lazima vilevile awe khaatamul mursaliin. Na muradi wa yeye (s.a.w.w.) kuwa wa mwisho wao (khaatamuhum) ni kwamba: baada ya yeye kusifika kwa Utume katika ulimwengu huu, kusifika kwa Utume kwa yeyote mwengine miongoni mwa watu na majinni, kumekoma... Na katika uk. 38, amesema: Yeyote atakayedai, baada yake, kuwa anapata wahyi wa Utume, huyo atakuwa ni kafiri, wala hakuna hitilafu yoyote baina ya Waislamu juu ya hilo... Na katika uk. 39: Na kuwa Muhammad ni Mwisho wa Mitume ni jambo ambalo limetajwa na Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na kuelezwa na sunna (ya Mtume (s.a.w.w.)), na kukomanganwa na umma (wake). Kwa hivyo, yeyote anayedai kinyume cha hivyo ni kafiri; na akishikilia vivyo hivyo, auwawe. 22. Mawlaa Muhammad Muhsin b. Shah Murtadhwaa, anayejulikana pia kama Alfaydhul Kaashaani ( H) amesema katika Tafsiri yake (uk , Jz. 4) iitwayo Tafsirus Swaafii: Wakhaataman nabiyyiin maana yake ni: wa mwisho wao (aakhiruhum) ambaye amewakhatimisha au wamekhatimishwa, kwa kutegemea visomo viwili... Wakaanal Laahu bikulli shay-in aliimaa; Anamjua anayefaa kutiwa ukomo utume kwaye, na vipi iwe. 23. Allaamah Sayyid Muhammad Husein Twabaatwabaaii katika uk. 325 wa Jz. 16 ya al-mizaan fii Tafsiiril Qur aan, amesema: Khaatam, kwa tee fat-ha, ni kinachokhatimishwa kwacho, kama muhuri...na muradi wa kuwa yeye (s.a.w.w.) ni khaataman nabiyyiin ni kwamba utume umekhatimishwa kwaye (s.a.w.w.); kwa hivyo hakuna mtume baada yake. Na ushajua, kwa yaliyotangulia humu, maana ya risaalat (ujumbe) na nubuwwat (unabii); na kwamba rasuul ni yule anayechukua ujumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwapelekea watu, na nabii ni yule anayechukua habari za ghaibu, ambazo ndizo dini, na ya kweli yake (haqaaiquhuu)... Na kutokana na haya, inadhihiria kwamba, kuwa kwake (s.a.w.w.) mwisho wa manabii, ni lazima awe vile vile mwisho wa wajumbe (khaatiman lirrusuli). 73

89 24. Aayatullaah Sayyid Muhammad al-huseinii ash-shiiraazii, katika kufasiri wakhaataman nabiyyin katika uk. 23 wa Jz. 8 ya Tafsiri yake iitwayo Taqriibul Qur aani ilal Adh-haan, amesema: Yaani mwisho wao (aakhiruhum). Utume umetiwa ukomo kwaye. Kwa hivyo inamlazimu kulibatilisha kila lile ambalo linakhalifu maslaha ya watu; wala yeye si kama mitume waliotangulia ambao, kama hawana uwezo wa kubatilisha jambo, huja mtume mwengine baada yao kulibatilisha Sheikh Muhammad Jawaad Mughniya, katika uk. 224 wa Jz. 6 ya Tafsiri yake iitwayo at Tafsiirul Kaashif amesema: Wakhaataman nabiyyiin; kwa hivyo hakuna mtume baada ya Muhammad (s.a.w.w.), wala sharia baada ya sharia ya Kiislamu. Wakaanal Laahu bikulli shay-in aliimaa; na katika ujuzi Wake ni kujua wapi auweke utume Wake, na vipi aukhatimishe kwa Muhammad (s.a.w.w.). Na katika uk. 225 amesema: Waislamu wamewafikiana kwa kauli moja kwamba hakuna wahyi utakaopelekewa yeyote baada ya Muhammad (s.a.w.w.); kwamba atakayelikanusha hilo, hawi Mwislamu; atakeyedai utume baada ya Muhammmad, ni wajibu kuuliwa, na yeyote atakayetaka kuonyeshwa dalili ya utume wa mdai huyo, akitizamia kumsadiki katika dai lake hilo, basi huyo ni kafiri... Na katika uk. 226 amesema: Na mtu akiuliza: Kwa nini Muhammad (s.a.w.w.) kuwa mwisho wa Mitume? Tutamjibu kwamba Muhammad, na dini ya Muhammmad, imetimiza sifa zote za ukamilifu, na kufikia kilele chake na ukomo wake kabisa kabisa, kama jua lilivyofikia kiwango cha juu kabisa cha nuru. Hivyo, hakuna sayari, wala umeme ambao ulimwengu hujaa nuru zao baada ya sayari ya jua... Hali kadhalika, hakuna mtume atakayeleta kipya chochote kwa maslaha ya watu baada ya Muhammad (s.a.w.w.). 26. Ustadh Muhammad Alii as-swaabuunii, katika uk. 529 wa Jz. 2 ya Tafsiri yake iitwayo Swaf-watut Tafaasiir, amefasiri wakhaataman nabiyyin hivi: Lakini yeye (a.s.) ni mwisho wa manabii (aakhirul anbiyaa) na wajumbe (mursaliin). Kwaye, Mwenyezi Mungu amezikhatimisha dini zote (risaalaat) za mbinguni. Kwa hivyo, hakuna mtume baada yake. Amesema Ibn Abbas: Amekusudia (Mwenyezi Mungu) kusema: Kama sikuwakhatimisha mitume kwaye, ningemjaalia kuwa na mtoto wa kuwa mtume baada yake. Lakini Mwenyezi Mungu hakufanya hivyo kwa sababu alitaka awe Mwisho wa Mitume. 27. Dk. Muhammad Mahmuud Hijaazii, katika uk. 11 wa Jz. 21 ya at Tafsiirul Waadhih, na katika kuieleza maana ya aya hii ya 33:40, ameandika: Enyi watu! Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu hata muulize: Vipi amemuowa mke wa mtoto wake na huru lake? Lakini yeye alikuwa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na khaataman nabiyyiin, na imamu (kiongozi) wa Wajumbe wa Mwenyezi Mungu; hakuna mtume baada yake. Kwaye, jumbe zote (risaalaat) zimetiwa ukomo, na kwake yeye umekwishia wahyi kutoka mbinguni na kukoma amri za Mwenyezi Mungu... Wakaanal Laahu bikulli shay-in aliimaa; kwa hivyo akamfanya Muhammad Mwisho wa 74

90 Mitume, na Ujumbe Wake kuwa ni kwa watu wote, uliokusanya kila kitu na kukamilika. Ndani yake mna kheri mpaka Siku ya Kiyama. 28. Allaamah Jalaalud Din as-suyuutwi (911H), katika ad Durrul Manthuur yake (uk. 617 wa Jz. 6), katika kueleza maana ya wakhaataman nabiyyiin, ameandika hivi:...imepokewa kwa Qataadah (r.a.) kuwa maana yake ni Mtume wa Mwisho; na kwa Hasan kuwa maana yake: Mwenyezi Mungu amewakhatimisha Mitume kwa Muhammad (s.a.w.w.), na alikuwa ni wa mwisho kupawa utume. Pia tiz. Na.15 hapo juu. Basi hao ni baadhi ya wanazuoni wa zamani, na hizi zama zetu wa madhihabi mbalimbali ya Kiislamu. Wote wamekomangana kwamba maana ya khaataman nabiyyiin ni Mwisho wa Mitume: hakuna mtume baada yake, kwa sababu hivyo ndivyo alivyoeleza Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwa ajili hii ndiyo pia wakakomangana kwamba: yeyote atakayeamini kuwa Muhammad (s.a.w.w.) si Mtume wa mwisho, basi huyo ni kafiri. Hayo ndiyo maelezo ya wanazuoni. Hebu sasa tumwangalie Mirza Ghulam Ahmad, yeye huyo anayedai na kudaiwa kuwa mtume baada ya Muhammad (s.a.w.w.), amelielewaje neno hili khaatam? Ushahidi wa Maneno ya Mirza Ghulam Ahmad Kwa mujibu wa madondoo ya maneno yake, kama yalivyonukuliwa na Ihsan Ilaahi Dhahiir katika kitabu chake kiitwacho al-qaadiyaaniyah, 35 Mirza Ghulam Ahmad Mtume wa Makadiani amesema hivi: 1. Mimi nilizaliwa, na pamoja nami alizaliwa binti. Yeye alitoka tumboni kwanza, kisha nikatoka mimi. Wala hakuzaliwa yeyote mwengine na wazazi wangu baadaye. Hivyo nikawa wa mwisho (khaatam) wa watoto wao wawili. (Tiryaaqul Quluub, uk. 379). 2. Jina la mwisho wa Mitume (khaatamul anbiyaai) wa wana wa Israeli lilikuwa Isa. (Nusratul Haqq, kijalizo katika Baraahiin Ahmadiyyah). Japokuwa baadaye alijimamasa na kudai utume, lakini kabla ya hapo Mirza Ghulam Ahmad alikubali kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ndiye Mtume wa Mwisho, kama madondoo yafuatayo ya maneno yake yanavyoonyesha: 3. Jee! Hujui kwamba Bwana Mwenye kurehemu na Mfadhili alimwita Mtume wetu (s.a.w.w.) Khaatamal anbiyaai (Mwisho wa Mitume) bila ya ati ati, na Mtume wetu (s.a.w.w.) akalifasiri hilo kwa: hakuna mtume baada yangu kwa ufafanuzi ulio wazi kwa wale watakao kujua? (Humaamatul Bushraa, uk. 32). 4. Aya hii (ya Sura 33:40) inaonyesha waziwazi kwamba hatakuja Mtume yeyote duniani baada ya Mtume wetu (s.a.w.w.). (Izaalatul Awhaam, uk. 614). 5. Kwa hakika Mtume (s.a.w.w.) alikariri mara nyingi kwamba hatakuja mtume baada 35 Chapa ya kwanza iliyochapishwa 1387 H/1967 BK na al-maktabatul Ilmiyyah ya Madina. 75

91 yake. Ile Hadith ya laa nabiyya ba dii (hakuna mtume baada yangu) ni mashuhuri sana kiasi cha kwamba hakuna wa kuutilia shaka usahihi wake. Na Qur ani Tukufu, ambayo kila neno lake ndivyo (qatw-iy), inamsadikisha kwa kusema: walaakin rasuulallahi wakhaataman nabiyyin. Kwa hivyo utume umekomea kwa Mtume wetu. (Pembezoni mwa Kitabul Bariyyah, uk. 184). 6. Mimi ninayaamini yote yanayoaminiwa na Waislamu na wafuasi wa sunna (Ahlus Sunnah). Nayakubali mambo yote yaliyothubutu kwa Qur ani na Hadith. Ninaamini kwamba kila anayedai unabii au ujumbe (risaala) baada ya kiongozi wetu na bwana wetu Muhammad (s.a.w.w.), Mwisho wa Mitume, ni mwongo na kafiri. Na ninaamini kwamba wahyi wa utume ulianza na Adam, aliyesafishwa na Mwenyezi Mungu (swafiyyullah), ukakomea na Muhammad Mteuliwa (s.a.w.w.). (Tabligh-i- Risaalat, Jz. 2, uk. 2). Zaidi ya yote hayo, amesema: 7. Muhyiddiin b. Arabii ameandika kwamba utume wa sharia umekomea kwa Muhammad (s.a.w.w.), lakini utume usio wa sharia sio hivyo. Lakini mimi ninaamini kuwa milango ya kila aina ya utume imefungwa. (Makala ya Mirza Ghulam Ahmad yaliyochapishwa katika gazeti la Makadiani la liitwalo al-hakam ). Hayo ni baadhi tu ya maneno ya Mtume wa Makadiani, yeye mwenyewe, yaliyomo vitabuni mwake. Kama, kama anavyodai katika Arabain Na. 3, uk. 43, yeye hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni wahyi ulioteremshwa, 36 basi kwa nini wafuasi wake wanayapuuza? Au ni kile kisa cha Mayahudi: cha kuiamini baadhi ya Kitabu na kuikataa baadhi nyengine (Sura 2:85)? Sasa tuangalie ya makamusi. Ushahidi wa Makamusi Kabla ya kuanza kutoa ushahidi wa makamusi ya Kiarabu ya Waarabu na wasio Waarabu, na ya Waislamu na wasio Waislamu kuhusu maana ya khaataman nabiyyiin, ni muhimu, kwanza kabisa, tuelewe kazi khaswa ya kamusi. Kazi khaswa ya kamusi ni kurikodi maneno ya lugha fulani na maana yake, kama yalivyotumika katika maandishi na mazungumzo ya lugha hiyo. Basi hebu tuangalie watunzi wa makamusi ya lugha ya Kiarabu ya kawaida na ya kitaalamu wamelielewaje neno hili khaataman nabiyyiinl Lina maana gani? 1. Ibn Faaras, katika uk. 245 wa Jz. 2 (chapa ya kwanza) ya Mu jam Maqaayiisil Lughah, ameandika: Khatama maana yake ni kufikia mwisho wa kitu. Na Mtume (s.a.w.w.) ni khaatamul anbiyaa kwa sababu ni aakhiruhum (mwisho wao). 36 Hii ni Sura 53:3 4 aliyoteremshiwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), ambayo Mtume wa Makadiani amejidaia yeye! 76

92 2. Imam Zubaydi, katika uk. 267 wa Jz. 8 (chapa ya kwanza) ya Taajul Aruus, ameandika: Na kati ya majina yake (s.a.w.w.) ni Alkhaatim na Alkhaatam. Yeye ndiye ambaye ametia ukomo utume kwa kuja kwake. 3. al-jawharii ameandika katika as-swahaah: Khaatima ya kitu ni mwisho wake (aakhiruhuu). Na Muhammad (s.a.w.w.) ni khaatamul anbiyaa (mwisho wa Mitume). 4. Abul Baqaa amesema katika Kulliyyaatu Abil Baqaa: Na Mtume wetu kuitwa khaatamal anbiyaa ni kwa sababu khaatam ni mwisho wa watu. Mwenyezi Mungu Aliyetukuka amesema: Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na Mwisho wa Mitume. 5. Imam Raaghib al-asfahaanii, katika uk. 142 wa al-mufradaat (chapa ya Misri), ameandika: Khaatamun nabiyyiin kwa sababu ameutia ukomo utume; yaani ameutimiza kwa kuja kwake. 6. Na mwenye Majma u Bihaaril Anwaar (uk. 330 wa Jz. 1) ameandika: Khaatim na Khaatam ni katika majina yake (s.a.w.w.). Khaatam ni jina; yaani aakhiruhum (mwisho wao). Na khaatim ni jina la mtenda (ismu faa il / subject). 7. Katika uk. 164 wa Jz. 12 ya Lisaanul Arab (chapa ya Beirut), Ibn Mandhuur ameandika: Khaatam na khaatimah ya kila kitu ni kikomo chake ( aaqibatuhuu) na mwisho wake (aakhiruhuu). Na ikhtitaam (mwisho) ya kitu ni kinyume cha iftitaah (mwanzo wake). Na khaatimus suurah ni mwisho wa sura. Na khitaam na khaatim na khaatam ya kaumu ya (watu) ni aakhiruhum (mwisho wao). Kwa mujibu wa al-lihyaanii: Muhammad ni Mwisho wa mitume (Khaatamul anbiyaa). Na kwa mujibu wa at-tahdhiib: Khaatim na Khaatam ni katika majina ya Mtume (s.a.w.w.). Katika Qur ani: Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na khaataman nabiyyiin; yaani aakhiruhum (mwisho wao). Hivyo ndivyo watunzi wa makamusi walio Waislamu walivyolielewa neno khaataman nabiyyiin: kuwa ni Mwisho wa Mitume. Jee! Wasio Waislamu wanalielezaje? 8. Profesa Hans Wehr (Mjarumani Mkristo), katika uk. 227 wa kamusi lake liitwalo A Dictionary of Modern Written Arabic, ameandika kwamba maana ya khaataman nabiyyin ni: the Seal (i.e. the last) of the Prophets = Mohammed. Kwa Kiswahili ni: Muhuri (yaani, mwisho) wa Mitume = Mohammed. 9. E. W. Lane (Mwingereza Mkristo) naye, katika kamusi lake la miaka mingi na mashuhuri sana liitwalo Arabic-English Lexicon, ameandika hivi: Khaatamun/Khaatimun nabiyyiin (the last of the prophets) in the Kur (xxxiii:40). Hayo yamo uk. 703 wa Sehemu ya Kwanza. Kiswahili chake ni: Khaatamun/khaatimun nabiyyin (mwisho wa mitume) katika Qur ani (Sura 33:40). 77

93 Hivyo basi ndivyo mabingwa na wataalamu wa lugha ya Kiarabu wanavyosema. Wote wamekomangana kwamba neno khaatam maana yake ni aakhir, yaani mwisho. Basi vipi Makadiani peke yao ndio wanaokataa maana hayo? Hebu tuzijadili hujja zao. Hujja za Makadiani na Majibu Yetu Mpaka hapa, tushaona jinsi Mwenyezi Mungu katika Qur ani, kulingana na ile kanuni ya aya za Qur ani kujifasiri zenyewe kwa zenyewe, alivyotufahamisha kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho. Tushaona pia jinsi Muhammad (s.a.w.w.) yeye mwenyewe, kama mfasiri Na.l wa Qur ani, alivyotufafanulia kwa Hadith zake sahihi kadhaa wa kadhaa kuwa hakuna mtume baada yake; yeye ndiye wa mwisho. Hilo likakaririwa na maimamu aliowaacha kuongoza Waislamu baada yake. Maswahaba nao, hawakubaki nyuma. Halafu tumeona jinsi wanazuoni wakubwa wakubwa wa Kiislamu, wa karne mbalimbali na madhihabi mbalimbali, walivyolithibitisha hilo katika Tafsiri zao za Qur ani Tukufu. Mbali na yale ya Mirza Ghulam Ahmad Qadiani mwenyewe kabla ya kujitoa kimasomaso! Tukamalizia kwa makamusi ya Waislamu na wasio Waislamu. Wote hao kwa kauli moja, wamekiri kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwisho; hakuna mtume baada yake. Lakini Makadiani hulikataa hilo, na hutoa hujja zao kujitetea. Hebu tuzijadili hujja hizo, zilizochapishwa katika uk wa Tafsiri yao ya Kiswahili ya Qur ani Tukufu, moja baada ya moja: WAMESEMA (uk ): Khaatamannabiyyiin, Muhuri wa Manabii. Neno Khaatam katika lugha ya Kiarabu lina maana ya Muhuri. Inasimuliwa ya kuwa siku moja Mtume s.a.w. alinuia kuandika barua za kuwabashiri wafalme, na masahaba wakasema ya kwamba Wafalme wa Kiajemi hawapokei barua mpaka iwe na muhuri wa mwandikaji. Mtume s.a.w. alitengenezesha khaatam na juu yake yakaandikwa maneno: Muhammad Mtume wa Mungu (Bukhari jalada 1; Muslim Kitaab-ul-Libaas). Hadith hii inaonyesha ya kuwa kazi kubwa ya muhuri ni kuhakikisha. Mtume s.a.w. alipoitwa na Mwenyezi Mungu Khaatamannabiyyiin (muhuri wa Manabii), ni kudhihirisha ya kuwa bila muhuri wa Mtume s.a.w. ukweli wa Nabii yeyote hautathibitika; yaani Mtume s.a.w. amepewa cheo cha kusadikisha. Asingefika yeye ukweli na utakatifu wao ungekuwa katika hali ya giza. Tena, kama muhuri unapigwa juu ya kitu, chapa inaonekana juu ya kitu hicho. Hivyo Mtume s.a.w. alipoitwa Muhuri wa Manabii ilitabiriwa ya kuwa kama muhuri wake utapigwa unabii utapatikana. Yaani utakatifu wake umekamilika hata umefika kwenye cheo cha kutoa kuwapa wengine daraja ya unabii kwa kupigwa muhuri wake. Kwa mujibu wa maana hii Seyidna Ahmad 37 amesema, Mwenyezi Mungu amempa Mtume s.a.w. muhuri, yaani amepewa ili awape wengine sifa ya unabii, na hakuna Nabii mwingine aliyepewa muhuri namna hii. Kwa sababu hii ameitwa Khaatamannabiyyiin, maana kumfuata kunatoa sifa za unabii, na nguvu yake ya utawa inamfanya mtu awe Nabii; na hakuna Nabii mwingine aliyepata nguvu hii ya utakatifu. (Haqiiqatulwahyi uk. 97) Yaani huyo mtume wao wa uwongo. 38 Katika madondoo ya hujja zao, tumetumia alama ya nyota ( ). Hii ni kuonyesha zile nukta tulizonuia kuzijibu. 78

94 NASI TUNASEMA: (i) Ni kweli kwamba, katika lugha ya Kiarabu, neno khaatam lina maana ya muhuri. Lakini hiyo siyo maana yake peke yake. Neno hilo vilevile lina maana ya pete, kizibo, wa mwisho, kitobwe kilicho nyuma ya shingo, na weupe wa miguu ya farasi. Jee! Kama Makadiani wameipenda hiyo maana ya muhuri, kwa nini wanaikataa hiyo ya wa mwisho, ambayo pia ni maana yake, na ambayo, kwa ushahidi tuliokwisha kuutoa katika uk humu, ina nguvu zaidi kuliko hiyo yao? Hebu nawatutolee ushahidi, kama tulivyoutoa sisi, kubatilisha hiyo maana ya wa mwisho. (ii) Tukumbuke kwamba linalozozaniwa hapa sio maana ya neno khaatam linapokuwa peke yake, bali ni linapounganishwa na neno nabiyyiin na kuwa khaataman nabiyyiin. Sisi tumekwisha onyesha kwa mujibu wa Qur ani Tukufu, Hadith za Mtume (s.a.w.w.), wanazuoni wakubwa wakubwa wa Tafsir, makamusi ya lugha ya Kiarabu, bali hata Mirza Ghulam Ahmad Qadiani mwenyewe kwamba maneno mawili hayo yanapounganishwa pamoja huwa na maana ya Mwisho wa Mitume. Sasa, kama wao wanaikataa tafsiri hii, na kushikilia hiyo yao ya muhuri ambao kwawo wanaweza kupawa utume wengine, basi nawatutolee ushahidi wao; sio wa neno khaatam liwapo peke yake. (iii) Hiyo Hadith ya Bukhari na Muslim waliyoitaja hapo juu, ya Mtume (s.a.w.w.) kutengenezesha muhuri aliokiupiga juu ya barua zake, ni sahihi; hatuikatai. Tunalolikataa ni kuamini kwamba, kwa kutengenezesha muhuri huo, naye pia akawa muhuri! Tena muhuri wa mitume yote! Kwa mantiki gani? Hivi yeyote anayetengenezesha kitu, na yeye mwenyewe naye hugeuka akawa kitu hicho?! Kwa nini, kwa hujja ya Hadith hiyo, wasiseme khaatam ina maana ya muhuri wa barua za Mtume, ambalo ndilo linalolekea, badali ya kusema kwamba ina maana ya Muhammad ni muhuri wa mitume. Khaatam ni ipi hapo? Ni ile iliyokipigwa juu ya barua za Mtume (s.a.w.w.), au ni yeye Mtume (s.a.w.w.) aliyekiipiga hiyo khaatam juu ya barua zake? (iv) Kama kazi kubwa ya muhuri ni kuhakikisha, bila shaka utakuwa uwo (muhuri) ndio mhakikishaji, na kile kilichopigwa muhuri huo kitakuwa ndicho kinachohakikishwa. Sasa, kwa kawaida, kipi kinachotangulia mwenzake hapo? Muhuri unaohakikisha, au maandishi yanayohakikishwa na muhuri huo? Ukimuuliza mtu yeyote atakujibu kwamba, kwa kawaida, kwanza huandikwa maandishi; na mwisho, baada ya kukamilika maandishi hayo, ndipo muhuri unapopigwa kuyahakikisha. Hakuna mtu anayepiga muhuri kwanza, akaandika maneno yake baadaye. Kwa hivyo muhuri hupigwa mwisho kufungia maneno; na chochote kinachoandikwa baadaye huwa kimezidi; hakitambuliwi. Hata Qur ani Tukufu inatufahamisha hivyo. Kwa mfano, katika Sura 6:92 tunasoma kwamba Qur ani ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu kilichoteremshwa kuhakikisha yale yaliyokitangulia. Jee! Qur ani hapo imekuja mwanzo au mwisho? Hali kadhalika, tunaposoma Sura 5:48 tunaona jinsi Mwenyezi Mungu alivyomwambia Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwamba amemteremshia Qur ani kusadikisha/kuhakikisha vitabu vilivyokuwa kabla yake. Jee! Hapo ni kipi kilichomtangulia mwenziwe, na ni kipi kilichokuja mwisho? Ni hivyo vitabu vyengine vilivyohakikishwa, au ni Qur ani iliyokuja kuhakikisha? Mwisho, tuangalie Sura 61:6 inayotueleza kwamba Isa mwana wa Mariamu alitumwa kwa wana wa 79

95 Israeli awambie kuwa yeye alitumwa kwao ili awasadikishie yale yaliyokuwa kabla yake katika Taureti, na awabashirie (awape habari njema) ya Mtume atakayekuja baada yake, naye ni Ahmad (jina jengine la Mtume I Muhammad (s.a.w.w.)). Hapa tuna maswali mawili matatu yatakayosaidia kuelewa hujja yetu: Baina ya Nabii Isa (a.s.) na Taureti, ni nani anayemsadikisha mwenziwe? Na nani aliyekuja mwanzo, na nani mwisho? Baina ya Nabii Isa (a.s.) na Mtume Muhammad (s.a.w.w.), ni nani aliyekuja mwanzo, na nani mwisho? Jee! Kwa mujibu wa aya hiyo Nabii Isa (a.s.), aliyekuja mwanzo, alimsadikisha Mtume Muhammad (s.a.w.w.), aliyekuja mwisho, au alimtolea bishara? Kwa nini asimsadikishe/asimhakikishe kama alivyosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake? Kwa mifano hii michache, ni wazi kwamba mhakikishaji haji kabla ya mhakikishwaji; huja mwisho, baada yake. Hivyo ndivyo ilivyokuwa Qur ani na vitabu vyengine vya Mwenyezi Mungu, na ndivyo alivyokuwa Nabii Isa (a.s.) na Taureti. Lakini yalipokuja ya Nabii Isa (a.s.) na Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Nabii Isa (a.s.) hakuyahakikisha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kwa sababu Mtume Muhammad alikuja baada yake. Badali yake alimtolea bishara tu. Kwa hujja hizi, ambazo zote tumezitoa katika Qur ani, Mtume Muhammad (s.a.w.w.) hawezi kuhakikisha ya mitume watakaokuja baada yake. Maana hilo halijafanywa na Mtume yeyote wa Mwenyezi Mungu. Awezalo kufanya yeye ni kuwatolea bishara, kama vile alivyotolewa yeye na Nabii Isa (a.s.). Nasi hatuioni bishara hiyo mahali popote si katika Qur ani wala Hadith! Tunaloliona ni hakikisho lake kwamba yeye ni Mtume wa Mwisho; hakuna utume baada yake, na kwa hivyo hakuna mtume baada yake. Haya ndiyo aliyotuhakikishia. (v) Ni kweli kwamba Mtume (s.a.w.w.) amepawa cheo cha kusadikisha. Lakini sio cha kusadikisha ya mitume watakaokuja baada yake, maana kama tulivyokwisha ona humu yeye ni Mtume wa mwisho; hakuna mwengine atakayepawa utume baada yake. Alichopawa yeye ni cheo cha kusadikisha ya mitume waliotumwa kabla yake. Hilo ndilo tunalohakikishiwa na Mwenyezi Mungu katika Qur ani Tukufu Sura 2:97; 3:3; 5:48; 35:31 na 46:30. Jee! Wale wanaodai kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alitumwa kusadikisha, au amefanywa muhuri ili kusadikisha, yale ya mitume watakaokuja baada yake, wanaweza kututolea aya zinazosema hivyo, au zinazopinga hizi tulizozitaja sisi hapo juu? (vi) Mtume Muhammad (s.a.w.w.), pamoja na utukufu wote alionao, hana mamlaka hata chembe ya kumpa utume mtu yeyote awe ni muhuri au pete au mwisho wa mitume. Mamlaka ya hilo anayo Mwenyezi Mungu peke Yake. Hivyo ndivyo anavyotwambia Yeye Mwenyewe katika Qur ani Tukufu:...Mwenyezi Mungu ndiye anayejua mahali anapoweka ujumbe Wake... (Sura 6:124). 80

96 Na Mola wako huumba anachotaka, na huchagua anayemtaka. Wao hawana hiari... (Sura 28:68). Mwenye vyeo vya juu, Mwenye enzi. Hupeleka wahyi kwa amri Yake kwa amtakaye miongoni mwa waja Wake ili kuonya (viumbe) siku ya kukutana naye. (Sura 40:15). Hivyo ndivyo anavyosema Mwenyezi Mungu. Kwa sababu hii, hatuwezi kukubali madai ya Makadiani kwamba ati Mtume (s.a.w.w.), kwa kuwa Muhuri wa Manabii (khaatamannabiyyiin), amefika kwenye cheo cha kutoa kuwapa wengine daraja ya unabii kwa kupigwa muhuri wake. Kama Makadiani wanao ushahidi wa Qur ani wa kuthibitisha hilo, au kupinga aya tulizozinukuu hapo juu, tunawatafadhalisha watutolee. (vii) Makadiani wanaposema katika madai yao hapo juu, kwamba Mtume wao amesema: Mwenyezi Mungu amempa Mtume s.a.w. muhuri, yaani amepewa ili awape wengine sifa ya unabii..., tunakuwa na mushkili. Na mushkili wetu ni: Mtume yeye mwenyewe ndiye muhuri, au amepewa muhuri? Kama yeye ndiye muhuri, vipi basi atapawa muhuri? Muhuri hupawa muhuri?! Kama yeye siye muhuri, bali amepewa muhuri, basi tungelipenda kujua: Ni nani huyo aliyempa muhuri huo? Yamesemwa wapi hayo? Sura na aya au Hadith. Kisha tukumbuke kwamba maneno ya Mtume wao huyo yanapingana na yale tuliyoyanukuu humu (uk ) yake vilevile ambayo yanakubaliana na ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake (s.a.w.w.). Jee! Tuyaache ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, tushike ya anayepingana nao?! Zaidi ya hayo; kama, kwa kuwa Khaatamannabiyyiin ( Muhuri wa Mitume ), Mtume amepewa uwezo awape wengine sifa ya unabii, tusemeje kuhusu wale ambao wamewataja katika Tafsiri yao (uk. 736 na 737) kama Khaatamul Muhaajiriin, Khaatamul Auliyaa, Khaatamush-Shu araa na Khaatamul mufassiriin? Tuseme wao ni mihuri, wamepawa ili wawape wengine sifa ya uhamiaji, au uwalii, au utunzi wa mashairi, au ufasiri? Yanaingia akilini hayo? (viii) Wala mtu hapati sifa ya unabii kwa kumfuata Nabii hata awe ni Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Maana kama ni hivyo, maswahaba wakubwa wakubwa kadhaa wa kadhaa, waliofikia kilele cha utwiifu kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), kama Qur ani Tukufu inavyotueleza, tayari wangelikuwa mitume. Lakini hatusomi mahali popote kwamba yeyote kati ya maswahaba hao alipata utume kwa utwiifu wake huo. Wala hatusomi popote katika historia kwamba, katika karne zote 14 za Uislamu, pametokea mtu aliyedai kupata utume kwa kumtwii Mtume Muhammad (s.a.w.w.) isipokuwa huyo Mirza Ghulam Ahmad. Kama yuko, hebu natutajiwe! Kama hayuko na kwa kweli hayuko ndiyo tuseme kwamba wacha-mungu na mawalii wote wakubwa wakubwa, tunaosoma habari zao katika historia, kwa karne zote hizi 14, hawakukifikia kilele cha utwiifu kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) kama kile alichokifikia Mirza Ghulam Ahmad Qadiani? Jee! Linaingia akilini hilo? 81

97 Hata hivyo, tumekwishaona hapo juu na hapana ubaya kumdia tena kwamba utume ni cheo ambacho mtu hukipata kwa kutunukiwa na Mwenyezi Mungu peke Yake. Hakipatikani kwa njia yoyote nyengine, abadan. Wala si kweli kwamba Mtume (s.a.w.w.) ameitwa Khaataman nabiyyiin kwa kuwa kumfuata yeye kunatoa sifa ya unabii ; hasha! Ameitwa hivyo kwa sababu baada yake yeye, kama tulivyoona katika kurasa za nyuma humu, zile hali zote ambazo husababisha mitume watumwe, haziko. Muhammad (s.a.w.w.) tayari amekwisha kuikamilisha dini ya Mwenyezi Mungu ambayo, Yeye Mwenyewe Mwenyezi Mungu, ameahidi kuilinda na kuihifadhi mpaka Siku ya Kiyama. WAKASEMA (uk. 736): Neno khaatam pia lina maana ya pete. Imesimuliwa na sahaba mmoja ya kuwa Mtume s.a.w. alikataza kutumia vyombo vya fedha na khaatam (pete) ya dhahabu na nguo za hariri (Bukhari jalada 1, uk. 143). Katika Hadithi nyingine imesimuliwa ya kuwa Mtume s.a.w. alimwambia mtu mmoja aliyekuwa na pete ya chuma (khaataman min hadiidin), Imekuwaje nakuona umevaa pete ya chuma iliyo pambo la makafiri na la watu wa Jahanamu? Ni dhahiri katika hadithi hizi mbili ya kuwa neno la khaatam limekuwa na maana ya pete. Mtume s.a.w. alitumia pete ya fedha na akawaruhusu Waislamu kutumia pete ya fedha kwa wanaume, na ya dhahabu pia kwa wanawake; na kila mara alitumia neno la khaatam kwa pete. NASI TWASEMA: (i) Neno tunalozozania si khaatam likiwa peke yake, bali ni khaataman nabiyyiin. Jee! Makadiani wanaweza kututolea aya au Hadith yoyote isemayo kuwa maana ya khaataman nabiyyiin ni pete ya mitume? (ii) Hatukatai kuwa, katika lugha ya Kiarabu, kati ya maana kadhaa wa kadhaa ya neno khaatam ni pete. Lakini, kufuatana na kanuni za lugha yoyote, hatuwezi kuitumia maana hiyo popote palipo na neno khaatam. Kwa mfano, ni makosa kulifasiri neno khaatam kwa pete katika Hadith ambamo limekusudiwa muhuri, na kinyume chake. Kwa nini? Kwa sababu kufanya hivyo itakuwa ni kulitoa neno hilo katika fuo la maneno yake. Kwa sababu hii ndiyo tukasema kwamba, kati ya maana zote za neno khaatam, inayowiana nayo mno liwapo na nabiyyiin katika khaataman nabiyyiin, ni wa mwisho. Maana hiyo ndiyo inayowafikiana na Hadith nyengine za Mtume (s.a.w.w.) zinazosema kuwa yeye ni wa aakhir, hakuna mtume baada yangu na unabii na utume umekatika. WAMESEMA TENA (uk. 736): Pete hutumiwa kwa ajili ya mapambo. Mtume s.a.w. kuitwa khaatamannabiyyiin (Pete ya Manabii), Mwenyezi Mungu ameonyesha ya kuwa Mtume s.a.w. amefanywa pambo kwa ajili ya Manabii. Kama Mtume Muhammad s.a.w. asingefika duniani, Manabii wasingepata kupambwa, kwa kuwa wamepewa sifa mbaya katika vitabu vya Mayahudi na Wakristo kama tulivyoeleza mahali pengine humu katika tafsiri hii. Hivyo Mtume s.a.w. kwa kutangaza heshima na utakatifu wa Manabii wote amekuwa sababu ya uzuri na mapambo kwa ajili yao. Kama watu wapatavyo kupambwa kwa kuvaa pete ndivyo ambavyo Mtume s.a.w. amekuwa Pete kwa ajili ya Manabii. 82

98 NASI TUNASEMA: (i) Neno Khaataman nabiyyiin limo katika Qur ani Tukufu. Qur ani ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu alichomteremshia Mtume Wake, Muhammad (s.a.w.w.). Humo humo katika Kitabu hicho (Sura 16:64), Mwenyezi Mungu amempa yeye jukumu la kwanza la kutueleza maana na madhumuni ya maneno yaliyomo humo; pia ametuamrisha tuchukue lolote tuliloletewa na Mtume wetu (s.a.w.w.), na tuache lile alilotukataza nalo (Sura 59:7). Kwa sababu hii ndio sisi, tulipoona kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amelifasiri neno hili kwa maana ya Mwisho wa Mitume kwa Hadith zake sahihi tulizokwisha kuzinukuu humu (uk ), tukasema hivyo. Kama neno hili lingekuwa na maana ya Muhuri wa Manabii au Pete ya Manabii au Pambo la Manabii, kama wadaivyo Makadiani, bila shaka Bwana Mtume (s.a.w.w.) angelitueleza hivyo nagalwaga katika Hadith zake kama alivyotueleza maana ya Mwisho wa Mitume. Jee! Makadiani wanaweza kututolea angalau Hadith moja tu inayounga mkono maana zao hizo? Ikumbukwe! Hatutaki maana ya neno khaatam likiwa peke yake, maana hilo halina makindano. Tunataka Hadith inayoeleza maana ya khaataman nabiyyiin. (ii) Tuchukulie, kwa upande wetu, hata kama kusingelikuwa na Hadith tulizozitaja humu (uk ), lakini tukawa tunakubaliana na Makadiani kwamba kati ya maana za neno khaatam ni hizo wanazozishikilia wao na hii ya wa mwisho tunayoishikilia sisi, kwa nini hii yetu iwe siyo khaswa baada ya kuuzingatia ushahidi wote na hujja zote nyengine tulizozitoa humu kuanzia uk. 58 mpaka uk. 77? Wao Makadiani nawatutolee ushahidi mwengine wenye hujja kama huo. (iii) Hata kama tutakubali kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Pete ya Manabii tutakuwa na kosa gani tukikifasiri cheo hicho hivi? Kwamba: kwa kawaida pete huvikwa kidole, na hukizunguka pande zote. Hivyo huwa hapana nafasi tena ya kuingia kidole chengine. Basi ni vivyo hivyo Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kama pete ya Manabii, amewazunguka manabii wote kama vile pete inavyozunguka kidole chote. Na kama vile pete ya kidole ambavyo haiachi nafasi ya kuingia kidole chengine, ndivyo ambavyo Pete ya Manabii nayo haikuacha nafasi ya kuingia nabii mwengine! Jee! Ni kosa kuelewa hivyo? Kwa nini? (iv) Ikumbukwe kwamba, katika lugha yoyote, maneno huwa na maana yake ya kihakika na ya kimajazi (metaphorical). Kwa mfano, unapotaja neno bendera hujulikana kwamba ni kipande cha kitambaa chenye nakshi maalumu, kinachotumika kama alama ya nchi, chama au harakati fulani. Hiyo ndiyo maana yake ya kihakika. Lakini unaposema kwamba Fulani ni bendera, hakuna yeyote atakayeelewa kwamba fulani huyo ni kile kipande cha kitambaa chenye nakshi maalumu kwa sababu maana hiyo haiingii akilini hapo. Badali yake ataelewa kwamba fulani huyo ana tabia ya bendera: ya kufuata upepo. Yaani, hana msimamo wake mwenyewe: hufuata wengine. Na hii ndiyo maana ya kimajazi. Na mifano namna hii ni mingi sana katika lugha yoyote. Katika hii lugha yetu ya Kiswahili huitumia kwa kumwelezea mtu kuwa ni chuma, papa, fisi, nyoka, lumbwi (kinyonga) na kadhalika. Basi na vivyo hivyo ndivyo lilivyo neno khaatam katika lugha ya Kiarabu. Maana yake ya kimsingi na ya kihakika ni wa mwisho, japokuwa vilevile kama jina (ismun/noun) lina maana ya pete na muhuri. Hivyo, tunaposema kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume 83

99 wa Mwisho huwa tumelitumia neno khaatam kwa maana yake ya kihakika, kama ambavyo tukisema ni muhuri wa au pete ya mitume huwa tumelitumia neno hilo kimajazi. Wala kulitumia neno kimajazi hakulipokonyi neno hilo maana yake ya kihakika. Kama ambavyo kumweleza mtu fulani kuwa ni bendera hakuipokonyi bendera maana yake ya kihakika ya kipande cha nguo, hali kadhalika kumweleza Mtume (s.a.w.w.) kuwa ni pete ya au muhuri wa mitume, hakulipokonyi neno khaatam maana yake ya kihakika ambayo hapo ni wa mwisho. Hivyo Mtume Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho kihakika, na ni Pete ya au Muhuri wa mitume kimajazi. Na maana yake ya kimajazi ni kama tulivyoieleza hapo juu; sio kama walivyoipotoa Makadiani katika Tafsiri yao na vitabu vyao vyengine. WAMESEMA TENA (uk. 736): Katika Tafsir Fat hul Bayaan imesemwa, Mtume s.a.w. amekuwa khaatam (Pete) kwa ajili ya Manabii, na amekuwa pambo kwa ajili yao kwa kuwa yu mmoja wao (Jalada 7). Katika kitabu kingine cha kamusi mmeandikwa chini ya neno khaatam, Na Muhammad ni Khaatamannabiyyiin (kwa te yenye fat ha katika khaatam) kwa maana ya mapambo. Maana hii imechukuliwa katika neno khaatam (pete) ambayo ni pambo kwa anayeitumia (Majma ul-bahrain). Zurkani ameandika chini ya neno la khaatam maana ya mbora kwa kuumbwa na kwa tabia, maana Mtume s.a.w. ni pambo la Manabii kama ilivyo pete pambo la kidole. NASI TUNASEMA: (i) Kama tulivyotangulia kusema humu, sisi hatujakataa kwamba kati ya maana za neno khaatam likiwa peke yake, ni hizo ambazo Makadiani wamezinukuu hapo juu. Tunalozozania nao ni kule kukataa kwao kwamba neno hilo vilevile lina maana ya wa mwisho, na kwamba maana hiyo ndiyo inayowiana zaidi na chungu ya Hadith sahihi za Bwana Mtume (s.a.w.w.) tulizozinukuu humu. (ii) Ikumbukwe kwamba hao wote walionukuliwa hapo juu si mitume. Ni mashekhe tu. Maneno yao hukubaliwa pale tu yanapokuwa hayapingani na ya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Yanapopingana nayo, hutupiliwa mbali; hayashikwi kabisa! Hilo linakubaliwa na hata huyo Mtume wa Makadiani, pale aliposema: Sherehe (maelezo) wala tafsiri yoyote haizingatiwi baada ya ufafanuzi wa Mpokeaji wahyi mwenyewe. (Tabligh-i-Risalat, Jz. 1, uk. 121). Sasa, kama Mtume Muhammad (s.a.w.w.) amefasiri khaataman nabiyyiin kuwa ni Mwisho wa Mitume, kwa ushahidi wa Hadith zake tulizokwishazinukuu, tushike tafsiri ya nani mwengine? Na kwa hujja gani? (iii) Ikumbukwe pia kwamba kumwita Mtume (s.a.w.w.) Pambo la Mitume si sifa kwake; ni tusi! Maana pambo silo linalompa thamani au hishima mwenye nalo au anayelivaa, bali ni kinyume chake. Mwenye pambo au anayelivaa ndiye anayelipa thamani au hishima pambo hilo. Akitaka, atalinunua. Akitaka, atalivaa. Akitaka, atalivua. Na akitaka, atalitupilia mbali! Iko wapi hapo thamani au hishima ya pambo? Mwenyezi Mungu tayari ameshampa Mtume Wake (s.a.w.w.) daraja ambayo hakumpa 84

100 Mtume yeyote mwengine. Tiz. Hadith Na. 13 humu (uk. 65). Basi kwa nini tumpachikie na vyengine zaidi ya alivyopawa na Mwenyezi Mungu? WAMESEMA TENA (uk ): Ukiichungua lugha ya Kiarabu utaona ya kuwa neno khaatam pia lina maana ya ubora... Kwa mfano, Khaatamul mufassiriin maana yake ni mbora wa wanaofasiri. Khaatamul Muhaajiriin ni Mbora wa Wanaohama (Kanzul Ummal jalada 6, uk. 31). Khaatamul Auliyaa ni Mbora wa Mawalii (Tafsiir Saafiy). Khaatamush-Shuaraa ni Mbora wa Watunga mashairi (Wafiyatul Ayyan li Ibn Khalkan); n.k.w. Hivyo kwa kanuni hii ya nahau ya Kiarabu, neno Khaatamannabiyyiin litatafsiriwa Mbora wa Manabii, wala hakuna mfano hata mmoja katika lugha ya Kiarabu ulio kinyume na kanuni hii. NASI TUNASEMA: (i) Hivi watunzi wa makamusi yote tuliyoyataja humu (uk ), ambao wanakubaliwa kuwa mabingwa wa lugha ya Kiarabu, na ambao wamelifasiri neno khaataman nabiyyiin kwa aakhiruhum (mwisho wao), hawaijui kanuni hiyo isipokuwa wao Makadiani peke yao? Hata hao wafasiri wakubwa wakubwa wa Qur ani? Hata maswahaba? Hata maimamu? Hata Mtume Muhammad (s.a.w.w.)?! Tiz. tena uk humu uone maelezo ya wote hao ambao, kwa maoni ya Makadiani ati, hawaielewi kanuni ya nahau ya Kiarabu! Kanuni hiyo inajulikana na wao tu! (ii) Hakuna Mwislamu hata mmoja anayesema kuwa Muhammad (s.a.w.w.) si bora wa Mitume yote; bali husema ni bora wa viumbe vyote vya Mwenyezi Mungu. Katika Hadith Na. 13 tuliyoitaja hapo juu, Mtume (s.a.w.w.) ametumia maneno fudh-dhwiltu alal anbiyaai... ambayo Kiswahili chake ni nimefadhilishwa juu ya mitume... au nimefanywa bora... au, tukitaka kutumia Kiswahili cha kileo, nimeboreshwa juu ya... Kwa hivyo tayari Mwenyezi Mungu ameshampa yeye ubora kwa mambo sita, mojawapo likiwa ni hilo la wakhutima biyan nabiyyuuna (mitume wakatiwa ukomo kwa mimi). Neno wakhutima bii, katika Hadith hii, haliwezi asilan kufasirika kwa nikafanywa bora ya... Hakuna kamusi hata moja, la lugha ya Kiarabu, linalosema kwamba neno khatama (kitendo /verb) lina maana ya kufanya bora. Kama liko, tungependa tutajiwe. (iii) Katika hiyo Kanzul Ummaal, aliyetaja neno khaatamul muhaajiriin ni Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwa ukamilifu, Hadith yenyewe yasema hivi: Makinika ewe ami! Hakika wewe ni mwisho wa wahamiaji (khaatamul muhaajiriin) katika uhamiaji (hijrah) kama ambavyo mimi ni mwisho wa mitume (khaatamun nabiyyiin) katika utume. Hayo, kwa nuskha tuliyonayo sisi, tumeyapata katika uk. 699 wa Jz. 22 ya hiyo Kanzul Ummaal iliyochapishwa mwaka wa 1399 H/1979 B.K. na Muassasatur Risaalah, Beirut. Ama khaatamul mufassiriin; hatukuweza kuipata. Kwa hivyo, tutafurahi kama Makadiani watatueleza ilipo (kitabu, juzuu na mlango). Hata hivyo, neno khaatam katika khaatamul muhaajiriin halina maana ya mbora wa kama 85

101 wanavyodai Makadiani. Na hili ni kwa sababu mbili: (i) Hakuna kamusi lolote la lugha ya Kiarabu linalosema neno khaatam maana yake ni mbora wa hata kimajazi. (ii) Kwa ushahidi mwingi sana tuliotangulia kuutoa humu, tumeona kwamba neno khaatamun nabiyyiin maana yake ni mwisho wa mitume. Kwa hivyo, katika Hadith hii, kwa kujilinganisha yeye kama khaatamun nabiyyiin, na ami yake kama khaatamul muhaajiriin, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikusudia kutufahamisha kwamba ami yake, Abbas b. Abdilmuttwalib, alikuwa mwisho wa wahamiaji kama yeye (s.a.w.w.) alivyokuwa mwisho wa mitume. Na hili linakuwa wazi zaidi tunapoelewa yafuatayo: Kabla ya kufutahiwa Makka, ilikuwa ni wajibu kwa kila Mwislamu, mkazi wa Makka, kuhamia Madina. Abbas b. Abdilmuttwalib, ami yake Mtume (s.a.w.w.), inavyoelezwa na Ibn Hajar katika al-iswaabah, alisilimu muda mfupi tu kabla ya Makka kufutahiwa. Akahamia Madina muda mfupi vilevile kabla ya Makka kufutahiwa. Alipofika Madina ndipo Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama ilivyo katika Hadith tuliyoitaja hapo juu, alipomwambia: Makinika ewe ami!... Alimwita mwisho wa wahamiaji (khaatamul muhaajiriin) kwa vile ambavyo alikuwa ni Mwislamu wa mwisho kuhamia Madina kutoka Makka, kabla ya Makka kufutahiwa. Baada ya hapo, uhamiaji (hijrah) haukuwa wajibu tena. 39 (iii) Katika hiyo Tafsiir as-swaafii, vilevile hatukuweza kuliona neno khaatamul awliyaa. Hivyo, tutafurahi kama Makadiani watatueleza limo chini ya maelezo ya sura na aya gani katika Tafsiri hiyo ili tujue la kujibu. Tuliloliona sisi, chini ya maelezo ya aya ya 40 ya Sura al-ahzaab ya Tafsiri hiyo, ni khaatamul awswiyaa (mwisho wa mawaswii) katika maneno ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliyomwambia Imam Alii (a.s.) kuwa: Mimi ni mwisho wa mitume (khaatamul anbiyaa) na wewe, ewe Alii, ni mwisho wa mawaswii (khaatamul awswiyaa). Kama ambavyo, katika Hadith ya khaatamul muhaajiriin tuliyoitaja hapo juu, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alijilinganisha na Abbas b. Abdilmuttwalib, kadhalika katika Hadith hii anajilinganisha na Imam Alii b. Abii Twaalib. Alivyo yeye khaatamul anbiyaa, ndivyo alivyo Alii khaatamul awswiyaa. Kwa hivyo Alii ni mwisho wa mawaswii ; yaani hakuna waswii mwengine wa Mtume baada yake. Wala hili halipingani na maimamu wengine k.v. Hasan na Husein n.w. kuitwa mawaswii ; maana Alii (a.s.) huwa ni waswii wa Mtume (s.a.w.w.), na waliomfuatia yeye huwa ni mawaswii wa waswii wa Mtume (s.a.w.w.) au mawaswii wa waswii wa waswii wa Mtume (s.a.w.w.). Au, kwa maelezo mengine, tunaweza kusema kuwa waswia wa Imam Alii na kizazi chake (a.s.) ni waswia mmoja uliofungamana na yeye. Kwa hivyo kuwa yeye ni mwisho wa mawaswii ni kinaya (metonymy) cha kwamba ule waswia wake yeye na kizazi chake ndio wa mwisho kwa kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho; na kwa kuwa hakuna mtume mwengine baada yake, kwa hivyo waswia aliouacha yeye utakuwa ni wa mwisho, kwa vile ambavyo hakuna mtume mwengine atakayekuja na kuacha waswia. Kwa hivyo waswia wa Muhammad (s.a.w.w.) utakuwa ni waswia wa mwisho wa Mtume 39 Majashi b. Mas uud as-salmiy alipompeleka ndugu yake, Mujaalid b. Mas uud, kwa Mtume (s.a.w.w.) ili afanye bay ah (achukue kiapo) ya kuhama, Mtume (s.a.w.w.) alimwambia: Hakuna kuhama baada ya Makka kufutahiwa, bali lililobaki ni kufanya bay ah ya kushikamana na Uislamu. (Bukhari). 86

102 yeyote wa Mwenyezi Mungu. 40 Na hilo linathibitishwa na historia. Kuhusu khaatamush Shu araa (mwisho wa watunga mashairi). Hilo pia hatukuweza kulipata katika hiyo Wafayaatul A yaan. Kwa hivyo, tutafurahi kama Makadiani watatujulisha neno hilo limo katika ukurasa na juzuu ya ngapi, ndipo tutakapojua la kujibu. WAMESEMA TENA (uk. 737): Wako wanazuoni wengine waliosema ya kuwa neno Khaatamunnabiyyiin maana yake ni Nabii wa mwisho wa kuleta Sheria. Kisha wamenukuu maneno ya mashekhe kama sita hivi, mbali Bibi Aisha (mke wa Mtume (s.a.w.w.)) na huyo Mtume wao, kuunga mkono dai lao hilo. SISI NASI TUNASEMA: (i) Bila ya wasiwasi wowote, kama Waislamu, hatuwezi kabisa kabisa kuikubali tafsiri hiyo hata isemwe na shekhe mkubwa kadri gani. Na sababu yake ni kuwa tafsiri hiyo inapingana na zile Hadith sahihi za Bwana Mtume (s.a.w.w.) tulizotangulia kuzinukuu humu (uk ), na khaswa zile Hadith Na. 1-3, 7, 10,14 na 17. Kwa hivyo hatuwezi kuacha ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.) na kushika ya mashekhe. (ii) Tafsiri ya neno nabiyyiin katika khaatamannabiyyin kuwa maana yake ni mitume wa kuleta sharia haiowani asilan na matumizi ya neno hilo katika Qur ani. Kwa mfano, katika Sura 3:80 tunaambiwa: Wala Yeye (Mwenyezi Mungu) hawaamuru nyinyi kuwafanya Malaika na nabiyyiin (Manabii) kuwa miungu... Jee! Tuseme hapo kuwa Mwenyezi Mungu, kwa kutumia neno nabiyyiin, amekusudia kutwambia kwamba hatuamuru kuwafanya miungu Malaika na mitume wa kuleta sharia, lakini Mitume wengineo tunaweza kuwafanya miungu?! Na katika Sura 2:177, baada ya kuelezwa wema si nini, tunaambiwa:...bali wema ni wa anayemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na nabiyyiin (Manabii)... Jee! Linalotakikana hapo ni kuamini nabiyyiin ( mitume wa kuleta sharia ) peke yao? Kwa hivyo tunakubaliwa kutowaamini mitume wasioleta sharia?! (iii) La kushangaza zaidi ni kwamba Makadiani, wao wenyewe hapa, wameyasahau yale maneno aliyoyasema Mtume wao katika jarida lao la tarehe 10 Aprili 1903, liitwalo al-hakam. Katika kumjibu huyo Ibnul Arabi waliyemnukuu maneno yake katika hiyo tafsiri yao, alisema: Muhyuddin Ibnul Arabi ameandika kuwa utume wa kuleta sharia ulimalizika kwa Muhammad (s.a.w.w.), na kuwa utume wa kutoleta sharia haukwisha. Lakini mimi ninaamini kwamba milango ya aina zote za utume imefungwa. WAKASEMA TENA (uk. 737): Bibi Aisha, mke wa Mtume s.a.w. alisema: Semeni yeye ni Khaatamannabiyyiin lakini msiseme hakuna Nabii baada yake. (Tafsir Durri Manthur). NASI TUNASEMA: (i) Kama alivyosema Sheikh al-amin b. Aly Mazrui katika uk. 28 wa kitabu chake kiitwacho Mirzai Na Jinsi Wawadanganyavyo Islamu, Hatuwezi kusema ya 40 Tiz. uk. 160 wa Jz. ya Mafaahimul Qur an ya Sheikh Ja far Subhaani. 87

103 kuwa maneno haya aliyatamka kweli Mwana Aisha, kwa sababu hapana sanadi 41 yoyote ilio sahihi wala ilio dhaifu. Na hadith ya Mtume au athari 42 ya Sahaba ikiwa haina sanadi sahihi haitumiwi kabisa, si kefu 43 ikiwa haina kabisa kama hii. (ii) Hata kama maneno hayo yangelikuwa na sanadi, pia tusingeliyakubali kwa sababu nzima! Bibi Aisha alikuwa mke wa Mtume tu (s.a.w.w.). Hakuwa Mtume mwenyewe. Kwa hivyo endapo akasema neno, na neno lenyewe likawa linapingana na la Mtume (s.a.w.w.), bila shaka amri ya Kiislamu ni kuliacha neno hilo na kulishika la Mtume (s.a.w.w.). Na hivyo ndivyo tulivyoamua sisi kufanya; kwamba Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa Mwisho. (iii) Kwa nini Makadiani wakashika maneno ya Bibi Aisha yasiyo na sanadi, na kuziacha Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.) zenye sanadi sahihi, zilizopokewa kwa yuyo huyo Bibi Aisha, zionyeshazo wazi kwamba hakuna mtume baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.)? (Tiz. Hadith Na. 12 na 14 humu, uk. 65). MWISHO WAMESEMA (uk. 738): Hata Mtume s.a.w. mwenyewe amevunja mawazo ya namna hii aliposema wakati alipofariki mtoto wake Ibrahimu, miaka minne baada ya kushuka Aya Khaatamannabiyyiin katika mwaka wa tisa baada ya kuhama, Angeishi Ibrahimu angekuwa Nabii mkweli (Ibni Majah). Basi ingekuwa muradi katika Aya ni kwamba Mtume Muhammad s.a.w. ni wa mwisho na haji tena baada yake Nabii, Mtume angethubutuje kusema, Kama Ibrahimu angeishi angekuwa Nabii? NASI TUNAJIBU: (i) Hadith hiyo si sahihi, bali ni baatil. Hivyo ndivyo alivyosema Imam Nawawi katika uk. 176 wa Asnal Matwaalib. Katika sanadi ya Hadith hiyo mna mtu aitwaye Ibrahim b. Uthmaan. Huyu, kwa komangano la wanazuoni wa Hadith, ni dhaifu. Kwa mujibu wa Miizaanul I tidaal ya adh-dhahabii, Shu bah amesema ni mwongo ; Imam Ahmad amesema ni dhaifu ; Ibn Ma iin amesema si thiqah ; 44 Na an-nasaaii amesema ni matruuk. 45 Kwa hivyo hatuwezi kuikubali Hadith hiyo. (ii) Hata kama tungelikubali kuwa Hadith hiyo ni sahihi, isengelikuwa inapingana na imani ya kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume wa mwisho. Sababu ya hilo ni kwamba maana yake ingekuwa hivi: Lau Ibrahimu angeishi, angekuwa Nabii mkweli. Lakini hakuwa ni wa kuishi, kwa sababu Muhammad (s.a.w.w.) kuwa ni Mtume wa Mwisho kulimzuilia yeye kuendelea kuishi. Na hayo ndiyo aliyoyanukuu Haafidh b. Hajar kutoka Musnad Ahmad kwamba Mtume (s.a.w.w.) amesema: Lau Ibrahimu angebaki, angekuwa Nabii. Lakini hakuwa ni wa kubaki kwa kuwa miongoni mwenu yumo Mwisho wa Mitume (aakhirul anbiyaa). (Fat hul Baarii). 41 Sanadi hapa ni ile orodha ya watu waliompokea Bibi Aisha akisema maneno hayo. 42 Athari ya swahaba ni maneno yaliyosemwa na swahaba yeyote. 43 Si kefu maana yake ni: sambe, seuze au sikwambii. 44 Si mtu wa kutegemeka. 45 Ni mtu wa kutoshikwa maneno yake. Ni wa kuachwa. 88

104 Na haya yanatiliwa nguvu na Hadith ya Bukhari na Ibn Maajah na wengineo, iliyosimuliwa na Ibn Abii Awfaa kwamba: Tbrahimu alikufa alipokuwa yu mtoto. Lau ingekuwa imeamuliwa kuwe na Nabii baada yake (s.a.w.w), basi mtoto wake huyo angeishi, lakini hakuna mtume baada yake. (iii) Neno la Kiarabu la law lililomo katika Hadith hii, na ambalo tumelifasiri kwa kama, ni neno ambalo katika nahau (sarufi) ya Kiarabu huitwa neno la sharti. Na litumiwapo, huwa si lazima lile lililowekewa sharti hilo kuwa. Mfano mzuri ni ule wa Sura 21:22 isemayo: Lau (kama) katika mbingu na ardhi kungelikuwa na miungu isipokuwa Mwenyezi Mungu, bila shaka zingeharibika... Kwa kutumiwa neno law katika aya hiyo, hakumaanishi kwamba uko uwezekano wa kuwako miungu katika mbingu na ardhi; hasha! Hali kadhalika, kwa kutumiwa law katika Hadith hiyo hata kama ingekuwa ni sahihi, sikwambii si sahihi hakumaanishi kwamba uko uwezekano wa kuwako mtume mwengine baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Haya ndiyo majibu yetu ya madai ya Makadiani yaliyochapishwa katika uk wa Tafsiri yao ya Kiswahili chini ya maelezo ya aya ya 40 ya sura hii ya al-ahzaab. Madai yao mengine, chini ya maelezo ya aya nyengine za Qur ani, inshallah tutakuwa tukiyajibu tunapofikia aya hizo katika Tafsiri yetu ya Qur ani Tukufu ambayo tumo katika kuiandika. 89

105 KIJALIZO III HIKIMA YA NDOA ZA BWANA MTUME Moja kati ya hujuma nyingi na kubwa ambazo Wazungu wamemhujumia Mtume (s.a.w.w.) ni ile ya kupenda wake. Hujuma hii imeenezwa sana katika maandishi mengi ya Wazungu hao na kurithiwa na warathi wayo ambao wengi wao ni Wakristo na Mayahudi. Hivyo, baada ya miaka kupita, hujuma hiyo ikawa sio tena ya Wazungu peke yao, bali ya Wakristo na Mayahudi wote kwa jumla. Msingi wa hujuma hii ni ile ruhusa aliyopawa Bwana Mtume (s.a.w.w.) ya kuendelea kukaa na wake zake waliokuwa zaidi ya wane (Sura 33:50). Kwa kuwa wafuasi wake hawaruhusiwi kuwa na wake zaidi ya wanne katika wakati mmoja (Sura 4:3), wapinzani wake wamelitumia hilo kumhujumia yeye kwa kujaribu kuonyesha kwamba amejipendelea nafsi yake kuliko wafuasi wake. Wala hilo si kweli kwa hujja kadhaa: (i) Ruhusa ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kubaki na wake zake waliokuwa zaidi ya wanne hakujipa yeye mwenyewe. Alipawa na Mwenyezi Mungu, kama tulivyokwishaona hapo juu. Kwa hivyo Waislamu, kama waumini wowote, hawawezi kuuingilia uamuzi wa Mwenyezi Mungu. (ii) Japokuwa Mwislamu haruhusiwi kuwa na zaidi ya wake wanne katika wakati mmoja, lakini inapopungua idadi hiyo, anaruhusiwa kuikamilisha - akitaka - kwa kuowa mke au wake wengine. Lakini Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakuruhusiwa hilo. Yeye alilazimika kubaki na haohao aliokuwa nao; hakuruhusiwa kuwaacha wala kuwaolea wake wengine (Sura 33:52). Kwa hivyo, baina yake na wafuasi wake, ni yupi aliyedhikika zaidi hapo? (iii) Tunapozitaamali ndoa za Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama tutakavyozitathmini sasa hivi hapa chini, itatudhihirikia kwamba hazikuwa ni kwa ajili ya kupenda wake. (iv) Kama Wazungu wanamtia ila Mtume Muhammad (s.a.w.w.), na wamewafundisha wafuasi wao wafanye vivyo hivyo, kwa sababu ya kuwa na wake tisia, mbona wamenyamaza ya aliyekuwa na wake mia sabaa na masuria mia tatu? (1 Wafalme 11:3). Lakini pamoja na yote hayo, hebu tutizame ndoa zote za Bwana Mtume (s.a.w.w.) zilikuwa katika vipindi gani vya maisha yake ili tuweze kuzitathmini. Kwa ufupi, maisha ya Bwana Mtume (s.a.w.w.), kuhusu ndoa zake, tunaweza kuyagawa katika vipindi vine: Cha kwanza ni kile cha uvulana mpaka kufikia miaka 25. Cha pili ni kile cha tangu miaka 25 hadi miaka 54. Cha tatu ni kile cha tangu miaka 54 hadi miaka 60. Cha nne ni kile cha tangu miaka 60 mpaka pale alipofariki dunia, alipokuwa na umri wa miaka

106 Kipindi cha Kwanza Hiki ni kipindi cha uvulana wake (kuanzia alipobaleghe) hadi kufikia umri wa miaka 25. Kwa kawaida, kipindi hiki ni kipindi cha utundu - khaswa kwa watu wanaokaa nchi za joto kama Makka. Pia ikumbukwe kwamba zama hizo, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipokuwa na umri huo, zilikuwa huko Makka ni zama za uhasharati na uhuni; washairi na wenye mahaba wakiweza kuzunguka na kujitangaza dhahiri shahiri - hata ndani ya al-kaaba yenyewe! Mwanamke aliyekuwa na mume akiweza kuonana na mwanamume mwengine ili tu apate mtoto kwa mwanamume huyo! Mwanamke yeyote akiweza kumkaribisha mgeni yeyote afanye kitendo naye. Wala hapakuwa na aibu yoyote, wala kitatusi, kwa mwanamume na mwanamke kutembea kabla ya kuowana! Katika hali kama hiyo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikaa mpaka akafikisha miaka 25 bila ya kuujua uchi wa mwanamke yeyote! Jee, hivyo kweli ndivyo anavyokaa mpenda wake yeyote? Kipindi cha Pili Hiki ni kipindi cha kuanzia miaka 25 mpaka alipofikia umri wa miaka 54; jumla ya miaka 30. Katika muda wote huo alikuwa na mke mmoja tu: Bi. Khadija bt. Khuwaylid (r.a.). Hakuwa na mke yeyote mwengine. Hapa ni muhimu tuelewe kwamba, kwanza, mke wenyewe hakuwa rika lake. Alikuwa mkubwa wake kwa miaka 15. Bi. Khadija alikuwa na umri wa miaka 40, hali Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na miaka 25. Pili, Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakuwa mumewe wa kwanza; alikuwa wa tatu. Kabla yake yeye, aliolewa na waume wawili: Hind b. Nabash (Abuu Haala) na, baada ya kufiliwa na huyo, Atiiq b. Abid. Tatu, Bwana Mtume (s.a.w.w.) siye aliyemtaka Bi. Khadija (r.a.); ni Bi. Khadija aliyemtaka Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama inavyoelezwa kwa urefu katika vitabu vya historia. Jee, mtu yeyote ambaye ni mpenda wake, ambaye wa pwani wakimwita na wa bara wakimpungia mikono, kama alivyokuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.), angekaa na mke mmoja miaka yote hiyo ya ujana wake? Tena mke wenyewe awe ni mjane mara mbili, na anayeweza kumzaa?! Kipindi cha Tatu Hiki ni kipindi cha miaka sabaa: baina ya umri wa miaka 54 mpaka alipofikia miaka 60. Katika kipindi hiki ndipo alipoowa wake zake wote waliobaki; na ndipo maadui zake walipopata nafasi ya kumhujumia. Kwa hivyo, ili kuzikinga hujuma hizo, na ili kuzielewa khalfia na sababu za ndoa hizo (na hikima zake) itatubidi tuzidondoe kwa tafsili, moja baada ya moja: (i) Bi. Sawda bt. Zam ah b. Qays (r.a.). Huyu ni mke wa pili wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) Kama mke wa kwanza, yeye pia alikuwa mjane. Mumewe wa kwanza alikiitwa Sakran. 91

107 Baada ya Bi. Khadija kufariki dunia katika mwaka wa 3 kabla ya Hijra, kazi nyingi za nyumbani zilimwangukia Bwana Mtume (s.a.w.w.). Japokuwa Zayd b. Haaritha, aliyekuwa huru lake, alikimsaidia sana katika kazi hizo, lakini nyingi zilimlemea mwenyewe. Ndipo Bi. Khawla bt. Haakim, mke wa Uthmaan b. Madh uun, alipoiona hali hiyo, alipomtolea shauri Mtume (s.a.w.w.) aowe mke mwengine ili apate kumsaidia ulezi. Akamtajia Bi. Sawda (r.a.), ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 55, na mkubwa wa Mtume (s.a.w.w.) kwa umri. Mtume (s.a.w.w.) alipokubali, Bi. Khawla alipeleka uposo na ndoa ikafungwa. (ii) Bi. Aisha bt. Abu Bakar (r.a.). Huyu ndiye mke wake wa tatu; ndiye mke pekee aliyemuowa bikra. Yeye alikuwa binti ya Bwana Abu Bakar aliyekuwa rafikiye Mtume (s.a.w.w.) na aliyekuja akawa Khalifa wa kwanza baadaye. Kwa kauli iliyo mashuhuri, 1 bibi huyu aliolewa akiwa na umri wa miaka 6 au 7. Hilo lilikuwa Makka. Lakini Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakumwingilia mpaka baada ya kuhamia Madina kwa miaka 3. Kwa hivyo alipoingiliwa alikuwa ashatimiza miaka 9 au 10. Kabla ya kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), Bi. Aisha alikuwa ameposwa na mtu aliyekiitwa Jubayr b. Mut im. Lakini kwa kuwa mlango wao ulikuwa ni wa makafiri, na kwa ajili ya khofu waliyokuwa nayo ya kuathiriwa na Uislamu lau Bi. Aisha ataingia katika mlango huo, uposo huo ulivunjwa. Ndipo Bwana Abu Bakar alipopata fursa ya kumwomba Bwana Mtume (s.a.w.w.) awe mkwewe. Hivyo, ndoa alizofunga Bwana Mtume (s.a.w.w.), akiwa bado yuko Makka hajahamia Madina, zilikuwa ni hizo tatu tu - ya Bi. Khadija, Bi. Sawda na Bi. Aisha. Halafu akahamia Madina, na baada ya kuhamia huko - kama historia inavyoeleza - alilazimika kupigana vita vingi na Makureshi (adui zake wakubwa) pamoja na marafiki zao. Katika vita hivyo maswahaba wengi walifariki na kuacha wajane ambao jukumu la kuwatizama na kuwatunza lilimwangukia Bwana Mtume (s.a.w.w.) pamoja na maswahaba wake wengine. Hapo, katika hali kama hiyo, ndipo Waislamu waliporuhusiwa na Mwenyezi Mungu kuowa wake wengi. Kwa upande wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), mke wake mwengine alikuwa ni: (iii) Bi. Hafswa bt. Umar al-khattwaab (r.a.). Huyu, kama jina lake linavyoonyesha, alikuwa ni binti ya Khalifa wa pili baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kabla ya kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), bibi huyu aliolewa na swahaba aliyekiitwa Khumays b. Hudhaafa. Swahaba huyo aliuliwa katika Vita vya Badri (2H). Hivyo Bi. Hafswa, aliyekuwa na umri wa miaka 19 wakati huo, akawa mjane. Kuona hivi, babake akamwendea Bwana Abu Bakar kumtaka amuoze binti yake. Lakini hilo halikuwa. Akamwendea Bwana Uthmaan b. Affaan. Pia lisiwe. Ndipo alipomkabili Bwana Mtume (s.a.w.w.), ambaye alimkubalia. Akamuowa katika mwaka wa 3H. Wakati huo, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka Kauli mashuhuri ni ile yenye nguvu iliyokubaliwa na wanahistoria/wanazuoni wengi. 92

108 (iv) Bi. Zaynab bt. Khuzayma (r.a.). Huyu naye, kama baadhi ya wake wengine wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), alikuwa mjane mara mbili kabla ya kuolewa na yeye. Kwanza aliolewa na Tufayl b. Haarith ambaye alikuja akamwacha. Kisha akaolewa na mdogo wake aliyekiitwa Ubayda. Huyu aliuliwa katika Vita vya Uhud (3H). Baada ya kufiliwa na mume wake huyo, hali ya maisha ya Bi. Zaynab ilikuwa mbaya sana. Japokuwa maswahaba wengi walimpelekea. uposo, lakini hakukubali. Ila alipoendewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.); hapo ndipo alipokubali. Akaolewa katika mwaka wa 3H akiwa na umri wa miaka 30. Kwa bahati mbaya, maisha yake na Bwana Mtume (s.a.w.w.) hayakuwa marefu. Alifariki miezi mitatu tu baada ya ndoa yao, katika huo huo mwaka wa 3H. (v) Bi. Ummu Salama (r.a.). Hilo silo jina lake khaswa; ni kun-ya 2 yake tu. Jina lake khaswa ni Hind bt. (Abii Umayya) Suhayl b. al-mughiira. Yeye pia alikuwa mjane. Alifiliwa na mume wake wa kwanza, aliyekiitwa Abdallah b. Abdul-Asad, miezi minane tu baada ya kupata majaraha makali katika Vita vya Uhud. Alipofariki (4H), mume wake alimwachia watoto watatu na tumbo ya mimba. Kwa hivyo alikuwa na mzigo mkubwa wa kuubeba; mzigo uliomlemea na kumpa dhiki maishani. Mara tu baada ya kumaliza eda yake, Bwana Abu Bakar alimpelekea uposo; lakini alikataa. Halafu ndipo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipomuowa, baada ya kumpelekea maneno na kumkubali. Wakati huo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 57, na yeye miaka 30 hivi. (vi) Bi. Zaynab bt. Jahsh (r.a.). Nasabu ya bibi huvu, jinsi iiivyokuwa hata akaolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), na sababu zake - yote hayo yameelezwa kwa urefu katika maelezo ya aya ya Kwa hivyo yatizame huko. La kukumbushana hapa ni kwamba, alipomuowa bibi huyu katika mwaka wa 5H, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 58; na Bi. Zaynab alikuwa miaka 35 au 38 hivi. (vii) Bi. Ummu Habiba (r.a.). Hii nayo ni kun-ya tu ya bibi huyu; halikuwa jina lake khaswa. Jina lake khaswa ni Ramla bt. Abii Sufyaan - yule aliyekuwa adui mkubwa wa Bwana Mtume (s.a.w.w.) na Uislamu kwa jumla, japokuwa mwishowe alikuja akasilimu. Yeye, na mume wake wa kwanza aliyekiitwa Ubaydullaah, ni kati ya wale waliosilimu mwanzo mwanzo wa Uislamu na kuwahi hata kuhamia Uhabashi (Abyssinia au Ethiopia). Lakini kwa bahati mbaya, baada ya kufika huko, huyo mumewe aliritadi na kuwa Mkristo, na asichukue muda mrefu; akafa. Akamwachia binti aliyekiitwa Habiba ambaye ndiye sababu ya yeye kuitwa Ummu Habiba (yaani: Mama Habiba). 2 Kun-ya ni jina la hishima ambalo mtu huitwa kwa kutanguliziwa neno abuu (baba) au ummu (mama), k.m. Abuu (Baba) Zakariya au Ummu (Mama) Salama. 93

109 Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipopata habari hii ya kuhuzunisha, na baada ya kuelewa shida na dhiki zilizomkabili bibi huyo, alimpelekea salamu za kutaka kumuowa, naye akakubali. Ndoa ikafungwa kwa wakala 3 katika mwaka wa 5H ambapo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 58, na Bi. Ummu Habiba miaka 36 au 37 hivi. (viii) Bi. Juwayriya bt. al-haarith (r.a.). Huyu naye pia alikuwa mjane. Mume wake, aliyekiitwa Musaafi b. Swaf-waan, aliuliwa lcatika vita ambavyo kabila lao la Banii Mustwaliq lilipigana na Waislamu katika mwaka wa 5H. Babake Bi. Juwayriya, aliyekiitwa al-haarith b. Abii Dhwiraar, alikuwa ndiye mkubwa wa kabila hilo. Katika huo mwaka wa 5H, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alipata habari kuwa Banii Mustwaliq wamejiandaa kuwashambulia Waislamu. Alipohakikisha kwamba habari hiyo ilikuwa kweli, Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliwambia maswahaba wake wajiandae kupambana nao. Kwa hivyo Waislamu wakatoka Madina na kupiga kambi mahali paitwapo Muraysii, si mbali sana na Madina. Hapo vita vikauma. Banii Mustwaliq 10 wakauliwa, na zaidi ya 700 wakashikwa mateka. Upande wa Waislamu aliuliwa mtu mmoja tu; na huyo aliuliwa na Mwislamu mwenzake kwa makosa. Kati ya mateka hao alikuwamo huyu Bi. Juwayriya ambaye, kabla ya kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), alikuwa akiitwa Barrah. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akaligeuza jina hilo na kumwita Juwayriya. Wakati alipomuowa bibi huyo, katika huohuo mwaka wa 5H, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 58. (ix) Bi. Swafia bt. Huyayy b. Akhtwab (r.a.). Babake alikuwa mkubwa wa kabila la Kiyahudi la Banii Nadhiir. Aliolewa na waume wawili kabla ya kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.). Mumewe wa pili, aliyekiitvva Kinaana b. Abil Huqaya, aliuliwa 4 katika Vita vya Khaybar (7H) ambapo bibi huyu alishikwa mateka. Baada ya kushikwa mateka na kukubali kusilimu, bibi huyu aliolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.) katika huohuo mwaka wa 7H, ambapo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 60. (x) Bi. Rayhana bt. Sham un (r.a.). Huyu alikuwa Yahudi wa kabila la Banii Nadhiir. Mume wake, aliyekuwa akiitwa Hakam, alikuwa Yahudi vilevile - lakini wa kabila la Banii Quraydhwa. Pale Banii Quraydhwa walipowafanyia khiana Waislamu, na Mwenyezi Mungu alipowaamrisha Waislamu wawaendee na kuzizingira ngome zao (tiz. maelezo ya aya ya 26 humu), ndipo Bi. Rayhana aliposhikwa mateka. Hilo lilikuwa katika mwaka wa 6H. 3 Kuowa kwa wakala ni kuowa kwa kumteua mtu mwengine akuolee kwa niaba yako. 4 Kinaana hakuuliwa vitani khaswa. Alishikwa mateka na kupelekwa akiwa hai mbele za Bwana Mtume (s.a.w.w.). Kabla ya hapo alichangia katika kumzika mtu akiwa hai. Mtu huyo akiitwa Mahmud aliyekuwa na ndugu yake aliyekiitwa Muhammad b. Muslima. Ili kulipiza kisasi cha kuuliwa ndugu yake, Muhammad alimuuwa huyo Kinaana. Na hivyo ndivyo alivyouliwa. 94

110 Kuna shaka shaka baina ya wanahistoria kuhusu bibi huyu: kwamba aliolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.) au la. Baadhi, k.v. Ibn Sa d na Ibn Hajar, wanasema kwamba aliolewa. Waliobaki wanasema la; hakuolewa isipokuwa alitiwa usuriani tu kama alivyofanyiwa Maria Mkibti. Wale waliosema aliolewa, wasema kuwa ilikuwa ni katika mwaka wa 6H. Hapo Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa na umri wa miaka 59. (xi) Bi. Maria Mkibti (r.a.). Huyu, kwa kauli iliyo mashuhuri, alitiwa usuriani 5 na Bwana Mtume (s.a.w.w.). Alikuwa ni Mkibti, kabila la wakazi wa asili wa Misri. Baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuandikiana mkataba wa Hudaybiya na makafiri wa Makka (6H), akawa yu katika amani nao, aliwapelekea wajumbe na barua wafalme na wakubwa wa nchi mbalimbali. Miongoni mwao ni Maqawqis, Gavana wa Misri. Alipoupata ujumbe wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), Maqawqis hakuukubali isipokuwa hakujibu vibaya. Alijibu jawabu ya hishima, na akatoa zawadi nyingi kupelekewa Bwana Mtume (s.a.w.w.). Miongoni mwa zawadi hizo ni wajakazi watatu, mmoja wao akiwa ni huyu Maria. Bwana Mtume (s.a.w.w.) akamtia usunani (7H); ndipo alipomzalia mtoto wa kiume, Ibrahimu, ambaye kwa bahati mbaya alikufa baada ya miezi 15 tu. Yeye na Bi. Khadija ndio peke yao waliomzalia Bwana Mtume (s.a.w.w.) watoto. (xii) Bi. Maymuna bt. al-haarith (r.a.). Bibi huyu alikuwa shemegi yake Abbas b. Abdil Muttwalib (r.a.), ami yake Bwana Mtume (s.a.w.w.). Kabla ya kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.), alitangulia kuolewa na waume wawili. Baada ya kuachwa na mumewe wa kwanza, na kufiliwa na nrumewe wa pili aliyekiitwa Abuu Rahm, ndipo alipoolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.). Hilo lilikuwa katika mwaka wa 7H ambapo yeye alikuwa na umri wa miaka 51, na Bwana Mtume (s.a.w.w.) miaka 60. Huyu ndiye aliyekuwa mke wa mwisho kuolewa na Bwana Mtume (s.a.w.w.). 6 Kipindi cha Nne Hiki ni kile kipindi cha alipofikia umri wa miaka 60 mpaka alipotawafii. Katika kipindi hiki Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakuowa tena asilan. Tathmini ya Ndoa Hizo Kama tulivyosema mwanzo wa makala haya, ndoa za Bwana Mtume (s.a.w.w.) zimetumiwa sana na Wazungu, na baadaye waandishi wengi wa Kikristo hata wasiokuwa Wazungu, kumhujuniia kwa kumtuhumu kuwa alikuwa mpenda-wake! Jee, tuhuma hii ni kweli? Inshallah hapa chini, kwa kueleza hikima ya ndoa hizo, tutaonyesha kwamba si kweli: 5 Suria ni mjakazi ambaye bwana wake aliyemmiliki alimwingilia na kumfanya ni mke wake. Kitendo hiki, ambacho kwacho mjakazi hutoka ujakazini na kuwa huru, ndicho kiitwaclio kutia usuriani. 6 Kuolewa bibi huyu na Bwana Mtume (s.a.w.w.) ndiko kulikosababisha Khalid b. Waliid, maarufu kwa ushujaa wake, kusilimu. Yeye alikuwa shangazi lake. 95

111 Kwanza, kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) kweli alikuwa ni mpenda-wake (i) wakati alipokuwa ni barobaro wa mialca 25, na wanawali wa tele, asingeowa mke aliyekuwa mkubwa wake kwa miaka 15! (ii) tena aliyekuwa ashaolewa vyuo viwiii kabla yake, (iii) akakaa naye miaka 30 bila ya kumuolea! na (iv) si kwa yeye kumtaka huyo mke, bali ni kwa mke kumtaka yeye. Pili, kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) kweli alikuwa ni mpenda-wake (i) asingekaa mpaka akafikia umri wa miaka 54 (wakati ambapo hakuwa na ujana tena) ndipo akaowa mke wa pili, na (ii) asingeowa wake wakuu, thuluthi yao walioolewa vyuo viwili, badali ya wasichana wachanga. Tatu, kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) kweli alikuwa ni mpenda-wake, bila shaka asingewawekea wake zake vikwazo vilivyotajwa katika aya ya 28 humu. Lijulikanalo ni kwamba yeyote anayependa wanawake hujaribu kuwashawishi na kuwavutia kwa kila aina ya anasa; hawambii wateue baina ya maisha ya raha na talaka, kama aiivyofanya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Wala hakufanya hivyo kwa kukosa cha kutoa; hasha. Alifanya hivyo kwa kuwa huo ndio uliokuwa msimamo wake. Nne, kama Bwana Mtume (s.a.w.w.) kweli alikuwa ni mpenda-wake, Mwenyezi Mungu (kama ilivyo katika aya ya 52 humu) asingemharamishia kuongeza wake wengine juu ya hao aliokuwa nao, wala kuwaacha na kuowa wanawake wengine mahali pao. Angaliachiwa uhuru wa kuowa na kuacha shibe yake. Isitoshe! Tunapoyataamali maisha ya Bwana Mtume (s.a.w.w.), khaswa baada ya kuhamia Madina na kuongeza idadi ya wake zake, tutaona kwamba haiwezekani kuwa ndoa hizo zilikuwa ni kwa kupenda wake. Hili ni kwa sababu mbili kubwa: (i) Katika kipindi hicho, Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikuwa yu katika jihadi isiyokoma. Aliutumia wakati wake mwingi kwa kutangaza Uislamu, kuipiga vita shirki, kuamrisha mema na kukataza maovu, kuwaunganisha Waislamu na kuwafunza dini yao, na kupambana na maadui wao kwa ulimi na kwa upanga. (ii) Kila alipokipata nafasi alikuwa akifanya ibada. Alikiswali usiku mpaka miguu yake ikavimba kwa kusimama kwa muda mrefu. Jee! Ni kweli kwamba, mtu aliyekuwa ameshughulika na mambo kama hayo, alikuwa na wasaa wa kutawaliwa na matamanio ya kijinsia? Hasha! Kwa hivyo ndoa zake zilikuwa na falsafa na hikima zake mbali. Miongoni mwa hikima hizo ni: (i) kuupatia Uislamu nguvu na kuupunguzia uadui kwa kujenga ukwe baina yake na yale makabila yaliyokuwa na nguvu ya Kiarahu, bali na hata ya Kiyahudi. (ii) kuwashughulikia wajane wa maswahaba wake, na kuwaondolea ukiwa wa kufiliwa na waume zao, pamoja na kuwawekea mfano wa hilo wale wafuasi wake kwa wenzao wengine walioacha wajane. 96

112 (iii) kupata walimu wa kike, watakaoweza kuwasornesha wanawake wenzao, baada ya wao kusomeshwa na Bwana Mtume (s.a.w.w.). (iv) kuvunja mila na dastuii iliyozowewa na Waarabu wa zama hizo ambayo Mwenyezi Mungu alitaka kuiondoa. Kwa lengo la (i) tuna mfano wa Bi. Aisha, Bi. Hafswa, Bi. Ummu Habiba, Bi. Juwayriya, Bi. Swafia, na Bi. Rayhana. Kwa lengo la (ii) tuna mfano wa Bi. Sawda, Bi. Hafswa, Bi. Zaynab (mjane mara mbili), Bi. Ummu Salama, Bi. Ummu Habiba, na Bi. Maymuna (mjane mara mbili). Kwa lengo la (iii) mfano ni wa wote wake zake kwa vile wao ndio waliokuwa wakiwafikishia wanawake wengine yale waliyokiyasikia kwa mume wao. Lakini, kati yao, waliotangaa mno ni Bi. Aisha, Bi. Ummu Salama, Bi. Zaynab, Bi. Juwayriya, Bi. Hafswa, Bi. Ummu Habiba, Bi. Swafiya, na Bi. Maymuna, Kwa lengo la (iv) tuna mfano wa Bi. Zaynab bt. Jahsh. Hizo basi ndizo ndoa za Bwana Mtume (s.a.w.w.), na hizo ndizo sababu na hikima zake. 97

113 KIJALIZO IV ATI NI KWELI MTUME HARITHIWI? Mas-ala ya kuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) anarithiwa ama harithiwi ni mas-ala ambayo kwayo Waislamu wamekhitalifiana. Kuna wale wanaoamini kwamba anarithiwa. Kuna na wale ambao wanaamini kwamba harithiwi. Khitilafu hii imetokana na utesi uliozuka baina ya Bibi Fatma, binti ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), na Bw. Abu Bakar b. Abii Quhaafa, Khalifa wa kwanza baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), kufariki dunia. Alipokwenda kwa Khalifa wa kwanza kudai urathi wake katika mali yaliyoachwa 1 na babake, Khalifa Abu Bakar alimjibu Bibi Fatma (a.s.) kwamba hawezi kumpa chochote katika tarka hiyo kwa sababu alimpokea Mtume (s.a.w.w.) akisema kuwa wao mitume hawarithiwi; chochote walichokiacha ni sadaka! Wanaoamini kwamba harithiwi Hujja kubwa za wanaoamini kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) harithiwi ni mbili: Ya kwanza ni ile Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w.) alisema: Sisi Mitume haturithiwi. Tulichokiacha ni sadaka... 2 Hadith hii ndiyo ambayo Khalifa Abu Bakar alimtolea Bibi Fatma (a.s.) kuwa ndiyo hujja yake ya kumkatalia kumpa urathi wake. Ya pili ni ile tafsiri ya aya fulani za Qur ani Tukufu inayotolewa na wanazuoni wanaounga mkono uamuzi wa Bwana Abu Bakar. Aya hizo ni: (i) ile ya Sura 27:16 isemayo:...na Sulaymaan alimrithi Daawuud... (ii) ile ya Sura ya 19:5-6 isemayo kwamba Mtume Zakariya alisema:...mola wangu nipe mrathi kutoka Kwako atakayenirithi mimi na kurithi kizazi cha Yakubu... Wanazuoni hao, ili tafsiri ya neno kwa neno ya aya hizo isigongane na ile Hadith iliyosimuliwa na Khalifa Abu Bakar, wamesema kwamba walichorithiana Mitume hao si mali 3 bali ni ilimu na utume. Hizo ndizo hujja za wanaosema kwamba Mtume Muhammad (s.a.w.w.) harithiwi. Hebu sasa tuzitizame za wale wanaozikataa hujja hizo na kuamini kwamba anarithiwa. 1 Alipofariki dunia, Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliacha mali yafuatayo: (i) mabustani sabaa aliyopawa na Mukhayriiq. Huyu alikuwa ni Yahudi aliyesilimu pale Mtume (s.a.w.w.) alipohamia Madina. Vilipokuja Vita vya Uhud, na kabla ya kwenda vitani, aliusia: Kama nitauliwa vitani, basi mali yangu ni ya Muhammad. Hivyo ndivyo alivyoyapata mali hayo. (ii) ardhi alizopawa na Answaar pale alipoingia Madina. (iii) zile ardhi za Banii Nadhiir alizozipata kwa mujibu wa Sura 59:6. (iv) sehemu 18 kati ya sehemu 36 ya ardhi za Khaybar. (v) ardhi za Waadil Quraa. 2 Bukhari, Muslim, Abuu Daawuud, Nasaai, Musnad Ahmad. 3 Hivyo ndivyo zisemavyo Tafsiri nyingi za wale mashekhe wanaounga mkono uamuzi wa Khalifa Abu Bakar. 98

114 Wanaoamini kwamba anarithiwa Hawa wana hujja kadhaa wa kadhaa za kupingia imani ya kuwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) harithiwi. Kati ya hizo ni kwamba ile Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar haikubaliki kwa sababu zifuatazo: (i) Hadith hiyo ni kinyume na misingi mikubwa ya sharia za mirathi zilizotajwa katika Qur ani Tukufu. (ii) vilevile ni kinyume na Hadith nyengine za Bwana Miume (s.a.w.w.) zilizo mashuhuri. (iii) Hadith hiyo imepokewa na Bwana Abu Bakar peke yake. Hali kadhalika wanakataa kuikubali hiyo tafsiri ya Sura 27:16 na 19:5-6 isemayo kwamba hicho kilichorithiwa hapo si mali bali ni ilimu na utume kwa sababu zifuatazo: (i) Bibi Fatma (a.s.) aliikataa tafsiri hiyo. (ii) tafsiri hiyo haiowani na dhahiri ya aya zenyewe. (iii) tafsiri hiyo ilitolewa na wanazuoni kwa jitihadi yao wenyewe ili kuiowanisha na Qur ani Tukufu ile Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar. Mfano wake ni kama ile nadharia (theory) ya Ukhalifa. Ni kinyume na Qur ani Tukufu (a) Kabla ya kuja Uislamu, Waarabu walikirithiana kwa mila yao. Na kwa mujibu wa mila hiyo, mwanamke halikiruhusiwa kurithi. Mwenyezi Mungu akaliondoa hilo kwa Sura 4:7 isemayo: Wanaume wana fungu katika mali yaliyoachwa na wazazi wawili na akraba (zao); na wanawake nao wana fungu katika yale yaliyoachwa na wazazi wawili na akraba (zao) - yawe kidogo au mengi. (Haya) ni mafungu yaliyofaradhiwa (na Mwenyezi Mungu). Kwa aya hii Mwenyezi Mungu aliifutilia mbali ile mila ya kijahilia ya kumtoa mwanamke katika urathi. Ikaweka sharia kwamba, kama vile ambavyo mwanamume ana haki ya kurithi, na mwanamke ni hali kadhalika - ni sawa mali hayo yawe ni mengi au kidogo. Kila mmoja atapata sehemu yake ( mafungu yaliyofaradhiwa ) katika mali yaliyoachwa na wazazi wake au jamaa zake kama ilivyoelezwa katika aya nyengine na Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwa tafsili. Kwa hivyo, kwa mujibu wa aya hii, Bibi Fatma (a.s.), kwa kuwa ni binti (mwanamke), alikuwa na haki ya kumrithi Bwana Mtume (s.a.w.w.) kwa kuwa ni mzazi wake. Na kwa hivyo vilevile, kumnyima Bibi Fatma (a.s.) urathi wake ni sawa na kwenda kinyume na aya hii. (b) Kabla ya kuja Uislamu, na hata mwanzo mwanzo wa Uislamu, mtu alikiweza kumrithi marehemu aliyefungiana naye ahadi, 4 au aliyefungishwa naye udugu na Bwana Mtume (s.a.w.w.), 5 japokuwa mrathi huyo na marehemu huyo hawakihusiana damu wala usaha. Lakini baadaye ada hii uiondolewa na Mwenyezi Mungu kwa Sura 8:75 iliyoweka sharia ya kwamba wanaostahiki kurithiana ni jamaa wa nasaba (ulul arhaami) tu. 4 Tiz. Sura 4:33. 5 Tiz. Sura 8:72. 99

115 Kwa hivyo kumnyima Bibi Fatma (a.s.) urathi wake ni kwenda kinyume na Qur ani Tukufu, na ni sawa na kumfanya Bibi Fatma (a.s.) kana kwamba hakuwa na nasaba na babake! (c) Kama tulivyokwisha kuona hapo juu, kabla ya kuja Uislamu mtoto wa kike halikiruhusiwa kumrithi babake. Lakini Uislamu uliiondoa mila hiyo, na badali yake uliiweka ile sharia isemayo kwamba wote wawili - mtoto wa kiume na wa kike - wana haki ya kuwarithi wazazi wao; isipokuwa kwamba, wanapokuwapo wote wawili, fungu la mwanamume ni kama fungu la wanawake wawili. (Sura 4:11). Kwa hivyo, kwa kuwa Bibi Fatma (a.s.) alikuwa binti ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), alikuwa na haki - kwa mujibu wa aya hii - ya kumrithi babake. Kwa sababu hii, kumzuia kufanya hivyo ni sawa na kwenda kinyume na aya hiyo. (d) Kabla ya kuja Uislamu, mtu alipokuwa na mali, alikuwa na uhuru wa kuusia mali yake yote yarithiwe na mtu yeyote anayemtaka, hata kama hana nasaba naye. Lakini Uislamu ulipokuja, ulilibatilisha hilo. Badali yake ulimlazimisha, kama ilivyo katika sunna za Bwana Mtume (s.a.w.w.), 6 ausie kisichozidi thuluthi moja tu ya mali yake, na kinachobaki akiache kirithiwe na wazazi wake na akraba zake. (Sura 2:80). Kwa hivyo, kama itakubaliwa kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliusia kwamba mali yake yote yende kwa Waislamu kwa jumla, na kumwacha kando binti yake na warathi wake wengine, basi hilo litakuwa ni sawa na kusema - Mwenyezi Mungu apishe mbali - kwamba alikwenda kinyume na aya hiyo, au hata Hadith zake mwenyewe, kama tutakavyoona hapo chini. Na hilo ni muhali. Ni kinyume na Hadith za Mtume (s.a.w.w.) Mpaka hapa tushaona vile ambavyo ile Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar inavyopingana na aya za Qur ani Tukufu. Hebu sasa tutizame jinsi inavyopingana na Hadith nyengine za Bwana Mtume (s.a.w.w.), kama hizi zifuatazo: (i)...hakika wewe, ni bora kuwaacha watoto wako ni matajiri kuliko kuwaacha ni maskini (wahitaji) wanaoomba watu... (Muslim, Daarimi). (ii)...hakika wewe, ni bora kuwaacha warathi wako ni matajiri kuliko kuwaacha ni mafakiri wanaoomba watu kwa mikono yao... (Daarimi). Hadith hizi zinatufahamisha wazi kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) aliwahimiza Waislamu, wanapokuwa na mali ya kurithiwa, wasiwanyime watoto wao na warathi wao, wakawa ni wahitaji au ni maskini wanaoomba watu, bali wawaachie vya kurithi ili wakwasike (watosheke). Kama ni hivyo basi, inaweza kukubalika kwamba baadaye yeye mwenyewe (s.a.w.w.) alirudi nyuma na kuyapinga maneno yake hayo kwa kumwambia Bwana Abu Bakar kwamba asirithiwe na binti yake wala warathi wake wengine? Kwa wale wanaoamini kwamba Mtume 6 Bukhari, Muslim, Daarimi, Naylul Awtwaar. 100

116 (s.a.w.w.) anarithiwa, hilo halikubaliki - khaswa kwa vile ambavyo, kwa mujibu wa sharia ya Kiislamu, binti yake na jamaa zake wengine wameharamishiwa kupokea sadaka na zaka. 7 Kwa maneno mengine, kwa kuikubali Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar ya kuwa Mtume (s.a.w.w.) harithiwi, bila ya kuzibatilisha Hadith tulizozinukuu hapo juu, zinazokubaliwa kuwa ni sahihi, ni sawa na kudai kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.), kinyume na mafunzo yake, alikusudia kumwacha binti yake ni maskini wa kuomba watu! Na hilo halimkiniki asilan. Kwa hivyo lililobaki ni kuikataa Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar. Ni ya Bwana Abu Bakar peke yake Mbali na kuwa Hadith hiyo iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar inapingana na aya za Qur ani na Hadith nyengine za Mtume (s.a.w.w.) tulizozinukuu hapo juu, vilevile haiwezi kukubalika kwa hujja ya kwamba, mbali ya Bwana Abu Bakar pekee, hakuna swahaba mwengine yeyote aliyempokea Bwana Mtume (s.a.w.w.) kusema hivyo! Hata binti yake na wake zake, 8 ambao ndio waliohusika zaidi, hawakumsikia Bwana Mtume (s.a.w.w.) akisema hivyo! Hata Imam Alii (a.s)., aliyekuwa ubavuni mwa Bwana Mtume (s.a.w.w.) saa zote, 9 na aliyekuwa msiri 10 wake, na aliyekuwa mlango 11 wa kuifikia ilimu yake, pia hakuipokea Hadith hiyo! Hivyo kwa kuzingatia hujja hizo, na kwa kuzingatia kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) alikiyajua vizuri sana yote yaliyosemwa na Mwenyezi Mungu katika Qur ani Tukufu na aliyoyasema yeye mwenyewe, kama tulivyoona hapo juu, haikubaliki kwa wale wanaoamini kuwa Mtume (s.a.w.w.) anarithiwa kwamba aweza kuchagua kumwambia mtu mmoja tu (tena asiyehusika na urathi wake) uamuzi muhimu na mkubwa kama huo unaokwenda kinyume na sharia nyengine za mirathi zilizokwisha kuenea. Mitume waliotangulia pia walirithiwa Wale wanaoikubali Hadith iliyosimuliwa na Bwana Abu Bakar, kuwa mitume hawarithiwi, wanapotajiwa Sura 27:16, kwamba Nabii Sulaymaan alimrithi Nabii Daawuud, na Sura 19:6, kwamba Nabii Zakariya alimuomba Mwenyezi Mungu ampe mtoto wa kumrithi, husema kwamba makusudio ya kilichorithiwa hapo si mali bali ni ilimu na utume! Lakini hilo, kwa wale wanaoamini kuwa mitume wanarithiwa, halikubaliki kwa sababu tatu zifuatazo: (i) alipofariki Bwana Mtume (s.a.w.w.), na baada ya Bwana Abu Bakar kuchaguliwa Khalifa, Bibi Fatma (a.s.) alimwendea na kudai urathi wake. Alipokataliwa, alitoa khutba ndefu na kali 12 mbele ya Khalifa Abu Bakar aliyekuwa amekaa na maswahaba wengine. Katika khutba hiyo aliikataa ile Hadith iliyosimuliwa na Khalifa Abu Bakar, kwamba mitume hawarithiwi, kwa kumtajia aya kadhaa za mirathi pamoja na hizo aya mbili, za Nabii Sulaymaan kumrithi Nabii Daawuud na Nabii Zakariya kuomba mtoto wa kumrithi. 7 Bukhari, Muslim, Abuu Daawuud, Daarimi. 8 An Nassu wal Ijtihaad, uk Nahjul Balaagha: Khutba Na Kanzul Ummaal. 11 Mustadrak, Usudul Ghaaba, al-istiiaab, Kanzul Ummaal na vyenginevyo. 12 Balaaghatun Nisaa, uk

117 Kwa hivyo, kama Bibi Fatma (a.s.) alielewa kwamba walichorithiana Mitume hao kilikuwa ni ilimu na utume, bila shaka asingejitetea kwa kuzitaja aya hizo. Bali kwa kuzitaja aya hizo alionyesha wazi kwamba aliamini kuwa Mitume hao walirithiana mali. Na la kukumbukwa hapa pia ni kuwa hakuna rikodi yoyote - katika vitabu vya tafsiri ya Qur ani, wala vya Hadith, wala vya Historia - inayofahamisha kwamba Bwana Abu Bakar alijitetea kwa kutoa tafsiri hiyo iliyotolewa na wanazuoni. (ii) tafsiri hiyo haiowani na dhahiri ya aya zenyewe, kama ambavyo haiowani na ukweli wa mambo ulivyokuwa. Tuanze na Sura 27:16. Wale wanaoikataa tafsiri ya kuwa Nabii Sulaymaan alirithi utume kwa Nabii Daawuud wanauliza: litawezekanaje hilo wakati ambapo Nabii Sulaymaan mwenyewe alipata utume wake pale babake, Nabii Daawuud, alipokuwa bado yu hai? Alipokufa babake alirithi utume gani mwengine? Hali kadhalika tafsiri ya kurithi ilimu ; pia wanaikataa kwa sababu, kwa mujibu wa Qur ani Tukufu (Sura 27:15), ilimu aliyokuwa nayo Nabii Sulaymaan haikuwa ni ya kurithi kwa babake, Nabii Daawuud, bali ilikuwa ni ya kupawa wote wawili na Mwenyewe Mwenyezi Mungu. Ikizidi, ile aliyopawa Nabii Sulaymaan, kwa maelezo ya Sheikh Abdulla Saleh Farsy ya Sura 21:79 katika uk. 421 wa Tafsir yake, ilikuwa kubwa kuliko ile ya babake! Sasa, kama ni hivyo, ni ilimu gani nyengine aliyoirithi Nabii Sulaymaan? Kwa hujja zilizotajwa hapo juu ni wazi kwamba haiwezekani ikawa alichorithi Nabii Sulaymaan kwa Nabii Daawuud ilikuwa ni utume wala ilimu isipokuwa ni mali tu. Sasa tuje kwenye Sura 19:6 ya Nabii Zakariya kuomba mtoto wa kumrithi. Hili, kwa wale wanaomuunga mkono Bibi Fatma (a.s.) halikubaliki. Wao hawakubali kwamba alichoomba ni mtoto wa kumrithi utume kwa sababu zifuatazo: (i) kama aliloomba Nabii Zakariya ni mtoto wa kumrithi utume, kwa nini aongeze kumuomba Mwenyezi Mungu amfanye mtoto huyo ni mwenye kumridhisha Yeye? Ipo haja gani ya kuongeza neno hilo? Kwani Mwenyezi Mungu anaweza kumpa utume mtu asiyemridhisha? (ii) Utume si kitu cha kuombwa. Ni hiba tu ambayo Mwenyezi Mungu, Yeye Mwenyewe, humtunuku wa kumpa (Sura 28:68). Kwa hivyo Mtume yeyote, akiwamo Nabii Zakariya, hawezi kuuomba wala kumuombea mtu mwengine - hata awe ni mwanawe. (iii) mtu anapoomba arithiwe, baada ya yeye kufa (min waraaii), na bila ya kuainia arithiwe nini, moja kwa moja hueleweka kwamba arithiwe mali. Kama ni kitu chengine kisichokuwa mali, lazima akiainie - k.m. nipe mtoto wa kunirithi ilimu yangu. Hivyo ndivyo lugha yoyote inavyokwenda. Ni jitihadi ya wanazuoni Kama tulivyoona hapo juu, tafsiri ya kurithi utume ni tafsiri ambayo haiowani na dhahiri 102

118 ya aya zenyewe, kama ambavyo haiowani na ukweli wa mambo ulivyokuwa. Ni tafsiri iliyotolewa kwa jitihadi ya wanazuoni tu (ambao pia hawakukomangana) waliyoifanya baadaye kumuungia mkono Khalifa Abu Bakar. Na hili si jipya. Jitihadi kama hizo zimefanywa pia katika kadhia nyengine, k.v. katika nadharia (theory) ya Ukhalifa. Katika Ukhalifa imedaiwa, kwa mfano, kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) hakuacha wasia wa nani ashike uwongozi baada ya yeye kufariki dunia; kwamba aliwaachia Waislamu wao wenyewe wamchague wa kuwaongoza. Nao wakamchagua Abu Bakar. Lakini Khalifa Abu Bakar, ionekanavyo, hakupendelea kufanya kama alivyofanya Bwana Mtume (s.a.w.w.). Badali ya kuwaachia Waislamu kumchagua kiongozi wao - wao wenyewe - baada ya yeye kufariki dunia, kama alivyofanya Bwana Mtume (s.a.w.w.), yeye alimteua Umar kabla ya kufariki kwake! Umar akawa khalifa baada yake! Lakini Khalifa Umar naye, kwa upande wake, hakupendelea kufanya alivyofanya Bwana Mtume (s.a.w.w.) wala alivyofanya Khalifa Abu Bakar! Badali yake alileta mfumo wake mpya! Aliteua kamati ya kumchagua khalifa baada ya yeye kufariki dunia; nayo, kufuatana na wasia aliouweka, 13 ilimchagua Uthmaan b. Affaan. Ndipo naye akawa khalifa wa tatu. Khalifa Uthmaan, kwa upande wake, hakuwahi kufanya lolote kuhusu khalifa wa baada yake kwa sababu yeye aliuliwa kabla ya kumakinika kufanya kitu. Kwa hivyo umma ukafanya uchaguzi, na ukamchagua Alii b. Abii Twaalib kuwa Khalifa wao wa nne. 14 Kifo cha Khalifa Uthmaan kilizusha fitna kubwa katika umma - fitna ambayo hapa si mahali pake kuieleza kwa tafsili. 15 Kukawa na kundi la Imam Alii (a.s.), aliyechaguliwa na umma, na kundi la jamaa zake Khalifa Uthmaan (Banuu Umayya), likiongozwa na Muaawiya, 16 lililokuwa likimpinga. Hatimaye fitna hiyo ikasababisha Imam Alii (a.s.) kuuliwa. 17 Lakini kabla ya Imam Alii kuuliwa, alikwisha kumteua mwanawe, Imam Hasan (a.s.) kushikilia uwongozi baada yake. 18 Hilo likawa na nguvu zaidi kwa kuungwa mkono na umma katika uchaguzi uliofuatia, baada ya kifo cha Imam Alii (a.s.). Hata hivyo Muaawiya, akiungwa mkono na jamaa zake, alikataa kumkubali Imam Hasan (a.s.). Hivyo alimpinga 13 Kamati hiyo ilikuwa ya watu sita: Alii b. Abii Twaalib, Zubayr b. al-awaam, Abdulrahmaan b. Awf, Sa d b. Abii Waqqas, Twalha b. Ubaydillaah na Uthmaan b. Affaan. Katika hao, kura ya turufu alipawa Abdulrahmaan b. Awf aliyekuwa mkwe wa Uthmaan b. Affaan. 14 Hivyo ndivyo ilivyokuwa kihistoria. Lakini, kusema kweli, yeye alikuwa ndiye wa kwanza kwa kuteuliwa na Mwenyewe Mwenyezi Mungu (s.w.t.) na Mtume Wake (s.a.w.w.) kama tulivyoeleza kwa tafsili katika kitabu chetu kiitwacho Waswia wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) (kitatoka karibuni). 15 Tizama, kwa mfano, kitabu cha maisha yake kilichoandikwa na Sheikh Muhammad Kasim Mazrui, aliyekuwa Kadhi Mkuu wa Kenya. 16 Huyu alikuwa mtoto wa Abuu Sufyaan aliyekuwa adui mkubwa wa Mtume (s.a.w.w.) na Uislamu. Mamake alikuwa ni Hind bt. Utba aliyetafuna ini la Sayyidna Hamza (r.a.) baada ya kufa shahidi katika Vita vya Uhud. 17 Kisa chake kwa urefu kimeelezwa katika kitabu cha Maisha ya Imam Aly cha Sheikh Muhammad Kasim Mazrui. 18 Hilo ni kulingana na Hadith za Bwana Mtume (s.a.w.w.) kuwa maimamu, baada yake, watakuwa 12; na wote watakuwa Makureshi (Bukhari na Muslim). Pia kwamba watatokana na kizazi cha Imam Alii (a.s.) na Bibi Fatma (a.s.). (Fadhwaailul Khamsa). 103

119 na kupigana naye vita khaswa. 19 Hatimaye, kama babake kabla yake, Imam Hasan naye akauliwa. 20 Uwanja sasa ukabaki ni wa Muaawiya peke yake!' Muaawiya akashikilia uwongozi wa Waislamu kwa muda wa miaka 19. Lakini kabla ya kufariki dunia alihakikisha, kwa kila hila na vitimbi, 21 kwamba mwanawe (Yaziid) ndiye atakayeshikilia uwongozi wa Waislamu baada yake, japokuwa alikuwa aswi mkubwa. 22 Na vivyo hivyo ndivyo ilivyokuwa. Kuanzia hapo, mpaka ulipokuja ukaondolewa na Wazungu 23 katika kame ya 20, mfumo wa ukhalifa uliendelea vile alivyouanzisha Muaawiya: wa mtoto kumrithi babake - kwa hiari au kwa nguvu! Ukawa sasa si Ukhalifa tena, bali ni Ufalme. Nadharia ya sawa ni ipi hapo? Mpaka hapa, kuanzia kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) mpaka kwa Muaawiya b. Abii Sufyaan, tumeona kwamba hakukuwa na mfumo mmoja wa kuamulia nani anayefaa kushikilia uwongozi wa Waislamu baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Sasa basi, mfumo upi hapo ndio wa sawa? Jibu: Kwa kuwa Muhammad (s.a.w.w.) ni Mtume, lazima awe ma sum. Kwa kuwa ni ma sum, hawezi kukosea. Kwa hivyo alilolifanya yeye, lazima liwe ndivyo; halina kasoro. Hali kadhalika; kwa kuwa wote - kuanzia Abu Bakar b. Abii Quhaafa mpaka Muaawiya b. Abii Sufyaan - walikuwa ni maswahaba; na kwa kuwa maswahaba wote ni waadilifu (aduul), 24 haturuhusiwi kuwakosoa! Kwa hivyo mifumo yote waliyotuachia wao nao, ni sawa; haina kasoro - hata kama mifumo hiyo ilitafautiana na ule wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.), au ilitafautiana yoo yenyewe kwa yenyewe!! Lakini hayo yanakubalika kiakili? Bila shaka hayakubaliki. Sasa? Ni tuwaulize wataalamu/ wanazuoni watufunulie. Ili wasimtie makosani Bwana Mtume (s.a.w.w.), na ili wasiwatie makosani maswahaba kwa kuleta mifumo iliyotafautiana na ule wa Bwana Mtume (s.a.w.w.), au iliyotafautiana baina yao wenyewe kwa wenyewe, wanazuoni walifanya jitihadi wakatuletea ile nadharia ya kuikubali mifumo yote hiyo kuwa ni sawa (sahihi)! 19 Tiz. Maisha ya Sayyidnal Hasan cha Sheikh Abdulla Saleh Farsy aliyekuwa Kadhi Mkuu wa Zanzibar, na baadaye Kenya. 20 Aliuliwa kwa sumu aliyotiliwa chakulani na mkewe kwa kushawishiwa na Muaawiya kama inavyosimuliwa na vitabu vya historia. 21 Kwa maelezo ya hila na vitimbi hivyo, tiz. kitabu kilichotajwa Na. 19 hapo juu. 22 Kwa maelezo ya uaswi wake, tiz. vitabu vya historia na pia cha Sheikh Farsy kilichotajwa Na. 19 hapo juu. 23 Wazungu ndio waliomuondoa Khalifa wa mwisho aliyekiitwa Abdulhamid, na aliyekuwa Mturki tarehe 3 Machi, Hiyo ndio imani ya Waislamu wengi ambayo, kwa kuikosoa, tumeijadili kwa urefu katika kitabu chetu, Shia na Sahaba: Majibu na Maelezo. 104

120 Kwa nadharia hiyo, kwa hivyo, Mtume (s.a.w.w.) kuondoka duniani bila ya kuusia 25 nani awe khalifa wake, ni sawa. Khalifa aliye hai, kumteua mwandamizi wake 26 kabla ya yeye kufariki dunia, pia ni sawa. Kikundi cha watu, kiwe kimeteuliwa 27 au kimejiteua chenyewe, 28 kuchagua khalifa, pia ni sawa. Umma kuchagua khalifa, 29 baada ya aliyekuwako kufariki dunia, ni sawa. Mtu kumpinga khalifa aliyeko kitini, kwa kupigana naye vita au kwa kutumia hila na vitimbi, na kumuondoa, halafii akashika ukhalifa, 30 pia ni sawa! Khalifa kumteua mtoto wake awe khalifa baada yake, na mtoto wake kumteua mtoto wake, na mtoto wa mtoto wake kumteua mtoto wake 31 n.k., pia ni sawa! Kwa nini? Kwa sababu tukiukataa mmojapo wa mifumo hiyo, itakuwa tumemtia swahaba anayehusika makosani. 32 Na swahaba ni aduul (mwadilifu); vipi tumtie makosani, hata kama hakufanya alilolifanya Bwana Mtume (s.a.w.w.)?! Hivyo ndivyo wanazuoni, katika kadhia ya Khalifa wa Kwanza kumnyima Bibi Fatma (a.s.) urathi wake, walivyofanya jitihadi yao ya kuziawili Sura 27:16 na 19:6, ili wasimtie Khalifa wa Kwanza makosani kwa uamuzi wake huo - hata kama ulikwenda kinyume na aya kadhaa wa kadhaa za Qur ani na Hadith mutawaatir (mashuhuri) za Bwana Mtume (s.a.w.w.) Hiyo ndiyo imani ya Waislamu wengi; lakini sivyo! Tiz. kitabu chetu: Waswia wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). 26 Kama Khalifa Abu Bakar alivyomteua Bwana Umar b. al-khattwaab. 27 Kama kile kilichoteuliwa na Khalifa Umar kikamteua Bwana Uthmaan b. Affaan. Tiz. kidokezo Na. 13 hapo juu. 28 Kama kile kilichokutana Saqiifa, mara tu baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kufariki dunia, kikamteua Bwana Abu Bakar b. Abii Quhaafa. 29 Kama alivyochaguliwa Imam Alii (a.s.). 30 Kama Muaawiya alivyomfanyia Imam Alii (a.s.) na Imam Hasan (a.s.) Ndipo ikawekwa hukumu kwamba anayeshinda kwa upanga mpaka akawa Khalifa, na kuitwa amiirul mu miniin, si halali kwa yeyote anayemwamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho kulala na asimwone mtu huyo kuwa ni Imamu - awe mwema au mwovu! (al-ahkaamus Sultwaaniyya). 31 Kama walivyofanya Banuu Umayya na Banuu Abbas na wengineo katika historia ya Waislamu. 32 La kushangaza humu mwetu, na kote ulimwenguni kwenye imani hiyo, ni kuona jinsi Waislamu walivyo tayari kugombana na kupigana wanapoambiwa kwamba baadhi ya maswahaba walikosa, lakini wakawa hawajali wanapoambiwa kwamba Bwana Mtume (s.a.w.w.) naye alikosa! 33 Kwa hivyo hii ni nadharia iliyowekwa baada ya Bwana Mtume (s.a.w.w.) kama ilivyowekwa hiyo ya Ukhalifa. 105

121 Hii ni tafsiri ya Sura Al-Ahzaab pamoja na maelezo yake kwa lugha ya Kiswahili. Mbali na kuzieleza kwa urefu aya mbalimbali zilizomo katika sura hii, Sheikh Abdilahi Nassir ameongeza vijalizo vine, baada ya kumaliza tafsiri ya sura yenyewe. Katika Kijalizo cha Kwanza amejadili suala la ahlul bayt ni nani. Kwa hujja za Qur'ani Tukufu na sunna za Mtume Muhammad s.a.w.w., alizozifafanua kwa uwazi sana, ameonyesha. kwamba ahlul bayt si wake wa Mtume s.a.w.w wala si Banii Hashim (masharifu) wote, bali ni watu maalumu. katika Nyumba ya Bwana Mtume s.a.w.w walioteuliwa na Mwenyezi Mungu s.w.t. na kuhifadhiwa na kufanya dhambi na makosa. Yote hayo ameyajadili kiilimu na kimantiki. Katika Kijalizo cha Pili amejadili suala la kuwa Mtume Muhammad s.a.w.w ni Mtume wa mwisho au la. Kwa kutoa hujja zake katika Qur'ani Tukufu, Hadith za Bwana Mtume s.a.w.w, na za baadhi ya maimamu wanaofuatwa na mashia, komangano la maswahaba watukufu, yaliyosemwa na wafasiri wa Qur'ani Tukufu wa madhihabi mbalimbali - tangu karne ya kwanza hadi hii ya kumi na nne - kwa ushahidi wa makamusi ya tafsiri ya Qur'ani na ya lugha ya Kiarabu, ya Waislamu na wasio Waislamu, amethubutisha kwa hujja zisizokanushika kuwa Muhammad s.a.w.w ni Mtume wa Mwisho; hakuji tena Mtume mwengine baada yake. Pia amezidondoa hujja zote zilizotolewa katika uk wa tafsiri ya Qur'ani Tukufu ya Makadiani na kuzijibu moja baada ya moja, kiilimu na kimantiki. Katika Kijalizo cha Tatu, ameeleza kwa urefu hikima ya Mwenyezi Mungu kumruhusu Mtume Muhammad s. a. w.w kuwa na wake zaidi ya wane kwa wakati mmoja, tafauti na wanavyoruhusiwa Waislamu wote: ya kuwa na wake wane tu, sio zaidi, kwa wakati mmoja. Pia ameeleza hikima ya kila moja ya ndoa hizo pamoja na kuzibatilisha zile tuhuma zinazotolewa dhidi ya 'Bwana Mtume s. a. w. w. kwa kuowa wake wengi. Katika Kijalizo cha Nne amethubutisha, kinyume na imani iliyoenea kwa Waislamu wengi, kwamba Mtume Muhammad s. a. w.w. - kama ilivyo kwa Waislamu wote - anarithiwa; na kwamba khatua iliyochukuliwa ya kumnyima binti yake (Bibi Fatma) urathi wake ni kinyume kabisa na Qur'ani Tukufu na Hadith mutawatir za Mtume Wake s. a. w. w. Hiki ni kitabu cha kila Mwislamu kuwa nacho.. i

John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane

John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane SN: John Lesson 18 Page 1 John Lesson Eighteen Yohana Somo la Kumi na Nane Read John chapter sixteen. Soma Yohana sura ya kumi na sita. 1. What "things" is Jesus referring to in these several verses? "Mambo"

More information

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES

Pre-Departure Program Swahili Unit 11 Worksheet UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES UNIT 11: LOCATIVES, PREPOSITIONS, AND RELATIVE AND OBJECT INFIXES TIP: READ ALOUD EVERY SWAHILI WORD TO PRACTICE YOUR SIGHT-READING FLUENCY. PART 1: LOCATIVES 1) Translate the following phrases a. Mimi

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF BOMAS OF KENYA CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF PLENARY PROCEEDINGS, HELD AT THE PLENARY HALL, BOMAS OF KENYA ON 16.03.04 Page 1 of 9 CONSTITUTION

More information

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013

MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013 102/3 KISWAHILI KARATASI YA TATU (FASIHI) JULAI/AGOSTI, 2013 MUDA: SAA: 2½ MTIHANI WA PAMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KIRINYAGA YA KATI MWAKA WA 2013 Hati Ya Kuhitimu Kisomo Cha Sekondari KISWAHILI

More information

NEW INTERNATIONAL VERSION

NEW INTERNATIONAL VERSION RUTH Swahili / English Page 1 RUTHU 1 RUTH 1 1:1 Ikawa zamani za Waamuzi walipoamua, kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja wa Bethlehemu ya Yuda, akaenda kukaa katika nchi ya Moabu, yeye na

More information

There is one God Mungu ni mmoja 1

There is one God Mungu ni mmoja 1 There is one God Mungu ni mmoja 1 God is Mungu ni Title Kichwa Jesus is Yesu ni Genesis 1:1 "In the beginning God (Elohim) created the heavens and the earth." Mwanzo 1: 1 "Hapo mwanzo Mungu (Elohim) aliziumba

More information

The First Ten or Last Ten Verses of Sūrah al-kahf

The First Ten or Last Ten Verses of Sūrah al-kahf K N O W I N G F A L S E M E S S I A H Protection from the Dajjāl s Tribulations Despite the great tribulations the Dajjāl brings by which Allah will test his servants, we are not left to face them alone.

More information

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume

Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtukufu Mtume > Lifuatalo ni jibu alilotoa mtukufu mtume (S.A.W) wakati alipoulizwa na imam Ali (A.S) kuhusu

More information

ITA AT: TO OBEY HIM WITHOUT QUESTION

ITA AT: TO OBEY HIM WITHOUT QUESTION ITA AT: TO OBEY HIM WITHOUT QUESTION جل جلالهAllah sent the Anbiya to be obeyed. This makes logical sense because this is the first principle of change, that the change must be implemented for people to

More information

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh)

BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh) BARUA YA TATU KWA SHEIKH UBAYD AL-JÂBIRĪ [AULIZWA SHEIKH UBAYD] NA Sheikh Sālim at-twawîl (hafidhahullāh) 8 December, 2014 Posted by Salafibayaan ClarificationsRefutations 1223 views Nauliza suali: Muheshimiwa

More information

Ukweli wa hadith ya karatasi

Ukweli wa hadith ya karatasi Ukweli wa hadith ya karatasi Kimeandikwa na: Abdilahi Nassir Haki ya kunakili imehifadhiwa na Abdilahi Nassir, 2003 Chapa ya Kwanza 2003 Kinatangazwa na MARKAZI YA AHLUL BAYT S.L.P. 84603 MOMBASA (KENYA)

More information

THE RIGHTS OF RASOOLULLAH ON HIS UMMAH ARE 7:

THE RIGHTS OF RASOOLULLAH ON HIS UMMAH ARE 7: THE RIGHTS OF RASOOLULLAH ON HIS UMMAH ARE 7: 1. Adab wa Ihtiraam: Our attitude of the utmost respect and honor; 2. Ita at: To obey him without question 3. Ittiba: To follow and emulate him in every way

More information

ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c

ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c Session 4: JCC; Tuesday 17 Dhul Qa dah 1434/ September 24, 2013 1 From the course outline In the name of Allah, the Beneficent, the Merciful. Session 4: Session 4: Tawādu

More information

Ways the Misguided Youth Bent on Takfīr & Bombings

Ways the Misguided Youth Bent on Takfīr & Bombings Ways the Misguided Youth Bent on Takfīr & Bombings Contradict Islam بذل النصح والتذكري لبقايا ااملفتونني بالتكفري والتفجري Title: Original Author: Abd al-muḥsin al- Abbād Source: http://islamancient.com/ressources/docs/101.doc

More information

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1

Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1 Imâm Al-Albâni, Katika Kumsifu Mwanafunzi Wake, Muheshimiwa Sheikh Ali Hasan 1 1. Mujaddid wa zama zetu hizi, Imâm al-albâni alisema katika mwaka wa 1412 AH (1991 CE), ulipokuwa ni wakati baadhi yetu bado

More information

The Virtues of Surah An-Nasr

The Virtues of Surah An-Nasr The Virtues of Surah An-Nasr Revealed in Makkah It has been mentioned previously that - it (Surah An-Nasr) is equivalent to one-fourth of the Qur'an and that - Surah Az-Zalzalah is equivalent to one-fourth

More information

Published on Al-Islam.org ( Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu

Published on Al-Islam.org (  Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu. Mahari ya Damu Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Mahari ya Damu > Mahari ya Damu Mahari ya Damu Authors(s): Ustadh Shahid Murtadha Mutahhari [3] Translator(s): S. Muhammad Ridha Shushtary [4]

More information

ALI 340: Elements of Effective Communication Session Four

ALI 340: Elements of Effective Communication Session Four Communication Session Four و و و أ م ا ح ق الل س ان ف إك ر ام ه ع ن ا ل ن وت ع و يد ه ا ل ي ت رك ال ف ض ول ال يت ال فائ د ة ل ا و ال ب بالن ا س ح س ن الق ول فيهم The right of the tongue is that you consider

More information

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu

Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Ukweli Uliopotea - Sehemu Ya Tatu Waliopotosha Ukweli Author(s): kh Mu tasim Sayyid

More information

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI)

BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI) BARAZA LA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA (Mawasiliano yawasilishwe kwa MSAJILI) Simu 255-022-2120261-7 Ext. 331 Ofisi ya Msajili Nukushi: 255-022-2139951 SLP 9083 DAR ES SALAAM FOMU NAMBA 11 TANZANIA MAOMBI

More information

ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c

ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c ALI 241: Akhlāq of the Ahlul Bayt c Session 3: JCC; Tuesday 11 Dhul Qa dah 1434/ September 18, 2013 1 From the course outline In the name of Allah, the Beneficent, the Merciful. Session 3: al-sidq and

More information

Quran Spelling Bee Second Level (Third to fifth grade) competition words

Quran Spelling Bee Second Level (Third to fifth grade) competition words Meaning Mercy Word From Quran 1. ر ح م ة And when و ل م ا. 2 That we are أ ن ا 3. Spelling Ra H a Meem Ta marbootah Fathatan, Waw Lam Meem Shaddah Alif Hamzah-on-Alif Noon Shaddah Alif The prophet Nooh(P.B.U.H)

More information

In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful.

In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful. Revealed in Makkah ب س م ال له ال رح م ن ال رح يم In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful. إ نا أ نز ل ن ه ف ى ل ي ل ة ال ق د ر 97:1 Verily, We have sent it down in the Night of Al-

More information

Ayatul Kursi (2: )

Ayatul Kursi (2: ) Ayatul Kursi (2:255-257) Ayatul Kursi (2:255-257) & Aamenar Rasul (2:285, 286) My Ayatul Kursi & Aamenar Rasul Workbook www.qfatima.com Name: AYATUL KURSI Suratul Baqara 2:255 257 The verse of the 'Throne'

More information

رسالة أصل دين اإلسالم وقاعدته

رسالة أصل دين اإلسالم وقاعدته رسالة أصل دين اإلسالم وقاعدته "Risālah Aslu Dīn Al-Islām wa Qā idatuhu" Written by Shaykh Al-Islām Muhammad ibn Abdul-Wahhāb Followed by The explanation of "Risālah Aslu Dīn Al-Islām wa Qā idatuhu " Written

More information

Revealed in Mecca. Consist of 34 verses LESSONS FROM LUQMAN. Br. Wael Ibrahim. How can we implement the lessons in our daily lives?

Revealed in Mecca. Consist of 34 verses LESSONS FROM LUQMAN. Br. Wael Ibrahim. How can we implement the lessons in our daily lives? Revealed in Mecca Consist of 34 verses LESSONS FROM LUQMAN Br. Wael Ibrahim How can we implement the lessons in our daily lives? The Chapter of Child Education The chapter is about Luqman s education and

More information

ALI 258: Qualities of a Faithful believer Khutba No. 87 March 25, 2014/ Jumadi I 23, 1435

ALI 258: Qualities of a Faithful believer Khutba No. 87 March 25, 2014/ Jumadi I 23, 1435 ALI 258: Qualities of a Faithful believer Khutba No. 87 March 25, 2014/ Jumadi I 23, 1435 What is the difference between faith and conviction? What are good qualities of speech and silence? How would you

More information

ISLAMIC CREED ( I ) Instructor: Dr. Mohamed Salah

ISLAMIC CREED ( I ) Instructor: Dr. Mohamed Salah ISLAMIC CREED ( I ) العقيدة اإلسالمية Instructor: Dr. Mohamed Salah Islamic Creed Series THE IMPORTANCE OF STUDYING AQEEDAH Imam Abu-Hanifa said, "The understanding of faith is better than understanding

More information

Chapter 31: Islamic Ethics Regarding Asylum, Refugees, and Migration

Chapter 31: Islamic Ethics Regarding Asylum, Refugees, and Migration !1 : Islamic Ethics Regarding Asylum, Refugees, and Migration بسم اهلل الرحمن الرحيم Abu Hurairah (ra) reported: The Messenger of Allah said, "He who gives respite to someone who is in (ﷺ) straitened circumstances,

More information

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU

MALAIKA: WAJUMBE WA MUNGU Kama unataka kujifunza zaidi njia ya Mkristo wa kweli anavyopaswa kuishi, basi ni lazima ujifunze Biblia. Ili kukusaidia; Kanise la Christadelphian Bible Mission limechapisha kijitabu kuhusu mafunzo ya

More information

Surah Mumtahina. Tafseer Part 1

Surah Mumtahina. Tafseer Part 1 Surah Mumtahina Tafseer Part 1 In the name of Allah the Gracious and Most Merciful 1. O you who have believed, do not take My enemies and your enemies as allies, extending to them affection while they

More information

K n o w A l l a h i n P r o s p e r i t y

K n o w A l l a h i n P r o s p e r i t y K n o w A l l a h i n P r o s p e r i t y H E W I L L K N O W Y O U I N A D V E R S I T Y Selections 1 from Jāmi al- Ulūm wal-ḥikam by: Ibn Rajab al-ḥanbalī 1 Taken from Ibn Rajab al-ḥanbalī s book Jāmi

More information

Qur'anic Stories. ALII 209: Deriving Lessons from

Qur'anic Stories. ALII 209: Deriving Lessons from COURSE OBJECTIVE: DERIVE ETHICAL LESSONS through: 1) Reciting & pondering over select passages 2) About stories of past prophets & people 3) Referring to renown tafaseer (commentaries) 4) Discussing related

More information

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags:

Tawasali. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Tawasali Tawasali At-Tawassul Author(s): Seyyid Abdul Rahim Al-Musawi [3] Publisher(s): Al Itrah Foundation [4] Kitabu

More information

F a i t h T H E B E L I E F S O F A M U S L I M

F a i t h T H E B E L I E F S O F A M U S L I M E X P L A I N I N G F a i t h T H E B E L I E F S O F A M U S L I M BY: Muḥammad Ibn Ṣāliḥ al- Uthaymīn 1 1 Adapted from Ibn al- Uthaymīn s books Sharḥ Uṣūl al-īmān and Sharḥ Thalāthah al-uṣūl. Page 1

More information

Chapter 26: The Sin of Favoritism Be Just With Your Children

Chapter 26: The Sin of Favoritism Be Just With Your Children !1 : The Sin of Favoritism Be Just With Your Children بسم اهلل الرحمن الرحيم It was narrated that An-Nu'man said: "My mother asked my father for a gift and he gave it to me. She said: 'I will not be contented

More information

ALI 256: Spiritual and Jurisprudential aspects Salaat

ALI 256: Spiritual and Jurisprudential aspects Salaat ALI 256: Spiritual and aspects Salaat SESSION 3: Al-Sadiq Seminary Surrey, BC March 1, 2014/ Rabi II 29, 1435 1 Getting closer thru Du ā, 2:186 و إ ذ ا س أ ل ك ع ب اد ي ع ي ن ف إ ي ن ق ر يب أ ج يب د ع

More information

His supplication in Asking for Water during a Drought

His supplication in Asking for Water during a Drought ALI 226: Du as 19 and 23 Sahifa February 2013/ Rabi I & II, 1434 و ك ان م ن د ع ائ ه ع ل ي ه الس ل ام ع ن د ال اس ت س ق اء ب ع د ال ج د ب His supplication in Asking for Water during a Drought 1 Quiz on

More information

The Principles of Imāmah in the Qurʾān

The Principles of Imāmah in the Qurʾān The Principles of Imāmah in the Qurʾān Learning Objectives Become familiar with important Qurʾanic verses relating to Imāmah Understand that only Allāh (SWT) has the right to choose His representatives

More information

ISTIGHFAAR Combined with The 99 Names of Allah

ISTIGHFAAR Combined with The 99 Names of Allah ISTIGHFAAR Combined with The 99 Names of Allah kwdwdsadsadsdsdfsfdswthis is a simple short Istighfaar formula to attain closeness to Allah and forgiveness of sins. The benefit of this formula is that a

More information

Adab 1: Prohibitions of the Tongue. Lecture 6

Adab 1: Prohibitions of the Tongue. Lecture 6 Adab 1: Prohibitions of the Tongue Lecture 6 1 Prohibitions In previous lectures we have established the grounds for why this book is important. Dangers of the tongue Rewards and benefits of the silent

More information

Recitation of Surah Ash-Shams in the Isha' Prayer

Recitation of Surah Ash-Shams in the Isha' Prayer Revealed in Makkah Recitation of Surah Ash-Shams in the Isha' Prayer The Hadith of Jabir which was recorded in the Two Sahihs has already been mentioned. In it the Messenger of Allah said to Muadh, Why

More information

One-Eyed, Blind in the Other

One-Eyed, Blind in the Other The Dajjāl s Physical Features One-Eyed, Blind in the Other Imām Muslim collected a ḥadīth from Ḥudhayfah ( رضي اهلل عنه ) who narrated that Allah s messenger ( صل ى اهلل عليه وسل م ) said: ف ن ار ه ج

More information

ALI 340: Elements of Effective Communication Session Six

ALI 340: Elements of Effective Communication Session Six Communication Session Six Imam Zaynul Abidin (a) when asked about speaking or silence, which was better, he said: For each of these two there are harms and when they are both safe from harm speaking is

More information

Welcome to ALI 440: Topical Tafsir of Quran Family Relationships

Welcome to ALI 440: Topical Tafsir of Quran Family Relationships Welcome to ALI 440: Topical Tafsir of Quran Family Relationships Check the following verses in your copy of the Quran Verses for today s session 1) Sura Nur, no.24, verse 36 2) Sura Nahl, no.16, verse

More information

Saudi Arabia s Permanent Council of Senior Scholars on Takfīr 1

Saudi Arabia s Permanent Council of Senior Scholars on Takfīr 1 Saudi Arabia s Permanent Council on Takfīr الفتاوى الشرعية يف القضايا العصرية Title: Original Author: Saudi Arabia s Permanent Council Saudi Arabia s Permanent Council of Senior Scholars on Takfīr 1 All

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) NATIONAL CONSTITUTIONAL CONFERENCE (NCC) VERBATIM REPORT OF PLENARY PROCEEDINGS HELD AT THE PLENARY HALL AT BOMAS OF KENYA ON 26.02.04 Page 1 of 7 CONSTITUTION

More information

The Reason for the Revelation of this Surah and its Virtues

The Reason for the Revelation of this Surah and its Virtues Revealed in Makkah The Reason for the Revelation of this Surah and its Virtues Imam Ahmad recorded from Ubayy bin Ka`b that the idolators said to the Prophet, "O Muhammad! Tell us the lineage of your Lord.''

More information

Story #4 Surah Al-Qasas [Verses 76- ]

Story #4 Surah Al-Qasas [Verses 76- ] Story #4 Surah Al-Qasas [Verses 76- ] You need to feel the importance of each story in the Quran! Never think that the situation is not for you or doesn t apply to you! Every story mentioned in the Quran

More information

Salah The Backbone of Islam

Salah The Backbone of Islam الحمد هلل الذ ي جعل الصالة للمؤمنين نورا وراحة وسرورا أحمد ه سبحان و حمد ا يليق بجال ل وأنيس وجه و وعظيم سلطان و و أ ش ه د أ ن ال إ ل و إ ال الل و و ح د ه ال ش ر يك ل و و ل ي الصالحين المتقين ولعبادت و

More information

Importance of Jama`ah & Ukhuah in Islam. Organize by Toronto Islamic Centre

Importance of Jama`ah & Ukhuah in Islam. Organize by Toronto Islamic Centre Importance of Jama`ah & Ukhuah in Islam Organize by Toronto Islamic Centre و اع ت ص م وا ب ح ب ل الل ه ج م يع ا و ل ا ت ف رق وا و اذ آ ر وا ن ع م ة الل ه ع ل ي ك م إ ذ آ ن ت م أ ع د اء ف ا ل ف ب

More information

Submission is the name of an Attitude

Submission is the name of an Attitude Submission is the name of an Attitude Mirza Yawar Baig Children are taught in kindergarten that A is for apple. If they go to Islamic school they are taught that it doesn t stand for apple but for.جل جلالهAllah

More information

ALI 249: Qur'anic Sciences, Lv 1

ALI 249: Qur'anic Sciences, Lv 1 1 Contents of the Qur an have to be separated from the general principles, qualities and attributes of the Quran So it is very important to understand these general principles and qualities in order to

More information

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili

Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili Kitabu Changu cha Mistari ya Biblia Swahili Compiled by Sandy Harris Designed by Norma Hays This book is lovingly dedicated to our precious grandchildren, the joys of our hearts. It is our prayer that

More information

Simple Daily Deeds for Jannah

Simple Daily Deeds for Jannah Simple Daily Deeds for Jannah Simple Daily Deeds for Jannah بسم الله الرحمن الرحيم All praises are due solely to Allah the Most High and The Most Merciful. We ask Allah to bestow His peace and blessings

More information

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES

ZABURI 91 mstari 1. KJV-lite VERSES This Psalm is a talk between those bringing the Good News and an individual who responds and then with our great God who has been listening to this conversation; and at the end, He also wants to jump in.

More information

A Comparison between Those Obsessed with Takfīr & Bombings and Those Who Call for Peace & Well- Being 1

A Comparison between Those Obsessed with Takfīr & Bombings and Those Who Call for Peace & Well- Being 1 A Comparison between Those Obsessed with Takfīr & Bombings and Those Who Call for Peace & Well-Being بذل النصح والتذكري لبقايا ااملفتونني بالتكفري والتفجري Title: Original Author: Abd al-muḥsin al- Abbād

More information

Islam and The Environment

Islam and The Environment Islam and The Environment By Sh Kazi Luthfur Rahman Human beings are representatives of Allah: Allah, the almighty appointed human beings as his representatives in this world and he made them responsible

More information

This is the last class of phase One and our next class will be phase Two in shaa Allaah.

This is the last class of phase One and our next class will be phase Two in shaa Allaah. بسم اهلل الرمحن الرحيم As-Sarf (Morphology) ~ Class Twenty-Three احلمد هلل رب العاملني وصلى اهلل وسلم وبارك على نبينا حممد وعلى آله وصحبه أمجعني, أما بعد Our teacher began with praising Allaah and sending

More information

In that context it is a contraction of the phase. adda wah ilallaah

In that context it is a contraction of the phase. adda wah ilallaah Da wah Concept DEFINITION The Arabic term د عاا da wa is derived from the verb da aa means to call; to invite; and to supplicate, i.e. to call on God. It is used to refer to the act of conveying or calling

More information

Chapter 28: The Rights of Aunts, Uncles, In-Laws, and the Extended Family

Chapter 28: The Rights of Aunts, Uncles, In-Laws, and the Extended Family !1 : The Rights of Aunts, Uncles, In-Laws, and the Extended Family بسم اهلل الرحمن الرحيم Ali ibn AbuTalib narrated: When we came out from Mecca, Hamzah's daughter pursued us crying: My uncle. Ali lifted

More information

SESSION 31 FREQUENT RECITATIONS. I. SPOKEN ARABIC: Use 3SP. For continuity, see Spoken Arabic in previous lesson.

SESSION 31 FREQUENT RECITATIONS. I. SPOKEN ARABIC: Use 3SP. For continuity, see Spoken Arabic in previous lesson. SESSION 31 FREQUENT RECITATIONS I. SPOKEN ARABIC: Use 3SP. For continuity, see Spoken Arabic in previous lesson. () cold. water I want II. GRAMMAR (Verb DF-3): Practice the 21 forms of ج اه د 31 (he struggled;

More information

Introduction to Sahifa Sajjadiyya

Introduction to Sahifa Sajjadiyya Introduction to Sahifa Sajjadiyya ALI 201, 2/6: Shawwal 1432/ September 2011 Objective: The course will cover a comprehensive discussion on the significance, role and authenticity of Sahifa Sajjadiyya.

More information

ا ح د أ ز ح ا س اح ني ح ث ع ا ت س اح ث ا بس أ ج ع ني, أ ال إ إ ال ا و ح د ال ش س ه ا ه ا ح ك ا ج ني و أ ش ه د أ س د ب

ا ح د أ ز ح ا س اح ني ح ث ع ا ت س اح ث ا بس أ ج ع ني, أ ال إ إ ال ا و ح د ال ش س ه ا ه ا ح ك ا ج ني و أ ش ه د أ س د ب ا ح د أ ز ح ا س اح ني ح ث ع ا ت س اح ث ا بس أ ج ع ني, و أ ش ه د أ ال إ إ ال ا و ح د ال ش س ه ا ه ا ح ك ا ج ني و أ ش ه د أ س د ب و ج ب ح د ا ع ج د ا و ز س ى, أ ا بس ل ج ب و أ و ث س ث س ا و ع ط ف ب ف ب ه

More information

A Glimpse of Tafsir-e Nur: Verses of Surah al-an am

A Glimpse of Tafsir-e Nur: Verses of Surah al-an am Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > A Glimpse of Tafsir-e Nur: Verses 162-165 of Surah al-an am A Glimpse of Tafsir-e Nur: Verses 162-165 of Surah al-an am Authors(s): Muhsin Qara'ati

More information

Understanding God s Mercy, Part 7

Understanding God s Mercy, Part 7 Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Understanding God s Mercy, Part 7 Understanding God s Mercy, Part 7 Authors(s): Mohammad Ali Shomali [1] Publisher(s): Ahlul Bayt World Assembly

More information

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO

EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO EVANGELISM FOR CHRIST UINJILISTI KWA AJILI YA KRISTO FISHERS OF MEN MINISTRIES CHURCH NAME 2 Fishers of Men Ministries uses a Christ centered approach to transform one life at a time by feeding their body

More information

Necessity of Qur an Tilawa during Ramadan. Sessions 1 & 2 of ALI 195 Ramadan 1432/ August 2011

Necessity of Qur an Tilawa during Ramadan. Sessions 1 & 2 of ALI 195 Ramadan 1432/ August 2011 Necessity of Qur an Tilawa during Ramadan Sessions 1 & 2 of ALI 195 Ramadan 1432/ August 2011 The Qur an & the month of Ramadan ش ه ر ر م ض ان ال ذ ي ا ن ز ل ف يو ال ق ر آن :2:185 Allah in the Qur an Month

More information

In the Messenger of Allah, we have an Excellent Example

In the Messenger of Allah, we have an Excellent Example In the Messenger of Allah, we have an Excellent Example 21/01/2012 www.detailedquran.com Some Muslims site the following Ayah (along with 53:3-4 dealt with in another document) to advocate giving books

More information

Surah al-kafiroon Chapter 109 Academy for Learning Islam (www.academyofislam.org) Shaykh Saleem Bhimji

Surah al-kafiroon Chapter 109 Academy for Learning Islam (www.academyofislam.org) Shaykh Saleem Bhimji Noble Qur an Surah al-kafiroon Chapter 109 Academy for Learning Islam (www.academyofislam.org) Shaykh Saleem Bhimji (saleem@al-mubin.org) Sūrah Al-Kāfirūn : Outline General details about this chapter.

More information

Divine Messages of nurturing. from your Creator

Divine Messages of nurturing. from your Creator رسالة : ٦ الد عوة إلى ضبط رسائل رب انية اللسان MESSAGE 6: CALL TOWARDS CONTROL OF THE TONGUE Divine Messages of nurturing The tongue which is guided by Allah will never utter hurtful or harsh words. There

More information

Rabi`ul Awwal 13, 1439 H Fatah 2, 1396 HS December 2, 2017 CE

Rabi`ul Awwal 13, 1439 H Fatah 2, 1396 HS December 2, 2017 CE Rabi`ul Awwal 13, 1439 H Fatah 2, 1396 HS December 2, 2017 CE ح ر ك ات ( There are three basic vowels ( and they have to be read in short single ح ر ك ة stroke ١ stroke: upper ف ت ح ة 1. stroke: front

More information

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO NEW LIFE IN CHRIST MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO DISCIPLESHIP SERIES I FULL LIFE MINISTRY KENYA NAME 2 Purpose: Provide teachings to equip the body of Christ to become warrior disciples of Jesus Christ.

More information

IN THE LIGHT OF QURAN & HADITH SUICIDE IS FORBIDDEN (A RESEARCH OVERVIEW)

IN THE LIGHT OF QURAN & HADITH SUICIDE IS FORBIDDEN (A RESEARCH OVERVIEW) 29 IN THE LIGHT OF QURAN & HADITH SUICIDE IS FORBIDDEN (A RESEARCH OVERVIEW) Hafiz Shakir Mahmood 1 & Hussain Muhammad Qureshi 2 & Ahmad Hassan 3 1 Deptartment of Islamic Studies with Specialization in

More information

QUR ANIC ARABIC - LEVEL 1. Unit ٢٦ - Present Passive

QUR ANIC ARABIC - LEVEL 1. Unit ٢٦ - Present Passive QUR ANIC ARABIC - LEVEL 1 Unit ٢٦ - Present Passive 1 Today s lesson Present Passive Classwork Unit 26 Correction Unit 21, 22, 23, 24 2 ا ل ف ع ل - Verb Present tense action is incomplete a) either being

More information

ALI 489: Qualities of Mutaqqīn

ALI 489: Qualities of Mutaqqīn ALI 489: Qualities of Mutaqqīn Session 1: JCC; Seniors Lounge Wednesday March 6, 2019 Jumādī al-akhar 29, 1440 1ALI 489: Qualities of Mutaqqin The best provision is taqwā و م ا ت ف ع ل وا م ن خ ي ي ع ل

More information

Suggested Global Islamic Calendar By Khalid Shaukat, prepared for

Suggested Global Islamic Calendar By Khalid Shaukat, prepared for Suggested Global Islamic Calendar By Khalid Shaukat, prepared for The Experts Meeting to Study the Subject of Lunar Months Calculation among Muslims Allah subhanahu wa ta ala says in Qur an: Rabat 9-10

More information

Quranic & Prophetic Nurturing Program

Quranic & Prophetic Nurturing Program Quranic & Prophetic Nurturing Program Surah An Noor Class 47 Date: 04 December 2018 / 26 Rabi Al Awal 1440 Obedience The human being is made of clay so he has the potential to be molded in order to progress

More information

Help in Goodness. Mirza Yawar Baig

Help in Goodness. Mirza Yawar Baig Help in Goodness Mirza Yawar Baig جل جلالهAllah ordered us, the Believers to help each other in goodness and not to help each other in evil. He said: و ت ع او ن وا ع ل ى ال بر و الت ق و ى و ال ت ع او ن

More information

HE NEEDS TO COMPLETE RECITATION OF THE WHOLE QUR AN IN AN

HE NEEDS TO COMPLETE RECITATION OF THE WHOLE QUR AN IN AN The carrier of the Qur an cannot have the same behavior as the one who is not a carrier of the Qur an. This is a big responsibility- to be a muslimah who is a carrier of the Qur an and to be a student

More information

(When he said to his father and his people: "What do you worship'') meaning: what are these statues to which you are so devoted

(When he said to his father and his people: What do you worship'') meaning: what are these statues to which you are so devoted ASH-SHU'ARA (69-110) How the Close Friend of Allah, Ibrahim spoke out against Shirk و ات ل ع ل ي ه م ن ب ا إ ب ر ه يم - إ ذ ق ال لا ب يه و ق و م ه م ا ت ع ب د ون - ق ال وا ن ع ب د أ ص ن اما ف ن ظ ل ل ه

More information

from your Creator طه Ta, Ha. 20:1

from your Creator طه Ta, Ha. 20:1 رسالة : ٢ إن ما أ ن ز ل الق ر آن ل سعادة اإلنسان رسائل رب انية MESSAGE 2: THE QURAN HAS BEEN REVEALED ONLY FOR Divine THE Messages HAPPINESS OF of HUMANITY nurturing from your Creator The way of the Quran

More information

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania

HAKIKA YA AHMADIYYA. Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania HAKIKA YA AHMADIYYA Watu wengi hawathamini ukweli. Hata hawashuhguliki kwa kuupeleleza wenyewe. Hata hivyo ukweli, hususa unohusika na Dini, ni muhimu sana kwa kila mwanadamu kwa ajili ya wokovu wake.

More information

KHOJA SHIA ITHNA-ASHARI JAMAAT MELBOURNE INC. In the name of Allah (swt), the Most Compassionate, the Most Merciful

KHOJA SHIA ITHNA-ASHARI JAMAAT MELBOURNE INC. In the name of Allah (swt), the Most Compassionate, the Most Merciful KSIJ MELBOURNE KHOJA SHIA ITHNA-ASHARI JAMAAT MELBOURNE INC. ABN: 17 169 570 29 In the name of Allah (swt), the Most Compassionate, the Most Merciful AMAAL OF LAYLATUL QADR 19TH RAMADHAN (TOTAL 1 HOUR

More information

Collection of Hadith on Faith Signs of Faith- Hadith #1

Collection of Hadith on Faith Signs of Faith- Hadith #1 Collection of Hadith on Faith Signs of Faith- Hadith #1 (30th April 2015-16th Rabi Al Akher, 1436) This section tells us about ahadith that show the signs of faith. ح د ث ن ا ال ق اس م ب ن د ين ار ال ك

More information

The Virtues of Surah Al-Infitar

The Virtues of Surah Al-Infitar Revealed in Makkah The Virtues of Surah Al-Infitar An-Nasa'i recorded from Jabir that Mu`adh stood and lead the people in the Night prayer, and he made the recitation of his prayer long. So the Prophet

More information

DINI JE, DINI NI MUHIMU?

DINI JE, DINI NI MUHIMU? SURA YA KWANZA DINI Hivyo, Mwislamu wa kweli ni yule ambaye hufuata mafundisho ya Uislamu wakati wote. Kama tu Waislamu wa kweli, basi lazima tufuate sheria za Ki-Islamu tukiwa ndani na nje ya nyumba zetu,

More information

Request: Sura 78 Aya 1 to 40. Aqa Mahdi Puya says:

Request: Sura 78 Aya 1 to 40. Aqa Mahdi Puya says: Aqa Mahdi Puya Commentary Surah Naba Request: Sura 78 Aya 1 to 40 [Shakir 78:1] Of what do they ask one another? [Pooya/Ali Commentary 78:1] ع م ي ت س اء ل ون }1{ Naba-il azim (the great news) here and

More information

Allah accepts only from the pious. (5:27)

Allah accepts only from the pious. (5:27) ه ح ي ا ع ف ق ح د أ ن ل ع ف ح ضل ال شام ل ه و إ ح حساى ال ح ك م ل ل ع ه و ح حد ه ال ش يك ح ن ال إ هل إ ه ال ا ل ل د ح شه أ ال ح هد ل ل ان و ص ي ان و أ ض ق ي ام ر م و أ ح شه د أ ه ن س ي د ى ا و ى ب ه يي

More information

As-Sarf (Morphology) ~Class Twenty

As-Sarf (Morphology) ~Class Twenty بسم اهلل الرمحن الرحيم As-Sarf (Morphology) ~Class Twenty احلمد هلل رب العاملني وصلى اهلل وسلم وبارك على نبينا حممد وعلى آله وصحبه أمجعني, أما بعد Our teacher began with praising Allaah and sending salaat

More information

INTERCESSION ON THE DAY OF JUDGEMENT

INTERCESSION ON THE DAY OF JUDGEMENT ARTICLE 3B (CONTINUED FROM 3A) INTERCESSION ON THE DAY OF JUDGEMENT 15. PROPHET TO BE A WITNESS AGAINST HIS OWN PEOPLE ON THE DAY OF JUDGEMENT Definition of Witness: One who is called upon to testify (give

More information

A Balanced Life Self Development

A Balanced Life Self Development ق د أ ف ل ح م ن ز ك اه ا He has succeeded who purifies it, و ق د خ اب م ن د س اه ا And he has failed who instills it [with corruption]. 91:9-10 A Balanced Life Self Development 15 ربیع الا خر 1439 2.1.18

More information

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.

Khadija-tul-Kubra. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam. Published on Books on Islam and Muslims Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Khadija-tul-Kubra Khadija-tul-Kubra Author(s): Sayyed A. A. Razwy [3] Publisher(s): Al-Itrah Foundation [4] Maisha

More information

Race to Jannah - 6 Group E: Surah Taha

Race to Jannah - 6 Group E: Surah Taha طھ{ 1 } Race to Jannah - 6 Group E: Surah Taha ب س م ال رح م ن ال رح یم In the name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful م ا أ ن ز ل ن ا ع ل ی ك ال ق ر آن ل ت ش ق ى إ لا ت ذ ك ر ة ل م ن ی خ ش

More information

1. In Islam there is NO hatred of others. WE DO NOT DIFFERENTIATE on Race, Ethnicity, Colour, Nationality or Religion.

1. In Islam there is NO hatred of others. WE DO NOT DIFFERENTIATE on Race, Ethnicity, Colour, Nationality or Religion. اى ح ذ ى ي اى ز ي أ ز ه اى ن ت اب و ى ج ع و ى ع ى ج ا و ج ع و ى ات ق ا ف ش ج ا و خ ش ج ا و أ ش ه ذ أ ال إ ى إ ال اىي و ح ذ ال ش ش ل ى أ ز ه اى ق ش آ ذ ا ة و ىس ا و أ ش ه ذ أ س ذ ا و ب ا ح ذ ا ع ب ذ اىي

More information

In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful.

In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful. Revealed in Makkah ب س م ال له ال رح م ن ال رح يم In the Name of Allah, the Most Gracious, the Most Merciful. و ال ع د ي ت ض ب حا 100:1 By the `Adiyat (steeds), snorting. ف الم ور ي ت ق د حا 100:2 Striking

More information

الكافي AL-KAFI. ج 1 Volume 1 اإلسالم الكليني المتوفى سنة 329 هجرية

الكافي AL-KAFI. ج 1 Volume 1 اإلسالم الكليني المتوفى سنة 329 هجرية الكافي AL-KAFI ج 1 Volume 1 للمحد ث الجليل والعالم الفقيه الشيخ محمد بن يعقوب الكليني المعروف بثقة اإلسالم الكليني المتوفى سنة 329 هجرية Of the majestic narrator and the scholar, the jurist, the Sheykh

More information

Spelling. Fa kasrah, Ya. Meem fathah, Alif. Lam fathah, Alif

Spelling. Fa kasrah, Ya. Meem fathah, Alif. Lam fathah, Alif Meaning Word from Quran Allah (Subhanahu wa taalaa) الل ه. 1 From In Not Indeed Not, No Except, Unless, But That On He said To them Then م ن ف م ا إ ن ل إ ل أ ن ع ل ى ق ال ل م ث.2.3.4.5.6.7.8.9.11.11.12

More information

Chapter 39: Without Justice, There Can Be No Peace

Chapter 39: Without Justice, There Can Be No Peace !1 : Without Justice, There Can Be No Peace بسم اهلل الرحمن الرحيم Ibn 'Abbas told Shahr (ibn Hawshab), "While the Prophet, may Allah bless him and grant him peace, was sitting in the courtyard of his

More information

Bilad Al Sham Media. Risalat on Tawhid. Presents: (2) The English translation of our release:

Bilad Al Sham Media. Risalat on Tawhid. Presents: (2) The English translation of our release: Bilad Al Sham Media Presents: (2) The English translation of our release: Risalat on Tawhid First edition: Three things obligated due to Shirk The three fundamentals Wajib upon us all to have Iman in Shirk

More information